Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 9 Oktoba 2018

MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE YANALETA ULEMAVU

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila akifungua semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa viongozi wa Mkoa na Wilaya kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa Jijini Mbeya.Kulia ni Ofisa mpango toka Wizara ya Afya Osca Kaitaba na mwisho ni Mkuu wa Wilaya ya Kyela Bi.Claudia Kitta.
 Ofisa Mpango toka Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Osca Kaitaba akifafanua jambo kwenye semina hiyo.
Wataalam mbalimbali kutoka Sekratariet ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa semina ya  uraghibishaji na uhamasishaji wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa viongozi na wataalam wa Sekretariet na Mamlaka za Serikali wa Mkoa wa Mbeya.

Na WAMJW - Mbeya

Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yamekuwa yakusumbua na kuleta athari kwa wananchi wa Mkoa wa mbeya hadi kusababisha ulemavu.

Hayo yamesemwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila katika ufunguzi wa semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa  iliyofanyika katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Oktoba 9, 2018.

Alisema Magonjwa hayo yamekuwa yakiathiri zaidi wananchi kwa kiasi kikubwa na kupunguza uwezo wa wananchi katika shughuli za uzalishaji na ujenzi wa taifa.

"Magonjwa haya, pamoja na kusababisha usumbufu mkubwa kwa waathirika pia yanaongeza matumizi ya rasilimali chache tulizonazo katika kuyakabili "alisema Mkuu huyo mkoa.

Aidha Chalamila alisema kwamba uwepo wa magonjwa hayo umefanya watoto kutokuwa na mahudhurio mazuri mashuleni kutokana na muda mwingi kutumika kwenye matibabu.

Hata hivyo alisema kuwa jambo la kutia moyo ni kwamba Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na wadau wamekuwa wakitoa kingatiba za kukinga magonjwa hayo katika mkoa wa Mbeya.

"Hii ni kutokana na lengo la Serikali ya awamu ya tano ambalo ni kudhibiti magonjwa haya na hivyo kupunguza gharama kwa wananchi kwa kugawa kingatiba hizo"Alisisitiza Chalamila

Akielezea zaidi Chalamila alisema Mkoa wa Mbeya walikuwa wanakabiliwa na magonjwa yote matano ambayo ni minyoo ya tumbo, kichocho, matende na mabusha katika Wilaya zote ila kutokana na usimamizi na uhamasishaji nzuri Mkoa wake hivi sasa wamepunguza magonjwa hayo na hivyo kuwataka viongozi wa mkoa na Wilaya zake kuzidi kuhamasisha na kuelimisha zaidi wananchi kujitokeza kumeze kingatiba ili kutokomeza magonjwa hayo.

Aliyataja magonjwa yanayoendelea kuwa changamoto kwa Wilaya za Mkoa wa Mbeya ukiwemo ugonjwa wa Trakoma kwa Wilaya za Kyela, Chunya na Mbarali pamoja na ugonjwa wa usubi kwa Wilaya za Rungwe, Kyela na Busokelo.

Kwa upande wake Ofisa Mipango kutoka Mpango wa Kudhibiti  Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bwana. Oscar Kaitaba alisema semina hiyo imejumuisha wajumbe kutoka Halmashauri tatu za Mkoa wa Mbeya ambazo ni Rungwe, Kyela, Busokelo.

Aidha Bw. Kaitaba alitaja wajumbe hao kuwa Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Waweka Hazina za Wilaya, Waganga Wakuu  Waratibu  pamoja na Maafisa Usalama wa Wilaya.



Mwisho.

0 on: "MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE YANALETA ULEMAVU"