Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 12 Juni 2020

WITO WATOLEWA WANANCHI KUENDELEA KIJIKINGA NA CORONA ILI PIA KUJIKINGA NA MAGONJWA MENGINE.

- Hakuna maoni



 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (kushoto) akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma kupata huduma ambapo amezungumza nao kuendelae kujilinda na ugonjwa wa corona kwa mbinu zinatotolewa na Wizara ya Afya ikiwemo tiba asili ya kujifukiza. 


 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (kulia) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika wakielekea kwenye kituo kilichotengwa kuhudumia wagonjwa wa corona  ambacho hakina mgonjwa yeyote.

 

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi akizunguma na watumishi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa alipotembelea hospitlai hiyo, Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika.




WITO WATOLEWA WANANCHI KUENDELEA KIJIKINGA NA CORONA ILI PIA KUJIKINGA NA MAGONJWA MENGINE.

Na WAMJW-DOM

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujikinga dhidi ya ugonjwa wa corona na kudhibiti magonjwa mengineyo ya kuambukiza.

Prof. Makubi ametoa wito huo leo alipofanya ziara ya kuona hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Jijini Dodoma.

“Katika kudhibiti ugonjwa wa corona wananchi walipokea kwa mikono miwili mbinu za kuepuka kuambukizwa ugonjwa wa corona ikiwemo unawaji mikono kwa maji yanayotirika na sabuni, uvaaji wa barakoa, kuepuka mikusanyiko na misongamano pamoja na mbinu za tiba asilia/tiba mbadala ili kutibu ugonjwa wa corona”. Amesema Prof. Makubi

Pamoja na kupungua kwa ugonjwa wa corona nchini, Prof. Makubi amesema kuwa bado Watanzania tunatakiwa kuendelea kuchukua tahadhari za kinga ili hatimae tuweze kutokomeza kabisa ugonjwa wa corona au pale ambapo bado utaendelea kuwepo tuweze kuishi nao bila madhara makubwa.

Prof Makubi amesema kuwa Serikali inawapongeza wananchi kwa kuipokea na kutumia njia zote zilizotelewa kukabiliana na ugonjwa wa corona pamoja na magonjwa mengine ya kuambukiza na kuwataka wananchi kuendelea na mbinu walizoelimishwa kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.

“Mwamko tulio nao sasa hivi wananchi juu ya mbinu hizi tusiziache, tukiendelea nazo zitatusaidia kujikinga na magonjwa mengine” amesisitiza Prof. Makubi.

Hatukuwa na utamaduni wa kunawa mikono mara kwa mara, lakini tuelewe pia usafi wa mikono unatusaidia pia kupunguza hatari ya kupata magonjwa mengine yanayotokana na uchafu yakiwemo magonjwa ya kuhara, au hata kipindupindu.
Prof. Abel Makubi amesema kuwa kufanya mazoezi ya mwili na kula lishe bora yanasaidia pia kujenga afya ya mwili uimara na pia kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama shinikizo la damu, kisukari na moyo.
Ni vema wanachi wakaendelea na utamaduni huu huku wakiendelea kupata lishe bora aili kujenga kinga zao dhidi ya mgonjwa mengine” Amesisitiza Prof. Makubi
Kuhusu mbinu ya tibaasili, Prof. Makubi amewapongeza wananchi kwa kuipokea na kuikubali mbinu hiyo katika kusaidia kutibu ugonjwa wa corona na kutumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuelekeza bajeti ya tiba asili/mbadala na tafiti za dawa asilia iweze kuongezwa ili kuwawezesha wataalam wanaotengeneza dawa hizo zinazosaidia kutibu magonjwa mbalimbali na kupambana na maambukizi ya virusi vya corona nchini.

Aidha Prof Makubi amewaagiza wataalam wa afya hasa Wakurugenzi, Waganga wa Mikoa, Wilaya, Maafisa wa afya ngazi za jamii, viongozi wa mashule, vyuo, michezo, na mamlaka za mitaa kuendelea kutoa elimu ya kupambana ugonjwa wa corona na kuendelea kuhamasisha mbinu za kuthibiti CORONA ambazo  zikiendelezwa zitapunguza uwezekano wa kuibuka magonjwa mengine hivyo kuokoa afya za wanachi na fedha nyingi ambazo zingetumika  kutibu wagonjwa.

Mwisho.

