Pages
▼
Jumamosi, 26 Januari 2019
5. HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018
5. Magonjwa ya Mlipuko
#Tanzania imeendelea kuwa salama licha ya tishio la kuwepo kwa Ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
#Wizara imechukua tahadhari za kulinda mipaka yake. Hivyo, hakukuwa na mgonjwa yeyote aliyegundulika kuwa na Ebola nchini kwa mwaka 2017 na 2018.
#Aidha, Serikali imeendelea na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kipindupindu ambapo Mwaka 2018 kulikuwa na wagonjwa 4,706 na vifo 84 ikilinganishwa na wagonjwa 4,626 na vifo 93 mwaka 2017.
#Ugonjwa wa Dengue watu 226 waliathirika mwaka 2018 ikilinganishwa na watu 65 mwaka 2017. Hakuna kifo kilichosababishwa na ugonjwa huu.
#Vilevile kulikuwa na wagonjwa 6 wa Chikungunya ambao walipatiwa matibabu mwaka 2018 na hakuna kifo kilichotokea.
Imetolewa na;
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
26/01/2019

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni