Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 29 Machi 2018

MWALIKO

- Hakuna maoni

MWALIKO

HOSPITALI YA KANDA YA RUFAA MBEYA YAPIGA HATUA KATIKA KUMALIZA TATIZO LA WAGONJ...

- Hakuna maoni


Ameyasema hayo Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Godlove Mbwanji katika ofisi yake jijini Mbeya, 
Dkt. Mbwanji hakusita kuupongeza Uongozi na Wafanyakazi wa Hospitali hiyo kwa kujitoa kwa moyo katika kuwatumikia wananchi, pia aliwashukuru wananchi wa Mbeya hususani madereva wa Boda boda kwa moyo wakujitolea katika kuboresha Sekta ya Afya ikiwemo kutoa michango yakifedha.

Jumatano, 28 Machi 2018

WAZIRI UMMY AKUTANA NA UGENI KUTOKA WHO.

- Hakuna maoni



Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akutana na ugeni kutoka WHO mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam,

Lengo la ugeni huo lilikuwa ni kujadili changamoto za Sekta ya Afya na namna ya kuimarisha Sekta hiyo nchini hususani katika kupunguza vifo vya mama na mtoto, namna ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko, ushirikiano katika huduma za kibigwa na suala la Bima ya Afya kwa wote.

Nae mwakilishi kutoka WHO Dkt. Adiele Onyeze ameishukuru Serikali ya Awamu ya tano kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa juhudi wanazofanya za kuimarisha Sekta hiyo hasa katika mapambano ya kupunguza vifo vya mama na mtoto.


WAZIRI UMMY APONGEZA JITIHADA ZA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA MBEYA

- Hakuna maoni

Jumanne, 27 Machi 2018

TANGAZO LA WATUMISHI WALIOPATA UFADHILI WA MASOMO YA UZAMILI MWAKA 2017/2018

- Hakuna maoni




DKT. MAGUFULI ATHIBITISHA UWEPO WA DAWA ZAKUTOSHA

- Hakuna maoni


ILI kufikia katika uchumi wa kati kwakutumia sekta ya viwanda Serikali inatak iw a kujikita katika kuimarisha sekta ya afya kwa watanzania ili kuwa na rasilimali watu wenye afya njema kwa ajili yakuleta mafanikio hayo kupitia viwanda.
Hayo yamesemwa na Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa magari 181ya kusambazia dawa uliofanyika leo katika Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD) jijini Dar es salaam.
“Tunatakiwa kuwekeza kwenye uchumi wa Viwanda ili tufikie uchumi wa kati hivyo ni lazima tuwekeze kwenye sekta ya afya kwa kiwango kikubwa ili kuwa na wananchi wenye afya njema tayari kutumikia viwanda vyetu kwa muda wote” alisema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania inatakiwa kujijengea viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini ili fedha zinazotumika kununua bidhaa hizo nje ya nchi zirudi mikononi kwa watanzania wenyewe pamoja na kutoa ajira kupitia viwanda hivyo.
Mbali na hayo Rais Magufuli amesema kuwa katika kuimarisha Sekta ya afya Serikali imetenga shilingi Bilioni 269 za kununua dawa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kutoka bilioni 31 katika bajeti ya fedha mwaka 2016/2017.
Kwa upande wake Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa katika kuimarisha Afya ya mama na Mtoto Serikali imepunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa asilimia 60 kutoka asilimia 20 ya upunguzaji wa vifo hivyo.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya dawa zina mawanyo ikiwemo asilimia 42 zahanati na vituo vya afya ,asilimia 16 zinatumika kwa chanjo za watoto ,asilimia 10.2 zianenda hospitali za wilaya ,asilimia  6.8 zinatumia hospitali za mikoa ,asilimia 3.4 zinaenda hospitali maalum na asilimia 3 zinatumika kwa ajili ya dawa za saratani.

Jumatatu, 26 Machi 2018

ILI KUWEPO NA UCHUMI WA VIWANDA IMARA NI LAZIMA KUWA NA SEKTA YA AFYA ILIYO BORA.

- Hakuna maoni
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto kwake) mapema leo jijini Dar es salaam wakati akizindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelekezo kutoka kwa Bw. Byekwaso Tabula wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kuhusu hali ya upatikanaji wa Dawa katika Bohari hiyo, wa pili kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo mbele ya Viongozi wa Serikali na wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakati akizindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Mhe. Laurean Bwanakunu akisoma taarifa ya utendaji ya Bohari ya Dawa (MSD) mbele ya mgeni rasmi Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wa Serikali.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimkaribisha mgeni rasmi Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akizindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi na Mkurugenzi wa ubora wa huduma Dkt Mohamed Ally Mohamed wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akizindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza meza kuu kuimba wimbo wa taifa wakati akizindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD).

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuonesha uzinduzi  rasmi wa magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kuzindua magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimsikiliza kwa makini Bibi aliyejumuika katika uzinduzi wa magari mapya 181 ya Bohari ya Dawa (MSD) yatayotumika kusambaza Dawa na Vifaa tiba.