DKT. MOLLEL ATETA NA MADEREVA WA MALORI, NAMANGA

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akiongea na madereva malori mpaka wa Tanzania na Kenya Namanga Jijini Arusha, lengo kuwasikiliza changamoto zao.





Baadhi ya madereva wa malori waliokwama katika mpaka wa Tanzania na Kenya Namanga Jijini Arusha wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel.




DKT. MOLLEL ATETA NA MADEREVA WA MALORI, NAMANGA 

Na WAMJW- Arusha. 

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amefanya ziara katika mpaka wa Tanzania na Kenya Namanga Jijini Arusha na kuzungumza na madereva wa malori yanayokwenda Kenya ili kusikiliza changamoto zinazowakumba. 

Dkt. Mollel amefanya ziara hiyo leo, ikiwa ni sehemu ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakumba madereva hao, katika kipindi hiki ambacho Dunia imekumbwa na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona. 


Dkt. Mollel amesema kuwa, Serikali imeliona tatizo hilo na kuweka wazi kuwa itaongeza kasi katika kuhakikisha inapata suluhu ya changamoto wanazokumbana nazo madereva hao katika eneo la mpaka wa Namanga. 

"Nimekuja kuwaambia poleni, lakini Serikali yetu itaenda kwa kasi ya ajabu kuhakikisha kwamba hili tatizo lenu katika mpaka huu linatatuliwa " alisema. 

Aidha, Dkt. Mollel amewataka madereva hao kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho, Serikali inatafuta utatuzi wa changamoto yao, huku akiwapa salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli na kusema anawapenda sana.

Mbali na hayo Dkt. Mollel alisema kuwa changamoto hii iliyojitokeza katika mpaka wa Namanga ni suala mtambuka ambalo linahusisha Wizara zaidi ya moja, huku akiweka wazi kuwa suala hili lina uhusiano wa kibiashara na uchumi baina ya nchi hizo.

Nae, dereva wa malori yanayokwenda nchini Kenya Bw. Abdullah Hassan amesema kuwa, kama madereva hawakubaliani na majibu ya vipimo wanavyopewa kutoka Kenya kutokana na vipimo hivyo kuonesha idadi kubwa ya madereva kuwa na ugonjwa wa Corona jambo ambalo sio kweli.

"Tunaishi maisha magumu sana kutokana na hali iliyojitokeza, na kunachosikitisha zaidi, sisi hatukubaliani na vipimo ambavyo tunapimwa upande wa pili. 

Kwa upande wake, Japhet Jeremiah alisema kuwa, wamekuwa wakiombwa kiasi cha shilingi 2000 za Kenya ili kuandikiwa kuwa hawana Corona, hali aliyeweka wazi kuwa ni uonevu kwa madereva kutoka Tanzania. 

"Sisi kero yetu, tumekuwa tukipima Kenya tumeambiwa tuna Corona, na mimi wiki mbili nilipima nikapewa cheti nina Corona lakini ukweli ni kwamba sina Corona na sijawai tumia dawa yoyote mpaka sasahivi" alisema 

Mwisho.

Alhamisi, 11 Juni 2020

WAZIRI UMMY AZINDUA BARAZA JIPYA LA MADAKTARI TANGANYIKA

- Hakuna maoni








Na WAJMW-DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu jana amezindua Baraza jipya la Madaktari Tanganyika katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dodoma.

Katika uzinduzi huo Waziri Ummy amelipongeza Baraza jipya linaloongozwa na Mwenyekiti  Prof. David Ngassapa na wajumbe wake wanane walioteuliwa lakini pia hakusita kulishukuru na kutaja baadhi ya mafanikio ya baraza lililopita ambalo lilikua linaongozwa na Prof. Muhammad Kambi ambaye alikua Mwenyekiti.

“Katika kipindi chao cha uongozi, Baraza limepata mafanikio mengi ikiwemo Sheria za Madaktari, Madaktari wa meno wa wataalamu wa Afya shirikishi ya Mwaka 2017, na kuitengenezea kanuni zake tano ambazo ni ya Watarajali, Usajili wa mitihani, Ada na Tozo, pamoja na Uchunguzi wa mashauri ya mafunzo endelevu”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema mabadiliko hayo yameboresha sana muundo wa Baraza na hivyo usimamizi wa taaaluma ya udaktari na udaktari wa meno umeongeza wigo wa usimamizi wa taaluma kwa kuongeza kada za Afya shirikishi ambazo mwanzo zilikua hazina usimamizi.

