Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 30 Agosti 2019

MAPACHA WALIOTENGANISHWA SAUDI ARABIA WAKABIDHIWA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

- Hakuna maoni
Pichani ni Kabla ya mapacha hawajafanyiwa upasuaji wakiwa wamebebwa na mama yao Jonesia Jovitus na Kaimu Balozi wa Saudia Arabia nchini Tanzania, Bandar Abdullah Al-Hazzan ,Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru.

Watoto pacha Melness Benatus Benard na Anisia Benatus Benard wakiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julias Nyerere,wakiwa wamebebwa na Balozi wa Saudi Arabia Mohamed Bin Malik (Kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw.Ramadhani Mwinyi (Kushoto).


Bi.Jonesia Jovitus akiwasili MNH pamoja na watoto mapacha kwa ajili ya uangalizi maalumu

Mama mzazi wa watoto mapacha Bi Jonesia Jovitus ,akipokelewa na ndugu yake katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julias Nyerere.


Na Mwandishi Wetu.
Watoto pacha Melness Benard na Anisia Benard waliozaliwa wakiwa wameungana na baadae kufanyiwa upasuaji na kutenganishwa nchini saudi arabia, wamerejea nchini na kukabidhiwa kwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa ajili ya uangalizi maalumu wa afya zao.
 

Akizungumza leo katika mapokezi ya watoto hao yaliyofanyika kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Elias Kwesi ameishukuru Serikali ya Saudi Arabia kwa kufanikisha upasuaji huo mkubwa wa kutenganisha watoto hao.

“Nawakabidhi watoto hawa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa ajili ya uangalizi maalumu wa afya zao kabla ya kuwaruhusu kwenda nyumbani kwao Wilayani Misenyi, Mkoani Kagera,” amesema Dkt. Kwesi.

Naye Balozi wa Saudi Arabia nchini, Tanzania, Mh. Mohamed Bin Malik amesema kuwa mapacha hao walifanyiwa upasuaji katika hospitali ya King Abdullah Specialist Children’s Hospital ikiwa ni upasuaji wa 47 wa aina hiyo kufanyika kwa mafanikio makubwa nchini Saudi Arabia.

Balozi huyo, ameishukuru Serikali ya Tanzania, Serikali ya Saudi Arabia na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kuratibu upasuaji huo kwa mafanikio.
Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto wa MNH Dkt. Zaituni Bokhary amesema watoto hao walipokelewa hospitalini hapa mwaka 2018 mapema mwezi wa pili na kufanya vipimo kisha kubaini maeneo walioungana.

“Baada ya kufahamu tatizo lao tuliwasiliana na wenzetu wa Saudi Arabia ambao huwa tunashirikiana kwenye kufanya aina mbalimbali za upasuaji na mara baada ya kuwashirikisha vipimo ilionekana watoto hawa wanatakiwa kusafiri kwenda kufanyiwa upasuaji nchini humo” alisema Dkt Zaituni.

Aliongeza kuwa baada ya taratibu kukamilika yeye pamoja na wataalamu wengine wa MNH waliongozana na mama mzazi wa mapacha hao kwenda nchini Saudi Arabia kushughulikia matababu yao.

Akizungumzia uzoefu wa wake kwa aina ya upasuaji waliofanyiwa mapacha hao Daktari Bingwa Mshauri  Mwelekezi wa upasuaji wa watoto kutoka MNH Dkt. Petronila Ngiloi, amesema aina hii ya upasuaji ni wa mfano wa kuigwa kwenye taaluma ya upasuaji.

Pia amewataka wasamaria wema kujitokeza kuwasaidia watoto hao katika malezi ili waweze kupata elimu bora na baadaye waweze kujitegemea.

Kwa upande wake mama mzazi wa watoto hao Bi. Jonesia Jovitus amewashukuru wataalamu wa Saudi Arabia, Serikali ya Tanzania pamoja na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa msaada mkubwa waliompa na kufanikisha.

HOSPITALI YA MLOGANZILA YAZIDI KUIMARISHA HUDUMA.

- Hakuna maoni
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila Dkt. Julieth Magandi (aliyesimama) akiwasilisha taarifa ya utendaji wa Hospitali hiyo kwa mwaka 2018/19 kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya Jamii jana Jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba (aliyesimama) akisema jambo kwneye kikao cha kamati hiyo kilichofanyika jana katika kumbi za Bunge Jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisema jambo kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya jamii  kilichofanyika jana katika kumbi za Bunge Jijini Dodoma.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya Jamii wakiwa kwenye kikao kujadili taarifa ya utendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila jana Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya Jamii wakiwa kwenye kikao kujadili taarifa ya utendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila jana Jijini Dodoma.


Wataalam kutoka Wizara ya Afya na taasisi zake wakisikiza uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Huduma na Maendeleo ya Jamii jana Jijini Dodoma.

Na Englibert Kayombo, WAMJW - Dodoma

Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila jana umewasilisha taarifa ya utendaji kwa mwaka 2018/19 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Akiwasilisha taarifa hiyo Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Dkt. Julieth Magandi amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja tangu hospitali hiyo kuwa chini ya usimamizi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)huduma za matibabu katika hospitali hiyo zimeimarika huku idadi ya wagonjwa waliopata huduma katika hospitali hiyo ikiongezeka.

“Mara baada ya kukabidhiwa Hospitali ya Mloganzila kwa Muhimbili juhudi mbalimbali zimefanyika kuhakikisha kwamba huduma nzuri inatolewa, kuongeza idadi wagonjwa pamoja na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali nyinginezo ikiwemo Muhimbili.

