Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 26 Julai 2018

TANZANIA YAPONGEZWA NA CDC UFUATILIAJI, UTOAJI TAARIFA ZA MAGONJWA KIMAT...

- Hakuna maoni

TANZANIA YAPONGEZWA NA CDC UFUATILIAJI, UTOAJI TAARIFA ZA MAGONJWA KIMATAIFA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akiongea na wadau wa Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto   akimsikiliza kwa makini na Mkurugenzi Mkuu wa  Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) Dkt. Robert Redfild kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini , katikati ni Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Balozi Inmi Petterson.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati chini akifuatilia takwimu zinazotolewa na mfumo wa ufatiliaji wa magonjwa nchini pamoja  na wadau wa Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) wakati wa kikao  kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini.

Mtaalamu wa kitengo cha mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa nchini Dkt. Ally Nyangi akitoa maelezo kwa Wadau wa Kituo cha kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) hawapo pichani kuhusu jinsi mfumo huo unayofanya kazi nchini.

NA WAMJW- DAR ES SALAAM


TANZANIA imepata pongezi kutoka kwa Kituo cha Kimataifa cha kufuatilia , kutathimini , kutoa taarifa na kuchukua hatua (CDC) kwa kufanya vizuri katika utekelezaji huo hasa katika magonjwa ya mlipuko.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa kikao cha kuangalia hali ya utendaji katika sekta ya Afya nchini.

"Wenzetu wa CDC kutoka  Marekani wanatusaidia kujenga uwezo wa kufuatilia , kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa ya mlipuko kama vile Ebora na Kipindupindu na wameridhika kwa utendaji wetu hapa nchini" alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Tanzania imeimarika katika kufanya uchunguzi , kutathimini ,  kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa mbalimbali.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema  kuwa magonjwa hayana mipaka hivyo ni lazima kuwa waangalifu na  kuchukua hatua mda wote kwa kujenga mifumo imara ya ufuatiliaji.

Kwa upande wake  Kaimu Balozi wa Marekani Nchini Bi. Inmi Petterson amesema kuwa wamefurahishwa na kazi ya wataalamu wa afya waliowekwa hapa nchini katika kupambana na magonjwa na kuahidi kuongeza nguvu kubwa ikiwemo vitendea kazi.

Aidha Balozi Inmi amesesema kuwa Serikali ya Tanzania inatakiwa kushirikiana na wananchi wa Tanzania katika kupata taarifa sahihi za magonjwa na kujenga nchi yenye wananchi wenye afya bora.


Ijumaa, 20 Julai 2018

DKT. NDUGULILE AHAIDI KUZIWAJIBISHA MAMLAKA HUSIKA ENDAPO KITUO CHA AFYA KITAFUNGIWA.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua cheti chá mmoja kati ya wagonjwa waliofika kupata huduma za Afya katika hospitali ya Mkoa wa Mwanza ya Sokotoure wakati akiendelea na Ziara yake Mkoani hapo.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (katikati) akikagua chumba chá Dawa katika hospitali ya kanda ya Bugando pindi alipofanya ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua incubator katika Zahanati ya Nyamizeze wakati alipofanya ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

Mwakilishi kutoka Zahanati ya Ihayabuyaga iliyo katika Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza akipokea zawadi ya cheti kutoka kwa Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) baada ya kushinda nafasi ya tatu katika kutoa huduma bora za Afya.

DKT. NDUGULILE AHAIDI KUZIWAJIBISHA MAMLAKA HUSIKA ENDAPO KITUO CHA AFYA KITAFUNGIWA. 

Na WAMJW-Mwanza

NAIBU Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii ,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile amesema kuwa hatosita kuziwajibisha mamlaka husika endapo kituo chá kutolea Huduma za Afya kitafungwa kutokana na uzembe wa aina yoyote. 

Amesema hayo wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya na kutoa vyeti na ngao kwa Halmashauri zilizofanya vizuri katika utoaji wa huduma za afya leo jijini Mwanza.

"Na Bahati nzuri tunapopita tunawapa na maelekezo wa nini chakufanya, tukishakamilisha hili zoezi letu lá kuweka mifumo ya usajili , ithibati, na utoaji wa leseni tutaanza kufungua visivyokidhi vigezo, Sasa tutapofungia kituo chá Afya Mamlaka husika,  iwe ni Rass, Mganga mkuu wa mkoa au wa Wilaya, Mkurugenzi utawajibika, Vingine ni uzembe wa baadhi ya mamlaka kutosimamia vizuri majukumu yake"Alisema Dkt Ndugulile. 

