Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 31 Oktoba 2017

- Hakuna maoni


Naibu Waziri Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akiwasilisha taarifa ya utendaji wa shughuli za Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania(TFNC) mbele ya  Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamiii inayoongozwa na Mwenyekiti wake Peter Serukamba(wa kwanza kulia) leo mjini Dodoma,ambapo imeonekana tatizo la ulaji wa chakula bora kwa Watanzania bado ni tatizo kubwa.




Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt.Vicent Assey akijibu maswali ya wajumbe wa kamati hiyo ambapo ilionekana licha ya uzalishaji chumvi kwa wingi bado kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto bado ipo chini kwa asilimia 30 kwenye Mikoa ya Simiyu,Mtwara na Lindi.wakati kiwango cha mahitaji ya mwili ni asilimia 61 kwa takwimu za mwaka 2015/2016 hivyo kiwango hicho kimepanda kutoka asilimia 47 cha mwaka 2010.


Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamiii wakifuatilia kwa umakini uwasilishaji wa taarifa kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Faustine Ndugulile(Hayupo kwenye picha) leo jijini Dodoma.




















LISHE BORA KWA WATANZANIA BADO NI TATIZO, ASEMA MH. PETER SERUKAMBA

- Hakuna maoni


Na.WAMJW.Dodoma

Taasisi ya Chakula na lishe nchini imetakiwa kujikita katika kutoa elimu kwa umma ili wananchi waweze kujua faida ya kula chakula bora na kuepukana na utapiamlo na udumavu
Hayo yamesemwa na Mwenyeketi wa kamati ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii  Mhe. Peter Serukamba wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utendaji wa shughuli za taasisi hiyo mjini Dodoma leo.
Mhe.Serukamba alisema bila elimu kwa umma wananchi watakuwa wanatumia fedha nyingi kwa ajili ya matibabu kwa kuwa hali ya udumavu ni mkubwa ,”watu wakiwa na chakula na lishe bora unakuwa na uhakika hutougua hovyo na kupoteza fedha nyingi kwa ajili ya matibabu,lakini wakijua wale mlo gani ambao ni sahihi hii itasaidia kutokomeza kabisa tatizo hili”
Aidha, alisema Tanzania haina tatizo la chakula ila hawafahamu ni mlo gani sahihi wanapaswa kula hivyo kwa kutoa zaidi elimu itakua ni kinga na itasaidia wananchi wasiugue
“Taasisi hii iboreshwe na mkishirikiana na Tamisemi,wakulima na wasafirishaji wa mazao kupitia maofisa maendeleo ya jamii mtawafikia wananchi wengi na hakutokuwa na vizazi vyenye udumavu na matatizo ya akili.
Awali akiwasilisha taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto dkt.Faustine Ndugulile alisema zaidi ya asilimia 35 ya vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano nchini vinachangiwa na matatizo ya lishe duni na  katika kipindi cha mwaka 199 hadi 2015/2016 vifo vya watoto vimepungua  kutoka 147 hadi 67 kwa kila vizazi hai 1000.
“Serikali inafanya jitihada kubwa  katika kumjenga mtoto ili akue vizuri kimwili na kiakili kuanzia siku elfu moja za mwanzo za mtoto ambazo ni muhimu kwa makuzi ya mtoto”.
Hata hivyo dkt.Ndugulile alisema hali ya lishe nchini inaendelea kuimarika kutokana na kupungua kwa viwango vya utapiamlo nchini kati ya mwaka 1992 na 2015.
Alisema udumavu (urefu wa umri) umepungua kutoka asilimia 49.7 hadi 34.4 na mikoa inayoongoza ni Rukwa (56%) na Ruvuma (44%) ,kwa upande wa ukondefu (uzito kwa urefu) kutoka asilimia 7.8 hadi 4.5 na mikoa inayoongoza ni Zanzibar-Kusini Pemba na Kaskazini Pemba(9%),Manyara (6.4%),Geita (6.2%),Kigoma (6%) na Morogoro (6.0%)
Kwa upande wa uzito pungufu alisema (uzito kwa umri) kutoka asilimia 25.1 hadi 13.7 na mikoa inayoongoza ni Rukwa (23%),Arusha (20%) pamoja na Kigoma (20%).
Vilevile,mwanamke mmoja kati ya kila wanawake 10 walio katika umri wa kuzaa ana uzito pungufu (underweight) wakati asilimia 18 wana uzito mkubwa (over weight) na asilimia 10 wana kiribatumbo(obesity).Mikoa inayoongoza kwa kiribatumbo ni Zanzibar mjini Magharibi kwa 22%,Unguja Kusini 19%,Dar es Salaam 21%,Kilimanjaro 19% na Tanga 17%.
Naibu Waziri huyo aliahidi kuwa watajipanga katika kutoa elimu ya afya kwa umma na kuwafikia wananchi wengi zaidi “bado Watanzania hawajui kula lishe iliyokamilika na matumizi bora ya chakula.

Jumatatu, 30 Oktoba 2017

TANZANIA HATUNA UHABA WA DAWA, ASEMA DKT. FAUSTINE NDUGULILE

- Hakuna maoni

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa mkutano wan ne wa chama cha wataalamu wa figo nchini uliofanyika leo mjini Dodoma.

UTAALAMU WA KUPANDIKIZA FIGO UPEWE KIPAUMBELE NCHINI, ASEMA DKT. NDUGULILE

- Hakuna maoni




Na WAMJW-DODOMA
UTAALAMU wa huduma ya kupandikiza figo kwa wagonjwa wenye magonjwa hayo upewe kipaumbele hapa nchini ili kuweza kuokoa watanzania wengi wenye matatizo hayo kwa muda mfupi na kupunguza gharama kubwa ya rufaa za kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa mkutano wan ne wa chama cha wataalamu wa figo nchini uliofanyika leo mjini Dodoma.
“Serikali imekuwa ikipeleka wastani wa wagonjwa 35  kwa mwaka nje ya nchi ikiwa ni pamoja na India kwa ajili ya kupandikiza figo ambapo inagharimu takribani shilingi milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja ikiwa ni gharama za malazi na kupandikiza figo” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa ikiwa  Tanzania itazalisha wataalamu wengi wa kupandikiza na kusafisha figo itafanikiwa kupunguza gharama hizo na kufanya huduma hiyo ipatikane kwa shilingi milioni 20.3 ikiwa huduma hiyo itapatikana hapa nchini.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuwekeza huduma ya kupandikiza figo Serikali imefunga mashine katika maeneo yafuatayo, UDOM 10, 5Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  42, Hospitali ya Rufaa Mbeya 5, Hospitali ya Rufaa Bugando 10, KCMC 10, Hospitali ya Misheni Serian  10, Hospitali ya NSK Arusha 5, TMK 10,Regency 15, Hurbert Kairuki 5, Aga Khan 10 na Access 10 ambapo takwimu zinaonyesha mashine hizi zina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 783 kupitia huduma ya NHIF na 391 kwa huduma malipo ya papo kwa papo.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa chama cha Wataalam wa Figo Tanzania Dkt. Paschal Rugajjo amesema kuwa wamepiga hatua kubwa katika kuongeza madaktari wa figo hapa nchini kwani mpaka sasa wapo madaktari 12 kutoka daktari mmoja miaka kumi iliyopita.
Mbali na hayo Dkt. Rugajjo amesema kuwa ushirikiano unahitajika kati ya chama hicho pamoja na Serikali kutoa kipaumbele kwenye elimu juu ya ugonjwa huo ili kuweza kupambana na tatizo hilo kuanzia ngazi ya wananchi mpaka kwenye taasisi za afya nchini.

DKT. FAUSTINE NDUGULILE AFUNGUA MKUTANO WA NNE WA CHAMA CHA WATAALAMU WA FIGO.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto dkt.Faustine Ndugulile akiongea kwenye mkutano huo wa wataalamu wa magonjwa ya figo nchini.Mkutano huo wa siku mbili unafanyika kwenye Hotel ya Morena Mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wataalamu mbalimbali kutoka Hospitali nchini,Wadau wa Maendeleo pamoja na wataalamu wengine kutoka nchi za Kenya,Sudan,India pamoja na Norway.







Makamu wa Rais wa Chama cha wataalamu wa magonjwa ya Figo Tanzania (NESOT), Dkt.Paschal Ruggajjo akiongea dhima kubwa ya mkutano huo  ni teknolojia ya upandikizaji wa viungo nchini ili kuweza kuhudumia wagonjwa takribani milioni 23.












Baadhi ya Wataalamu wa magonjwa ya figo waliohudhuria mkutano huo.Mkutano huo ni wa siku mbili ambapo watajadili dhana mbalimbali ya ugonjwa wa figo ikiwemo kutoa elimu kwa umma ili kuweza kukabiliana na magonjwa ya figo pamoja na upandikizaji.Tanzania imekua ikipeleka wastani wa wagonjwa thelathini na tano(35) kwa mwaka nje ya nchi kwa ajili ya kupandikiza figo na gharama ya kupandikiza nje ya nchi ikiwemo India ni shilingi milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja ikiwemo kupandikiza,nauli pamoja na malazi
 
Makamu wa Rais wa Chama hicho akimpa zawadi mmoja wa wataalamu wa figo ambaye amefanya tafiti na kuwasilisha mada ya katika mkutano huo Profesa Ainory Gesase ambaye ni mkufunzi wa Chuo cha Sayansi ya Tiba.











Picha ya pamoja ya Mgeni Rasmi wa mkutano huo Dkt.Ndugulile akiwa na wataalamu wa figo nchini pamoja na wadau wengine wa ndani ya nchi na nje ya nchi.
 
 
 
 
 
 
 
 
Naibu Waziri akisalimiana na washiriki wa Mkutano huo mara baada ya ufunguzi.Dkt.Ndugulile alisema Serikali mgonjwa mmoja anahitaji wastani wa shilingi za kitanzania 37,620,504 kwa mwaka kwa ajili ya kulipia gharama za kusafisha damu nchini.
 
 
 
 
 
 
Mashine za kusafisha figo (Dialysis Machine) ambazo zimefungwa kwenye hospitali nchini.Serikali imefunga mashine katika hospitali nchini ikiwemo UDOM (10),Hospitali ya Muhimbili (42), Hospitali ya Rufaa Mbeya(5), Hospitali ya Rufaa Bugando (10), KCMC(10),Hospitali ya Misheni Serian(10),Hospitali ya NSK Arusha(5),TMK(10),Regency(15),
Hurbert Kairuki(5), Aga Khan(10) na Access(10).Mashine hizo  zina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 783 kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) na 391 kwa huduma ya malipo ya papo kwa papo(Picha zote na Wizara ya Afya).
 