Dkt. Magandi alitaja juhudi hizo kuwa ni pamoja na kutumia wataalam wa Muhimbili kutoa huduma Mloganzila, kuongeza upatikanaji wa damu, dawa na kutoa motisha kwa wafanyakazi ili kuwaongezea hamasa ya kazi pamoja na kukekea lugha mbaya pamoja na rushwa.

“Hatua zilizochukuliwa zimepelekea kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa ambao wengi wao wameonyesha kuridhika na huduma tunatozitoa” alisema Dkt. Magandi.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alisema kuwa Hospitali ya Mloganzila itaendelea kuwa chini ya Bodi ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. “Msimamo wetu ni kwamba hizi ni Hospitali mbili tofauti, lakini chini ya menejimenti moja ya Bodi ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili” alisema Waziri Ummy.

Pamoja na kuanzishwa kwa Hospitali ya Mloganzila, lakini uendeshaji wa hospitali hapo awali haukuwa mzuri” alisema Waziri Ummy na kuendelea “Hospitali ile ina vitanda 608 lakini wagonjwa waliokuwa nao ni chini ya asilimia 30 kwahiyo Hospitali hiyo ilikuwa haiendeshwi kwa ufanisi.

Katika kipindi cha mwaka 2018/19 Hospitali ya Mloganzila imeweza kuwahudumia wagonjwa 85,532 wa nje, wagonjwa 8,480 wa ndani na 2,781 ambao walifanyiwa upasuaji.

MWISHO

Jumatano, 28 Agosti 2019

WIZARA YA AFYA YAJA NA MFUMO WA DHARURA NA UOKOZI

- Hakuna maoni


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa lengo namba tatu (AFYA BORA NA USTAWI) la Malengo Endelevu ya Maendeleo SDG"s kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Huduma na Maendeleo ya Jamii wakipitia taarifa ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo katika ukumbi wa mikutano Bungeni Jijini Dodoma.

Wataalam kutoka taasisi mbalimbali katika Sekta ya Afya wakisikiliza uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa lengo namba tatu (AFYA BORA NA USTAWI) la Malengo Endelevu ya Maendeleo SDG"s kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Huduma na Maendeleo ya Jamii leo katika ukumbi wa mikutano Bungeni Jijini Dodoma.


Na Englibert Kayombo, WAMJW - Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara nchini TANROADS iko mbioni kuanzisha mfumo wa huduma za dharura na uokoaji katika barabara kuu nchini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa lengo namba tatu (AFYA BORA NA USTAWI) kati ya malengo 17 ya Malengo Endelevu ya Maendeleo  (SDG’s) kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kwenye ukumbi wa mikutano bungeni Jijini Dodoma.

Waziri Ummy Mwalimu amesema “mfumo huu una lengo la kusaidia kupambana na dharura au maafa pindi yanapotokea na kuweza kusaidia upatikanaji wa huduma kwa haraka na tutaanza na vituo 7 vya huduma za dharura katika barabara kuu toka Mkoa wa Dar Es Salaam mpaka Ruaha Mbuyuni Mkoa wa Iringa.

Amevitaja vituo vya huduma za dharura ambayo vitaanzishwa kuwa ni Kituo cha Afya Kimara (DSM), Hospitali ya Tumbi, Kituo cha Afya Chalinze (PWANI), Zahanati ya Fulwe (Mikese Morogoro), Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, Hospitali ya St. Kizito (Mikumi, Morogoro) pamoja na Zahanati ya Ruaha Mbuyuni Darajani (Iringa)

“Tumeweza kununua gari za kubebea wagonjwa (Ambulance) 12 ambazo tutazisamba katika vituo vya huduma za dharura” amesema Waziri Ummy na kuendelea  “bado tuna lengo la kuongeza magari matatu  ya uzimaji moto yenye uwezo wa kuinua na kukata vyuma ili kuwaokoa majeruhi na kuwapatia huduma eneo la tukio”


Aidha Waziri Ummy amesema kuwa tayari watoa huduma 272 wamehitimu mafunzo ya huduma za dharura na uokoaji yaliyotolewa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi ambao kati yao, 1212 ni “basic provider” huku 160 ni watoa huduma ngazi ya Vijiji.

Akitoa maoni yake juu ya mfumo huo, Mbunge wa Jimbo la Ludewa Mhe. Deo Ngalawa ameipongeza Wizara ya Afya kwa kuja na mfumo huo ambao utaokoa maisha ya watanzania wengi huku akitumia fursa hiyo kuiomba Serikali kuhakikisha kuwa mfumo huo unasambaa maeneo yote ya barabara kuu ili kusaidia upatikanaji wa huduma za uokozi kwa haraka zaidi.

Waziri Ummy amesema kuwa wameanza na eneo hilo kwanza kwakuwa limekuwa na athari za kutokea kwa ajali nyingi kulinganisha na maeneo mengine huku akisema kuwa huo ni mpango endelevu na wataendelea maeneo yote ya barabara kuu nchini huku akisema kuwa mfumo huo utazinduliwa mwishoni wa Mwaka 2019.

