Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 31 Oktoba 2018

SERIKALI YARAHISISHA UKUSANYAJI WA TAKWIMU ZA VIFO VINAVYOTOKEA KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI.

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki  Ulisubisya akiongea na baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali na Maafisa Afya mkoani Iringa wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki  Ulisubisya katikati akionesha Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii pamoja na Maafisa afya wa kata mbalimbali Mkoani Iringa

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa iringa Bw. Fikira Kissimba akiongea nna na baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali na Maafisa Afya mkoani Iringa wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki  Ulisubisyakushoto akimkabidhi Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafinga Mji bw. Fredrick Kayombo kulia wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathimini kutoa Wizara ya Afya Bw. Tumainieli Macha wa kwanza kulia akifuatilia kwa makini maelekezo ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki  Ulisubisya hayupo pichani wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani Iringa.

NA WAMJW-IRINGA


SERIKALI kupitia Wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imerahisisha ukusanyaji wa takwimu za vifo vinavyotokea kwenye ngazi ya jamii nchini kwa kugawa vifaa maalumu vya kukusanyia takwimu hizo kwa Maafisa afya katika kata za mkoa wa Iringa.

Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki  Ulisubisya wakati akikabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu hizo  kwa Maafisa Afya leo  Mkoani Iringa.

“Takwimu zitakazokusanywa kuhusu vifo na  Maafisa hawa wa afya  kutokana na Mifumo hii zitawasaidia madaktari kujadili changamoto pamoja na sababu za vifo hivyo ili kupata ufumbuzi wa matatizo hayo na kuweza kupunguza idadi ya vifo nchini” alisema Dkt. Ulisubisya.

Aidha,Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa takwimu hizo zikikusanywa kikamilifu zitasaidia kutoa elimu kwa jamii na kupunguza imani za kishirikina kwa wananchi kwani zitaleta picha sahihi ya kugundua vyanzo vya  vifo hivyo kwenye jamii husika.

Hata hivyo Dkt. Ulisubisya amewataka maafisa hao kutumia vifaa hivyo kwa matumizi ya kazi ya kukusanyia takwimu na sio matumizi binafsi na kama itatokea afisa afya yeyote atakayehama kituo cha kazi  basi arudishe  ofisini kwa ajili ya mtumishi mwingine atakayekuja.

Kawa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa iringa Bw. Fikira Kissimba amesema kuwa mfumo huo wa ukusanyaji taarifa zitasaidia pia uandikishwaji wa mirathi ya marehemu wakati ndugu husika anapokwenda kufungua mirathi yake mahakamani.

Naye Mratibu wa usajili wa Takwimu wa Masuala muhimu ya Binadamu nchini kutoka wizara ya afya  Dkt. Gregory Kabadi amesema kuwa jumla ya Kompyuta kibao (Tablets) zilizogawiwa ni 106 kwa kila kata ya mkoani Iringa na thamani yake ni takribani shilingi Milioni 61.5.

Aidha , Dkt Kabadi amesema kuwa zoezi hilo limeanza kwa majaribio katika halmashauri tano kwenye mikoa mitatu ikiwemo Pwani,Tanga na Morogoro na kufanya tathimini ya utekelezaji wa mifumo hiyo katika mkoa wa Iringa kabla ya kutumika nchi nzima.

Kwa upande  wake Afisa afya wa kata ya Kitwilu Bw. Wilson Ntagondwa amesema kuwa kupitia mfumo huo waliokabidhiwa itawasaidia kukusanya takwimu kwa urahisi hivyo kupelekea kujua sababu zinazosababisha vifo na kusaidia kupanga maendeleo.

WANANCHI WAMETAKIWA KUBADILI MFUMO WA MAISHA NA KUZINGATIA LISHE BORA

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akinawa mikono baada ya Uzinduzi wa Mradi Mkubwa wa Maji  wenye uwezo wa kuzalisha lita za ujazo  Elfu 30 kutoka kijiji cha  Rurumakilichopo kata ya Kiomboi wilaya ya Ilamba, ikiwa ni muendelezo wa zaiara yake Mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia chanjo zilizohifadhiwa katika boksi maalum wakati alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Kiomboi iliyopo wilayani Iramba katika Mkoa wa Singida. Kushoto ni muhudumu wa chanjo Christowelo Palangyo na Dkt. Abbas Sepoko (kulia).

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiionesha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Iramba (hawapo pichani) dawa za serikali zilizo na alama maalumu ili zisiuzwe katika maduka binafsi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Gwaula.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipokea zawadi ya mbuzi kutoka kwa Diwani wa Kinyambuli Rubeni Charles wakati alipofanya ziara katika kijiji hicho ili kujionea hali ya ujenzi wa kituo pamoja na utoaji huduma za afya kijijini hapo.


WANANCHI WAMETAKIWA KUBADILI MFUMO WA MAISHA NA KUZINGATIA LISHE BORA

Na WAMJW-MKALAMA- SINGIDA

Watanzania kote nchini wametakiwa kufuata kanuni na taratibu bora za maisha ikiwemo kubadili mfumo wa maisha ili kuepuka kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza pamoja na udumavu kwa watoto wachanga.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katika Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida wakati alipotembelea kituo cha afya na kuongea na wananchi.