Waziri Ummy amesema majukumu ya Baraza hilo ni pamoja na kuwatambua wanataaluma inaowasimamia kwa njia ya kuwasajili na kuwapa leseni zinazowaruhusu kufanya kazi hizo na kuwakagua mara kwa mara ili kujiridhisha kuwa wako hai kitaaluma.

Aidha, Waziri Ummy amesema kwa mujibu wa takwimu zilizopo ofisi ya Msajili wa Baraza la Madaktari inaonyesha kuwa jumla ya madaktari wa kada mbalimbali 13,973 wamesajiliwa nchi nzima, hata hivyo madaktari walipo kwenye ajira ni 5568.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amelitaka Baraza jipya chini Mwenyekiti Prof. David Ngassapa kuhakikisha kuwa: Wananchi wanahudumiwa na wanataaluma kwa namna ambayo ni salama, Kuhakikisha kuwa mahusiano kati ya mgonjwa na Daktari yanakuwa ya kuaminiana, Wanataaluma wanapata mafunzo na elimu ya kujiendeleza (CPD) ili waendane sanjari na maendeleo ya sayansi na teknolojia yanayotokea duniani pamoja na Baraza kuhakikisha lina kumbukumbu na taarifa sahihi za wanataaluma linaowasajili na ambazo zinaweza kupatikana kirahisi ili kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi ya wanataaluma wanaoruhusiwa kutoa huduma.

Mwisho, Waziri Ummy amelitaka Baraza hilo kuwa na wajibu wa kutangaza majina ya wanataaluma wenye usajili halali na unaoendana na wakati.

MWISHO

Jumanne, 9 Juni 2020

UGONJWA WA CORONA UNAELEKEA KUISHA NCHINI-WAZIRI UMMY

- Hakuna maoni








Na WAJMW-DOM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa Corona unaelekea kuisha nchini ambapo mikoa zaidi ya 15 haijaripoti mgonjwa yeyote wa Corona kwa zaidi ya wiki.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati alipotembelea kituo cha afya cha Mkonze kilichotengwa kwa ajili ya kuwahudumia watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Corona jijini Dodoma na kukuta vitanda vikiwa tupu bila kuwa na mgonjwa yeyote kwa zaidi ya wiki.

Waziri Ummy amesema kupitia Waganga wakuu wa Mikoa 15 nchini wamethibitisha kutokua na mgonjwa wa Corona na Mikoa mingine yenye wagonjwa imeripoti kuwa wagonjwa hao wanaendelea vizuri.

Aidha, Waziri Ummy amewashukuru watoa huduma za afya wa kituo cha Mkonze kwa kazi nzuri walioifanya ya kuwahudumia wagonjwa na kuchukua tahadhari zilizosaidia wahudumu hao kutopata maambukizi ya Corona.

Pamoja na hayo Waziri Ummy amesema licha ya ugonjwa wa Corona kuelekea kumalizika nchini, amewataka wananchi kutobweteka na kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalam wa afya ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kuvaa barakoa za vitambaa wanapokua kwenye mikusanyiko.

Ijumaa, 5 Juni 2020

EWURA NA MOUNT MERU ZATOA MSAADA KWA AJILI YA UDHIBITI WA CORONA NCHINI

- Hakuna maoni




Na Emmanuel Malegi-Dodoma

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa leo amepokea msaada wa hundi ya kiasi cha Tsh. Milioni 100 kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA)uliokabidhiwa na Kaimu Mkurugenzi Bw. Godfrey Chibulunje akiwa na Meneja Mawasiliano na uhusiano wa mamlaka hiyo Bw. Titus Kaguo.

Aidha, Waziri Ummy amepokea msaada wa ndoo 480 sawa na Lita 9600 za vitakasa mikono (Hand Sanitizer) zenye thamani ya Tsh. Milioni 11 zilizotolewa na kampuni ya Mafuta ya Mount Meru ambazo zitatumika katika kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini. Vitakasa mikono hivyo vimekabidhiwa na Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Bw. Prabhat Yadau.

Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma, Waziri Ummy kwa niaba ya Waziri Mkuu ameshukuru kupata misaada hiyo ambayo itasaidia katika kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini na pia amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari licha ya maambukizi ya ugonjwa huo kupungua nchini.