MWISHO

Jumatatu, 26 Agosti 2019

56% YA VIFO VYA VICHANGA INASABABISHWA NA MAGONJWA YA HOSPITALI

- Hakuna maoni
Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Radenta Bahegwa akielekeza jambo wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti maambukizi kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Mfamasia kutoka Hospitali ya Rufaa  ya kanda Bugando akitoa mafunzo kuhusu njia bora ya kujikinga na kudhibiti maambukizi wakati wa kumuhudumia mgonjwa kwa  kufuata taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Radenta Bahegwa akijibu hoja kutoka kwa moja ya washiriki wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti maambukizi kwa kufuata  taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Baadhi ya Wataalamu wa Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) kutoka Kagera wakifuatia kwa makini mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti maambukizi kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), yaliyoandaliwa na Wizara ya Afya.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Maafisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya na Timu ya Wataalamu wa Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti maambukizi kwa taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).


56% YA VIFO VYA VICHANGA INASABABISHWA NA MAGONJWA YA HOSPITALI

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW-KAGERA

Asilimia 56 ya vifo vya watoto wachanga husababishwa na magonjwa yanayotokea wakati wa utoaji huduma za Afya (Healthcare Associated Infections) katika nchi zinazoendelea.

Hayo yamesemwa na Afisa kutoka kitengo cha uhakiki ubora wa huduma kutoka  Wizara Afya Dkt. Radenta Bahegwa kwenye semina ya mafunzo ya njia bora ya namna ya kujikinga dhidi ya   magonjwa yanayoendelea Mkoani Kagera, kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa IPC Guidline).

Alisema taarifa ya tafiti  inasema kuwa 75% ya vifo hivyo vilitokea katika nchi zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara ikiwemo nchi ya Tanzania, huku ukosefu wa huduma ya maji safi yakutosha katika baadhi ya zahanati ikionekana ni moja ya changamoto iliyosababisha tatizo hilo la vifo.

"Tafiti zinaonesha kuwa, 42% ya Vituo vya kutolea huduma za Afya vilivyo na wodi za kujifungulia havikuwa na maji na vifaa kwaajili ya kuoshea mikono, hali inayopelekea kuwa katika hatari yakupata maambukizi kwa vichanga, mama zao au Watoa huduma".

Aidha, alisema kutofuata kanuni na taratibu za utoaji huduma kwa wagonjwa kwa baadhi ya Watoa huduma ni moja kati ya visababishi vikubwa vya vifo vya vichanga vingi katika nchi zinazoendelea, jambo linalorudisha nyuma maendeleo ya Sekta ya Afya katika nchi hizo ikiwemo Tanzania.

Hata hivyo alisisitiza kuwa ni muhimu kwa Watoa Huduma kufuata misingi na taratibu za kutoa huduma kwa Wagonjwa (IPC Standard) ikiwemo kunawa mikono ili kupunguza hatari ya kupata maambukizi yanayotokea wakati wa utoaji huduma kwa Wagonjwa ikiwemo vichanga (Healthcare Associated Infections).

“Usafi wa mazingira kwa kufuata kanuni za usafi katika maeneo ya kutolea huduma za Afya, hauishii kusafisha maeneo tu, bali hata kupangilia kila kitu ili kikae katika eneo linalostahili”. Alisema Dkt. Radenta Bahegwa.

Aliongeza kuwa  kuweka mazingira safi kutasaidia kupunguza hatari za maambukizi kwa Mgonjwa au kwa Watoa huduma, pia kunaongeza hamasa ya kufanya kazi kwa bidi kwa Watoa huduma na kuvutia wagonjwa jambo litalosaidia kuongeza mapato katika Kituo cha Afya.

Kwa upande wake Afisa Afya, Mazingira kutoka Taasisi isiyo ya kiserikali (JBHN) Bw. Said Chibwana alisema kuwa, Lazima kuwe na choo angalau kimoja kwa kila watumiaji 20 kwa wagonjwa wa ndani, na watumiaji wote 25 kwa Wagonjwa wa nje.

Alisema upatikanaji wa huduma za maji safi katika Vituo vya kutolea huduma za Afya husaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia maambukizi ya ugonjwa, kulinda Afya za watoa huduma na Wagonjwa wakati wa utoaji wa huduma za Afya

Wizara ya afya inafanya  mafunzo kwa Watoa huduma za Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) katka Mkoa wa Kagera, lengo ni kuelekeza njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti  maambukizi kwa kufuata taratibu na miongozo ya utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC Guideline). 

Mwisho.

Ijumaa, 23 Agosti 2019

WAUGUZI FANYENI KAZI KWA PAMOJA

- Hakuna maoni
Katibu mkuu Wizara ya afya Dkt. Zainab Chaula akieleza jambo pindi aliposhiriki katika kikao cha kuwashirikisha wadau mwongozo wa utoaji huduma  kwa kuzingatia utu,heshima na maadili kilichofanyika jijini Dodoma.

 Bi. Jane Mazigo kutoka baraza la wauguzi tanzania akichangia kwenye kikao hicho

Aliyekua mganga mfawidhi wa zahanati ya uturo Wilson Chotamganga akielezea jinsi kijiji cha uturo kilivyofanikiwa kuondoa vifo vitokanavyo na uzazi

Washiriki wa kikao cha wadau cha kuwashirikisha muongozo wa utoaji huduma kwa kuzingatia utu,heshima na maadili ya wauguzi nchini



WAUGUZI FANYENI KAZI KWA PAMOJA

Na. Catherine Sungura, Dodoma
Wauguzi wote nchini wametakiwa kufanya kazi kwa pamoja na kuacha tabia za ubinafsi   ili kuweza kuwasaidia wananchi wanaofika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma bora na kwa wakati. 