"Serikali chini ya uongozi wa Rais Magufuli inataka kila mtanzania awe na afya bora, ndo maana tunajitahidi kutoa elimu kwa umma kuhusiana na kutunza afya zenu ikiwemo kufanya mazoezi na kuepuka vyakula ambavyo si salama kwa afya zetu pamoja na kubadili mfumo mzima wa maisha". Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha,Naibu waziri huyo ameendelea kusisitiza kwa upande wa  akina mama walio na watoto wadogo chini ya miaka miwili kuendelea kuwanyonyesha na kuwapa vyakula vyenye lishe bora watoto wao ikiwa ni sehemu ya kumsaidia mtoto kukua kiakili na kuwa  na afya bora huku akisisitiza siku 1000 za mwanzo kwa mtoto ndizo siku muhimu katika kumuwezesha kuwa na afya bora na kukua vizuri.

"Siku 1000 za mwanzo tunaanza kuzihesabu toka mimba inapotungwa, anapozaliwa na kufikisha miaka miwili, hiki ni kipindi muhimu sana cha mama kumnyonyesha mtoto ikiwa ni pamoja na kumpa vyakula vyenye lishe ili mtoto aweze kuwa na afya bora na ubongo unaofanya kazi sawa sawa". Alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Pamoja na hayo, Dkt. Ndugulile amekipongeza kituo cha afya cha Kinyambuli kwa kuzitendea haki fedha zilizotolewa na Serikali Shilingi milioni 400 ili kusaidia kupanua kituo hicho kwa kujenga majengo mapya ya kuhudumia wagonjwa pamoja na nyumba za watumishi.

"Nawapongeza sana wananchi wa Kinyambuli kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa kituo hiki, ninachokiona hapa kipo mara 300 nchi nzima, kwa kweli mnastahili pongezi na fedha za serikali tulizoleta milioni 400 mmezitendea haki". Alisema Dkt. Ndugulile.

Hata hivyo Dkt.Ndugulile  amesema serikali bado ina nia kubwa ya kuboresha hali ya utoaji huduma za afya nchini, huku ujenzi wa Hospitali kubwa ya wilaya ya Mkalama ukitarajiwa kuanza kabla ya mwisho wa mwaka huu. 

Dkt. Ndugulile amesema mkoa wa Singida umetengewa bajeti ya Bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Hospitali kubwa ya wilaya ya Mkalama pamoja na Singida DC.

Kwa upande wake diwani wa Kinyambuli, Rubeni Charles ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais John Magufuli kwa kuwakumbuka wananchi wa kijiji hicho kwa kutoa fedha za ujenzi wa kituo kikubwa cha afya.

"Kwakweli naishukuru sana serikali kwa kutukumbuka, wananchi wa kijiji hiki walikua wanapata shida sana kupata huduma za afya hasa wakinamama wajawazito ambao tulipoteza wengi kutokana na kukosa huduma hii muhimu". Alisema Rubeni.

Jumanne, 30 Oktoba 2018

SERIKALI YAAHIDI KUPELEKA GARI YA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MANYONI

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akikagua cheti cha mgonjwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akikagua madaftari ya wagonjwa waliolazwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya. kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo Bi. Rahabu Solomon.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (Kulia) akifafanua jambo wakati alipotembelea kitengo cha kuzalisha chakula cha lishe kwa mama wajawazito na watoto katika Hospitali ya Mtakatifu Gasper. Kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali hiyo Fr. Seraphine Lesiriam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wananchi waliokuwa wakisubiri huduma Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida wakati alipofanya ziara hospitalini hapo kuona hali ya utoaji wa huduma za afya.


SERIKALI YAAHIDI KUPELEKA GARI YA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MANYONI

NA WAMJW-SINGIDA

Serikali imetangaza neema ya kupeleka gari ya  wagonjwa (Ambulance)  katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni ili kutatua tatizo linaloikabidi Wilaya hiyo hususan ya vifo vitokanavyo na uzazi.

Ahadi hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipoitembelea hospitali hiyo kwa lengo la kutazama utoaji wa huduma za afya ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu katika mkoa wa Singida.

Dkt. Ndugulile amefikia uamuzi huo baada ya kusikiliza kero kutoka kwa wananchi wanaotumia hospitali hiyo ambapo wengi walisema kungekuwepo na gari ya wagonjwa kungeepusha vifo vya akina mama wajawazito na watoto pamoja na wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura.

"Naomba niwaahidi wananchi wa Manyoni, Serikali imeagiza magari ya kubebea wagonjwa ambayk yanaweza kufika mwezi Disemba mwaka huu,hivyo nitahakikisha katika mgao wa magari hayo basi na hospitali hii ya Wilaya  inapata gari moja kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa hapa. Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt.Ndugulile aliahidi kuwatafutia wataalam wa Afya watakaoweza kwenda  kupunguza uhaba wa watumishi wanaokabiliana nayo hospitali hiyo

Naye Mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Atupele Mohamed alisema hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa majengo ikiwemo chumba cha huduma za uzazi ambapo uwezo wake kwa mwezi ni  kuzalisha akina mama 90 lakini kwa sasa huzalisha  wastani wa akina mama 400.