TAHADHARI YA UGONJWA WA MARBURG

- Hakuna maoni

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

 

TAARIFA KWA UMMA

TAHADHARI YA UGONJWA WA MARBURG
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea taarifa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), mnamo tarehe 19 Oktoba 2017 kuhusu ugonjwa wa Marburg ambao umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda tangu tarehe 17 Octoba, 2017. Maeneo yaliyoathirika  na ugonjwa huo ni Wilaya ya Kween, Kanda ya Mashariki ya nchi, ambayo  inapakana n nchi ya  Kenya. Hadi kufikia  tarehe 19 Oktoba 2017, watu 4 walikwishapata maambukizo ya ugonjwa huo, ambapo wawili kati yao   wamepoteza maisha.

Wizara  inatoa tahadhari ya Ugonjwa huu kwa wananchi  katika mikoa yote ya Tanzania, hususan kwa wale wanaoishi  katika mikoa ambayo inapakana na na nchi  ya Uganda (Mikoa ya Mara, Mwanza na Kagera).

Ugonjwa wa Marburg  unafanana sana na ugonjwa wa Ebola. Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Marburg vinajulikana kama  “Marburg Virus”, navyo vipo katika jamii moja na virusi vinavyosababisha Ebola (Ebola virus). Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yajulikanayo kwa ujumla kama Homa za Virusi zinazosababisha kutokwa damu mwilini, (Viral Haemorrhagic Fevers). Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo.

Dalili kuu za ugonjwa huu ambazo huanza ghafla ni pamoja na Homa kali, maumivu makali ya kichwa pamoja na mwili kuishiwa nguvu ambapo baadaye huambatana na kuharisha sana (majimaji), maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika na kutokwa damu katika matundu yote ya mwili yaani pua, njia ya haja kubwa na ndogo, mdomoni, masikioni, machoni, hali inayopelekea kifo kwa muda mfupi. Kipindi cha kuonekana kwa dalili za ugonjwa ni kati ya siku 3 hadi 9 baada ya kupata maambukizi.

Ugonjwa huu unaenea kwa urahisi sana na ha­raka kutoka mtu mmoja hadi mtu mwingine iwapo mtu atakuwa karibu na mgonjwa na kugusana na mate, damu, mkojo, machozi, kamasi, maji maji mengine ya mwili, ikiwa ni pamoja na jasho au kumgusa  mtu aliyekufa kwa ugonjwa wa Marburg. Ugonjwa huu pia unaweza kuenezwa iwapo mtu atagusa nguo au mashuka ya mgonjwa wa Marburg.

Wizara ya Afya , imechukua hatua zifuatazo katika kukabiliana na tishio la ugonjwa huu:

o   Kutoa taarifa ya tahadhari ya ugonjwa huu kwa Waganga Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya kupitia OR-TAMISEMI.  Taarifa hiyo imejumuisha namna  Ukweli kuhusu ugonjwa (Fact sheet),

o   Kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huu kupitia kwa Wataalamu wa Afya katika Mikoa, Wilaya na maeneo ya mipaka ya nchi kavu na maji. Aidha watalaamu hawa wa Afya pia wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu dalili za ugonjwa huu ili endapo ugonjwa huo utatokea uweze kutolewa taarifa mapema na kushughulikiwa.

o   Vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa afya na vipima joto maalum (thermoscan) tayari vipo katika maeneo husika ya mikoa.


Wananchi wanashauriwa kutokuwa na hofu kwani hadi  sasa hakuna mgonjwa yeyote wa Marburg aliyeripotiwa nchini. Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa kuwa na dalili za ugonjwa huu.



Kitengo cha mawasiliano Serikalini,
30/10/2017.

UONGOZI WA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA DODOMA WAPOKEA KWA MASIKITIKO JUU YA TAARIFA YA RUSHWA ILIYORIPOTIWA KWENYE MTANDAO WA JAMII FORUM

- Hakuna maoni
 
 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

                                                                                      
                                                                                                                 