Hayo yamesemwa na Katibu mkuu Wizara ya afya Dkt. Zainab Chaula aliposhiriki kikao cha kuwashirikisha wadau mwongozo wa utoaji huduma  kwa kuzingatia utu,heshima na maadili kilichofanyika jijini hapa.

Dkt. Chaula alisema kuwa taaluma ya uuguzi ni ya wito hivyo wanatakiwa kuzingatia weledi wa fani yao ili kuwa na mafanikio ya utoaji huduma za afya nchini ili kuokoa maisha ya watanzania ambao wanahitaji msaada wa kuokoa kutoka kwa wataalam hao.

“Lazima turudishane kwenye mstari ili tuweze kuokoa maisha ya akina mama wajawazito,watoto na wagonjwa wengine ,tujiulize kwanini akina mama wajawazito wanafariki?nyinyi ndio chachu ya mabadiliko katika utoaji wa huduma”.Alisisitiza Dkt.Chaula.

Aidha, katibu mkuu huyo alisema kuwa katika kutimiza wajibu wa wauguzi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya anatamani kusiwepo na kifo hata kimoja hususani upande wa akina mama wajawazito hivyo inahitajika nguvu ya pamoja na uelewa miongozi mwa wauguzi kote nchini ili ifikapo 2020.

Mkakati wa kitaifa wa kupunguza vifo wa vitokanavyo na uzazi tanzania imekusudia  ifikapo mwaka 2020 kupunguza vifo hivyo kufikia   292 katika vizazi hai laki  moja ukilinganisha na mwaka 2015 vya vifo 556 kwa vizazi hai laki moja.

Alhamisi, 22 Agosti 2019

SERIKALI YA MAREKANI YAAHIDI KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UGONJWA WA SELI MUNDU (SICKLE CELL) NCHINI

- Hakuna maoni





Na WAJMW-Brazzaville

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir na kufanya mazungumzo na kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na ugonjwa wa Sickle Cell (Seli Mundu) hasa kwa watoto wachanga na wale walio chini ya miaka mitano.

Waziri Ummy amemueleza Waziri huyo kuwa watoto wapatao 11,000 wanazaliwa na ugonjwa huo Tanzania na wengi hupoteza maisha kwa sababu ya kuchelewa kufanyiwa vipimo na kugundulika mapema.

Waziri Ummy amemueleza kuwa muelekeo wa nchi sasa ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anayezaliwa anapimwa Sickle Cell na watakaogundulika matibabu yaanze mapema ili kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.

Mawaziri hao wamekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika kudhibiti vifo vinavyoweza kutokea kwa sababu ya ugonjwa huo huku Waziri Brett akiahidi kuimarisha upatikanaji wa vipimo, pamoja na matibabu kwa watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kuanzia ngazi ya zahanati na vituo vyote vya kutoa huduma za afya ya msingi nchini.

“Ni muhimu huduma hizi zikatolewa katika ngazi ya afya ya msingi mpaka taifa ili kuwapa huduma stahiki wananchi, hii ikiwa ni utekelezaji wa afya kwa wote. Suala la upimaji wa Seli Mundu, elimu kwa jamii na pia suala la matibabu katika ngazi zote za utoaji huduma ni muhimu vikapewa kipaumbele”. Aliongeza Waziri Ummy.

Hivi sasa huduma hii hapa nchini inapatikana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Hospitali za Rufa za Mikoa za Amana na Temeke pekee kwa nchi nzima.

Kwa upande wake Waziri Brett amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kujenga viwanda vya dawa nchini ikiwa ni pamoja na za Sickle Cell. Pia ameahidi kutembelea Tanzania kuona na kujadiliana zaidi namna nchi hizi mbili zitavyoshirikiana katika kushughulikia ugonjwa huu nchini.

Mawaziri hao wanahudhuria mkutano wa 69 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaojumuisha Mawaziri wa Afya toka nchi mbalimbali za Afrika unaoendelea jijini Brazzaville nchini Jamhuri ya Kongo.



CHUPA 51819 ZAIDI ZA DAMU SALAMA ZAKUSANYWA KWA MWAKA 2018/2019

- Hakuna maoni
Meneja Mpango wa Taifa wa Damu Salama Dkt.Magdalena Lyimo akiwasilisha mada ya hali ya upatikanaji damu kwenye kikao cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaoendelea jijini Dodoma

Wadau wa sekta ya afya ambao ni wastaafu Dkt.Deo Mtasiwa ambaye alikua ni Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI  na Bi.Jane Ndyetabula ambaye alikua kamishna wa ustawi wa jamii wakifuatilia uwasilishaji wa mada wakati wa kikao kazi hicho.

Mmoja wa washiriki wa kikao kazi hicho akiuliza swali


CHUPA 51819 ZAIDI ZA DAMU SALAMA ZAKUSANYWA KWA MWAKA 2018/2019

Na. Catherine Sungura,WAMJW-Dodoma

 Mpango wa damu salama umefanikiwa kukusanya chupa  51819 sawa  na asilimia ishirini zaidi ya malengo waliyojiwekea kwa mwaka 2018/2019.

Hayo yameelezwa leo na meneja mpango wa taifa wa damu salama Dkt. Magdalena Lyimo wakati akiwasilisha mada ya upatikanaji wa damu kwenye kikao kazi cha waganga wakuu wa mikoa na halmashauri  kinachoendelea jijini hapa.

Dkt. Lyimo amesema kwamba kwa mwaka 2018/2019
wizara ya afya kupitia mpango huo uliweka malengo ya kukusanya kiasi cha chupa 309376 nchi nzima ikilinganishwa na chupa 257557 zilizokusanywa mwaka 2017/2018.