Aidha, Dkt. Atupele alisema Hospitali hiyo ina upungufu mkubwa wa watumishi wenye sifa, ambapo ina jumla ya watumishi 107 sawa na asilimia 53 ya watumishi wanaohitajika.

Dkt. Atupele alitaja   uhaba mkubwa wa watumishi hao  ni Madaktari, Wauguzi, Wataalamu wa mionzi na wataalamu wa kutoa huduma za usingizi.

Katika Wilaya hiyo Naibu Waziri huyo aliweza kutembelea  kutembelea kituo cha kulea wazee na wasiojiweza cha Sukamahela pamoja na Hospitali ya rufaa ya Mtakatifu Gasper iliyopo  Itigi na  kuridhika na hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali hiyo.

Jumatatu, 29 Oktoba 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - TAMKO LA SIKU YA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA UGONJWA WA KIHARUSI (STROKE) DUNIANI, TAREHE 29/10/2018

- Hakuna maoni








WAGANGA WAFAWIDHI NCHINI WATAKIWA KUWEKA VIKAO KUJADILI VIFO VYA UZAZI

- Hakuna maoni
Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara mbalimbali kutoka Wizara ya Afya wakifuatilia kwa makini mawasilisho kutoka kwa wawezeshaji wa mkutano wa Waganga wafawidhi wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma.





Baadhi ya Waganga Wafawidhi kutoka mikoa mbalimbali wakifuatilia kwa makini mawasilisho kutoka kwa wawezeshaji wa mkutano wa Waganga wafawidhi wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma.


Baadhi ya Wawasilishaji wa mada mbalimbali wakiwasilisha mada kwa waganga wafawidhi wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa Waganga afawidhi uliofanyika jijini Dodoma.
 
WAGANGA WAFAWIDHI NCHINI WATAKIWA KUWEKA VIKAO KUJADILI VIFO VYA UZAZI
 
Na WAMJW- DODOMA
 
WAGANGA Wafawidhi nchini wametakiwa kukaa vikao kila baada mara kwa mara ili kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye hospitali zao ili kuzifanyia kazi changamoto hizo na kurudisha taarifa Wizara ya Afya.
 
Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Wizara ya Afya Dkt. Otilia Gowelle wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Waganga Wafawidhi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma
 
“Waganga Wafaidhi mnatakiwa kukaa vikao vya kitabibu kujadili tiba pamoja na kujadili kifo cha kila mgonjwa ili kujua changamoto iliyotokea na kuipatia ufumbuzi na kuandikia taarifa ili kuondokana na vifo hasa vitokanavyo na Uzazi” alisema Dkt. Gowelle.
 
Aidha, Dkt. Gowelle amewataka wataalam wa tiba kuzingatia vikao vya tiba na kufanyia kazi changamoto au maboresho ili kuzitolea taarifa na kuzitatua pamoja na kushirikisha wadau wengine.
Dkt. Gowelle amewataka pia Waganga wafawidhi kuweka mifumo ya ufuatiliaji wagonjwa pamoja na kupokea malalamiko  katika hospitali zao ili kufanya maboresho ya huduma za afya wanazozitoa na kuchukua hatua zinazostahili.
 
“Kupitia kikao hiki, nawataka mkae kama timu na kuandaa Mipango kazi ya kuanza kushughulikia kikamilifu yale yote yaliyobainika katika taarifa hiyo ili kuondokana na kero wanazokabiliana nazo wananchi wanapokuja kupata huduma katika hospitali zenu” alisema Dkt. Gowelle.
 
Aidha, Dkt. Gowelle amewasihi Waganga Wafawidhi waliohudhulia kikao hiko kuhakikisha  kwamba wanatumia  timu zao za Uendeshaji za Hospitali za Rufaa za Mikoa kubaini changamoto zilizopo katika maeneo yenu ya kazi ikiwa ni pamoja na watumishi, majengo na vifaa vya kuzifanyia kazi ili kuboresha huduma mnazotoa kwa wananchi.
 
Mbali na hayo Dkt. Gowelle ametoa pongezi kwa timu yote ya inayoratibu utekelezaji wa Mradi wa RRHMP pamoja na Serikali ya Japan kupitia Shirika la Maendeleo JICA kwa kuendelea kuisaidia Serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za Afya nchini.

Jumatano, 24 Oktoba 2018

IDADI YA WANACHAMA WACHANGIAJI WA MFUKO WA BIMA YA AFYA NCHINI YAONGEZEKA.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (aliyesimama) akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mfuko huo kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Bungeni jijini Dodoma.



Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakipokea taarifa ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto


Na.WAMJW,Bungeni, Dodoma

Idadi ya wanachama wachangiaji wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya imeongezeka kutoka wanachama 164,708 waliokuwa wameandikishwa  mwaka 2001/2002 hadi wanachama 873,012 mwezi Septemba 2018.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha  taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mfuko huo kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Bungeni jijini Dodoma.

