Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 30 Novemba 2018

DKT. MPOKI -"MADAKTARI TIMIZENI WAJIBU WENU"

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Utawala wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Beatrice Erasto wakati alipotembelea Taasisi hiyo kujionea hali ya utoaji wa huduma leo jijini Dar Es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Ubora wa Huduma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mohamed Mohamed.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya (katikati) akiongea na Mgonjwa wa Saratani (Jina halijafahamika) aliyelazwa katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road iliyoko Jijini Dar Es Salaam wakati alipofanya ziara kujionea hali ya utoaji wa huduma katika Taasisi hiyo. Kushoto ni Kaimu Meneja wa huduma za tiba Dkt. Sadik Siu na kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Ubora wa Huduma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mohamed Mohamed.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na wananchi waliofika kupata huduma za uchunguzi na matibabu katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kujionea hali ya utoaji huduma.


Na.WAMJW, Dar es Salaam

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya amewataka Madaktari wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road   kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wagonjwa  wanaofika hospitalini hapo kila siku  na kumuagiza Mkurugenzi wa Huduma za  Uhakiki na Ubora kutoka Wizarani kwake kufuatilia.

Dkt.Mpoki ametoa agizo hilo alipotembelea taasisi hiyo ili kujionea hali ya utoaji huduma pamoja na kusikiliza wagonjwa wanaofika kupata huduma kwenye taasisi hiyo kutokana na kulalamikiwa kwa baadhi madaktari na wauguzi “Taasisi hii ni ya faraja lazima mtengeneza mazingira mazuri yakuwahudumia wagonjwa,kwani ndugu wanafuatilia hali za wagonjwa wao hivyo jamii inapolalamika tusiseme moja kwa moja ni waongo bali tushughulikie malalamiko yao ,kama huna jibu muelekeze kwa mtu ambaye anaweza kumpa jibu ili aweze kupata faraja”.Alisisitiza Dkt.Mpoki.

Aidha, aliwataka watumishi wa taasisi hiyo kuvaa vitambulisho ambavyo vinaweka wazi utambulisho wao ili ndugu na wagonjwa waweze kuwatambua na kutaja ni nani ambaye hajatimiza wajibu wake ipasavyo.

“watakaoshindwa kwenda nasi tutawapeleka kwingine,hatutaki maumivu yawe sehemu ya uzoefu wa wagonjwa wanaolazwa Ocean Road,nyinyi kazi yenu ni kuwahudumia wagonjwa”.

Hata hivyo aliwataka madaktari wabobezi (Mabingwa) kutimiza wajibu wao na sio kuwaachia jukumu la kuwahudumia wagonjwa madaktari waliopo mafunzo kwa vitendo”kuanzia sasa tukigundua mgonjwa ameachiwa daktari wa mafunzo kwa vitendo tutawaondoa wasifanye mazoezi hapa lazima tuishi kwa kutii na kufuata miiko ya taaluma zetu”alisema dkt.Mpoki

Aliagiza kufanyika mikutano ya ndani mara kwa mara ya kufuatilia utendaji kazi wa taasisi  na kujibu malalamiko yanayotolewa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na masanduku ya maoni ili kupata mrejesho kutoka kwa wananchi ili kuboresha huduma zinazotolewa kwenye taasisi.

Kuhusu adha ya umbali wa kufuata huduma kwenye taasisi hiyo Dkt. Mpoki aliwathibitishia wagonjwa na ndugu waliopo hospitalini hapo kuwa Serikali kupitia wizara ya afya iko mbioni kupeleka huduma za saratani kanda ya kusini mara tu itakapokamilika hospitali ya Rufaa ya kanda,pia huduma kama hizo zipo mbioni kupelekwa kwenye hospitali ya rufaa ya Tabora pamoja na hospitali maalum ya Benjamin Mkapa iliyopo jijini Dodoma kwani ni wajibu wao kuhakikisha huduma hizo karibu na wananchi.

-Mwisho-

ASILIMIA 85 YA WANAWAKE MKOANI MARA WANAJIFUNGUA KATIKA VITUO VYA AFYA.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisikiliza maoni ya mmoja kati ya wagonjwa waliofika kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akihoji juu ya gharama za huduma za Afya zinazotolewa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara, pindi alipofanya ziara ya kukagua ubora wa huduma na miundombinu katika Hospitali hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Watumishi wa sekta ya Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara(hawapo kwenye picha)
Watumishi wa Kada mbali mbali za Afya wakimsikiliza mgani rasmi Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na uboreshaji wa miundombinu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara.


Na WAMJW - MARA.

Asilimia 85 ya Wanawake Mkoani Mara wanajifungua kwenye vituo vya Afya, hali iliyosaidia kupunguza idadi kubwa ya  vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati alipotembelea Hospitali ya Mkoa wa Mara kukagua hali ya utoaji Huduma.