Hata hivyo Dkt. Lyimo alisema kuwa wameweza kukusanya chupa 309,376 sawa na,asilimia sitini ya mahitaji ya nchi kulingana na idadi ya wananchi waliopo “tumeweza kufanikiwa kuvuka lengo la kukusanya chupa za damu zaidi na hii ni kutokana na uelewa mkubwa wa wananchi wa kuelewa umuhimu wa kuchangia damu katika kuokoa maisha hususani akina mama wajawazito na wahitaji wengine wa damu".Alisema.

Aidha, Dkt. Lyimo alitaja makundi ya wachangia damu kuwa wanawake  ni asilimia 14 pekee huku idadi ya wanaume ikiwa ni asilimia 86 hapa nchini.

Hata hivyo alisema hali ya maambukizi  ya magonjwa kwa damu zinazobainika katika ukusanyaji huo  ameeleza kuwa ugonjwa wa homa ya Ini ndio inayoongoza kwa asilimia 5.9 ikifuatiwa HIV kwa asilimia 2.8.

Dkt. Lyimo amewashukuru wananchi  wanaoendelea kuchangia damu ikiwemo vijana watumishi wa umma, taasisi na mashirika mbalimbali  kwa moyo wa kutekeleza zoezi hilo ili kufikia malengo yanayotarajiwa.

Jumatano, 21 Agosti 2019

WAZIRI UMMY AIPONGEZA WHO KWA KUSAIDIA KUDHIBITI EBOLA NCHINI KONGO

- Hakuna maoni







Na WAMJW- Brazzaville

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amelipongeza Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo kwa juhudi inazofanya kwa pamoja katika kudhibiti ugonjwa wa Ebola.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati akiwasilisha taarifa ya mkakati wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola katika mkutano wa 69 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaojumuisha Mawaziri wa Afya kutoka nchi mbalimbali za Afrika unaoendelea jijini Brazzaville nchini Jamhuri ya Kongo.

Aidha, Waziri Ummy amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhanom kwa kutangaza Ebola kuwa janga la Kimataifa, na kuongeza kuwa Tanzania imefaidika na msaada wa WHO ambao umeiwezesha nchi kujenga uwezo wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo iwapo utaingia nchini.

Waziri Ummy amesema kumekua na uboreshaji wa mpango mkakati wa Ebola uliofanyika Mwezi Machi Mwaka 2019 ambao umelenga kuimarisha ufuatiliaji wa mgonjwa maeneo ya mipakani, kujenga uwezo wa watumishi wa afya kumtambua mgonjwa na kutoa matibabu, kununua vifaa vya kujikinga (PPE) na uratibu huu wa kukabiliana na Ebola umeshirikisha sekta mbalimbali zaidi ya Afya.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy ametaja maeneo ambayo WHO isaidie ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kutekeleza mpango mkakati wa kukabiliana na Ebola, kuimarisha ufuatiliaji katika ngazi ya jamii na kufanya mazoezi zaidi ya kupima utayari wa nchi.  

Pia Waziri Ummy alitaka kujua chanjo ya ugonjwa Ebola inachukua muda gani kuanza kufanya kazi baada ya mtu kuchanjwa ambapo majibu yalitolewa kuwa chanjo hiyo inaanza kufanya kazi baada ya siku kumi huku muda wake wa kumkinga mtu ukiwa bado katika utafiti.

Vile vile Waziri Ummy alitaka kupata ufafanuzi kuwa chanjo hiyo ni kwa ajili ya aina gani ya virusi vya Ebola na ufafanuzi ulitolewa kuwa chanjo hiyo ni kwa ajili ya kirusi cha Zaire ambacho kwa sasa ndicho kinachosababisha mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.

MWISHO

PONGEZI KWAKO MHE. RAIS; DKT. CHAULA

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula


Na.Catherine Sungura, WAMJW-Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula  amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa uwekezaji mkubwa aliouweka katika sekta ya afya nchini.

Dkt. Chaula ameyasema hayo jana wakati wa mahojiano na kituo cha runinga cha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) wakati wa taarifa ya habari baada ya Mhe. Rais kutembelea Mamlaka ya Maabara  ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyopo jijini Dar es Salaam.

Katika mahojiano hayo Dkt. Chaula alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano sio kwamba imewekeza tu kwa mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali bali katika sekta yote ya afya  kwa kuboresha huduma za afya kwa upande wa   miundombinu, dawa, vifaa na vifaa tiba katika hospitali pamoja na taasisi zake.

Kwa upande kwa mamlaka ya maabara  ya mkemia mkuu  wa serikali alisema kuwa serikali kupitia wizara ya afya  imefanya jitihada kubwa za kusogeza huduma  za mamlaka hiyo katika kanda zote nchini na hivi karibuni inatarajia kuwa na kanda nyingine  jijini Dodoma.

“Sisi hapa kwa afrika mashariki, Tanzania tunaongoza kwa kuwa na mitambo ya uchunguzi ya  kisasa vya kufanya utambuzi wa miili na tuna imani tutapokea hata vinasaba kutoka nchi za jirani pale panapotokea mkanganyiko hususani kwenye kesi za jinai,ajali,sumu,madawa ya kulevya pamoja na kemikali.

Dkt. Chaula alisema mitambo hiyo ya kisasa inatoa majibu ndani ya  siku saba tofauti na zamani ambapo sampuli thelathini na tano zilichukua  mwezi kuthibitisha ila kwa sasa wanachukua sampuli hadi mia mbili.