“Ongezeko hili limetokana na kanuni na misingi  inayotumika katika kuendesha utaratibu wa mfuko huu ikiwa ni pamoja na uchangiaji wenye usawa kwa kuzingatia viwango vya mshahara,usawa katika kupata huduma na ushiriki wa Serikali katika usimamizi kwa faida ya wanachama” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa kwa upande wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), jumla ya kaya zilizojiunga hadi Septemba mwaka huu ni 2,220,953 ikiwa ni sawa na wanufaika wapatao 13,506,330 sawa na asilimia 25 ya watanzania wote’ kwa hiyo mifuko hii yote inatoa huduma kwa watu 17,656,697 sawa na asilimia 33 ya watanzania wote kwa mujibu  wa idadi ya makadirio ya watanzania kwa sasa.

Idadi ya wanufaika imeongezeka  kutoka 691,774  mwaka 2001/2002 hadi wanufaika 4,150,367 sawa na asilimia 8 ya watanzania wote” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa mpaka sasa idadi ya wanachama wengi waliojiunga  asilimia 67 ni watumishi wa umma ambao wanajiunga kwa mujibu wa sharia.

Hata hivyo Waziri Ummy alisema mfuko unaendelea kutoa elimu na kubuni vifurushi mbalimbali vitakavyovutia wananchi wengi kujiunga na kufaidika  na mfuko ambapo utawawezesha wanachama wengi zaidi kujiunga hasa wale wa sekta isiyo rasmi na kujiwekea malengo ya kuwafikia watanzia asilimia 50 mwaka 2020.

“Mfuko umekamilisha uandaaji wa vifurushi vya michango na mafao kulingana na uwezo wa wananchi kulipia bima  ya afya,suala hili lipo katika hatua za mwisho kabla ya kuanza kwa utekelezaji”. Alisisitiza Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa mpango huo utamwezesha mwananchi kuchagua vifurushi vya aina mbalimbaliu vya huduma  anayoitaka  kwa utaratibu utakaojulikana kama ‘JIPIMIE’ na wanachama watalipa kidogo kidogo kwa utaratibu ujulikanao kama ‘DUNDULIZA’ ambao tayari umeshakamilika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa NHIF wanatakiwa kuweka mfumo wa kutoa huduma za bima ya afya kwa mashirika makubwa ya hapa nchi na yale ya nje kwa kuwauliza  huduma zipi wangependa kuhudumiwa katika hospitali za hapa nchini  hususan zile za binafsi na hivyo kuweza kuongeza idadi kubwa ya wateja watakaohudumiwa na NHIF.

Naye Mkurugenzi wa NHIF Bw. Bernad Konga akijibu maswali ya wajumbe wa kamati hiyo alisema kwamba NHIF imekubali kuboresha huduma zao na hivyo wapo tayari kuanza huduma za vifurushi za  ‘JIPIMIE’ mara moja  ili wananchi waweze kupata huduma za afya kulingana na vipato vyao.

Aidha, alisema hivi sasa wameajiri madaktari wapatao kumi na nane  na kuwaweka kwenye hospitali kubwa za Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutatua changamototo za wateja wa huduma za bima hiyo zikiwemo za kunyanyapaliwa  pamoja na kukagua fomu zinazojazwa na wataalam wa hospitali hizo ili kupunguza malalamiko ya wateja wa huduma za bima ya NHIF na kuahidi wataongeza hospitali zingine awamu inayofuata


Jumanne, 23 Oktoba 2018

SERIKALI YAAINISHA DAWA MUHIMU ZINAZOPATIKANA MSD.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifafanua hali ya upatikanaji wa dawa nchini  kwa wajumbe wa kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini  hawapo pichani wakati wa kikao cha kamati ya hiyo kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , katikati aliyekaa ni Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akichangia mada wakati wa kikao cha kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , wa kwanza kulia  aliyekaa ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bw. Peter Serukamba akitoa mwongozo kwa wajumbe wa kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini  wakati wa kikao cha kamati hiyo kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,wa kwanza kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

Katibu Mkuu Wizara ya afya Dkt. Mpoki Ulisubisya aliyesimama  akichangia mada wakati wa kikao cha kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , waliokaa kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto  Mhe. Ummy Mwalimu na katikati ni Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi aliyesimama akielezea jambo kwa wajumbe wa kamati ya Bunge ya Huduma za jamii wakati wa kikao cha kamati ya hiyo nchini kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa nchini (MSD) Bwa. Laurean Bwanakunu akichangia mada wakati wa kikao cha kamati ya Bunge ya Huduma za jamii nchini kinachoendelea  katika ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekaa kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

NA WAMJW, BUNGENI DODOMA


SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeainisha dawa aina 135 kama dawa muhimu na za kipaumbele cha wizara  kwa lengo la kuhakikisha kuwa zinapatikana  nyakati zote katika bohari zote za kanda za MSD.

Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Janii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati  akitoa taarifa ya utendaji ya Bohari Kuu ya Dawa nchini(MSD)  aliyowasilisha katika kamati ya kudumu ya Bunge huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma.

Waziri Ummy alisema tathimini ya upatikanaji wa dawa hizo  ni wa hadi mwezi Julai 2018  ambapo ni sawa na asilimia 93 hivyo Wizara yake imeitaka MSD kuongeza idadi ya dawa muhimu 177  na kufikia  dawa za kipaumbele 312 ambapo upatikanaji wa dawa hizo ni asilimia 73 kufikia robo mwaka ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019.