"Mko Asilimia 85, kitaifa tupo Asilimia 51, kwahiyo niwapongeze kwa hilo, lengo letu ilikuwa ifikapo 2020 tunataka angalau Asilimia 80 ya wanawake wajawazito wajifungulie kwenye vituo vya Afya" Alisema Waziri Ummy.

Pia Waziri Ummy ameitaka Mikoa mingine nchini kuiga jitihada zinazofanywa na mkoa wa Mara za kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kuhakikisha wanawake wajawazito wanajifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

"Sitaielewa mikoa mingine kwa kushindwa kuhamasisha na kuweka Mazingira mazuri kwa wanawake kwenda kujifungulia katika vituo vya kutoa huduma za Afya" alisema Waziri Ummy

Hata hivyo Waziri Ummy Mwalimu amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara kuhamasisha jamii hususan wanawake katika maeneo mbali mbali kuhudhuria kliniki angalau Mara 4 katika kipindi cha ujauzito.

"Wanawake ambao wanahudhuria Kliniki angalau mara 4 ni Asilimia 45 hivyo hamjafanya vizuri  kwasababu kitaifa ni Asilimia 51, mjenge tabia ya kuwahamasisha wanawake kuhudhuria kliniki angalau Mara 4, kama watoa huduma za Afya wanavyotushauri" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Francis Mwanisi Kuhakikisha ifikapo Disemba 30 mwaka huu angalau kaya zote mkoani Mara ziwe na vyoo bora, na kumtaka kutoa elimu na kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa matumizi ya vyoo bora kiafya na kiuchumi kwa mwanadamu.

"Kaya zilizo na vyoo bora kwa Mkoa wa Mara naona ni Asilimia 40, Kwahiyo tunahitaji kuongeza elimu na kutoa mwamko kwa jamii kuhusu kujenga vyoo bora na kuvitumia" alisema Waziri Ummy

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za Afya Mkoani Mara kupitia kuboresha Vituo vya Afya 14, na kujenga Hospitali 3 za Wilaya ambazo ni Lorya, Musoma DC na Bunda, jambo ambalo litalopunguza mzigo kwa Hospitali ya Mkoa ili iweze kujikita katika kutoa huduma za rufaa.

Sambamba na hilo Waziri Ummy amesema kuwa Serikali itaendelea  kuboresha huduma Bora kwa wananchi kwa  kupeleka jumla ya Watumishi 25 katika Hospitali ya Mkoa wa Mara huku akiwahasa Viongozi mkoani hapo kujenga Mazingira mazuri yakuwavutia Watumishi ili wafanye kazi kwa bidii na wabaki katika vituo vya kazi.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Mara Dkt. Hosea Bisanda alisema kuwa Hospitali ya Mkoa imeweza kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 23 mwaka 2015, vifo 14 mwaka 2016, vifo 10 mwaka 2017, na vifo 6 hadi kufikia Oktoba mwaka huu.

Dkt. Bisanda amesema kuwa licha ya Serikali kuwaletea Watumishi 25  Hospitali ya Mkoa wa Mara inatakiwa kuwa na Watumishi 684, lakini Watumishi waliopo sasa ni 305, hivyo kupelekea kuwa na upungufu wa Watumishi 379 sawa na Asilimia 55.

"Hospitali ya Mkoa wa Mara ina uhaba wa Watumishi hasa Madaktari Bingwa, Madaktari wasaidizi, Wauguzi, wateknolojia, Maabara pamoja na wateknolojia madawa" alisema Dkt. Hosea Bisanda

Mwisho.

Alhamisi, 29 Novemba 2018

TAASISI YA MIFUPA (MOI) YATAKIWA KUWASILIANA NA WATEJA KWA NJIA YA SIMU

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiangalia mashine ya mionzi ya CT SCAN katika Taasisi ya mifupa (MOI) wakati alipoitembea ili kujionea hali ya utoaji wa huduma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Ubora wa Huduma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mohamed Mohamed na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi hiyo.


Picha mbalimbali zikionesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na wananchi waliofika kupata huduma za uchunguzi na matibabu katika Taasisi ya mifupa (MOI) wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kujionea hali ya utoaji huduma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya mifupa (MOI) Dkt. Samuel Swai kuhusiana na kuboresha utoaji wa huduma kwa wagonjwa wakati alipoitembelea Taasisi hiyo Leo Jijini Dar Es Salaam.



TAASISI YA MIFUPA (MOI) YATAKIWA KUWASILIANA NA WATEJA KWA KWA NJIA YA SIMU

Na.WAMJW,Dar es Salaam

Taasisi ya mifupa (MOI) imetakiwa kuanzia leo kuwasiliana na wateja wao kwa njia ya simu pale panapotokea mabadiliko ya watoa huduma kutokuwepo mahali pa kazi ilikuepusha usumbufu wa kukaa hospitalini muda mrefu.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati alipofanya ziara katika taasisi hiyo na kukuta wagonjwa wakisubiri kwa muda mrefu kupata matibabu pamoja na vipimo.