Hata hivyo katibu Mkuu huyo amewashauri watanzania kupenda na  kujenga mazoea ya kutumia taasisi za serikali zilizopo nchini hususani mamlaka ya mkemia mkuu wa serikali pale panapotokea mkanganyiko kwa kisheria au utambuzi wa vinasaba mbalimbali.

Jumanne, 20 Agosti 2019

WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA.HALMASHAURI IMARISHENI LISHE

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika jijini Dodoma.

Picha ya pamoja  wakati wa kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika jijini Dodoma.


WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA.HALMASHAURI IMARISHENI LISHE

Na.Catherine Sungura,WAMJW-Dodoma

Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini wametakiwa kuweka mikakati ya kuimarisha hali ya lishe katika ngazi ya jamii ili kupunguza   hali ya udumavu kwa jamii.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile kwenye  kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika jijini hapo.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa ili kuwe na taifa lisilo na  kiwango cha chini cha hali ya lishe waganga wakuu hao lazima wapange mikakati ambayo itaanzia ngazi ya jamii ili wananchi waweze kuelewa umuhimu wa lishe bora  na inayostahili kwa familia hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa weledi ili mikakati hiyo ifanikiwe.

Hata hivyo alisisitiza  watoa huduma  kutoa huduma bora kwa wananchi kwa  kuimarisha huduma za afya katika maeneo yao ili wananchi wanaoenda kupata huduma wapate huduma hizo kwa haki na usawa" na katika hili ni vyema mwananchi anayekuja  kupata huduna ni vyema  aridhike na huduma anayopata katika vituo vyetu  vyote nchini”.Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile aliwataka waganga wakuu hao kusimamia utendaji wa kazi katika maeneo yao ili kuweza kutoa huduma bora za afya kwa jamii“inasikitisha  kuona mama mjamzito  anafariki kwenye kituo cha afya kwa ajili ya uzembe  au kutokupata huduma sahii jambo hili halikubariki”.

Kikao kazi cha waganga wakuu wa mikoa na halmashauri  mwaka huu kinafanyika jijini hapa ambapo kilifunguliwa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleiman Jafo na kauli mbiu ya kikao hicho ni “Uwajibikaji ni nguzo muhimu katika utoaji huduma bora za afya kuelekea uchumi wa kati na utakua wa siku tano.

Jumatatu, 19 Agosti 2019

CHMTs MWANZA ZAAGIZWA KUSIMAMIA MIONGOZO YA KUKINGA NA KUDHIBITI MAAMBUKIZO

- Hakuna maoni
Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Chrisogone Justine German akitoa mafunzo kwa Watoa huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya Mkoa  wa Mwanza wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga dhidi ya magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata  taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC sstandard)

Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Joseph Hokororo akifafanua jambo mbele ya Watoa Huduma na Watumishi wa Sekta ya Afya Mkoa wa Mwanza wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga dhidi ya, kwa kufuata kanuni za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC standard ).

Afisa kutoka Kitengo cha Dharura na Maafa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Alex Sanga akielekeza umuhimu wakufuata taratibu kwa mgonjwa wakati wa kumuudumia (IPC Standard) kwa Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya Mkoa wa Mwanza.


Baadhi ya Watoa  huduma za Afya kutoka Halmashauri za Jiji la Mwanza wakifuatilia Mafunzo kwa makini ya jinsi yakujikinga dhidi ya maambukizi kwa kufuata kanuni na taratibu (IPC Standard) wakati wa kumuudumia mgonjwa.

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya kutoka Halmashauri mbali mbali jijini Mwanza wakifuatilia kwa makini  Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga dhidi ya magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC Standard)

Picha ya pamoja ikiongozwa na Maafisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakiwa na Watoa huduma kutoka Halmashauri mbali mbali za Mwanza baada ya kumaliza mafunzo ya namna ya kujikinga na kudhibiti  magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa Mkoani hapo.



CHMTs MWANZA ZAAGIZWA KUSIMAMIA MIONGOZO YA KUKINGA NA KUDHIBITI MAAMBUKIZO

Na Rayson Mwaisemba WAMJW- MWANZA

Timu za uendeshaji huduma za Afya za Halmashauri (CHMTs) za Mkoa wa Mwanza zimeelekezwa kusimamia miongozo ya kukinga na kudhibiti maambukizi (Magonjwa) wakati wanatoa huduma za Afya kwa Wagonjwa.  

Hayo yamejiri wakati wa Semina ya mafunzo ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti  magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa, iliyofanyika Jijini Mwanza ikiwa ni moja kati ya mikoa iliyo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola.

Kwa upande mwingine mafunzo hayo yametumika kama njia ya kusambaza muongozo mpya wa namna ya kujikinga na kudhibiti  maambukizo (IPC Guidline), ambayo yameandaliwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ikiwa ni njia ya kuboresha huduma za Afya nchini. 

Katika mafunzo hayo imedaiwa kuwa Tanzania ipo kwenye hatari ya kupata wagonjwa wa Ebola kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu na ukaribu na Nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo ambako Mlipuko unaendelea.

Inakadiriwa kuwa watu Bilioni 2.5 Duniani wapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola, huku kati yao 60% ikiwa ni watu kutoka Kusini mwa Jangwa la Sahara, huku nchi za Sudan, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikiripoti kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo ambao ulisnza tangu 1976.