“Hali ya upatikanaji dawa muhimu  umeimarika kuanzia mwaka 2016/2017  na kufikia asilimia 93 nchi nzima  katika mwaka 2017/2018  na hivyo kuweza kufanikiwa  katika maeneo mengi na kufikisha  dawa moja kwa moja katika vituo  vya kutolea huduma za afya nchi nzima”.Alisema Waziri Ummy Mwalimu.

Aidha, Waziri Ummy alisema MSD imeweza kusambaza dawa moja kwa moja hadi vituo vya kutolea huduma za afya vinavyofikia 5,432 nchi nzima kwa kutumia magari  215 na hivyo kusambaza dawa zenye thamani za shilingi bilionini 600 kwa mwaka kupitia mfumo wa ugavi ulio enea nchi nzima.


Hata hivyo Waziri Ummy amesema kuwa hivi sasa MSD inapeleka dawa mara 6 kwa mwaka na pale kwenye mahitaji ya dharura tofauti na zamani ambapo ilikua inapeleka dawa mara nne kwa mwaka.

Mbali na hayo Waziri Ummy alisema Bohari ya dawa imeendelea kuimarika kifedha katika kipindi cha miaka mitano iliyopita hususan katika mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo Serikali iliongeza bajeti ya dawa, vifaa na vifaa tiba  na kuweza kutoa kiasi cha shilingi bilioni 80.1  na kwa mwaka wa bajeti 2018/2019 kwa robo hii ya mwaka imepokea shilingi bilioni 20.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewataka wafamasia wote wa Hospitali na vituo vya afya kupeleka orodha ya dawa  zilizopo kwenye stoo  kwa madaktari  kila mwanzo wa wiki.

“Wafamasia wote wa Hospitali na zahanati za Serikali wanatakiwa kuwapelekea madaktari orodha ya dawa zilizopo kwenye stoo ili kama dawa ya ugonjwa Fulani haipo Daktari awe na uwezo wa kuandika dawa mbadala kwa mgonjwa” amesema Dkt. Ndugulile.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya dawa nchini Bw. Laurean Bwanakunu amesema kuwa katika kuhakikisha upatikanaji wa dawa unadumu nchini wapo katika hatua za mwisho za kukamilisha ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi kujenga kiwanda cha dawa nchini.

“Tunatarajia mpaka kufikia Machi 2019 kukamilisha ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi kujenga kiwanda cha dawa nchini ambapo utafanyika kwa haraka ili kukamilikia mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2019” alisema Bw. Bwanakunu.

DKT. NDUGULILE AAGIZA WATUMISHI WA AFYA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA KATIKA UTENDAJI WAO.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua ujenzi wa majengo mapya katika kituo cha afya cha Lupiro wilayani Luanga, Mkoa wa Morogoro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisikiliza kero kutoka kwa Florence Kilumanga wakati alipotembelea Hospitali ya Mahenge iliyopo wilayani Luanga mkoa wa Morogoro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Rajabu Risasi (kushoto) wakati alipotembelea Hospitali ya Mahenge iliyopo wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro. Kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Ngollo Malenya.

NA WAMJW-ULANGA


Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaasa watumishi wa afya nchini kote kuzingatia maadili katika utendaji ili kutoa huduma za afya kwa wananchi kwa kiwango kilicho bora.

Dkt. Ndugulile amesema hayo wakati alipofanya ziara na kukagua hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Mahenge iliyopo wilaya ya Luanga mkoani Morogoro.

Katika ziara hiyo, Dkt. Ndugulile alionekana kushangazwa na baadhi ya watoa huduma hospitalini hapo kutozingatia muda wa kuwepo kazini muda wote.

 Amebaini hilo wakati alipotembelea maabara ya Hospitali na kukuta kumbukumbu za mnyororo wa baridi hazijaandikwa ipasavyo, damu na vitendanishi vikiwekwa katika Friji moja na mpangilio mzima wa maabara hiyo kuwa mbovu.

“Niwakumbushe wataalamu wa maabara, taaluma ambazo wamezisoma hazibadiliki hata wakiwa kazini, kuna misingi ya taaluma ambayo tunayo, vitu vidogo kama Temperature Chart vinaonesha umakini na weledi kwa mwana taaluma ambaye tumemkabidhi jukumu lile”. Amesema Dkt. Ndugulile.

Kutokana na hali hiyo, Dkt. Ndugulile aliagiza kuondolewa msimamizi wa maabara Donald Masamaki na kuletwa mtu mwingine atakayezingatia taaluma na weledi katika utoaji wa huduma za maabara na afya kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Ndugulile alishangazwa na malalamiko ya wananchi kuhusu wahudumu wa maabara kuwaagiza wagonjwa kwenda kupima Malaria katika vituo vya watu binafsi huku kipimo cha MRDT kikiwepo stoo ya dawa. Kufuatia hali hiyo Naibu Waziri huyo aliagiza Kamat ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na Mkuu wa Wilaya hiyo Ngollo Malenya kufuatilia kwa ukaribu na kubaini ukweli wa jambo hilo na wale watakaobainika wachukuliwe hatua.