Dkt. Mpoki alisema alichokiona kwenye taasisi hiyo ni mawasiliano ambayo inasababisha wagonjwa wengi kutokupata taarifa za kutokuwepo kwa madaktari wao hivyo kufanya wagonjwa kusubiri kwa muda mrefu.

“kuanzia leo taasisi hii itawasiliana nanyi kila inapotokea changamoto inayofanya mabadiliko ya mida yenu na madaktari, mtapigiwa simu sasa wewe utafanya maamuzi yakuja au kusubiri hadi muda ulioambiwa ili uonane na daktari wako muda utakaombiwa”. Alisema Dkt. Mpoki.

Aidha, aliwataka madaktari na wauguzi wawe wanawajulisha wagonjwa mapema wao kwa wale wenye simu kwani kwenye kila jarida la mgonjwa huwa wanaandika namba za simu za wateja wao.

Hata hivyo Dkt. Mpoki alisema hii ni kutokana na mkakati wa Serikali wakutatua changamoto za wananchi wanaofika kupata matibabu kwenye taasisi zake na hivyo kuboresha huduma kwa wahitaji kadri ya uwezo unavyopatikana.

Katibu Mkuu huyo alifanya ziara katika taasisi hiyo kwa kutembelea idara ya Mionzi, wagonjwa wa nje pamoja na kuongea na wagonjwa waliofika kupata matibabu katika hospitali hiyo.

-Mwisho-


WAZIRI UMMY AAGIZA HOSPITALI ZOTE ZA RUFAA ZA MIKOA KUTOA MATIBABU YA KINYWA NA MENO.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee hma Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Madaktari wa Afya ya kinywa na meno (hawapo kwenye picha) wakati akifungua mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Baadhi ya Madaktari na Wadau wa Afya ya kinywa na meno wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi, Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya (hayupo kwenye picha) wakati wa mkutano wa mwaka wa madaktari wa Afya ya kinywa na meno uliofanyika mkoa wa Mara.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu baada ya ufunguzi rasmi wa mkutano wa Madaktari wa Afya ya kinywa na meno uliofanyika mkoa wa Mara.


Na WAMJW - MARA.

 WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amemwagiza Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya kuhakikisha kuwa kabla ya Machi 30, 2019 Hospitali zote za Mikoa kutoa Huduma za matibabu ya kinywa.

Ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Mwaka wa Madaktari wa Kinywa wenye lengo la kujadili njia bora za kuboresha huduma za Afya ya kinywa na meno na namna ya kuikuza kada hiyo, tukio lililofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Waziri Ummy alisema kuwa "hatuwezi kusema kuwa afya ya kinywa na meno ni muhimu alafu leo ni  hospitali za rufaa za Mikoa 10 kati ya 28 ndio zinavitendea kazi" alisema Waziri Ummy.

Pia Waziri Ummy aliwahasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa ya kinywa na meno kwa kujiepusha matumizi ya sigara, tumbaku, unywaji wa pombe kupita kiasi, ulaji wa vyakula na vinywaji vyenye sukari.

"Magonjwa ya kinywa na meno yana visababishi vyake ikiwemo uvutaji wa sigara,sigara, tumbaku, unywaji wa pombe kupita kiasi, ulaji wa vyakula na vinywaji vyenye Sukari" alisema Waziri Ummy

Kwa upande mwingine Mhe. Ummy amewataka madaktari wa kinywa na meno kuwahamasisha wananchi ili kufahamu umuhimu wa kupiga mswaki japo mara mbili kwa siku ili kujiepusha katika hatari yakupata magonjwa ya kinywa na meno.

"Mnatuambia kwamba angalau tupige mswaki mara mbili kwa siku, hapo mnakazi kubwa sana ya kutushawishi, hivyo niwaombe tushirikiane nasi ili kuhakikisha kwamba tunaongeza elimu na hamasa kwa jamii katika suala hiki" alisema Waziri Ummy.

Akiwasilisha taarifa mbele ya mgeni rasmi, Rais wa chama cha Madaktari wa kinywa na meno Tanzania Dkt. Mwakitobe amesema kuwa idadi ya Wataalamu wa Afya ya kinywa na meno bado ni ndogo sana ukilinganisha uwiano wa watoa huduma na wagonjwa hali inayopunguza ufanisi kutokana na kufanya kazi kwa muda mrefu bila kupumzika.

"Idadi ya Wataalamu wa Afya ya kinywa na meno bado ni ndogo sana ukilinganisha uwiano wa watoa huduma na wagonjwa. Wataalamu hao no pamoja na dental therapist, Madaktari wasaidizi wa kinywa na Meno, Wataalamu wa maabara wa kinywa na meno, mafundi wa vifaa na vifaa tiba vya kinywa na meno, Madaktari wa kinywa na meno na Wabobezi kwenye maeneo hayo ya kinywa na meno" alisema Dkt. Mwakitobe.