Kulingana na Taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) inakadiriwa kuwa Wagonjwa 1790 wapoteza maisha tokea mlipuko huo ulipojitokeza Agosti 2018 Wagonjwa 2577 wamethibitika kuwa na Ugonjwa wa Ebola, huku Wagonjwa 1790 wakipoteza maisha tokea mlipuko huo ulipojitokeza Agosti 2018, huku Wataalamu wa Afya 131 walipata maambukizi, ambapo 41 kati yao wamepoteza maisha.

Hata hivyo, Serikali ya Tanzania tayari imekwisha kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha utayari wa kukabiliana na tishio la Ugonjwa huo ili kuhakikisha hauingii nchini, ikiwemo kuelimisha jamii njia za kujikinga na Ugonjwa ili kuzuia usiingie nchini, na kutoa Elimu kwa Watoa huduma za Afya juu ya kumuhudumia mtu mwenye dalili za Ebola endapo atatokea.

Katika mafunzo hayo, Watoa huduma wameaswa kuzingatia taratibu za kujikinga na kudhibiti maambukizo (IPC Standard precautions) kwa kadri Miongozo inavyoelekeza wakati wote wa kutoa huduma kwa Wagonjwa, jambo litalosaidia kuwaepusha kupata maambukizi, au kumsaidia mgonjwa kupata maambukizi mapya wakati wa matibabu.

Akitoa mafunzo hayo, Afisa kutoka Kitengo cha Uhakiki Ubora Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Joseph Hokororo amesema kuwa Watoa Huduma za Afya wapo katika hatari kubwa za kupata maambukizi ya ugonjwa huu, endapo hawatofuata miongozo na taratibu za utoaji huduma kwa kadri ya muongozo huu

“Mara kwa mara ni muhimu kuwa na tahadhari wakati unahudumia Wagonjwa, hususan kunawa mikono kabla na baada ya kutoa huduma kwa wagonjwa na wasio wagonjwa kwani Watoa huduma mpo kwenye hatari kubwa sana yakupata maambukizo” alisema Dkt. Joseph Hokororo.

Ameendelea kusema kuwa, Shirika la Afya Duniani (WHO) inakusudia kuzuia Ugonjwa wa Ebola kwa kuimarisha huduma za uchunguzi na kusaidia nchi zilizo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola.

Pia alisisitiza kuwa Dunia imekumbwa na tatizo la Usugu wa vimelea vya magonjwa ambukizi dhidi ya dawa (antimicrobial resistance), hivyo amesisitiza juu ya umuhimu mkubwa wa kufuata taratibu za kutoa huduma (IPC Standard) ili kusaidia kutokomeza vimelea hivyo.   

Akitoa mafunzo kwa Watoa Huduma za Afya, juu ya namna ya kukinga maambukizi wakati wa kujifungua, Afisa kutoka Kitengo cha Uhakiki Ubora Wizara ya Afya Dkt. Chrisogone German amesema kuwa ni muhimu kwa Watoa huduma kufuata viwango vya kukinga na kudhibiti maambukizo (IPC Standard) ili kudhibiti ya ugonjwa wakati wa kutoa huduma ikiwemo kuhakikisha kunawa mikono kabla ya kufanya kazi za kuhudumia wagonjwa.

Aliendelea kusisitiza kuwa, si jambo zuri kwa Watoa huduma za Afya, kufanya mambo kwa mazoea, hali inayopelekea kufanya kazi kwa mazoea na kujikuta kunasambaa maambukizi kutoka kwa mtu anaepokea huduma za Afya au kinyume chake 

Mwisho.

Jumanne, 13 Agosti 2019

WATOA HUDUMA ZA AFYA MWANZA WAFUNDWA

- Hakuna maoni
Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Joseph Hokororo akieleza jambo mbele ya Watoa Huduma na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), inayoendelea Jijini Mwanza.

Afisa Afya ya Mazingira kutoka Taasisi ya JBHN Said Chibwana akitoa Elimu kwa Wataalamu wa Huduma za Afya na baadhi ya  Watumishi wa Sekta ya Afya  wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Radenta Bahegwa akijibu hoja kutoka kwa Wataalamu wa Huduma za Afya na baadhi ya  Watumishi wa Sekta ya Afya  wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Mtaalamu wa Maabara Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikikishi MUHAS Akili Mawazo Mwakabhana akisisitiza jambo mbele ya Watoa Huduma na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), Semina hiyo inaendelea Jijini Mwanza.

Afisa kutoka Kitengo cha Dharura na Maafa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Alex Sanga akifafanua jambo mbele ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), inayoendelea Jijini Mwanza

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando wakifuatilia mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Seketoure wakifuatilia mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini  Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), mafunzo yanaendelea Jijini Mwanza.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto sambamba na Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya baada ya kumaliza Wiki ya kwanza ya Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), Jijini Mwanza.



WATOA HUDUMA ZA AFYA MWANZA WAFUNDWA

Na Rayson Mwaisemba WAMJW-MWANZA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yawafunda Watoa Huduma za Afya Jijini Mwanza  kuwakumbusha namna ya utoaji huduma kwa kufuata misingi na taratibu za utoaji huduma kwa Wagonjwa ili kupunguza maambukizi mapya na vifo visivyo na ulazima.

Hayo yamejiri wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa, iliyofanyika Jijini Mwanza ikiwa ni moja kati ya mikoa iliyo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola.

Katika Mafunzo hayo yaliyo andaliwa na Wizara ya Afya imedaiwa kuwa Tanzania ipo kwenye hatari ya kupata wagonjwa wa Ebola kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu na ukaribu na Nchi ya Uganda na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo ambako Mlipuko unaendelea.