“Niwakumbushe watu wa maabara, nimkumbushe mganga mfawidhi kuhakikisha kwamba vipimo vyote vinakuwepo Hospitali. Nimepata malalamiko kutoka kwa wananchi, mpaka vipimo vya MRDT vya Malaria watu wanaambiwa wakapime nje”. Ameongeza Dkt. Ndugulile.

Pamoja na hayo, Naibu Waziri aliagiza kufanyiwa marekebisho kwa baadhi ya kasoro zilizoonekana Hospitalini hapo ikiwa ni pamoja na kuagiza kununuliwa mafaili ya kutunzia kumbukumbu za mgonjwa, kujengwa kwa sehemu ya kuchomea taka, kurekebisha mfumo wa mapato na kuiagiza bohari ya dawa (MSD) kuhakikisha dawa zote muhimu zinapatikana Hospitalini hapo.

Katika kuhitimisha ziara yake wilayani Ulanga, Dkt. Ndugulile aliahidi kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga gari la wagonjwa (Ambulance) katika mgao unaofuata.

Naibu Waziri Dkt. Ndugulile alihitimisha ziara yake mkoani Morogoro kwa kutembelea kituo cha afya cha Lupiro na kukagua ujenzi wa majengo mapya ya chumba cha kuhifadhia maiti, wodi ya wanawake, maabara na nyumba ya daktari. Huku kwa kiasi kikubwa akionekana kuridhika na ujenzi wa kituo hicho.

Jumatatu, 22 Oktoba 2018

MAAFISA AFYA WATAKIWA KUSIMAMIA USAFI WA MAZINGIRA ILI KUTOKOMEZA MALARIA

- Hakuna maoni



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Wabunge wa kamati ya Huduma za Jamii na Wadau wa Masuala ya Afya (hawapo kwenye picha) katika uzinduzi wa taarifa ya utafiti wa Viashiria vya Malaria nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya TAKWIMU Dkt. Albina Chuwa akionesha Kitabu cha Taarifa ya Takwimu za Viashiria vya Ugonjwa wa Malaria mbele ya Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii na Wadau wa Masuala ya Afya wakati wa uzinduzi wa taarifa ya utafiti wa Viashiria vya Malaria nchini.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakioneshana jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya TAKWIMU Dkt. Albina Chuwa (wakatikati).

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa taarifa ya utafiti wa Viashiria vya Malaria nchini uliofanyika leo jijini Dar es salaam.

Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii na Wadau wa Masuala ya Afya wakifuatilia taarifa ya Utafiti ya Viashiria vya ugonjwa wa Malaria nchini iliyokuwa ikisomwa na Mgeni rasmi Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye Picha) jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa  uzinduzi wa taarifa ya utafiti wa Viashiria vya Malaria nchini.

 
MAAFISA AFYA WATAKIWA KUSIMAMIA USAFI WA MAZINGIRA ILI KUTOKOMEZA MALARIA

Na WAMJW – Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewaagiza Maafisa Afya nchini kusimamia kwa ukamilifu usafi wa mazingira katika jamii ili kutokomeza ugonjwa wa Malaria.
 
Waziri Ummy ametoa agizo hilo leo Oktoba 22, 2018 wakati akizindua Taarifa ya Utafiti wa Viashiria vya Ugonjwa wa Malaria wa Mwaka 2017 katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar Es Salaam
“Nawaagiza Maafisa Afya,  badala ya kupoteza muda mwingi wa kukagua migahawa, bucha za nyama na sehemu ambazo wanajua zinaleta fedha, tunataka pia wajikite katika kusimamia usafi wa mazingira  katika Kata, Vijiji na Mitaa yetu”Alisema Mhe. Ummy.
 
Katika kuhakikisha hali ya usafi wa mazingira inakuwa endelevu, Waziri Ummy ameagiza Mabalaza yote ya Halmashauri nchini kuweka Sheria na adhabu kali kwa wote ambao wamekuwa wagumu katika kushiriki katika usafi wa mazingira huku Waganga Wakuu wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia vyema utekelezaji wa kanuni na sheria za afya na usafi wa mazingira jambo ambalo litaibua chachu ya ushindi katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria.

“Niyatake Mabalaza ya Hamashauri kuweka hatua kali, sheria kali na adhabu kali kwa wote ambao hawashiriki katika usafi wa mazingira” alisema Waziri Ummy.
Licha ya hivyo Waziri Ummy alisema kuwa Serikali kupitia Wizara inaendelea kutekeleza Mpango endelevu wa ugawaji vya ndarua kupitia wanafunzi wa shule za msingi, kupitia Kliniki za wajawazito na watoto, ambayo hujulikana kama Chandarua Kliniki huku hadi sasa jumla ya vyandarua milioni 31 vimeshagawiwa nchini kote.
 
Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa Matokeo ya mpango endele u wa ugawaji wa vyandarua yameonesha kuwa asilimia 78 ya kaya nchini Tanzania zinamiliki angalau chandarua kimoja chenye dawa, Katika utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa mwaka 2015-16, ni asilimia 66 tu za kaya zilikuwa zinamiliki angalau chandarua kimoja chenye dawa huku Umiliki wa vyandarua vyenye dawa ni wa kiwango cha juu kwa kaya za mijini (asilimia 81) ikilinganishwa na kaya za vijijini (asilimia 77). 
 
Kwa upande mwingine Waziri Ummy alitaja Halmashauri zenye maambukizi ya kiwango cha juu ni pamoja na Kakonko 30.8%, Kasulu DC 27.6%, Kibondo DC 25.8%, Uvinza 25.4%, Kigoma DC 25.1%, Buhigwe 24%, Geita DC 22.4%, Nanyamba TC 19.5%, Muleba DC 19.4%, Mtwara DC 19.1%, huku Halmashauri zenye  maambukizi ya kiwango cha chini ya asilimia 0.1 ni Mbulu TC, Mbulu DC, Hanang, Hai, Siha, Moshi MC, Mwanga, Kondoa TC, Meru DC, Arusha CC, Arusha DC,  Munduli, Ngorongoro, Rombo DC

MWISHO

Ijumaa, 19 Oktoba 2018

DKT. NDUGULILE AAHIDI UJENZI WA HOSPITALI MPYA YA WILAYA YA RUFIJI.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua dawa zilizopo katika stoo ya Hospitali ya Utete wilayani Rufiji kuhakikisha kama zina nembo ya serikali wakati wa muendelezo wa ziara yake katika mkoa wa Pwani.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akifafanuliwa jambo na Mganga Mkuu wa wilaya ya Rufiji Dkt. Juma Abdallah wakati alipofanya ziara katika Hospitali ya Utete iliyopo wilayani humo. Wengine ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Ibrahim Mohamed (katikati) na mbunge wa Rufiji Mohamed Mchengelwa.

NA WAJMW-RUFIJI
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameahidi ujenzi wa Hospitali mpya ya Utete ili kuboresha huduma za afya wilayani Rufiji.

Dkt. Ndugulile amesema hayo  wakati alipokuwa anaendelea na ziara katika Mkoa wa Pwani ambapo alionekana kutoridhishwa na majengo ya Hospitali hiyo kongwe iliyojengwa kipindi cha ukoloni na majengo yake yakionekana chakavu.

"Naomba niwe balozi wenu, nimejionea mwenyewe majengo ya Hospitali hii, kwa kweli ni chakavu sana” alisema Dkt. Ndungulile na kuendelea “sasa baada ya nyinyi kuomba serikali ifanye ukarabati wa Hospitali hii, mimi nitahakikisha tunapata pesa ya kujenga Hospitali mpya"

Aidha, Dkt. Ndugulile alionekana kutoridhishwa na nyumba wanazoishi madaktari wa Hospitali hiyo huku zikionekana kuwa chakavu zinazohatarisha maisha ya watu wanaoishi humo na kuahidi kuzifanyia ukarabati ikiwa ni pamoja na kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga nyumba mpya za kisasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Juma Abdallah amesema hali ya watumishi katika sekta ya afya siyo nzuri hasa kwa wenye taaluma mbalimbali. Amesema kuna upungufu wa asilimia 49 ya watumishi wenye ujuzi unaohitajika, huku akifafanua upungufu mkubwa katika kada ya wauguzi.

"Katika kada ya wauguzi tuna upungufu wa wauguzi 146, Madaktari 4, madaktari wasaidizi 11, wataalam wa mionzi 15, wataalam wa maabara 8, ustawi wa jamii 5, maafisa afya 12, makatibu wa afya 3 na watunza kumbukumbu za Hospitali 10". Amesema Mkuu huyo wa wilaya.

Pia amesema wilaya hiyo haina daktari bingwa wa aina yeyote na mtaalamu wa mionzi baada ya aliyekuwepo kuondoka mara baada ya kuripoti kwa maelezo kuwa mazingira ya Rufiji siyo rafiki kwake.

Kwa upande wa hali ya upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi, Mkuu wa Wilaya hiyo amesema upatikanaji wa wake ni wa wastani.  Hadi kufikia mwezi Septemba 30, 2018 dawa zinazofuatiliwa Tracer Medicine upatikanaji wake ni asilimia 90.6 na dawa zingine upatikanaji wake ni kwa zaidi ya asilimia 55.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Waziri amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Dkt. Yudas Ndungile kuhakikisha anatafuta mtaalam wa mionzi kutoka Wilaya nyingine ili kutoa huduma katika wilayani humo. Aidha Dkt. Ndugulile ameahidi kufanyia kazi suala hilo la upungufu wa watumishi hao muhimu.

Wakati huo huo Dkt. Ndugulile alihitimisha ziara yake katika Mkoa wa Pwani kwa kutembelea vituo vya afya vya Ikwiriri ambacho kimekamilisha ujenzi ya Wodi ya watoto, wodi ya Wanawake, jengo la kuhifadhia maiti na jengo la kufulia nguo.