Aliendelea kusema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea kuweka mikakati thabiti katika kuboresha hali ya utoaji huduma za Afya nchini ili wananchi wanufaike zaidi na hali hiyo. 

"Tunaongeza rasilimali watu, tumetangaza ajira mpya 8000 katika sekta ya Áfya,  ambapo na ninyi mtapata,  pia Vituo vyote tutavisajili, kiwe cha umma Au chá binafsi, kitu chá pili tutaweka ithibati kama usipofikisha kigezo katika ngazi husika tutakushusha kigezo unaenda kuanza hatua upya" Alisema Dkt Ndugulile

Aidha Dkt.  Ndugulile alimtaka Mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa kuyasimamia vizuri ili kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa Ubora unaostahili kwa wananchi .

Nae Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa alisema kuwa Mkoa unatarajia kuanza uboreshaji wa miundombinu ya huduma za afya hususani eneo lá uzazi na Mtoto kupitia mradi wa "Improving access to maternal and Newborn health (IMPACT)  umaotekelezwa na Aga Khan Development Network  (AKDN)  chini ya Ufadhili wa Serikali ya Canadá pamoja na Agriteam kupitia mradi wa Mama na Mtoto ambapo zaidi ya Bilioni 2.8 zinatarajiwa kutolewa na kutumika katika vituo 30

Dkt. Thomas Rutachunzibwa aliendelea kusema kuwa mkoa wa Mwanza Unaendelea kuimarishwa ambapo madirisha maalum 35 yameanzishwa katika hospitali zote 7 za Serikali, vituo vya Áfya 11 na Zahanati 17 ili kuhakikisha wazee wanapata huduma kwa haraka na Ubora unaotakiwa, jumla ya wazee 43,046 wamepatiwa vitambulisho na mabaraza ya wazee 172 yameundwa 

SERIKALI YAIPATIA MKOA WA MARA BILION 5.9 KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akitoa maelekezo kwa mhandisi wa Majengo wakati alipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa hospitali ya Mkoa wa Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisikiliza kero kutoka kwa mgonjwa aliyefika kupata huduma za afya katika kituo chá Afya Nyasho Mkoani Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisikiliza maoni ya mama alipofanya ziara katika wodi ya kujifungulia katika kituo chá Afya chá Nyasho Mkoani Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akimjulia hali Mtoto aliyefika na mama yake katika kituo chá Áfya chá Nyasho

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akimsalimia moja kati ya wazee aliyefika kupata huduma za afya katika kituo chá Áfya chá Nyasho Mkoani Mara huku akimsisitiza kuwa matibabu ni bure kwa wazee wote wasio na uwezo wakuchangia.

Dkt. Faustine Ndugulile (wakatikati) akiendelea na ziara yake ya kutembelea ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti.


SERIKALI YAIPATIA MKOA WA MARA BILION 5.9 KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

Na WAMJW-MARA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto imeupatia Mkoa wa Mara kiasi cha shilingi Bilion 5.9 ikiwaq ni moja ya jitihada za kuboresha hali ya utoaji huduma za Afya kwa wananchi katika mkoa huo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile mapema leo wakati akiwa katika ziara yake ya Kukagua hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara.

“Mkoa wa Mara umepokea Bilion 5.9 kwaajili ya kuboresha vituo vya kutolea huduma za Afya 13, ikiwa ni jitihada za Serikali katika kuboresha hali nya utoaji huduma kwa wananchi wake “ alisema Dkt Ndugulile.

Pia Dkt. Ndugulile aliagiza kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Tarime ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Vicent Naano kusimamia vizuri manunuzi ya Dawa, huku akiagizi Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mwanisi kuhakikisha  dawa zote zinunuliwe kutoka Bohari ya Dawa (MSD).

“Hutaratibu wa kuagiza Dawa kwa  mawakala sitaki kuusikia, MSD tuna dawa karibia zote za msingi,  utaratibu wa mawakala tuliuweka kama mbadala endapo MSD watakosa aina Fulani ya dawa” Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa  mimba na ndoa za utotoni bado ni tatizo kubwa ambapo mkoa wa Mara ni wa tano kitaifa kwa kuwa na asilimia 37.

