Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 23 Agosti 2019

WAUGUZI FANYENI KAZI KWA PAMOJA

Katibu mkuu Wizara ya afya Dkt. Zainab Chaula akieleza jambo pindi aliposhiriki katika kikao cha kuwashirikisha wadau mwongozo wa utoaji huduma  kwa kuzingatia utu,heshima na maadili kilichofanyika jijini Dodoma.

 Bi. Jane Mazigo kutoka baraza la wauguzi tanzania akichangia kwenye kikao hicho

Aliyekua mganga mfawidhi wa zahanati ya uturo Wilson Chotamganga akielezea jinsi kijiji cha uturo kilivyofanikiwa kuondoa vifo vitokanavyo na uzazi

Washiriki wa kikao cha wadau cha kuwashirikisha muongozo wa utoaji huduma kwa kuzingatia utu,heshima na maadili ya wauguzi nchini



WAUGUZI FANYENI KAZI KWA PAMOJA

Na. Catherine Sungura, Dodoma
Wauguzi wote nchini wametakiwa kufanya kazi kwa pamoja na kuacha tabia za ubinafsi   ili kuweza kuwasaidia wananchi wanaofika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma bora na kwa wakati. 

Hayo yamesemwa na Katibu mkuu Wizara ya afya Dkt. Zainab Chaula aliposhiriki kikao cha kuwashirikisha wadau mwongozo wa utoaji huduma  kwa kuzingatia utu,heshima na maadili kilichofanyika jijini hapa.

Dkt. Chaula alisema kuwa taaluma ya uuguzi ni ya wito hivyo wanatakiwa kuzingatia weledi wa fani yao ili kuwa na mafanikio ya utoaji huduma za afya nchini ili kuokoa maisha ya watanzania ambao wanahitaji msaada wa kuokoa kutoka kwa wataalam hao.

“Lazima turudishane kwenye mstari ili tuweze kuokoa maisha ya akina mama wajawazito,watoto na wagonjwa wengine ,tujiulize kwanini akina mama wajawazito wanafariki?nyinyi ndio chachu ya mabadiliko katika utoaji wa huduma”.Alisisitiza Dkt.Chaula.

Aidha, katibu mkuu huyo alisema kuwa katika kutimiza wajibu wa wauguzi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya anatamani kusiwepo na kifo hata kimoja hususani upande wa akina mama wajawazito hivyo inahitajika nguvu ya pamoja na uelewa miongozi mwa wauguzi kote nchini ili ifikapo 2020.

Mkakati wa kitaifa wa kupunguza vifo wa vitokanavyo na uzazi tanzania imekusudia  ifikapo mwaka 2020 kupunguza vifo hivyo kufikia   292 katika vizazi hai laki  moja ukilinganisha na mwaka 2015 vya vifo 556 kwa vizazi hai laki moja.

0 on: "WAUGUZI FANYENI KAZI KWA PAMOJA"