TAARIFA KWA UMMA JUU YA TUHUMA YA UWEPO WA VITENDO VYA RUSHWA KATIKA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA, DODOMA KAMA ILIVYORIPOTIWA KWENYE MTANDAO WA KIJAMII WA JAMII FORUM TAREHE 28/10/2017
Uongozi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma umepokea kwa masikitiko taarifa iliyotolewa kwenye mtandao tajwa hapo juu kwamba, “Serikali na Takukuru muimulike Hospitali ya Mkapa Dodoma” kwamba, “imekuwa kawaida kabisa kwa mgonjwa kutopata huduma ya aina yoyote bila kutoa chochote na kuna mgonjwa ana wiki matokeo ya vipimo hayajatoka na hajapewa huduma yoyote zaidi ya dawa za kuondoa maumivu”.
Uongozi wa Hospitali unapenda kuwahakikishia watumiaji wa huduma za hospitali hii kwamba, madai husika hayana ukweli wowote. Mara baada ya kupokea malalamiko na tuhuma tajwa hapo juu, siku hiyo hiyo ya tarehe 28/10/2017 uongozi wa hospitali ulichukua hatua ya kufanya ufuatiliaji kwa kuwatembelea wagonjwa wote waliokuwa wamelazwa wodini na kuzungumza nao pamoja na ndugu zao ili kubaini kero walizonazo kuhusu huduma za Hospitali.
Ufuatiliaji huu ulizingatia kubaini tarehe ya kulazwa, ugonjwa alio nao, vipimo alivyoandikiwa, vipimo ambavyo havijafanyika na sababu za kutofanyika.  Aidha, kila mgonjwa/ndugu aliridhia na kutoa ushirikiano mkubwa ili kubaini ukweli na pia wote walitoa mawasiliano yao ya simu ya mkononi iwapo ufuatiliaji zaidi ungehitajika.
Yatokanayo na ufuatiliaji huo ni;
Jumla ya wagonjwa 34 ndio walikuwemo wodini siku ya tarehe 28/10/2017. Tarehe za kulazwa kwao zilikuwa kati ya 20/9/2017 na 28/10/2017. Kati ya hao, wanawake watu wazima walikuwa 20 na wanaume 14 ambapo kati yao 2 walikuwa watoto wachanga.
Wagonjwa 24 tu ndiyo matibabu yao yalikuwa yanahitaji vipimo mbalimbali na wengine hawakuhitaji kutokana na asili ya magonjwa waliyokuwa wanaugua.
Wagonjwa waliombwa kutoa maoni yao kuhusu hali ya huduma kwa ujumla pia kuhusu upatikanaji wa vipimo vya uchunguzi wa maabara na mionzi na kama kuna ucheleweshaji wa vipimo husika na dalili za kuombwa rushwa. Jumla ya wagonjwa 18 kati ya 24 waliohitaji vipimo, walikuwa wamepimwa na kupewa majibu. Wagonjwa sita (6) waliobakia; wawili (2) kati yao walikuwa wamelazwa tarehe 27/10/2017 na tayari walikuwa wameshaanzishiwa matibabu na kupangiwa kupimwa ECHO na ECG tarehe 30/10/2017. Aidha, wagonjwa wengine wawili (2) walikuwa wamepimwa tarehe 27/10/2017 na walikuwa wanasubiri majibu na waliobakia 2 ndiyo kwanza walikuwa wamelazwa siku hiyo ya tarehe 28/10/2017.
Hakukuwa na mgonjwa yeyote aliyelalamikia kusumbuliwa kuhusu vipimo wala kuona dalili za rushwa na badala yake, wote walishukuru kwa juhudi zinazofanywa na watumishi wa hospitali katika kuwapatia huduma.


Hata hivyo, tangu awali hospitali hii imeweka mifumo mbalimbali ya kuhakikisha inabaini vitendo vinavyo athiri utoaji wa huduma bora na salama vikiwemo vitendo vya rushwa. Mifumo hii ni pamoja na:-
1.       Utoaji wa elimu kwa wateja maeneo ya  mapokezi, maabara na kliniki.
2.       Uwepo wa Sanduku la Maoni
3.       Uwepo wa namba za simu za kutolea malalamiko ya wateja.
4.       Viongozi wa hospitali kutembelea sehemu mbalimbali za kutolea huduma na kuongea na wateja.
5.       Wateja kujaza dodoso la kutoa maoni baada ya huduma (client exit interview).
Elimu inayotolewa huelekeza juu ya haki za wateja, huduma zinazopatikana, mfumo wa malipo, kujiepusha na kutoa au kupokea rushwa, na jinsi ya kutoa maoni na malalamiko juu ya huduma wanazopata kwa kutumia sanduku la maoni, kupiga namba za simu zilizobandikwa sehemu mbalimbali na kuwaelekeza mahala palipo na dawati la malalamiko na jinsi ya ujazaji wa dodoso la mteja baada ya huduma (Client Exit Interview). Elimu hii hutolewa na Idara ya Ustawi wa Jamii iliyopo hapa hospitalini.
Aidha, tangu awali, hospitali iliweka Sanduku la Maoni maeneo ya mapokezi ili  wateja waweze  kuweka maoni yao wakati wowote wanapohitaji. Tangu sanduku la maoni lianze kufunguliwa, hakuna aliyelalamikia uwepo wa vitendo vya rushwa au viashiria vyake.
Vilevile, hospitali imebandika namba Nne (4) tofauti za Simu mkononi za Viongozi katika sehemu mbalimbali za kutolea huduma ili kuwarahisishia wananchi/wateja kuwasilisha maoni yao kuhusu huduma. Namba ya kwanza kwenye orodha ni ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, ikifuatiwa na ya Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Katibu wa Hospitali. Tangu Wananchi waanze kutumia namba hizi hakuna aliyewahi kulalamikia uwepo wa rushwa ndani ya hospitali hii.
Uongozi wa Hospitali umejiwekea utaratibu wa kutoka ofisini na kupita sehemu mbalimbali za kutolea huduma na kuongea na wagonjwa ili kubaini kama kuna changamoto wanazozikabili wakati wa kupokea huduma. Maeneo hayo ni pamoja na mapokezi, eneo la wagonjwa wa nje (OPD), Kliniki mbalimbali, maabara, eneo la kutolea huduma za mionzi, na mawodini. Zoezi hili huongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali na hufanyika angalau mara tatu kwa wiki zikiwemo siku za mapunziko za Jumamosi na Jumapili. Tangu zoezi hili lianze, hakuna mwananchi/mteja aliyewahi kulalamikia uwepo au viashiria vya rushwa.
Hospitali pia ilianzisha Dodoso Maalumu la Mteja (Client Exit Interview) linalojazwa na mteja baada ya kupewa huduma ili kubaini sehemu zenye changamoto. Tangu madodoso haya yaanze kujazwa, hakuna mteja/mgonjwa aliyelalamikia uwepo au viashiria vya rushwa.
Uongozi wa Hospitali unatoa Shukrani za pekee kwa watumiaji wa huduma za hospitali hii na wote wanaotoa maoni kwa ajili ya kuboresha zaidi huduma. Tunapenda kuwahakikishia kuwa, tutaendelea kusimamia maadili ya tiba na kuhakikisha wateja wote wanafurahia huduma zetu. Hata hivyo, hatutasita kuchukua hatua stahiki za kisheria endapo tutabaini kwamba taarifa iliyotolewa ni ya upotoshaji na / au imetolewa kwa lengo la kuichafua hospitali, wizara au Serikali.
Uongozi wa hospitali unatoa wito kama kuna ambaye hajatendewa haki ajitokeze na kutumia fursa za mawasiliano zilizoainishwa hapo juu ili kero yake iweze kufanyiwa kazi au afuate utaratibu rasmi wa kuripoti tukio husika la vitendo vya rushwa kwenye vyombo husika vya kisheria ili taratibu za kisheria zichukuliwe.
Aidha, milango ya hospitali iko wazi wakati wowote kwa ajili ya kupokea kero na maoni toka kwa wateja wake ili kuboresha zaidi huduma.