“Serikali imeandaa Mpango wa kazi wa Kitaifa wa Kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa mwaka 2017/18-2021/22 na moja kati ya msisitizo katika mpango huu ni kutokomeza ukatili wa kijinsia shuleni” alisisitiza Dkt. Ndugulile

Aidha Dkt. Ndugulile amekemea mahusiano ya kingono yaliyopo baina ya walimu na wanafunzi na kuwataka wanafunzi kuacha kufanyiana vitendo vya ukatili na kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Mwanisi alisema kuwa Idara ya Afya ina upungufu mkubwa wa watumishi mkoani hapo ambao ni 3477 sawa na Asilimia 60.9 ikilinganishwa na watumishi 2237 sawa na Asilimia 39.1 waliopo sasa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya hadi kufikia mwezi Juni 2018.

Dkt. Mwanisi aliendelea kusema kuwa hali ya maambukizi ya VVU yamepungua kutoka Asilimia 4.5 mwaka 2011 hadi Asilimia 3.6 mwaka 2016/2017 kulingana na utafiti wa kitaifa uliofanyika mwaka  2011-2012 na 2016-2017 huku akisema kuwa wanaendelea kufanya juhudi mbali mbali za kupambana na UKIMWI ili kuhakikisha maambukiz mapya yanaendelea kupungua.

Kwa upande mwingine Mganga Mkuu wa Mkoa alisema hali ya chanjo hadi kufikia Disemba 2017 kwa watoto chini ya mwaka mmoja waliomaliza chanjo zote kimkoa ilikuwa Asilimia 143 ambayo ipo juu ya lengo la kitaifa ambalo ni Asilimia 90.

DKT. NDUGULILE AUGIZA UONGOZI WA MKOA WA MWANZA KUHAKIKISHA 80% YA VITUO VYA AFYA HAVISHUKI CHINI YA NYOTA 3.

- Hakuna maoni
 Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akikagua list ya vituo vilivyofanya vizuri kupitia utaratibu wa ugawaji wa nyota katika vituo hivyo  wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

 Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile  akikagua Fiji ya kuhifadhia damu salama pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza, kulia kwake ni mtaalamu wa maabara katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe.

Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile  akiongea na wagonjwa waliofika katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.


DKT. NDUGULILE AUGIZA UONGOZI WA MKOA WA MWANZA KUHAKIKISHA 80% YA VITUO VYA AFYA HAVISHUKI CHINI YA NYOTA 3.
Na WAMJW – UKEREWE, MWANZA
Serikali kupitia Wizara ya Afya imeuagiza uongozi wa Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kwamba vituo vyote vya Afya vya Serikali na vya binafsi hazishuki chini ya nyota 3, hii ikiwa moja ya jitihada za kuboresha hali ya utoaji wa huduma Afya nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utaji huduma leo katika Wilaya ya Ukerewe Mkoa wa Mwanza.
“Tuhakikishe kwamba Asilimia 80 ya vituo vyetu vyote vya kutolea huduma za Afya vyote kuwa na nyota 3 hicho kiwe ni kiwango cha chini sana,” Alisema Dkt. Faustine Ndugulile.
Dkt. Ndugulile aliendelea kusisitiza kwa watoa huduma za Afya juu ya nidhamu na matumizi ya lugha nzuri pindi wanapokuwa wanawahudumia wagonjwa ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi  yasiyo na lazima,
Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kwamba Serikali imeweka utaratibu wa kuzitambua dawa zake kwa  kuziwekea rebo ya MSD GOT katika dawa zote inazizitoa na kusisitiza kwamba dawa hizo zinastahili kupatikana katika  vituo vya Afya vya Serikali au kwa mgonjwa tu.
“Sisi kama Serikali tumeanza kuweka utaratibu wa kuziwekea rebo dawa zote za Serikali lebo ya MSD GOT, tumeziweka kwenye boksi na kwenye dawa , anaepaswa kuwa nazo ni hospitali zetu na mgonjwa tu, mtu yoyote wa katikati akiwa na hizo dawa basi huyo ametuibia, msimfumbie macho” Alisema Dkt Ndugulile.
Pia, Dkt Ndugulile ameahidi kuwapelekea huduma za dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe jambo linalopelekea kupoteza maisha kwa wahitaji wa huduma hizo kutokana hali ya ugumu wa usafiri kutoka kisiwani Ukerewe mpaka kufika katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza SoukeToure
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Ukerewe Mhe. Joseph Mkundi  amefarijika juu ya ujio wa Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile jambo lililompa fursa ya kuona mazingira halisi na kuziona changamoto ambazo wananchi kutoka Ukerewe wanakumbana nazo.
Kisha Mhe. Joseph Mkundi alimuomba Dkt. Faustine Ndugulile (MB) kuwasaidia  kuboresha huduma za hospitali hiyo ya Wilaya ya Ukerewe kwa kuwajengea chumba cha upasuaji , chumba cha wagonjwa mahututi na boti kwaajili ya kubebea wagonjwa ili kuwavusha kwenda hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza .

“Mambo ambayo nimekuwa nikiyapigania ni juu ya kuboresha hospitali yetu ya Wilaya ili iweze kutoa huduma kamilifu, kwa maana kwa mazingira yetu tunaichukulia kuwa ndio Hospitali ya Rufaa, ikitokea mgonjwa kakosa usafiri inakuwa ni vigumu sana kuweza kusaidia hali yake,” alisema Mhe. Mkundi.


ZIARA YA WAZIRI UMMY KUJUA HALI YA UTOAJI HUDUMA ZA AFYA URAMBO TABORA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa pili kulia akikata utepe kuashiria kuweka jiwe la msingi kwenye jengo la wodi ya wazazi lilitokana na mpango wa malipo kwa ufanisi katika Zahanati ya Itebulanda wilayani Urambo Mkoani Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo,wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Bi. Magreth Sitta.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikakati akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi kitabu cha mpango wa malipo kwa ufanisi katika Zahanati ya Vumilia Wilayani Urambo Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikakati akionesha kitabu cha mpango wa malipo kwa ufanisi pamoja na watumishi wengine wa sekta ya afya  katika vituo vya fya mara baada ya uzinduzi huo uliofanyika  katika Zahanati ya Vumilia Wilayani Urambo Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo wa tatu kushoto ni mkuu wa Wilaya ya Urambo Bi. Angelina Kwinga,.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Urambo Bi. Angelina Kwinga kushoto kitabu cha muongozo wa mpango wa malipo kwa ufanisi  mara baada ya uzinduzi huo uliofanyika  katika Zahanati ya Vumilia Wilayani Urambo Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akifunua pazia kuashiria  kuashiria kuweka jiwe la msingi kwenye jengo la upasuaji katika Zahanati ya Uyogo wilayani Urambo Mkoani Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo,kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Bi. Magreth Sitta.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitembelea maeneo ya Zahanati ya Uyogo wilayani Urambo Mkoani Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo.

PICHA NA WAMJW-TABORA

Alhamisi, 19 Julai 2018

WAZIRI UMMY ATEMBELEA HOSPITAL YA RUFAA MKOA TABORA KITETE

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu Kulia akipata maelezo juu ya Chumba cha Upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete mkoani Tabora kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora  Dkt. Gunin Komba kushoto wakati wa ziara yake mkoani humo.


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimsalmia mama aliyejifungua mapacha Bi. Debora Erasto (29) mkazi wa Ullyankulu mkoani Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimsalmia mama aliyejifungua mapacha Bi. Debora Erasto (29) mkazi wa Ullyankulu mkoani Tabora wakati wa ziara yake mkoani humo.



Ijumaa, 13 Julai 2018

MARUFUKU KUAJIRI WATOA HUDUMA NGAZI YA JAMII NJE YA ENEO HUSIKA.

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akiongea na Wananchi wa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu wakati wa ufunguzi wa mradi wa Tuwatumie ambao unawaajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii katika vijiji vyote vya halmashauri hiyo chini ya ufadhili wa AMREF

Wadau mbalimbali wa sekta ya afya walifuatilia hotuba ya mgeni rasmi(hayupo pichani) aliyekaa kushoto ni Niall Morris Mkuu wa Arish Aid,Dar.Aisa Muya -Kaimu Mkurugenzi Mkazi Amref Tanzania(katikati) na kulia ni Dkt.Helen Senkoro Mkurugenzi wa Benjamin Mkapa Foundation

Wananchi waliojitokeza kushuhudia ufunguzi wa mradi huo ambapo watoa huduma hao watakua kiungo kati ya wananchi na vituo vya kutolea huduma.

Waziri Ummy Mwalimu akifungua mradi huo


MARUFUKU KUAJIRI WATOA HUDUMA NGAZI YA JAMII NJE YA ENEO HUSIKA. 