Dkt. Mwakitobe aliendelea kusema kuwa tafiti za hivi karibuni zinonesha uhusiano mkubwa wa magonjwa ya kinywa na meno na magonja yasiyo yakuambukiza kama vile kisukari, ugonjwa wa moyo  Saratani na hata magonjwa ya HIV/AIDS.

Kwa upande mwingine Dkt. Mwakitobe alisema kuwa Huduma za msingi za kinywa na meno zinahitaji ushiriki mkubwa wa kila mtaalamu wa fani hiyo ya kinywa na meno, pamoja na kundi la wauguzi wa kinywa na meno, ambapo kwa sasa nchi yetu haina chuo kinachotoa mafunzo ya fani ya kinywa na meno.

Aidha, Dkt. Mwakitobe alisema kuwa idadi ya Madaktari bingwa wa kinywa na meno bado no chache na licha ya uhaba uliopo bado hawapati kipaumbele cha kujiendeleza.

"Katika kipindi cha masomo cha mwaka 2018/2019 kipaumbele hakikutolewa kwa waombaji wanaodahiliwa katika fani za uzamili kwenye masomo ya Afya ya kinywa na meno kwani kada hiyo ni muhimu na inasaidia wananchi kama kada nyingine za Afya" alesema Dkt. Mwakitobe.

Mwisho.

Jumatano, 28 Novemba 2018

DKT. NDUGULILE AIPONGEZA TAASISI YA NIMR KWA KUFANYA TAFITI ZENYE TIJA KWA TAIFA.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia sampuli za mbu katika maabara ya Taasisi ya Nimr Muheza, Tanga


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo (kushoto)  alipotembelea kituo cha utafiti wa magonjwa ya binadamu Nirmr.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia vifaa vya zamani vilivyotumika kufanya tafiti katika kituo cha utafiti wa magonjwa ya binadamu Nirmr Amani Muheza.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia lililokuwa jengo la posta ya zamani kabka ya uhuru ambalo lipo katika ofisi za Nimri Amani, Muheza.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisoma kitabu cha tafiti za zamani katika kituo cha tafiti Nimr Amani, Muheza.

Na WAMJW- Muheza, Tanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) kwa kufanya tafiti nzuri zinazoisaidia serikali katika mabadiliko ya sera ya afya kwenye matibabu ya ugonjwa wa Malaria.

Dkt. Ndugulile ametoa pongezi hizo mara baada ya kutembelea katika kituo cha tafiti cha ya ugonjwa wa Malaria Nirmi kilichopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.  “Serikali tunajivunia kuwa na taasisi hii, katika udhibiti wa ugonjwa wa Malaria tumepiga hatua kubwa, tumepunguza maambukizi ya Malaria kwa zaidi ya asilimia 50, tulikuwa na asilimia 14 sasa hivi tuna asilimia 7. Kwa juhudi ambazo tunaenda nazo katika tafiti hizi naamini kiwango cha maambukizi kitaendelea kushuka.” Alisema Dkt Ndugulile.

Licha ya kunufaika na tafiti hizo, Serikali imejiwekea malengo ya kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria nchini, Dkt Ndugulile amesema kuwa Serikali imejiwekea mikakati mbalimbali ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria kwa kutoa vyandarua, dawa za kuuwa vimelea vya Malaria, kila mgonjwa kupimwa ugonjwa wa Malaria pamoja na kunyunyizia dawa katika makazi ili kuuwa mazalia ya mbu.

Aidha Dkt. Ndugulile ameipongeza taasisi hiyo ya Nimr kwa kutambulika na mashirika ya kimataifa kutokana na tafiti inazozifanya kuwa na ubora wa hali ya juu. “Niwapongeze kwa tafiti zetu kutambulika kimataifa, siyo tuu kwa kutusaidia katika mabadiliko ya sera bali pia 
“Tafiti zetu zinatambulika kimataifa, hivi sasa kituo hiki kinatambulika na Shirika la Afya Duniani (WHO) kutokana na tafiti mbalimbali kuhusiana na ugonjwa wa Malaria, kwa hiyo nawapongeza wote kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya” alisema Dkt Ndugulile.

Awali kabla ya kufika katika Kituo hicho, Dkt Ndugulile alifika katika kituo cha tafiti cha Amani kilichopo umbali wa Kilometa 40 nje ya mji wa muheza ambapo amekuta kituo hicho chenye majengo zaidi ya 100 kutofanya kazi za kitafiti. Kituo hicho cha kale ambacho kimeanza kufanya tafiti mbalimbali tangu kabla ya uhuru kimebaki kuwa maktaba ya tafiti za kale ambapo wataalam hufika na kujisomea tafiti za zamani.