AHSANTENI SANA.

30/10/2017.

UGONJWA WA KIHARUSI UNAZUILIKA NA KUTIBIKA

- Hakuna maoni


Ukiona mojawapo ya dalili hizi nenda haraka kwenye kituo cha huduma za Afya kwa matibabu.
Hakikisha unafanya uchunguzi wa Afya yako mara kwa mara.


Pitia :https://www.facebook.com/afyatz/?ref=bookmarks

Jumamosi, 28 Oktoba 2017

MH. UMMY AAGIZA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA VYOTE VYA SERIKALI KUTOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI.

- Hakuna maoni
Na WAMJWW

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu aagiza Hospitali na Vituo vya Afya vyote vya Serikali nchini kuanzia leo October 28 kutoa huduma ya uchunguzi wa Saratani kila siku wakati wa kliniki ya mama na mtoto, sambamba na huduma hizi, kila mwezi vyatakiwa kuwa na siku moja kwaajili ya kuchunguza na kufanya matibabu ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti.
Ameyasema hayo wakati alipofungua matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti, yalifunguliwa  katika viwanja vya hospitali ya Ocean Road mapema leo jijini Dar es salaam.
Aidha Mh. Ummy ameipongeza kazi nzuri inayofanywa na Uongozi wa Hospitali ya Ocean Road katika kutimiza majukumu yake ikiwemo kuongeza vitanda  40 mpaka vitanda 100  kwa gharama zao kwaajili ya wagonjwa wa saratani pindi wanapopata huduma za matibabu ya Chemotherapy.
“Katika kuwaunga mkono Serikali ya awamu ya tano ya Mh. Magufuli imewapatia Bilioni 5 kwajili yakukamilisha mashine za kisasa za matibabu ya Saratani kwa kutumia mionzi.” Alisema Mh. Ummy Mwalimu
Aidha Mh. Ummy Mwalimu ametoa maelekezo kwa Uongozi wa Hospitali ya Ocean Road kuwa wanatakiwa kwenda kwenye shule za Msingi na Sekondari ili kuwajengea watoto uelewa kuhusu ugonjwa wa Saratani,  lakini ni vipi wataweza kujikinga na magonjwa yasiyo yakuambulizwa ikiwemo ugonjwa wa Saratani.
Pia Mh. Ummy alitoa rai kwa wananchi wote hususani wanawake kujitokeza kupima ugonjwa huo kwani unatibika endapo itagunduliwa mapema,  
Nae  Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Grace Maghembe ambae pia alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar Es salaam , ameipongeza Serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto kwa kazi kubwa wanayoifanya ikiwemo kuongeza kwa bajeti ya Dawa , vifaa tiba vya uchunguzi na matibabu.
Kwa upande mwingine Dkt. Grace Maghembe kwa niaba ya bodi ameahidi kuendelea kufanya kazi kwa  uaminifu na bidii kubwa katika kuhakikisha kwamba wanakabiliana na ugonjwa huu wa Saratani kwa wananchi hasa wale wa hali ya chini na kuahidi kuendelea kuboresha huduma hii.
“Niwaombe wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam kwenda kupima Saratani kwani ni bure, usisubiri mpaka kuugua, ukichelewa grarama zinaongezeka lakini pia uwezekano wa kupona unakuwa ni mdogo”. Alisema Dkt Grace Maghembe
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage amemhakikishia Mh. Ummy Mwalimu kwamba upatikanaji wa dawa katika Hospitali hiyo ni 80% na dawa za wagonjwa wengi zinapatikana kwa 100%, ukilinganisha na  2015/2016 upatikanaji wa dawa ilikuwa 4% tu,  jambo ambalo lilikuwa ni changamoto kubwa na kufanya malalamiko ya dawa kuwa makubwa sana katika hospitali hiyo, hivyo kuishukuru Serikali ya Magufuli kwa niaba ya Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu.
Mwisho Dkt. Julius Mwaiselage amemhakikishia Mh. Waziri kwamba Hospitali ya Ocean Road ipo katika hatua ya Mwisho ya kuweka mashine mpya mbili (Linear accerelators), hivyo zitasaidia kupunguza muda wa kusubiri kwa wagonjwa kusubiri huduma , lakini kubwa kupunguza wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi.

