Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 23 Oktoba 2017

PICHA ZA BAADHI YA MATUKIO YAKUKABIDHI MASHINE ZA KUCHUNGUZA SARATANI.






Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo tarehe 23 Oktoba, 2017 amekabidhi mashine 100 za tiba mgando (cryotherapy) na mashine  9 za upasuaji mdogo (LEEP) ambazo zitatumika kwa ajili ya matibabu ya awali ya saratani kwa wanawake watakaofanyiwa uchunguzi na kukutwa na mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa kizazi
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye Ofisi ndogo za Wizara hiyo zilizopo Jijini Dar es Salaam ambapo Mhe. Waziri Ummy amesema katika kuhakikisha tunaongeza upatikanaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya awali ya Saratani ya Mlango wa Kizazi, Wizara ya Afya imekuja na mkakati wa kuboresha huduma hizi kwa kununua mashine na vifaa hivyo ambavyo vimegharimu kiasi cha shilingi bilioni moja na vitasambazwa katika mikoa 10 ikijumlisha halmashauri 31 ambazo tumebaini zina vituo vichache vya kutolea huduma  hizi ukilinganisha na Mikoa mingine.

0 on: "PICHA ZA BAADHI YA MATUKIO YAKUKABIDHI MASHINE ZA KUCHUNGUZA SARATANI."