Mkuu wa kituo cha tafiti Nimr Muheza, Dkt William Kisinza alisema kuwa tafiti zote za Nimr zilihamishiwa katika majengo mapya yaliyopo Bombo na muheza mjini tangu mwaka 2005. Dkt. Kisinza amesema kuwa taasisi ya Nimr kwa kushirikiana na vyuo vya kimataifa wamekuja na mpango wa kuanzisha chuo cha utafiti wa magonjwa mbalimbali katika kituo cha amani ambapo hadi sasa hivi wamekwisha wasilisha mpango huo ngazi za juu kwa ajili ya utekelezaji.

Baada ya kutembelea majengo hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa ni jambo linalosikitisha kuona rasilimali zilizopo kutotumika vizuri huku akishauri vyuo vya sayansi nchi kutumia fursa hiyo kuanzisha chuo shirikishi kinachotoa elimu ya utafiti wa wagonjwa ya binadamu katika majengo hayo au katika kipindi cha muda mfupi Taasisi iangalie uwezekano wa kuanzisha kozi za muda mfupi katika maeneo ya kipaumbele ili tuweze kuzitumia vizuri rasilimali tulizonazo.

Katika hatua nyingine Dkt. Ndugulile amezitaka taasisi za Serikali kusaidiana katika kazi pale inapobidi ili kuokoa gharama na muda unaotumika katika kazi. Akiwa Jijini baada ya kutembelea hospitali ya rufaa ya Bombo na kituo cha utafiti Nimr, Dkt. Ndugulile amebain vipimo kutoka hospitali ya Bombo hupelekwa Moshi Kilimanjaro huku kituo cha Nimr chenye vifaa vya kisasa kikiwa jirani na hospitali hiyo ambacho kingetumika kufanyia vipimo.

 “Tuna maabara nzuri sana pale tanga yenye mashine za kisasa lakini baada ya tafiti hazitumiki, huku vipimo vya hospitali vikipelekwa moshi. Maabara ingeweza kutusaidia kutoa huduma” Alisema Dkt. Ndugulile na kuzitaka taasisi za serikali kuacha ukiritimba na kuboresha mahusiano kwa manufaa ya taifa.

Mwisho.

Jumatatu, 26 Novemba 2018

WADAU WA SEKTA YA AFYA KUENDELEA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa maendeleo na wakurugenzi wa wizara (Hawapo Pichani) wakati wa mkutano wa mwaka wa wadau wa sekta ya afya wa kujadilia njia zitakazowezesha kufikia malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020 uliofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya (Katikati) akisaini makubaliano ya malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020. Kushoto ni Naibu Katibu mkuu anayeshughulikia ya Afya TAMISEMI Dkt. Zainab Chaula na Kulia ni Mwakilishi wa wadau wa maendeleo.
Wadau mabalimbali wa maendeleo wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokua yanaendelea katika mkutano wa mwaka wa wadau wa sekta ya afya wa kujadilia njia zitakazowezesha kufikia malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020 uliofanyika jijini Dodoma.
Wakurugenzi mbalimbali kutoka wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakimsikiliza Waziri wa wizara hiyo Mhe. Ummy Mwalimu (Hayupo Pichani) katika mkutano wa mwaka wa wadau wa sekta ya afya wa kujadilia njia zitakazowezesha kufikia malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020 uliofanyika jijini Dodoma.


WADAU WA SEKTA YA AFYA KUENDELEA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA NCHINI

NA WAJMW-DODOMA

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kuboresha huduma afya nchini kwa kukarabati vituo vya afya vipatavyo 350 ili  utoaji wa huduma za afya ya mama na mtoto hususani  huduma za dharura wakati wa kujifungua.

Hayo yamesemwa leo na  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa mkutano wa mwaka wa wadau wa sekta ya afya wa kujadilia njia zitakazowezesha kufikia malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020 uliofanyika mapema  jijini Dodoma.

“Sekta ya afya tunaona inaendelea kupiga hatua kubwa sana katika maeneo mbalimbali ikiwemo suala la kuimarisha miundombinu ambapo vituo vya Afya takribani 350 vimekarabatiwa kwa  kuongeza miundombinu kwa ajili ya kutoa huduma za afya za dharura ikiwemo huduma za kumtoa mtoto tumboni”.

Waziri Ummy amesema serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo duniani inahakikisha sekta ya afya inapata mafanikio kwa kuboresha huduma nchini ikiwemo na kufikia asilimia zaidi ya 90 ya dawa zinapatikana katika sehemu zote za kutoa huduma.

Aidha, Waziri Ummy amesema mkutano huo ulikua na lengo la kukubaliana kutekeleza vipaumbele nane (8) ambavyo serikali pamoja na wadau wa maendeleo itahakikisha vinatekelezwa ipasavyo katika mwaka 2019/2020.