MH. UMMY MWALIMU (MB) AFUNGUA MATEMBEZI YA HISANI YAKUHAMASISHA UCHUNGUZI WA SARATANI YA MATITI.

- Hakuna maoni
Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu watatu kutoka kushoto wakati alipofungua matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti, kulia kwa Mh. Waziri ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage na kushoto  ni Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Grace Maghembe.




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akimkabidhi cheti moja ya wadau waliofanikisha matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti iliofanyika mapema leo katika viunga vya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es salaam.




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakirusha Maputo juu kuashiria ufunguzi rasmi wa matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti, iliofanyika katika viunga vya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es salaam.





Wadau kutoka taasisi mbali mbali walioungana na Mh. Ummy Mwalimu na watumishi wa Hospitali ya Ocean Road katika matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti yaliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.
 
 
 
 
 
 
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiambatana na Binti yake katika matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti yaliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.
 
 
 
 
 
 
 

Ijumaa, 27 Oktoba 2017

AFYA YANGU, MTAJI WANGU

- Hakuna maoni

"Hakikisha unamkinga mwanao dhidi ya ugonjwa wa Polio kwa kukamilisha Dozi 4 za Polio"

AFYA YANGU,MTAJI WANGU

- Hakuna maoni



Zuia Mtoto Kuzaliwa na Mgongo Wazi au Kichwa Kikubwa kwa kutumia Vyakula vilivyowekwa Virutubishi zaidi kwa Afya Bora.

MH. UMMY AWAJIA JUU VIONGOZI WANAOWAKAMATA MADAKTARI BILA KUFUATA UTARATIBU

- Hakuna maoni

Aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 49 la Afya na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Madaktari yaliofanyika jijini Dar es salaam, huku likihudhuliwa na Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Samia Suluhu.

MH. UMMY AHIMIZA UTARATIBU UFUATWE ILI KUWACHUKULIA HATUA MADAKTARI.

- Hakuna maoni





Na WAMJWW  
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ahimiza weledi na kukemea vitendo vya baadhi ya Viongozi  kuwachukulia hatua madaktari na badala yake kuwataka wafuate utaratibu uliowekwa.
Mhe. Ummy aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 49 la Afya na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Madaktari.
Nae Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameliagiza Baraza la Mitihani kufanya uhakiki haraka ili wataalamu wa Sekta za Afya wapangiwe vituo.
“Tangu tuingie madarakani  serikali imeweza kutoa vibali vya ajira mpya vipatavyo 3,410 kwa awamu mbili, awamu ya kwanza vibali vya madaktari 258 na awamu ya pili vibali 3,150 kwa wataalamu wa kada ya afya na taratibu za ajira kwa wataalamu hawa 3150 zimekamilika na imebakia hatua ya uhakiki wa vyeti katika Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA)” alisema Mh. Samia Suluhu.
Makamu wa Rais aliwapongeza Chama cha Madaktari kwa kuweza kuandaa Kongamano la 49 na kuweka historia ya kuandaa Makongamano tangu mwaka 1965.
Kauli mbiu ya mwaka huu inayosema “ Malengo ya Maendeleo Endelevu: Uweledi wa Kitaaluma na Utoaji Bora wa Huduma za Afya Nchini Tanzania.” Mada hii ni muhimu sana katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza kwa vitendo wajibu wake wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapatiwa huduma za afya zenye viwango na zinazokidhi mahitaji.

Jumatano, 25 Oktoba 2017

Mh. UMMY MWALIMU(MB) AGAWA MASHINE ZA KUCHUNGUZA SARATANI

- Hakuna maoni


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh.Ummy Mwalimu agawa mashine 100 za tiba mgando (Cryotherapy) na mashine 9 za upasuaji mdogo (LEEP) ambazo zitatumika kwaajili ya matibabu ya awali ya Saratani kwa Wanawake. Makabidhiano hayo yalifanyika katika viunga vya ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam. Pia makabidhiano hayo yalihudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Faustine Ndugulile, Baadhi ya Watumishi wa Wizara hiyo na Waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali.

Jumanne, 24 Oktoba 2017

BALOZI WA IRANI MH. MOUSA FARHANG ATETA NA WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU KATIKA OFISI NDOGO ZA WIZARA JIJINI DAR ES SALAAM.

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu watatu kutoka kushoto akimsikiliza Balozi wa Irani nchini Tanzania Mh. Mousa Farhang mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam huku lengo la ugeni huo likiwa ni kuimarisha ushirikiano wa nchi hizo hususani katika sekta ya Afya. Kulia mwa Barozi Mousa ni Dkt. Mahmoud.




