Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 25 Juni 2022

BILIONI 4.4 ZATOLEWA NA SERIKALI KUBORESHA HUDUMA ZA RADIOLOJIA NA UZALISHAJI WA HEWA YA OKSIJENI HOSPITALI RUFAA YA JESHI LUGALO

- Hakuna maoni

 



Serikali kupitia Wizara ya Afya imetoa kiasi cha Bilioni 4.4 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya kutolea Huduma za Radiolojia, jengo la kufua hewa ya oksijeni pamoja na uboreshaji wa huduma za dharura na wagonjwa mahututi katika Hospitali Rufaa ya Jeshi Lugalo.


 

Prof. Abel Makubi Katibu Mkuu Wizara ya Afya.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi mara baada ya kutembelea miradi hiyo ya ujenzi inayoendelea kutekelezwa ndani ya Hospitali hiyo iliyopo Jijini Dar Es Salaam.
“Shilingi Bilioni 4.4 zimetolewa na Serikali chini ya Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya miradi ya ujenzi hapa Lugalo, lakini pia tumetoa zaidi ya Bilioni 4.8 kwa utekelezaji wa miradi ya afya kwenye Idara nyingine za Ulinzi na Usalama ikiwemo Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza.” amesema Prof. Makubi na kuongezea kuwa Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na Wizara na Taasisi nyinginezo kuboresha huduma za Afya.

Prof. Makubi ameipongeza Hospitali hiyo kwa usisamizi hodari wa miradi hiyo huku akiwataka viongozi kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ndani ya wakati ili wananchi waanze kupata huduma.

“Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutoa huduma za afya kwa wananchi lakini pia kwa kutoa fedha za UVIKO-19 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini” amesema Prof. Makubi ambaye pia alifikisha salaam za Waziri wa afya , Mhe Ummy Mwalimu kwa Uongozi wa Hospitali ya Lugalo.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Faraji Mnyepe amesema kuwa Wizara yake itaendela kushirikiana na Wizara ya Afya kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma bora za matibabu kwa wananchi.

Ujenzi wa jengo la Huduma za Radiolojia.

"Tunajenga hivi kwa ajili ya nchi wala sio kwa ajili ya jeshi pekee, huduma hizi tunazifanya kwa manufaa ya nchi” amesema Dkt. MnyepeKwa upande wake Mkuu wa Hospitali ya Jeshi Lugalo Brig. Jenerali Agatha Katua amesema kuwa Hospitali ya Jeshi Lugalo ilipokea fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 4.4 ambapo mpaka sasa tayari wameshanunua mashine ya kufua hewa ya oksijeni kutoka Borahi Kuu ya Dawa, huku ujenzi wa jengo la kuwekea mashine hizo na kutoa huduma ukiwa unaendelea.

Ujenzi wa jengo la kufua hewa ya oksijeni.

Brigedia Jenerali Agatha Katua amesema kuwa wanaendelea na ujenzi wa jengo la Radiolojia ambapo wataweka huduma zote za radiolojia sehemu hiyo kwa kuweka mashine za CT, Scan, MRI, X-Ray, Ultra Sound.
Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa jengo la radiolojia na jengo la kufua hewa ya oksijeni, Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT Kanali Petro Ngata amesema ujenzi wa jengo la radiolojia umefikia asilima 62 huku wakitarajia kukamilisha ujenzi ifikapo Mwezi Septemba 2022 huku Jengo la kufua hewa ya oksijeni ujenzi umefikia asilimia 45 na wanatarajia kukamilisha ifikapo Mwezi Agosti 2022.

Mwisho

Jumatatu, 20 Juni 2022

WADAU WA MAENDELEO KUCHAGIA BILIONI 98.1 KUPITIA MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

Waziri wa Afya, Mheshimiwa Ummy Mwalimu akisema jambo kwenye Mkutano na Wadau wa Maendeleo wanaochangia kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja (hawapo pichani) uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange akisema jambo kwenye Mkutano na Wadau wa Maendeleo wanaochangia kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja (hawapo pichani) uliofanyika Jijini Dar Es Salaam.





Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu (wa kushoto) akisema jambo na wadau wa maendeleo wanaochangia fedha kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja (Health Basket Fund)


Na Englibert Kayombo - Dar es Salaama

Wadau wa Mfuko wa Afya wa pamoja nchini (Health Basket Fund) wamepanga kuchangia kiasi cha shilingi Bilioni 98.1 kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini kwa mwaka 2022/2023.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa kikao cha kujadili uboreshaji wa mfuko huo kupitia ushirikiano wa pamoja  kati ya Serikali na wadau Jijini Dar Es Salaam.

“Kwa niaba ya Serikali tunawashukuru wadau wetu wanaochangia kwa pamoja kwenye Mfuko wa Afya na tunatarajia kwa Mwaka wa fedha ujao wa 2022/23 wadau wetu kwa pamoja kuchangia Shilingi Bilioni 98.1 na fedha hizo zitaingizwa moja kwa moja kwenye akaunti za Vituo vya kutolea huduma za Afya nchini” amesema Waziri Ummy Mwalimu

Waziri Ummy amesema katika mwaka wa fedha uliopita wadau kupitia Mfuko walichangia kiasi cha shilingi bilioni 74.3 ambapo asilimia 90 ya fedha zimekwenda kwenye Halmashauri na zimeingizwa moja kwa moja kwenye Zahanati, Vituo vya Afya pamoja na Hospitali za Wilaya nchini.