Maeneo hayo ni pamoja na Kuimarisha huduma za afya ya uzazi ,mama na mtoto ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, kwa kuweka miundombinu ya huduma za uzazi wa dharura na watoto wachanga kwani kwa takribani hivi sasa watoto wachanga wapatao elfu tisini hufariki ndani ya siku ishirini na nane (28) za mwanzo. Kuongeza huduma za uzazi salama sambamba na uzazi wa mpango, kupunguza maambukizi ya UKIMWI kutoka mama kwenda kwa mtoto.

Eneo la pili linahusu Afya za wasichana na wavulana walio katika umri wa kubalehe ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kuepuka ngono katika umri mdogo na mimba zisizotarajiwa.
Alitaja eneo jingine  ni kuongeza nguvu kazi katika sekata ya afya ikiwa ni pamoja na kuajiri watumishi wa afya katika ngazi zote, kuongeza ujuzi kwa kutoa nafasi za kusomesha watumishi ili kukidhi vigezo vilivyoweka na shirika la afya duniani (WHO).

Kipaumbele cha Nne, ni kuimarisha ubora wa huduma za afya utakaoenda sambamba na uboreshaji wa miundombinu ya sehemu za kutolea huduma za afya za serikali pamoja na kuongeza rasilimali fedha kwa ajili ya kutatua changamoto za afya kwa kuongeza  ya bajeti ya afya   kutoka kutoka Bilioni 31 hadi Bilioni 270 mwaka 2018/2019.

Naye Naibu katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia afya dkt.Zainabu Chaula amesema kwamba wao kama sehemu ya utekelezaji wamejipanga kutekeleza maboresho ya afya ngazi ya msingi kuanzia vijijini hadi Taifa kupitia sera ya afya hivyo wamejipanga kuongeza kutoa elimu ya afya kwa umma kuanzia zahanati  kwa kupanga mipango endelevu ili iende sambamba kuanzia ngazi husika kwa kutumia kamati za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.   

VITUO VYA DAMU SALAMA VYATAKIWA KUBORESHA HUDUMA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa ameketi kwenye kiti maamul kinachotumika wakati wa kutoa damu alipitembelea kituo cha damu salama kanda ya kaskazini.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua taarifa zilitunzwa kwenye kompyuta  katika Kituo cha Damu Salama Kanda ya Kaskazini.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikaguanjofoku linatotunza damu salama katika Kituo cha Damu Salama Kanda ya Kaskazini.

Kaimu Meneja Kituo cha Damu Salama Bw. Richard Komanga akiwasilisha taarifa ya kituo kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani)

Moshi, Kilimanjaro

Vituo vya ukusanyaji damu salama nchini vyatakiwa kuboresha huduma zaidi katika ukusanyaji wa damu na kuwa na benki ya damu itakayowasaidia wenye uhitaji muda wote bila kutegemea ndugu au jamaa wa mgonjwa kuchangia damu.

Hayo yamesemwa jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile alipotembelea kituo cha ukusanyaji damu salama kanda ya kaskazini kinachohudumia mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Tanga na Manyara.

“Tangia tumeanzisha mpango huu wa ukusanyaji wa damu salama mwaka 2004 ukuaji wake umekuwa ni wa kusuasua naona bado hatujapiga hatua sana” alisema  Dkt Ndugulile  na kuendela “Zipo changamoto katika upimaji wa damu, huku idadi ya damu salama inayokusanywa ikiwa ni ndogo kulinganisha na uhitaji uliopo”

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) imetenga bajeti ya kununua vitendea kazi vya kisasa vitakavyosaidia vituo vya ukusanyaji wa damu salama kukusanya kiasi kingi cha damu ndani ya muda mfupi na kuitaka bohari ya dawa kushughulikia suala hilo haraka ili vituo hivyo vipate vifaa hivyo haraka.

Aidha Dkt. Ndugulile amekiri kuwa kazi ya ukusanyaji wa damu salama hugharimu muda mrefu na fedha nyingi huku damu salama inayokusanywa ikiwa ni kidogo kulishanginsha na muda na gharama zinazotumika na kuwtaka watendaji toka Vituo vya ukusanyaji wa damu salama kuja ma mifumo itakayowawezesha kutumia muda na rasilimali fedha kidogo katika ukusanyaji wa damu salama huku kiwango cha ukusanyaji kikiongezeka.

“Hiki ni kituo cha kanda, ni lazima tuongeze kasi ya ukusanyaji wa damu. Haiwezekani kwa kituo hiki kuwa na damu uniti 70, kiwango hiki bado ni kidogo huku gharama za ukusanyaji bado zipo juu” alisema DKt. Ndugulile
Aidha Dkt. Ndugulile amevitaka vituo vyote vya upimaji wa damu salama nchini kutoa majibu ya vipimo kwa haraka na kuacha mara moja urasimu wa kuchelewesha matokeo ya vipimo vya damu. “tuhakikishe sasa tunaweka mifumo mizuri kuhakikisha damu zinazokusanywa katika vituo vyetu vinatoa majibu kwa haraka ili damu hizo ziweze kutumika kwa walengwa waliokusudiwa.