Kwa upande wa kituo cha afya Kibiti, Naibu Waziri huyo ameonekana kutoridhika na huduma za afya zinazotolewa katika kituo hicho na kuona kuna ubadhirifu wa fedha za umma katika ujenzi wa miundombinu ya maabara, wodi na chumba cha upasuaji huku akiagiza kamati ya ulinzi na usalama kuchunguza na kuwachukulia hatua wote watakaobainika na ubadhirifu wa fedha za umma.

Katika kuhitimisha ziara yake katika Mkoa wa Pwani Dkt. Ndugulile alitembelea ujenzi wa kituo cha Bungu kwa lengo la kukagua miundombinu na hali ya utoaji huduma za afya, ambapo aliridhishwa na maendeleo ya kituo hicho na kuahidi serikali kuendelea kusaidia katika ujenzi huo lengo likiwa ni kusogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.

MWISHO

Jumatano, 17 Oktoba 2018

MARUFUKU MGONJWA KWENDA KUNUNUA DAWA NJE IKIWA DAWA ZIPO

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Fundi msanifu wa wilaya ya Mafia Ramadhan Madenge kuhusiana na mchoro wa kituo cha afya cha Kilongwe.
 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Kifinge Hamis Omary   (kushoto) wakati alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.
 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akionesha moja ya dawa za serikali wakati alipofanya ziara kuona hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya wilaya ya Mafia kuona.
 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisikiliza maelezo kutoka kwa mganga mkuu wa wilaya ya Mafia Dkt. Zuberi Mzige kuhusiana na mchoro wa jengo la huduma kwa wagonjwa wa bima ya afya wakati wa ziara katika Hospitali ya Wilaya hiyo.

MARUFUKU MGONJWA KWENDA KUNUNUA DAWA NJE IKIWA DAWA ZIPO. 

Na WAMJW-MAFIA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepiga marufuku kwa watoa dawa kuwaandikia wagonjwa kwenda kununua kwenye maduka binafsi ikiwa kwenye kituo kuna dawa na vifaa tiba vya kutosha. 

Hayo yamezemwa na Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipotembelea Hospitali ili kuangalia hali ya utoaji huduma Wikayani Mafia . 

"Nauagiza uongozi wa hospitali ya wilaya ya Mafia mkoani Pwani kuwarudishia wagonjwa wote gharama za vifaa tiba na dawa walizonunua katika maduka binafsi ambazo zinapatikana Hospitalini hapo" alisema Dkt.  Ndugulile. 

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa  amebaini baadhi ya wagonjwa walioandikiwa kwenda kununua dawa na vifaa tiba katika maduka binafsi huku baadhi ya dawa hizo zikiwepo katika stoo ya kuhifadhia dawa.

Dkt. Ndugulile amemuagiza  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri na Mganga Mkuu wa Wilaya ahakikishe wanawarudishia wagonjwa wote gharama walizotumia kununua dawa nje ya Hospitali hiyo.  

Pia Dkt. Ndugulile alishangazwa na Hospitali hiyo kutokuwa na dawa na vifaa tiba muhimu huku serikali ikiwa imetenga kiasi cha Tsh. Bilioni 270 kuanzia mwaka 2015/16 kutoka bilioni 31 za hapo awali, ikiwa na lengo la kuhakikisha dawa zote zinapatikana katika Hospitali na vituo vyote vya afya nchini.

Vikevike Dkt. Ndugulile  ameuagiza uongozi wa wilaya ya Mafia kuhakikisha bajeti ya dawa inapitiwa yakinifu na kutekelezwa ili kuepuka changamoto ambazo zinaweza kuepukika za ukosefu wa dawa na vifaa tiba muhimu na kuleta usumbufu kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Amebaini upungufu huo wa dawa na vifaa tiba baada ya kutembelea wodi za watoto na akina mama waliojifungua na kuelezwa na baadhi ya wagonjwa hao kununua dawa na vifaa tiba vya kusaidia kujifungua nje ya Hopitali hali ambayo imekua kero kwa wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika Hospitali hiyo.

Wakati huo huo Dkt. Ndugulile amesitisha ukarabati wa jengo la wagonjwa wa bima baada ya kuona kuna ubadhirifu wa fedha ambao hauendani na mazingira halisi ya ukarabati huo.

Pamoja na hayo Dkt. Ndugulile amefanya  ziara katika kituo cha afya cha Kilongwe na zahanati ya kifinge na kutoridhishwa na  maendeleo ya vituo hivyo huku akibaini utaratibu usiofaa wa manunuzi ya vifaa vya ujenzi na kuamuru Halmashauri hiyo ifuate utaratibu wa manunuzi wa Force Account. 

Sambamba na hilo Dkt. Ndugulile alisitisha   mara moja ukarabati wa jengo katika zahanati hiyo  huku akiagiza kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ikishirikiana na kamati ya ujenzi kufuatilia uhalisia wa gharama hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mafia Shaibu Mnunduma amemshukuru Naibu waziri huyo kufanya ziara kisiwani humo huku akiahidi kuzifanyia kazi changamoto zote zilizobainika ili kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Naye   Fundi msanifu wa Wilaya ya Mafia Ramadhan Madenge alisema kuwa kuna  ukarabati wa jengo hilo unagharimu takribani Tsh. Milioni 94. 

 

TAARIFA KWA UMMA

- Hakuna maoni