Alhamisi, 4 Juni 2020

UVUTAJI WA TUMBAKU UNA ATHARI UCHUMI WA MTU MMOJA MMOJA ANAYETUMIA

- Hakuna maoni






Na Emmanuel Malegi-Dodoma

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Tanzania kama nchi nyingine za Kiafrika wavutaji wa tumbaku wako hatarini kuyumba kiuchumi na kupata magonjwa yasiyoambukizwa kama tahadhari hazitachukuliwa mapema.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa matumizi ya tumbaku kwa watu wazima wa mwaka 2018 nchini uliofanyika mapema leo katika Ukumbi wa Takwimu jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema utafiti huo umeonesha kuwa kwa wastani matumizi ya tumbaku kwa mtu mmoja kwa mwezi inagharimu Shilingi za Kitanzania 28,840/= fedha ambayo ingetosha kupunguza kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi kwa mtu mmoja mmoja kwa mwezi kwa asilimia 58 na umaskini wa kupindukia (mahitaji ya chakula) kwa mtu mmoja mmoja kwa mwezi kwa asilimia 85.

Kwa kutumia taarifa za Matokeo ya Viashiria Muhimu vya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya binafsi kwa Tanzania Bara wa Mwaka 2017-18, fedha za kujikimu kwa ajili ya mahitaji ya msingi kwa mwezi kwa mtu mmoja ni Shilingi za Kitanzania 49,320/= na mahitaji ya chakula kwa mwezi kwa mtu mmoja ni Shilingi za Kitanzania 33,748/=”. Amesema Waziri Ummy.

Kwa mujibu wa utafiti huo, Matokeo yameonesha kuwa mtu mmoja kati ya 10 (8.7%), wenye umri wa miaka 15 au zaidi nchini Tanzania wanatumia tumbaku ya aina yeyote na hivyo kuwa na watu milioni 2.6 kati ya watu zaidi ya  milioni 55. Wanaume ni asilimia 14.6 na wanawake ni asilimia 3.2.

Aidha, Waziri Ummy amesema watu 4 kati ya 10 (40.3%) nchini wamewahi kuona onyo la matumizi ya tumbaku kupitia redio au runinga. Pia matokeo ya utafiti yameonesha kuwa, watu 9 kati ya 10 (92.3%) wenye umri wa miaka 15 au zaidi wanaamini uvutaji wa sigara husababisha magonjwa, wakati watu 8 kati ya 10 (84.4%) wanaamini kuvuta hewa ya mtu anaevuta sigara kunaweza kuwasababishia magonjwa hata kama wao hawavuti sigara.

katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.  Taarifa inaonesha kuwa watu 4 kati ya 10 (32.9%) wameathiriwa na moshi wa tumbaku sehemu za kazi ikiongozwa na sehemu za mabaa na kumbi za starehe kwa asilimia 77 (watu milioni 3), maeneo ya huduma za biashara za vyakula asilimia 31.1(watu milioni 3.5) na majumbani asilimia 13.8 (watu milioni 4.1).

Waziri Ummy amesema utafiti huo una umuhimu wa kipekee katika Wizara, kwani matokeo yake yatasaidia katika kutathmini hatua zilizofikiwa katika kupambana na magonjwa makuu manne yasiyoambukiza ambayo ni Saratani, magonjwa ya moyo, magonjwa ya mfumo wa hewa na kisukari.

katika kuhakikisha elimu dhidi ya athari ya tumbaku inaifikia jamii ipasavyo. Waziri Ummy ametoa maelekezo kwa  Watendaji wa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na wadau wengine, kutengeneza au kupitia upya Sheria ya kudhibiti matumizi ya Tumbaku ili iendane na Mkataba wa Kimataifa wa kudhibiti matumizi ya Tumbaku na kuendelea kutoa Elimu kwa jamii kuhusu madhara yake; Wizara ya Elimu kuendelea kuimarisha juhudi za kuwakinga wanafunzi dhidi ya tumbaku na bidhaa zake; Wizara ya mambo ya ndani kuhakikisha wale wanaokiuka miongozo kama vile kuendelea kuvuta sigara kwenye maeneo ya wazi wanachukuliwa hatua stahiki; Watengenezaji na wauzaji wa sigara, kufuata miongozo iliyowekwa na Serikali ikiwemo kutokuweka mabango au kutangaza na kuhamasisha matumizi ya sigara, kupitia bidhaa kama miamvuli, T-Shirts, kofia, na kutowauzia watoto wenye umri chini ya miaka 18; jamii kuacha kutumia tumbaku na bidhaa zake na Taasisi za Utafiti kufanya Tafiti za kuangalia vifo vitokanavyo na matumizi ya tumbaku ilikuwe na takwimu za nchi na siyo kutegemea za kutoka nje.