NA WAMJW-SIMIYU. 

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imepiga marufuku kuajiri watoa huduma wa afya ngazi za jamii kutoka nje ya Halmashauri husika. 

Katazo hilo limetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa mradi wa TUWATUMIE uliofanyika mkoani Simiyu wilaya ya Itilima. 

"Nataka kuwaambia viongozi wa Mkoa na Wilaya nchi nzima pamoja na taasisi zisizo za kiserikali ni marufuku kuajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii (CHW) kutoka nje ya  makazi yao ili kusiwe na  kutotofautiana kimazingira,kwani wenyeji wanajua tamaduni na mila za wakazi wanapotoka" alisema Waziri Ummy. 

Waziri Ummy amesema kuwa watoa huduma ngazi ya jamii wanatakiwa kuwa kipaumbele katika kukinga kuliko kutoa tiba ili kupunguza idadi ya wagonjwa na kuokoa fedha. 

"Nataka kuwaambia wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanatakiwa kuweka kipaumbele kinga kuliko tiba kwani mimi ni Waziri wa Afya na sio Waziri wa wagonjwa,siwezi kusubiri watu wale ,nitawatumia CHW kuwakinga ama kuwazuia wanaoumwa kupata matibabu" alisema Waziri Ummy. 

Alisema nchi ipo kwenye mikakati ya kufikia malengo endelevu ya millennia ya kumfikia kila mtanzania kwa wakati na popote,hivyo kwa kuanza CHW wanaanza eneo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania Dkt. Aisa Muya amesema kuwa asilimia 50 ya miradi yao wanatumia watoa huduma za afya ngazi ya jamii . 

Aidha, Dkt. Muya amesema kuwa wametoa mafunzo kwa watoa huduma  2,265 na mradi huo utawaajiri watoa huduma 2,015 mbapo Wilaya ya Itilima watakuwa 102 na Misungwi 113 ambao wataenda kwenye vijiji vyote vya wilaya hizo. 

Dkt. Muya amesema kuwa matarajio ya mradi huo ni kuwatumia watoa huduma hao kama kiungo kati ya jamii na vituo vya kutolea huduma za afya. 

TAARIFA KWA UMMA

- Hakuna maoni



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO


KUITWA  KAZINI

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwataarifu wote walioomba nafasi mbalimbali za Ajira za Kada ya Afya tarehe  11 Mei  hadi  26  Mei, 2018  kuwa  walioorodheshwa  katika tangazo hili wamechaguliwa na kupangiwa vituo vya kazi kama jedwali linavyoonyesha kwenye Tovuti ya Wizara ya  Afya  www.moh.go.tz.

Waombaji  waliochaguliwa wanatakiwa kuzingatia kwa ukamilifu maelekekezo yafuatayo:

1).   Kuripoti  Ofisi  za Wizara  ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Dodoma katika  muda  wa  siku  kumi  na  nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili, kwa ajili ya kukamilisha taratibu za Ajira Serikalini.  Ambao hawataripoti ndani ya siku kumi na nne (14) nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa.  Aidha, wakati wa kuripoti kila aliyechaguliwa atapaswa kuwasilisha vyeti halisi (Original Certificates) ambavyo nakala zake zilitumiwa wakati wa kuomba ajira zao, ikiwa pamoja na:-

a)      Vyeti halisi vya Elimu ya Sekondari, Vyeti vya Taaluma, Usajili wa Baraza/Bodi ya Kitaaluma na cheti cha kuzaliwa.

b)     Nakala ya picha mbili ndogo (passport size). Picha ziwe na muonekano kamili wa sura na ziwe zimepigwa si zaidi ya miezi mitatu iliyopita.

2)      Waombaji  wote  ambao  majina  yao  hayakuonekana  katika  tangazo  hili  watambue  
kuwa hawakupata nafasi hiyo, hivyo wanashauriwa  wasisite  kuomba  mara  nafasi  nyingine za  kazi zitakapotangazwa.

3)  Waombaji waliopangiwa  Kada ya Uhudumu wa Afya majina yao yatatangazwa baadae.


Imetolewana:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Afya
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
13 Julai, 2018

Alhamisi, 12 Julai 2018

SERIKALI KUFUTA TOZO YA USAJILI,KUHUWISHA NA KUSHIKILIA USAJILI KWA WAWEKEZAJI WA NDANI.