Hata hivyo Dkt. Ndugulile amesema kuwa zipo changamoto katika uhifadhi wa damu salama na Serikali katika bajeti ya mwaka huu wa fedha 2018/19 imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo 10 vya uhifadhi wa damu salama katika hospitali za rufaa za mikoa huku huku upimaji ukiwa bado unafnayika kwa ngazi ya kanda na kuvitaka vituo vinayohusika na upimaji na uhifadhi wa damu salama kuboresha mifumo ya usafirishaji wa damu salama ili damu ziweze kupimwa kwa haraka na kurejeshwa haraka kwa ajili ya matumizi.

Awali akiwasilisha taarifa yake, Kaimu Meneja Kituo cha Ukusanyaji wa Damu Salama Kanda ya Kaskazini Bw. Richard Komanga, amesema kuwa Kituo hicho cha ukusanyaji wa damu salama huhusisha timu 36 zilizojengwa uwezo wa ukusanyaji wa damu katika ngazi za Halmashauri na Mikoa 4 iliyopo katika Kanda ya kaskazini ambapo wananchi huchangia damu bila malipo. Kituo hicho pia hupima damu zenye maambukizi ambapo damu hupimwa magonjwa ya homa ya ini (b), (c) kasendwe na Virusi Vya Ukimwi.

HOSPITALI YA KIBONG’OTO KUWA KITUO CHA TAFITI, TIBA NA MAFUNZO YA MAGONJWA AMBUKIZI


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akipata maelekezo namna wanavyopima wagonjwa wa kifua kikuu toka kwa Mganga Mfawidhi Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto Dkt. Riziki Kisonga (kulia)

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akikagua maabara katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wa kwanza kushoto) akikagua vyumba vya wagonjwa katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua stoo ya dawa zilizopo katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua ramani ya jengo la maabara litakalojengwa katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo  kwa watumishi (hawapo pichani) wa Hospitali Maalum ya magonjwa ambukizi ya Kibong’oto.

Watumishi toka Hospitali Maalum ya Kibong’oto wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani)

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akitoa cheti kwa Dkt. Stellah Mpagama (kulia) mara baada ya kuzindua mpango wa Remodel. 

Na WAMJW - SIHA, KILIMANJARO

Serikali kuifanya Hospitali ya Kibong’oto kuwa kitovu cha utafiti, tiba na mafuzo ya magonja yakuambukiza na magonjwa yanayopatikana maeneo ya kazini.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea Hospitali hiyo ya magonjwa yakuambukiza iliyopo Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro jana Novemba 25, 2018.

“Nataka kuona hospitali hii inakuwa kitovu cha mafunzo katika ugonjwa huu wa kifua kikuu, magonjwa yanayopatikana maeneo ya kazi pamoja na magonjwa mengine yakuambukiza” alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa “Wapo watu wanaougua maeneo ya kazini na hufika hospitalini wakiwa katika hatua za mwisho kabisa za ugonjwa, hivyo kundi hilo nalo inabidi tulifikie kwa wakati”

Pia, Dkt. Ndugulime amesema kuwa takribani watu 150,000 huugua ugonjwa wa kifua kikuu kwa mwaka, huku idadi ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu ikiwa ni 63,000 sawa na asilimia 42 huku tafiti zikionyesha kuwa mgonjwa mmoja wa kifua kikuu ndani ya mwaka mmoja anaweza kuwaambukiza watu 20 ugonjwa huo, hivyo kuwataka watendaji kuja na mkakati wa kutoka ofisini kwenda kuwatafuta wagonjwa wa Kifua Kikuu katika maeneo ya makazi.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile Dkt. Ndugulile, amezindua Mpango wa Remodel unaolenga kuongeza uwezo katika tafiti za tiba ili kuweza kudhibiti magonjwa yakuambukiza, kutoa mafunzo ya sayansi  kwa ngazi ya shahada ya uzamili na uzamiri pamoja na kuandaa miongozo ya namna ya kudhibiti magonjwa yakuambukiza  yaliyopo na ambayo hayategewi kutufikia.

Mpango huo unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya unawaunganisha madaktari wazalendo kutoka hapa nchini ukiongozwa na Dkt. Stellah Mpagama pamoja na madaktari wenza kutoka katika hospitali ya KCMC.

Dkt. Mpagama anasema kuwa wamekuja na mpango huo baada ya kubaini mataifa yaliyopo kusini wa jangwa la sahara yanakabiliwa na idadi kubwa ya magonjwa yakuambukiza  huku miongoni mwa magonjwa hayo kuwa ni Ebola, Homa ya manjano, Homa ya Bonde la Ufa pamoja na ugonjwa wa Kipindupindu.

Dkt. Mpagama amesema kuwa jamii nyingi za nchi za afrika zipo katika mazingira magumu ambayo hupelekea magonjwa yakuambukiza  kusambaa kimzunguko huku idadi ya madaktari waliopo ni ndogo.