Na WAMJWW
Balozi wa Irani nchini Tanzania Mh.Mousa Farhang mapema leo amemtembelea Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam, lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano wa nchi hizo mbili hususani katika nyanja za teknolojia na matibabu ya kibingwa.
Aidha Balozi Mousa amemtoa hofu Mh. Ummy na kumuahidi Irani itaendelea kushirikiana na Tanzania bega kwa bega katika kuhakikisha kwamba wanasukuma gurudumu la maendeleo hasa katika nyanja ya Afya kwa kuimarisha huduma za kibingwa.
Kwa upande mwingine Balozi Mousa ameishukuru Serikali yake ya Misri kwa kuisaidia Tanzania ikiwemo uchimbaji wa visima maeneo ya vijijini jambo lililosaidia kupunguza hadha ya maji kwa jamii hususani wanawake.
Hata hivyo Balozi Mousa Farhang ameahidi kuendeleza ushirikiano huo na Serikali ya Tanzania huku akiwataka wawekezaji kutoka Irani kuja kufanya uwekezaji mkubwa nchini hapa hususani katika viwanda vya dawa.
Nae Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu ameshukuru ugeni huo kutoka Irani ulio na tija kwa taifa la Tanzania huku akisisitiza na kuweka  mkazo wa ushirikiano huo katika uwekezaji wa chanjo, kutoa madawa,vifaa na vifaa tiba, ufadhili wa mafunzo ya muda mfupi kwa watoa huduma wa Tanzania na kujenga uwezo wa Ushirikiano katika maeneo ya utafiti wa tiba.

Jumatatu, 23 Oktoba 2017

PICHA ZA BAADHI YA MATUKIO YAKUKABIDHI MASHINE ZA KUCHUNGUZA SARATANI.

- Hakuna maoni





Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo tarehe 23 Oktoba, 2017 amekabidhi mashine 100 za tiba mgando (cryotherapy) na mashine  9 za upasuaji mdogo (LEEP) ambazo zitatumika kwa ajili ya matibabu ya awali ya saratani kwa wanawake watakaofanyiwa uchunguzi na kukutwa na mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye Ofisi ndogo za Wizara hiyo zilizopo Jijini Dar es Salaam ambapo Mhe. Waziri Ummy amesema katika kuhakikisha tunaongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi, Wizara ya Afya imekuja na mkakati wa kuboresha huduma hizi kwa kununua mashine na vifaa hivyo ambavyo vimegharimu kiasi cha shilingi bilioni moja na vitasambazwa katika mikoa 10 ikijumlisha halmashauri 31 ambazo tumebaini zina vituo vichache vya kutolea huduma  hizi ukilinganisha na Mikoa mingine.

SERIKALI YAONGEZA VITUO 100 KWA AJILI YA KUTOA HUDUMA ZA UCHUNGUZI NA MATIBABU YA AWALI YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NCHINI

- Hakuna maoni



Ndugu wanahabari,
Tanzania ni mojawapo ya nchi za kusini mwa Afrika zinazokadiriwa kuwa na  idadi kubwa ya wagonjwa na vifo vingi vitokanavyo na Saratani.  Takribani wagonjwa wapya 50,000 kila mwaka wanagundulika kuwa na Saratani, na idadi hii inakadiriwa kuongezeka kwa asilimia hamsini (50%) ifikapo mwaka 2020.

Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road kwa kipindi cha mwaka 2006 hadi 2015 zinaonyesha kwamba aina za Saratani zinazoongoza hapa nchini ni kama ifuatavyo; Saratani ya mlango wa kizazi (34%),Saratani ya Ngozi (kaporsis Sarcoma)(13%), Saratani ya matiti (12%), Saratani ya mfumo wa njia ya chakula (10%), Saratani ya Kichwa na shingo (7%), Saratani ya Matezi (6%), Saeatani ya Damu (4%), Saratani ya Kibofu cha mkojo (3%),Saratani ya ngozi (3%), Saratani ya Macho (2%), na saratani ya tezi dume (2%).  Mbaya zaidi, asilimia 80 ya  wagonjwa wote hao wanafika Ocean Road wakiwa katika hatua za mwisho za  ugonjwa na kufanya matokeo ya matibabu kutokuwa mazuri.


Ndugu wanahabari,
Kupitia takwimu hizi ni dhahiri kuwa Saratani ya Mlango wa Kizazi husababisha vifo vingi kwa wanawake, ikifuatiwa na saratani ya matiti. Na kama ilivyo kwa saratani nyingine, asilimia 80 ya wanawake wanaougua saratani hiiwanafika katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya tiba wakiwa katika hatua za mwisho za ugonjwa, ambapo hufanya  matibabu kutokuwa na matokeo mazuri. Aidha Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kutibu wagonjwa  hawa.  Saratani ya Mlango wa kizazi inatibika endapo itagundulika mapema sambamba na kusaidia kupunguza gharama za matibabu ambazo Serikali, familia na mgonjwa wamekuwa wakikabiliana nazo.

Tangu mwaka 2008, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilianza kutoahuduma ya uchunguzi kwa kutumia siki(acetic acid) na matibabu ya mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kutumia tiba mgando (cryotherapy).Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, Wizara imeshaanzisha vituo 459 (vituo 343 vya serikali na 116 vya mashirika na watu binafsi) vinavyotoa huduma ya uchunguzi na matibabu ya mabadiliko ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi. Wizara inawapongeza na kuwashukuru wadauwote wanaoshiriki katika kuimarisha upatikanaji wa huduma hizi. Kipekee tungependa kutambau mchango wa Jhpiego, ICAP, EGPAF, THPS, Marie Stope, PSI, Umati, MEWATA, T Marc na WAMA.  Tunawashukuru sana!