- Hakuna maoni




Waziri wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikagua shughuli za ujenzi wa jengo la wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo hilo jijini Mwanza.

 Waziri wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kushoto wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la Mamlaka hiyo jijini Mwanza. Kulia ni Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya kutoka Wizara ya afya Dkt. Mohammed Mohammed.

 Waziri wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akipata maelezo juu ya sukari zinazopimwa ubora wake  kutoka kwa Mkuu wa Maabara wa TFDA  Kanda ya Ziwa Bw. Salum Kindoli wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la Mamlaka hiyo jijini Mwanza.

Waziri wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia  akipata baadhi ya maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya kutoka Wizara ya afya Dkt. Mohammed Mohammed kushoto wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la Mamlaka hiyo jijini Mwanza.

Baadhi ya mafundi wakiendelea na shughuli za ujenzi wa wa jengo la wodi    ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure jijini Mwanza.


SERIKALI KUFUTA TOZO YA USAJILI,KUHUWISHA NA KUSHIKILIA USAJILI KWA WAWEKEZAJI WA NDANI.
NA WAMJW-MWANZA
SERIKALI kupitia wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imefuta tozo ya usajili , kuhuwisha pamoja na kushikilia usajili wa bidhaa zao kwa wawekezaji wa ndani kupitia Mamlaka ya chakula na Dawa TFDA .
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea kuangalia ujenzi wa jengo la TFDA ambalo linajengwsa Jijini Mwanza ili kusogeza huduma kwa wananchi wa mkoa huo.
“Ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kukuza nchi kupitia uchumi wa viwanda hivyo TFDA msiwe kikwazo kwa wawekezaji hao hivyo kuanzia leo nafuta tozo za kusajili bidhaa,kuhuwisha bidhaa na tozo ya kushikilia usajili wa bidhaa”, alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa kuendana na juhudi hizo pia Serikali  imefuta tozo ya udhibiti  ya thamani ya 0.25 za dawa,vifaa na vifaa tiba zinazoingizwa kwenye hospitali za Umma kutoka kwa wafadhili.
Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa TFDA ina wajibu wa kusimamia Tanzania isiwe jalala la bidhaa zisizo na ubora kwa watanzania hivyo wanatakiwa kuweka afya ya wananchi mbele kuliko manufaa binafsi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi. Agness Kijo amesema kuwa ujenzi wa jengo hilo ukikamilika utasaidia kuhudumia huduma za kimaabara kwa bidhaa zinazoingia nchini kwani itakuwa sio lazima tena kwenda kupima bidhaa hizo jijini Dar es salaam.
“Maabara hizi zikikamilika zitasaidia kufanya vipimo na udhibiti wa bidhaa katika mipaka mingi ya kanda ya ziwa ikiwemo Silali,Lusumo na Mtukula ili kuweka usalama wa bidhaa zinazoingia na kutoka nje ya nchi kwa usalama wa wananchi.
Sambamba na hilo Waziri Ummy alipata nafasi ya kutembelea kukagua ujenzi wa jengo la wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure na kuhakikisha ujenzi unakamilisha ili kuokoa vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.
“Kama watu wa mwanza wanaridhishwa na huduma zinazotolewa katika hospitali hii basi ni lazima huduma za afya ziboreshwe ikiwemo afya ya mama na mtoto hivyo ninaleta mashine ya CT Scan kwa ajili ya kuboresha matibabu hapa” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy aliwataka watendaji wa Hospitali  kutoa taarifa za utendaji kwa Waziri wa Afya na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo pamoja na kusimamiwa na Wakuu wa Mikoa yao ili kuimarisha huduma za afya nchini.

Jumatatu, 9 Julai 2018

WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA

- Hakuna maoni
Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akifungua Mkutano wa mafunzo wa nchi 21 ambazo zina maambukizi ya Ugonjwa wa Trakoma (Vikope) uliofanyika katika jiji la Arusha.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Timothy Wonanji  akiongea na Wadau  kutoka nchi mbali mbali wa magonjwa ya Trakoma(Vikope) katika kikao kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi katika nchi hizo 21.

Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele chini ya Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazeee na watoto  Dkt . Upendo Mwingila akionga kwa kifupi juu ya hali ya ugonjwa wa Trakoma nchini mbele ya Wadau wa ugonjwa wa Trakoma kutoka nchi 21.