*MWISHO*








Jumapili, 31 Mei 2020

TANZANIA IPO TAYARI KUPOKEA WATALII - DKT. KIGWANGALLA

- Hakuna maoni
 Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pindi walipofanya ziara ya kukagua utayari katika uwanja wa KIA.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akieleza jambo katika sehemu ya kukagua mizigo pindi aliooongozana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla katika uwanja wa ndege wa KIA.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pindi walipofanya ziara ya kukagua utayari katika uwanja wa KIA.

Magari manne yakubeba wagonjwa yaliyotolewa na yametolewa na wakala wa huduma za utalii kama sehemu ya tahadhari katika kuhakikisha usalama wa Watalii wataoingia nchini kwaajili ya utalii.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel wakisikiliza jambo kutoka  kwa Mtaalamu kutoka wakala wa huduma  za utalii nchini wakati wa makabidhiano wa magari hayo manne.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel wakikagua maendeleo ya utengenezaji wa gari linalotumia umeme.


TANZANIA IPO TAYARI KUPOKEA WATALII - DKT. KIGWANGALLA

Na WAMJW- Kilimanjaro

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla ameweka wazi kuwa, Tanzania ipo tayari kupokea wageni kutoka sehemu yoyote Dunia kwa ajili ya utalii, kufuatia kuimarisha mifumo ya tahadhari zote za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Dkt. Kigwangalla ameyasema hayo leo katika ziara iliyomjumuisha Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ikiwa na lengo la kukagua utayari wa nchi katika kudhibiti ugonjwa wa Corona katika uwanja wa ndege wa KIA na kupokea magari manne ya kubeba wagonjwa endapo watatokea pindi wawapo nchini kwenye utalii.

Dkt. Kigwangalla amesema kuwa, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kudhibiti maambukizi ya Virusi vya Corona, ikiwemo kuweka miongozo wakati wa kuingia na kutoka uwanja wa ndege, muongozo wa namna ya kusafirisha watalii pamoja na muongozo wa namna ya kuandaa chumba cha wageni

"Katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona Duniani, tumeweka miongozo kwa pale uwanja wa ndege, tumeweka muongozo wakati wa kuingia na kutoka tumeweka muongozo namna ya kusafisha Watalii kutoka uwanja wa ndege mpaka hotelini, tumeweka muongozo namna ya kuandaa chumba cha mgeni, namna ya kuandaa chakula, kila kitu tumeweka muongozo " alisema

Aliendelea kusema kuwa, Serikali imechagua baadhi ya vituo vya Afya mahususi kwa ajili ya watalii Mkoani Arusha, Serengeti na Ngorongoro lengo ni kuthibitisha usalama wa afya ya Watalii waingiapo nchini.

Naye Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa, Serikali imepokea magari manne ya kubeba wagonjwa(ambulance) yaliyokidhi miongozo ambayo yametolewa na wakala wa huduma za utalii nchini ikiwa ni sehemu ya tahadhari katika kuhakikisha usalama wa Watalii wataoingia nchini.

"Tumeona magari ambayo yamezingatia zile taratibu  na miongozo yote ambayo inatakiwa kuhakikisha Watalii wetu wapo salama na endapo kutakuwa na tatizo litaweza fanyiwa utatuzi mara moja " alisema Dkt. Mollel.

Aidha, alisema kuwa, katika kuboresha tahadhari zaidi magari yaliyotolewa yanalenga kuwakinga madereva na Watalii kwa kutenganishwa kwa kioo ili kudhibiti mnyororo wa maambukizi ya virusi vya Corona endapo atatokea.

"Magari yenyewe yatakuwa Dereva anaingia ndani, lakini kunakuwa na kinga inayowatenganisha Watalii na madereva wetu jambo litalosaidia kudhibiti maambukizi endapo yatatokea " alisema.

Mwisho.