Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 28 Septemba 2021

TAHADHARI YATOLEWA KWA WANANCHI DHIDI YA UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA

Dkt. Jamed Kiologwe
Mkurugenzi Msaidizi Magonjwa Yasiyoambukiza - Idara ya Tiba


Na Englibert Kayombo

Katika kuadhimisha Siku ya Kichaa cha Mbwa Duniani kila mwaka ifikapo tarehe 28 ya kila mwezi Septemba, Wizara ya Afya imewatahadharisha wananchi kujikinga na ugonjwa huo hatari ambao unaweza kusababisha vifo.


Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi Magonjwa Yasiyo ambukiza Dkt. James Kiologwe akitoa Tamko la Serikali kwa niaba ya Katibu Mkuu katika kuadhimisha siku ya ugonjwa huo Duniani.

“Kwa mwaka huu kati ya mwezi Januari hadi Agosti, watu 39,787 wametolewa taarifa ya kung’atwa na mbwa au wanyama wa jamii hiyo ikiwa ni ongezeko la zaidi ya watu 5,000 ukilinganisha na kipindi kama hicho cha mwaka uliopita” amesema Dkt. James Kiologwe na kuendelea kusema kuwa takwimu hizo hazijumuishi matukio yaliyotokea katika vituo vya kutolea huduma bila kutolewa taarifa au yaliyotokea nyumbani na waathirika ambao hawakufika katika vituo vya kutolea huduma za afya, hivyo tatizo hilo ni linaweza kuwa kubwa kuliko tunavyofikiri” amefafanua zaidi Dkt. James Kiologwe.

Ameitaja Mikoa inayoongoza kuwa ina idadi kubwa ya wagonjwa kuwa ni Mkoa wa Morogoro ambao una wagonja 4329 ukifuatiwa na Mkoa wa Dodoma wenye wagonjwa 4233.

“Waathirika wakuu wa ugonjwa huu ni watoto chini ya miaka 15 na hii inaweza kuwa ni kwa sababu wao ndio wanaokuwa karibu na mbwa (anayefugwa) muda mwingi, na pia hupenda kucheza au kuchokoza mbwa wasiowafahamu njiani” amesema Dkt. Kiologwe.

Dkt. James amesema kuwa Ugonjwa wa kichaa cha mbwa husababishwa na Kirusi wa Kichaa cha Mbwa (Rabies Virus) kutoka kwa wanyama jamii ya mbwa ambao wameathirika na kirusi hiki (Mbwa, paka, mbweha, fisi na wengineo) na humwingia mwanadamu kupitia mate ya mnyama huyo kuingia katika jeraha na dalili huanza kuonekana baada ya kuathirika kwa mfumo wa kati wa fahamu, ambazo ni pamoja na kuwashwa sehemu ya jeraha, homa, kuumwa kichwa, maumivu ya mwili, kuogopa maji na mwanga, kutokwa mate mengi mfululizo, kuweweseka (kushtuka mara kwa mara na kuogopa), kupooza na hatimae kupoteza maisha. Wakati mwingine watu huhusisha dalili hizi na imani potofu za kishirikina. 

“Endapo mtu ameng’atwa na mbwa, hatua ya kwanza muhimu ni kuosha jeraha kwa dakika 10 au zaidi kwa maji mengi yanayotiririkika na sabuni. Kidonda kisifungwe na kisha apelekwe au afike haraka katika kituo cha kutolea huduma za afya ili kupata chanjo ya kuzuia kichaa cha mbwa” amesema Dkt. James Kiologwe. 

Amesisitiza kuwa ni muhimu aliyeng’atwa na mbwa afanyiwe tathmini ya kina katika kituo cha kutolea huduma ili aweze kupatiwa chanjo kamili na iwapo chanjo itatolewa ni budi kumaliza kozi zote za chanjo. 
Ameendela kusema kuwa wanyama jamii ya mbwa, paka wasiruhusiwe kulamba vidonda, kwani mate yao huweza kuleta maambukizi endapo wameathirika, huku Wamiliki wa mbwa wahakikishe wanachanja mbwa wao dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa mara moja kila mwaka na kupata cheti. 

Amesema kuwa mbwa wafungiwe ndani wakati wa mchana na wasiachwe kuzurura hovyo, kwani wanaweza kupata maambukizi endapo watakutana na mnyama aliyeambukizwa  pamooja na kuhakikisha mazingira yote ni safi, ili kutowapa chakula mbwa wanaozurura mtaani na kuzoea kuja katika mazingira tunayoishi.