Picha ya Wadau zaidi ya 100 kutoka nchi 21 ambao walihudhuria kikao chenye lengo la kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi kilichofanyika jijini Arusha

 Kundi namba 1 la Wataalamu likiongozwa na madaktari (Graders) wakijadili kuhusu ugonjwa wa Trakoma katika nchi zao.

Kundi namba 2 ni Wataalamu wa masuala ya Takwimu wakijadil namna ya uingizaji wa takwimu kwa usahihi.
Picha ya Pamoja ya Wadau  kutoka nchi 21 wa ugonjwa ya Trakoma(Vikope) walioshiriki katika kikao kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi katika nchi hizo 21.

WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA

Na WAMJW - ARUSHA

Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amethibitisha kuwa halmashauri 58 nchini zimefanikiwa kutibu ugonjwa wa trakoma kutokana na jitihada mbali mbali zilizofanywa na Serikali kwa ushirikiano na Wadau.

Alisema hayo wakati akifungua Mkutano wa Uzinduzi wa Mafunzo kwa wawakilishi wa nchi 21 ambazo zinamaambukizi ya ugonjwa wa Trakoma/ vikope huku lengo likiwa ni kuwajengea wataalamu hao uwezo ili waweze kupambana dhidi ya ugonjwa huu. 
"Mwanzoni tulikuwa na Wilaya takribani 75 ambazo zilikuwa na ugonjwa huu,  jitihada zimeweza kufanyika  tangu 2014 hadi leo Hii  Karibu Wilaya 58 zimeweza kushinda dhidi ya ugonjwa huu, tumebakiza Wilaya 13 na kama Serikali tutaendelea kutoa dawa na Elimu kwa umma ili waweze kujikinga  dhidi ugonjwa huu ", Alisema Dkt. Subi

Dkt Subi aliendelea kusema kuwa sifa mojawapo ya kudhibiti ugonjwa huu ni kupitia mafunzo yanayomjengea uwezo mtaalamu kuweza kujua namna ya kujua ugonjwa, na kuweza kudhibiti dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu  

Kwa upande mwingine Dkt. Subi ametoa wito kwa wananchi wote hususani waliokatika hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu wa trakoma kuwa Safi wakati wote kwa kunawa uso, kujenga vyoo na kusafisha mazingira yanayotuzunguka mara kwa mara. 
"ugonjwa huu unatokana na uchafu, kama huogi, kama hunawi uso, unaweza sababisha macho yako yakahathirika, ni vizuri kutumia Fursa ya maji vizuri kwa kufanya usafi vizuri mda wote" alisema Dkt. Subi 

Pia Dkt Subi aliwahasa wananchi kutumia dawa Kwani ni  salama na nzuri ndiomaana zimeponya watu katika halmashauri 58 kufanikiwa kupambana dhidi ya ugonjwa huu wa trakoma. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt Thimothy Wonanji alisema kuwa bado Wilaya tatu jijini Arusha zinaendelea kusumbuliwa na tatizo hili lá trakoma, Wilaya hizo ni Longido,  ngorongoro pamoja na Monduli na kusema kuwa tatizo kubwa limeonekana kuwa ni changamoto ya upatikaaji wa maji katika maeneo hayo.

Aliendelea kusema kuwa Serikali katika ngazi ya Mkoa kuna uratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambao kwa kushirikiana na wadau wamekuwa na mradi wa kwenda kijijini na kupita nyumba kwa nyumba kuwapima wakazi wa maeneo hayo na kuwaanzishia dawa (zitromas) kwa wanaogundulika kuwa na ugonjwa huu. 

Nae Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt Upendo Mwingila alisema kuwa idadi ya wagonjwa wamepungua kutoka 160 Mpaka mwaka huu wagonjwa elfu 25,000 hii inatoka na juhudi za Wizara ya Áfya kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na Wadau mbali mbali katika kupambana dhidi ya ugonjwa huu wa trakoma jambo lililosaidia kufanikisha kufanya upasuaji wa vikope takribani 12,000 kwa mwaka.

Jumamosi, 7 Julai 2018

DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.

- Hakuna maoni
Mtabibu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Bw.  Wilfred Mandala akiwaelekeza Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund namna ya  kusafisha mguu wa Bw. Juma ambae ni mwasilika  wa ugonjwa wa Matende

Afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Hope Rusibamayila akishirikiana na wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro kutoa maelekezo kwa wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund namna ya Kibuyu Chirizi kikifanya kazi ya kuosha mikono kwa sabuni baada yakutoka Chooni.

Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakiendelea na ziara yao yakukagua baadhi ya miundombinu waliyoisaidia katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro.
Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakigawa kalamu za kuandikia kwa wanafunzi wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro 

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method akiongea na Wanafunzi pamoja na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakati walipotembelea katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyopo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro

 Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi akifanya utambulisho kwa Wanafunzi pamoja na Wageni waliofika katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni kutembelea na kujionea maendeleo ya mchango waliotoa katika shule hiyo.

 Afisa Mipango wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya  Bw. Oscar Kaitaba akitoa salam kutoka Wizara ya Afya mbele ya Wanafunzi pamoja na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund

Mwanafunzi Kutoka Shule ya Msingi ya Kilari Vaileth Wilfred akimkabidhi ujumbe Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi baada ya kumaliza Shairi lao, kulia kwake ni  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method na wa mwisho ni Afisa Mipango wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya Bw. Oscar Kaitaba.

Picha yapamoja ya Watumishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund baada ya kumaliza shughuli ya kutembelea na kukagua miundombinu katika Shule ya Msingi Kilari wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro.

Picha ya Pamoja ya Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Kilari wakionesha kalamu zao juu kuonesha furaha zao baada ya kupokea kutoka katika Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund


DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.

Na WAMJW - SIHA KILMANJARO

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Endrew Method amesema kuwa Wilaya ya Siha imepiga hatua kubwa katika kukabiliana na changamoto ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, huku akidai kuwa  97% ya watoto tayari wameshapata dawa hizo za minyoo.
Ameyasema hayo alipowapokea wageni kutoka Bill and Melinda Gate na THE END FUND waliokuja kuangalia utekelezaji wa miradi waliyoifadhili na kufuatilia namna ya wanufaika wanavyofaidika na miradi hiyo katika Wilaya ya Siha.
“Ukiangalia utoaji wa Dawa za minyoo mashuleni kwa Wilaya tulifikia 97% jambo ambalo linasaidia watoto kutopata changamoto za ugonjwa wa minyoo, hata hivyo kwa wagonjwa wa  n je tu matatizo ya minyoo yanafikia hadi nafasi ya tatu hivyo kuna umuhimu mkubwa wa wa kuufanya uwe mkakati endelevu” Alisema Dkt. Method
Dkt. Method aliendelea kusema kuwa Taasisi ya Bill and Melinda Gate na THE END FUND wamekuja kuangalia ni jinsi gani miradi hiyo imekuwa ikitekelezwa na namna ambavyo matumizi ya fedha wanazotoa yamekuwa yakiwanufaisha wahusika.
 “Wamekuja kuangalia, ni jinsi gani yale mambo waliyokuwa wakititusaidia tunatekeleza, na miongoni mwa mambo hayo ni  unyweshaji wa watoto dawa za minyoo kwaajili ya kukabiliana na minyoo mashuleni, usafi wa vyoo na ujenzi wa vyoo bora katika mashule yetu ambayo tumefanya kwa zaidi ya miaka Sita, pia wamekuja kuangalia namna ya kukabiliana na ugonjwa wa trakoma”. Alisema Dkt. Method 
Aidha, Dkt. Method amewashukuru wafadhili hao kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na THE END FUND kwa msaada mkubwa ambao wamekuwa wakitoa katika kuisaidia Serikali ya Tanzania na jamii kwa ujumla kwaajili ya kupambana na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.
Kwa upande wake Afisa Mipango kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Oscar Kaitaba akieleza namna Taasisi ya THE  FUND na Bill and Melinda Gate ilivyosaidia Wizara amesema kuwa ;-
“THE END FUND imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Afya katika kudhibiti ugonjwa wa Vikope (Trakoma) na ugonjwa wa Matende na Mabusha kwa kuwafanyia upasuaji katika Mikoa ya Tanga, Pwani na sehem chache Mkoa wa Dar es salaam”,Alisema Oscar Kaitaba
Oscar Kaitaba aliendelea kuwa Kwa ugonjwa wa Trakoma wamesaidia kufanya upasuaji wa Kope katika Mikoa ya Kilimanjaro katika Wilaya ya SIHA na Arusha katika maeneo ya watu waliohathirika zaidi na ugonjwa huu.