“Takwimu toka shirika la afya duniani zinaonyesha katika nchi za afrika kuna daktari mmoja kwa wagonjwa 100,000. Kupitia mpango huu, tunaamini magonjwa haya yakuambukiza tunaenda kuyadhibiti” alisema Dkt Mpagama.

Hospitali Maalum ya magonjwa yakuambukiza  Kibong’oto ilianzishwa mwaka 1925 na Dkt. Noman Davis (raia wa Uingereza) ikiwa ni kituo cha kutibu watu waliokuwa wanaugua ugonjwa wa Kifua Kikuu na mnamo mwaka 2006 Wizara ya Afya iliipa jukumu Hospitali hiyo kutibu ugonjwa sugu wa Kifua Kikuu hadi sasa hospitali hiyo inatoa huduma ya tiba na uchunguzi kwa wagonjwa wa nje na ndani wa Kifua Kikuu huku wastani wagonjwa 120 wa nje na 110 wa ndani hupatiwa huduma za matibabu kila siku.

Mwisho.

Ijumaa, 23 Novemba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA, ZIARA YA DKT. NDUGULILE MKOANI KILIMANJARO.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile jana Novemba 22, 2018 ameanza ziara yake ya kikazi kwa Mkoa wa Kilimanjaro.

Akiwa mkoani kilimanjaro jana alifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na mwenyeji wake Bi.Anna Mghwira  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ambapo alipata taarifa ya Mkoa huku sekta ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kisha kuendelea na ziara yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi pamoja na Hospitali ya Rufaa na Kanda ya Kaskazini ya KCMC. yafuatayo ni matukio katika picha kama yalivyojiri.




Dkt, Ndugulile (kushoto) akisalimiana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi. Anna Mghwira (kulia)
Dkt, Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba kati kati ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi. Anna  Mghwira


Dkt. Ngugulile (aliyesimama) akizungumza na waganga wakuu wa wilaya pamoja na wakurugenzi katika zoezi la ugawaji vyeti vya ubora kwa kwa Hospitali na Vituo vya afya vilivyopo Mkoani Kilimanjaro.



Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa cheti cha ubora kwa Hospitali ya Mt. Joseph iliyotunukiwa hadhi ya nyota nne.



Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa cheti cha ubora kwa Kituo cha afya cha Moshes kilichotunukiwa hadhi ya nyota nne.

Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa zawadi ya ngao kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Bw. Valerian Juwal kwa kuongoza Mkoani Kilimanjaro kuwa na Vituo bora vya afya.

Dkt. Ndugulile (kushoto) akiwa ameshika vipeperushi vya elimu ya afya kwa umma vilivyokuwa vimewekwa sehemu isiyo rasmi na kuuagiza uongozi wa Hospitali ya Mawenzi kuhakikisha ndani ya wiki moja vipeperushi hivyo vitolewe kwa wananchi kwa lengo la kuelimishwa, aliye kulia ni Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro- Mawenzi dkt. Japhet Boniphace.

Dkt. Ndugulile akikagua jokofu linalotunza dawa za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

Dkt. Ndugulile(kushoto) akikagua nyaraka za kitengo cha maabara ambapo amewaagiza watumishi wote hospitalini hapo kuandika rekodi muhimu zote za wagonjwa wakiwa hospitalini.

Ukaguzi ukiendelea....

Dkt Ndugulile (aliyesimama kulia) akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Mawenzi kupata huduma za matibabu.

Dkt. Ndugulile akifurahi mara baada ya kukutana na Mzee franley Mnzava mwenye umri wa Miaka 98 aliyefika Hospitali ya Mawenzi kupata matibabu. Licha ya umri mkubwa alionao Mzee Mnzava bado yu mwenye nguvu na mcheshi muda wote ambapo amewasihi vijana kutunza miili yao ili kuishi miaka mingi.

Dkt, Ndugulile akikagua ramani ya jengo la kituo cmaalum cha uangalizi wa magonjwa ya mlipuko kinachojengwa pembeni ya Hospitali ya mawenzi kinachotarajiwa kukamilika mwezi Machi 2019.

Dkt. Ndugulile akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro.

Dkt. Ndugulile akipokelewa na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini Dkt. Gileard Masenga.

Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Longini Mtalo, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika sampuli ya kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.
wanafunzi wakiwa katika mafunzo ya vitendo kwenye Kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini.


Mafuta Maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanayotengenezwa na Kituo cha Kilimanjaro Sunscreen Production Unit ndani ya Hospitali ya KCMC, mafuta haya huwaliwa walemavu wa ngozi dhidi ya jua kali linalodhuru ngozi ya miili yao.

Dkt. Ndugulile akizungumza jambo huku akiwa amebeba mafuta maalum kwa ajili ya wenye ulemavu wa ngozi yanayotumika kuwakinga dhidi ya jua kali.