Kwa taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO) inakadiriwa kuwa Wagonjwa 2577 wamethibitika kuwa na Ugonjwa wa Ebola, huku Wagonjwa 1790 wakipoteza maisha tokea mlipuko huo ulipojitokeza Agosti 2018, huku Wataalamu wa Afya 131 walipata maambukizi, ambapo 41 kati yao wamepoteza maisha.

Aidha, Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha utayari wa kukabiliana na tishio la Ugonjwa huo ili kuhakikisha hauingii nchini, ikiwemo kuelimisha jamii njia za kujikinga na Ugonjwa ili kuzuia usiingie nchini, na kutoa Elimu kwa Watoa huduma za Afya juu ya kumuhudumia mtu mwenye dalili za Ebola endapo atatokea.

Watoa huduma wanatakiwa kuzingatia taratibu za kujikinga na kudhibiti maambukizi (IPC Standard precautions) kwa kadri Miongozo inavyoelekeza wakati wote watoapo huduma kwa Wagonjwa, jambo litalosaidia kuwaepusha kupata maambukizi, au kumsaidia mgonjwa kupata maambukizi mapya wakati wa matibabu.

Afisa Mkuu Uhakiki Ubora kutoka Wizara ya Afya Dkt. Joseph Hokololo amesema kuwa zaidi ya watu milioni 1.4 Duniani wanaugua magonjwa yanayosababishwa na kupata maambukizi mapya wakati wakupata huduma ya afya, hii hutokana na Watoa huduma za Afya kutofuata taratibu za namna ya kutoa huduma.

Aliendelea kusema kuwa Asilimia 15 ya Wagonjwa hupata maambukizi ya magonjwa mapya pindi waendapo kupata huduma za Afya katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya, kutokana na kutofuatwa kwa taratibu, kanuni za miongozo ya kutoa huduma za Afya (IPC Guideline, SOP).

Kwa Upande wake Afisa kutoka Kitengo Uhakiki Ubora Wizara ya Afya Dkt. Chrisogane Justine amesema kuwa kufuata taratibu za utoaji huduma kama kanuni za uoshaji sahihi wa mikono kutamsaidia Mtoa huduma kuzuia kusambaza maambukizi ndani ya Kituo cha kutolea huduma za Afya na nje.

Licha ya changamoto za upatikanaji wa huduma za maji safi kwa baadhi ya Vituo vya Afya, Dkt. Chrisogone Justine German amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Mtoa huduma za Afya kuhakikisha ananawa mikono yake vizuri kwa sabuni na maji safi ili kuepuka kusambaza maambukizi kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Akitoa Elimu juu ya namna ya kujikinga dhidi ya maambukizi mapya yanayotokea wakati wa matibabu kutokana na baadhi ya Watoa huduma kutofuata taratibu na miongozo Dkt. Radenta Bahegwa amesema kuwa asilimia 40 ya magonjwa yanayopatikana katika vituo vya kutolea huduma za Afya nayosababishwa na kutofuata kwa taratibu za miongozo ya utoaji huduma.

“Asilimia 40 ya ya magonjwa yanayopatikana katika Vituo vya kutolea huduma za Afya husababishwa na kutofuata miongozo (IPC Guidline), ndiomaana asilimia 80 ya UTI zinazoibuka katika Vituo vya Afya zinatokana na kukosea kuweka kifaa cha kupitisha haja ndogo” alisema Dkt. Radenta.

Mtaalamu kutoka Kitengo cha Dharura na Maafa Dkt. Alex Sanga amesema kuwa katika watu 100, watu 5 hadi 10 wanakuwa katika hali mbaya ya ugonjwa wa kipindu pindu, hivyo ametoa wito kwa Watoa huduma kuhakikisha wanafuata miongozo na taratibu wakati wa kutoa huduma ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi mapya katika jamii.

“Tafiti za Shirika la Afya Duniani zinonesha kuwa ndani ya miaka 3 (2015-2018) kati ya watu 33,421, watu 542 walipoteza maisha, huku katika watu 100, watu 5 hadi 10 wanakuwa katika hali mbaya ya ugonjwa wa kipindu pindu, hivyo juhudi za makusudi zinatakiwa kuchukuliwa” alisema Dkt. Sanga.

Naye Mtaalamu wa Maabara kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS Akili Mawazo Mwakabhana amesisitiza umuhimu wa kufuata taratibu na miongozo wakati wa kutoa huduma kwa mgonjwa kuzuia maambukizi mapya kwa Mgonjwa au Mtoa huduma za Afya jambo ambalo litasaidia kupunguza idadi ya Wagonjwa na kuokoa fedha ambazo zingetumika katika matibabu. 

Kwa upande wake Mfamasia kutoka Hospitali ya Kanda Bugando Francisco Chibunda ametoa wito kwa watoa huduma za Afya kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kufuata miiko na taratibu na miongozo inavyoelekeza jambo litalosaidia kuondoa tatizo la usugu wa magonjwa (Wadudu) kutokana na matumizi mara kwa mara ya dawa, ambayo daktari angeweza kuyazuia kwa kufuata taratibu na miongozo wakati wakutibu ugonjwa.

“Tunapoteza nguvu kubwa, tunapoteza rasilimali nyingi kwenye dawa na matibabu, mwisho wa siku tunasababisha maambukizi mapya, nah ii hupelekea usugu wa magonjwa , kwa hiyo tubadilike” Alisema Chibunda.

Mwisho.