Ametoa rai kwa wazizi kutoa elimu kwa watoto na  kuwakataza kuchokoza mbwa wasiowajua (mfano: kuvuta mkia au masikio, kumpanda mgongoni)


Amesema kuwa Wizara ya Afya kwa kushirikia na sekta nyingine ikiwemo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) - Dawati la Afya Moja pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Chakula Duniani (FAO) pamoja na wadau mbalimbali wamefanya juhudi mbalimbali za kudhibiti ugonjwa huo na kuhakikisha inapunguza ukubwa wa tatizo linalohusiana na ugonjwa huo kwa; Kutoa elimu kwa umma; Kuboresha dhana ya Afya Moja nchini; Kurahisisha upatikanaji wa huduma ya chanjo ya Kichaa cha Mbwa kwa wananchi; Kurahisisha upatikanaji wa huduma ya chanjo kwa kwa wanyama hasa mbwa.

“Serikali inatambua gharama kubwa za upatikanaji wa chanjo, hata hivyo kupitia WAMJW, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) na sekta nyingine imeweza kuchangia gharama za upatikanaji wa chanjo ili ziwafikie wananachi kwa gharama wanazoweza kumudu” amesema Dkt. James Kiologwe.

Amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau katika kutekeleza mikakati na juhudi za pamoja za sekta zote zinazohusika kudhibiti ugonjwa huo inaandaa  ‘Mkakati wa Kudhibiti Kichaa cha Mbwa’ wenye lengo la kutokomeza ugonjwa huu ifikapo 2030.

MWISHO.

17 on: "TAHADHARI YATOLEWA KWA WANANCHI DHIDI YA UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA"
  1. They will be able to draw attention to their essay skills and create documents for their chosen field.
    경마사이트
    파칭코
    토토사이트

    JibuFuta
  2. Hi there, I found your site by the use of Google whilst searching for a similar topic, your site got here up, it looks good. 카지노사이트원
    카지노사이트777
    카지노사이트가이드

    JibuFuta
  3. This is really interesting, You’re a very skilled blogger. I’ve joined your feed and look forward to seeking more of your fantastic post. Also, I’ve shared your website in my social networks! Feel free to visit my website; 카지노사이트원
    카지노사이트777
    카지노사이트가이드

    JibuFuta
  4. The article presents an interesting information on the topic, it provides useful content. The author’s argument is clear and supported. This is a great resource for anyone and it is well-written and informative.
    Indian Divorce lawyers NY
    lawyer for bankruptcy near me

    JibuFuta
  5. Nakupongeza kwa kushirikisha habari muhimu kama hizi na jamii. Uwasilishaji wako wa tahadhari hii ni wa kuelimisha sana. Careless Driving New Jersey Asante kwa kutoa mwanga juu ya suala hili muhimu kwa wananchi. Endelea kutoa elimu na taarifa zinazohitajika.Protección Orden Nueva Jersey

    JibuFuta
  6. i am impressed with your great article with excellent ideas,keep posting. lawyer for contract dispute

    JibuFuta
  7. Stay up the good work! You know, many people are looking round for this info.

    JibuFuta
  8. I’m happy that you simply shared this helpful information with us.

    JibuFuta
  9. woooow, amazing blog to read, thanks for sharing, and move on. finally

    JibuFuta
  10. this type of useful article to read, keep it up

    JibuFuta
  11. And that is rare to come by nowadays!

    JibuFuta
  12. We are grateful that you have such high-quality information on your blog.
    alexandria traffic lawyer||bankruptcy chapter 7 attorneys near me||abogado trafico petersburg va

    JibuFuta
  13. Looking for the best urologist in Chennai? Dr. Karthikeyan is a well-known specialist who has treated patients with urological problems for more than ten years. He is an expert in the diagnosis and treatment of a wide range of disorders pertaining to the male reproductive system and urinary tract, including varicocele surgery, hydrocele, male sexual dysfunction, and blood in the urine (hematuria). Dr. Karthikeyan is skilled in difficult diagnosis such testicular surgery and nephrectomy (removal of the kidney).

    JibuFuta
  14. Architectural Drafting Services: Transforming Visions into Precision

    In the dynamic world of architecture drafting services play a pivotal role in translating creative concepts into tangible reality. Whether you’re an architect, designer, or part of a construction team, understanding architectural drafting is essential. Let’s delve into the intricacies of this crucial discipline.

    JibuFuta