Ndugu  wanahabari,
Katika kuhakikisha tunaongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi, Wizara ya Afya imekuja na mkakati wa kuboresha huduma hizi kwakununuamashine 100  za tiba mgando  (cryotherapy) na mashine  9 za upasuaji mdogo (LEEP) ambazo zitatumika kwa ajili ya matibabu ya awali ya saratani kwa wanawake watakaofanyiwa uchunguzi na kukutwa na mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi. Pia tumenunua mitungi 173 ya gesi ya ‘’carbon dioxide‘’ itakayowezesha mashine hizo kufanya kazi. Vilevile, tumeshatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watoa huduma ili kuweza kutoa huduma hizi bila vikwazo. Vifaa hivi vimekwishawasili nchini na vinaanza kusambazwa katika vituo vya Tiba 100 nchini kuanzia kesho. Vifaa hivyo vitasambazwa katika mikoa 10, halmashauri 31 ambazo tumebaini zina vituo vichache vya kutolea huduma  hizi ukilinganisha na Mikoa mingine. Mikoa hii ni Mara, Singida, Geita, Dodoma, Tanga, Arusha, Manyara, Ruvuma, Lindi na Mtwara.

Ndugu  wanahabari,
Kupitia hatua hii, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais, Mhe Dr. John Pombe Magufuli inaongeza idadi ya vituo vinavyotoa huduma za uchunguzi na matibabu ya awali ya saratani kutoka vituo 343 (2015) hadi vituo 443 (2017). Huduma hizi zinapatikana katika Hospitali zote za Rufaa za Kanda na Mikoa, Hospitali zote za Wilaya, na baadhi ya Vituo vya Afya na Zahanati.


Ndugu wanahabari,
Kupitia kwenu, napenda kuwahimiza wanawake kujitokeza kwa wingi kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi katika vituo hivi. Huduma hizi zinatolewa katika kliniki ya afya ya mama na mtoto kila siku na bila malipo yoyote. Aidha ninavielekeza vituo vyote vya umma nchinikutenga siku maalumu katika kila mwezi ambayo kituo kitahamasisha wanawake kuja kwa wingi kupata huduma hizi. Na kwa kuwa mwezi wa Octoba kila mwaka ni mwezi wa uhamasishaji wa upimaji wa saratani ya matiti duniani kote,  nitumie fursa hii kutoa rai kwa wananchi hasa wanawake wenzangu kuhudhuria vituoni kupata huduma za uchunguzi mapema. Wananchi wengi wamekuwa wakipoteza maisha aidha kwa kutofahamu au uelewa mdogo kuhusu saratani.

Ndugu wananchi,
Aidha, katika kuhakikisha huduma hizi zinakuwa endelevu, nazielekeza halmashauri zote kutenga fedha za kutosha kuhakikisha huduma hizi zinaingizwa kwenye mipango yao ya bajeti ya vituo na halmashauri. Pia ni lazima wahakikishe mashine hizi zinatunzwa na kufanyiwa ukarabati inapobidi.Kwa upande wetu Wizara ya Afya, tutaendelea kusimamia ubora wa huduma zinazotolewa kulingana na miongozi, kujenga uwezo wa watoa huduma. Vilevile, tutahakikisha mafundi sanifu tiba wanapatiwa uelewa na nyezo za kufanya matengenezo madogo na ukarabati wa mashine hizi kwa kushirikiana na Halmashauri husika.

Kwa ujumla, Serikali  itaendelea kuhakikisha vituo zaidi vinaanzishiwa huduma hii ili ipatikane karibu zaidi na wananchi hasa wa vijijini. Vilevile, tutahakikisha tunapanua huduma za Rufaa za Matibabu ya saratani  nchini kwa kuhakikisha huduma za Tiba kwa kutumia dawa (Chemotherapy ) na Mionzi (Radiotherapy) zinapatikana katika  Hospitali za Rufaa za Kanda- Mbeya, Bugando na KCMC ili kupunguza msongano wa wagonjwa katika Hospitali ya Ocean Road, Dar es salaam.

ASANTENI  KWA KUNISIKILIZA

MH. UMMY MWALIMU (MB) AKABIDHI MASHINE ZA UCHUNGUZI SARATANI.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa Habari (hawapo kwenye picha) wakati wakati akikabidhi  vifaa vya uchunguzi wa Saratani kwa Bohari ya Dawa (MSD), tukio lililofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam, pembeni yake ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu  pamoja na Naibu Waziri wake Dkt. Faustine Ndugulile wakipokea vifaa vya uchunguzi wa magonjwa ya Saratani kutoka kwa Mkurugenzi  wa ugavi na ununuzi Wizara ya Afya Casto Simba katika tukio lililofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.








Waandishi wa habari wakifuatilia kwa umakini taarifa iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu kuhusu Saratani wakati akikabidhi  vifaa vya uchunguzi wa Saratani kwa Bohari ya Dawa (MSD) mapema leo jijini Dar es salaam.
 







Waandishi wa habari kutoka vituo mbali mbali hapa nchini wakifanya kazi yao kwenye  tukio la kukabidhi  vifaa vya uchunguzi wa magonjwa ya Saratani kwa Bohari (MSD),tukio  lililofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam










Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akitete jambo na Naibu wake Mh. Faustine Ndugulile wakati wa tukio la kukabidhi  vifaa vya uchunguzi wa magonjwa ya Saratani lililofanyika mapema leo