Aidha Waziri Ummy Mwalimu amesema upo umuhimu kwa wadau wa maendeleo kuchanga fedha kwa pamoja na kuweka kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuzingatia Mifumo na taratibu za Serikali za kutoa fedha kwa ajili ya Huduma za Afya nchini pamoja na kuwekeza fedha kwenye maeneo ya vipaumbele vya Serikali.

“Fedha zinazoingizwa nchini kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za afya tunapenda ziingizwe kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja ili tuweke kushirikiana kufanya kazi pamoja na kupata matokea ya haraka kwa pamoja.

mapendekezo yetu wadau wengine wachangia kupitia mfuko huo kwani tumeona mafanikio makubwa" amefafanua Waziri Ummy Mwalimu.

Kwa upande wake Naibu Waziri kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Mheshimiwa Dkt. Festo Dugange ameshukuru wadau hao kwa kuendela kutoa ushirikiano na Serikali na kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Mhe. Dugange amepongeza wadau hao kwa kuongeza kiwango cha fedha kutoka Shilingi Bilioni 74.3 mwaka wa fedha 2021/22 hadi Bilioni 98.1 kwa mwaka wa fedha 2022/23 na kusema kuwa kupitia mchango huo pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanyika, Serikali kufanya mapinduzi makubwa kwenye ubora wa huduma za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Mhe. Dkt. Dugange amesema kuwa asilimia 33.3 ya fedha hizo hutumika kwenda kununua dawa, vifaatiba na ‘reagents’ kwa ajili ya vipimo vya maabara ikiwa na pamoja kuboresha huduma za mama na mtoto katika vituo vya kutolea huduma za afya.

“Kwa mwaka huu wa fedha 2022/23 vituo zaidi ya 175 vimepata vifaatiba kwa ajili ya huduma za upasuaji, lakini kwa mwaka ujao wa fedha, tunatarajia vituo zaidi ya 225 vitapata vifaatiba” amefafanua Mhe. Dugange

Akizungumza kwa niaba ya Wadau wanaochangia katika Mfuko wa Afya wa pamoja, akizungumza na vyombo vya Habari Dkt. Peter Nyela Meneja wa Program ya Afya kutoka Ubalozi wa ‘Ireland’ wanafanya hivyo kusaidia Serikali ili kuhakikisha Vituo vya kutolea huduma za afya nchini vinakuwa na dawa, kurahisisha huduma nyinginezo ikiwemo huduma za rufaa, pamoja na motisha kwa watoa huduma za afya nchini.

Huu ni ushirikiano mzuri sana baina ya Serikali na Wadau wa Maendeleo kuweza kufanya kazi kwa pamoja kuweza kusaidia kuboresha huduma za Afya nchini, Sisi kama Wadau kwa pamoja tutaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kuboresha Sekta ya Afya nchini” amefafanua Dkt. Nyela.

Mfuko wa Afya wa Pamoja umedumu kwa miaka 23 hadi kufikia leo ambapo ni muunganiko wa pamoja baina ya Serikali na Wadau wa Maendeleo kutoka Denmark, Korea, Ireland, Switzerland, Canada, UNFPA, UNCEF na Benki ya Dunia ambao huchangia katika huduma za afya nchini kwa kutoa fedha na kuziweka kwenye akaunti moja na fedha hizo kutolewa moja kwa moja kwenye vituo vya  kutolea huduma za afya nchini.

Ijumaa, 17 Juni 2022

WAZIRI UMMY AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI KUTOKA UN-WOMEN

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Mwakilishi Mkazi kutoka UN-WOMEN Bi. Hodan Addou baada ya kumalizika kwa kikao chao kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi kutoka UN-WOMEN Bi. Hodan Addou aliyeambatana na wenzake.

Picha ikionesha kikao kati ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu na Mwakilishi Mkazi kutoka UN-WOMEN Bi. Hodan Addou aliyeambatana na wenzake kutoka UN-WOMEN


 Kutoka Dodoma, Juni 17, 2022.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo Juni 17,2022 amekutana na kufanya mazungumzo na mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa upande wa wanawake (UN - WOMEN) katika ofisi za Wizara Jijini Dodoma. 

Katika mazungumzo yao kwa pamoja wamekubaliana kushirikiana katika masuala ya afya, hususan katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto na usawa wa kijinsia katika Sekta ya Afya. 

Waziri ummy amempongeza Mwakilishi huyo kwa kazi nzuri anazoendelea kufanya na ameahidi kuendelea kushirikiana nae ili kufikia malengo ya kuboresha huduma za afya hasa zinazowahusu wanawake katika Sekta ya Afya. 


#AfyaKwanza 

#JaliAfyaYako