Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 7 Oktoba 2018

WATANZANIA WAASWA KUPIMA MACHO MARA KWA MARA.


Washiriki kutoka taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi wakiwa katika maandamano kuadhimisha wiki ya afya ya macho yaliyofanyika jijini Dodoma mapema leo
Kaimu Mganga Mkuu Wa Serikali Dkt. Eliud Eliakim akipata maelezo kutoka Titus Nyange jinsi mashine ya Perkins inavyochapa nukta nundu zinazosomwa na watu wenye ulemavu wa macho wakati wa maadhimisho ya wiki ya afya ya macho duniani yanayofanyika jijini Dodoma. 

Mganga Mkuu Wa Mkoa wa Dodoma  Dkt. Charles Kiologwe akisisitiza jambo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya afya ya macho uliofanyika katika viwanja vya Nyerere jijini Dodoma mapema leo.

Kaimu mganga mkuu wa serikali Dkt. Eliud Eliakim (Kushoto) akimkabidhi Kaimu Meneja wa Mpango  wa Taifa wa huduma za macho Dkt. Bernadetha Chilio kitabu cha muongozo wa utoaji huduma za macho katika maadhimisho ya wiki ya afya ya macho yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere jijini Dodoma.

Wananchi kutoka sehemu mbalimbali za mkoa wa Dodoma wakiwa wamejipanga katika mstari ili kupata huduma za macho katika maadhimisho ya wiki ya afya ya macho duniani yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere mkoani humo.

NA WAMJW-DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imewaasa Watanzania kujijengea tabia ya kupima macho mara kwa mara ili kuweza kuepuka aina mbalimbali za magonjwa ya macho ikiwemo vikope.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Eliud Eliakimu wakati wa kufungua hafla ya kuelekea siku ya Afya ya Macho Duniani ambayo huadhimishwa kila alhamisi ya Pili ya mwezi Octoba.
“Asilimia kubwa ya magonjwa ya macho yanatibika ikiwemo upeo mdogo wa macho kuona  ambao yanazuilika kwa miwani  endapo mtu akiwahi katika kituo cha kutolea huduma za Afya na akigundulika ana tatizo la macho basi atapata matibabu mapema”alisema Dkt. Eliakimu.
Aidha, Dkt. Eliakimu alisema kuwa kwa Tanzania watu wasioona kabisa ni asilimia moja sawa na watu laki 5.7 huku watu wenye matatizo mbalimbali ya macho wanakadiriwa kuwa mara tatu ya wasioona kabisa sawasawa na mil.7.
Kwa mujibu wa Dkt. Eliudi amesema kuwa takwimu zinaonesha kwamba ugonjwa wa macho umepungua kutoka asilimia 4.6 mwaka 1990 na kufikia asilimia 3.4 mwaka 2015 kutokana na hamasa ya juu ya upimaji toka kwa wananchi.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Mpango wa Huduma za Macho Nchini kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Benadertha Chilio amesema kuwa tatizo la macho linaloongoza nchini ni mtoto wa jicho ambapo wagonjwa wanafikia kwa asilimia 50 na wengi wao ni wanawake.
“Watanzania wanatakiwa kuacha matumizi ya mitishamba na badala yake wanatikwa kuhudhuria hospitali pindi wanapohisi wanamatatizo ya macho kwani matumizi ya mitishamba kunaweza kusababisha makovu katika kioo cha jicho hivyo kunaweza kusababisha jicho kutofanya kazi kabisa” alisema Dkt. Chilio.
Aidha,Dkt. Chilio amewataka wanaohitaji tiba ya kuvaa miwani kwa ajili ya kuona vizuri waende hospitali zilizosajiliwa wapate vipimo stahiki na kupewa miwani kutokana na uwezo wao wa kuona na sio kupata huduma hizo kwenye vituo visivyosajiliwa.
Naye Mkanga Mkuu wa Mkoa Dodoma Dkt. Charles Kiologwe amewataka wakazi wa Dodoma kujitokeza kupata huduma za macho ili kutokomeza ugonjwa huo  mkoani humo ili kuendelea katika shughuli za  kujenga uchumi wa viwanda.
“Nawaomba wakazi wenzangu wa Dodoma tujutokeze kwa wingi kupata huduma za macho ili kulinda afya zetu pamoja na kuondoa ule usemi uliopo vichwani kwa watu wengi kwamba kila mgonjwa wa macho anatokea Dodoma” alisema Dkt. Kiologwe.

0 on: "WATANZANIA WAASWA KUPIMA MACHO MARA KWA MARA."