Na WAMJW-DAR ES SALAAM.
ILI kufikia katika uchumi wa kati kwa kutumia sekta ya viwanda Serikali inatakiwa kujikita katika kuimarisha sekta ya afya kwa watanzania ili kuwa na rasilimali watu wenye afya njema kwa ajili ya kuleta mafanikio hayo kupitia viwanda.
Hayo yamesemwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa magari 181 ya kusambazia dawa uliofanyika leo katika Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD) jijini Dar es salaam.
“Tunatakiwa kuwekeza kwenye uchumi wa Viwanda ili tufikie uchumi wa kati hivyo ni lazima tuwekeze kwenye sekta ya afya kwa kiwango kikubwa ili kuwa na wananchi wenye afya njema tayari kutumikia viwanda vyetu kwa muda wote” alisema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania inatakiwa kujijengea viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini ili fedha zinazotumika kununua bidhaa hizo nje ya nchi zirudi mikononi kwa watanzania wenyewe pamoja na kutoa ajira kupitia viwanda hivyo.
Mbali na hayo Rais Magufuli amesema kuwa katika kuimarisha Sekta ya afya Serikali imetenga shilingi Bilioni 269 za kununua dawa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kutoka bilioni 31 katika bajeti ya fedha mwaka 2016/2017.
Kwa upande wake Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa katika kuimarisha Afya ya mama na Mtoto Serikali imepunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa asilimia 60 kutoka asilimia 20 ya upunguzaji wa vifo hivyo.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya dawa zina mgawanyo ikiwemo asilimia 42 zahanati na vituo vya afya ,asilimia 16 zinatumika kwa chanjo za watoto ,asilimia 10.2 zianenda hospitali za wilaya ,asilimia  6.8 zinatumia hospitali za mikoa ,asilimia 3.4 zinaenda hospitali maalum na asilimia 3 zinatumika kwa ajili ya dawa za saratani.
“Fedha hizo za dawa zipatazo Shilingi Bilioni 269 asilimia kubwa zinaenda kwenye vijiji na kata pamoja na zahanati na vituo vya afya na kufanya hali ya upatikanaji wa dawa kuwa juu mpaka kufikia hivi sasa” alisema Waziri Ummy.
Waziri Ummy amesema kuwa licha ya kuwa tu kuna upatikanaji dawa wa hali ya juu nchini lakini Serikali kupitia Wizara ya Afya imetengeneza muongozo wa matibabu kwa ajili  na kuwataka waganga wafawidhi wote nchini kutumia muongozo huo ili kutoa matibabu sahihi kwa wagonjwa .
Kwa mujibu wa Waziri ummy amesema kuwa katika kuimarisha sekta ya Afya nchini Serikali imejitahidi kuongeza huduma za matibabu ya kibingwa kwani hivi sasa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili inapandikiza figo pamoja na vifaa vya usikivu kwa watoto ambapo imepelekea kupunguza rufaa za nje na kuokoa fedha nyingi.

Naye Mkurugenzi wa Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa nchini (MSD) Bw. Laurean Bwanakunu amesema kuwa wanasambaza dawa za shilingi bilioni 18 kila mwezi na lengo ni kufikia bilioni 21 kufika mwezi julai mwaka huu.
Aidha Bw. Bwanakunu amesema kuwa mbali na upatikanaji wa dawa kuongezeka lakini kuna chanagamoto za maoteo kutoka ngazi ya zahanati kwani wanashindwa kujua mahitaji yao sahihi ya dawa zinazohitajika kwa mwaka hivyo kufanya MSD kushindwa kupeleka dawa kwa wakati.
Samabamba na uzinduzi huo wa magari  hayo 181 ya kusambazia dawa na vifaa tiba hapa nchini yaliyotolewa kwa ushirikiano wa Seikali ya Tanzania pamoja na Mfuko wa Dunia wa pamoja (Global Fund) pia Mhe. Rais Magufuli alipata kutembelea maghala ya dawa yaliyopo  MSD jijini Dar es salaam.

Jumapili, 25 Machi 2018

SIKU YA KIFUA KIKUU DUNIANI (World TB Day) 24 March 2018

- Hakuna maoni


SIKU YA KIFUA KIKUU DUNIANI (World TB Day) 24 March 2018

Kifua Kikuu (TB) bado ni tatizo nchini kwetu.  Jumla ya watu 160,000 wanakadiriwa kuwa na ugonjwa huu nchini Tanzania. Mwaka 2016, jumla ya watu 65,908 waligundulika na kuwekwa kwenye matibabu ya TB. Asilimia 90 ya waliopata matibabu walipona kabisa.

Hata hivyo, takwimu pia zinaonyesha kuwa, wagonjwa wapatao 94,000 (59%) nchini hawakuweza kugundulika na hivyo kukosa kupewa matibabu ya TB. Na hivyo kuweka hatarini maisha yao na ya watu wengine kwa kuwa ugonjwa huu unaambukiza kwa njia ya hewa.

Katika kuadhimisha Siku ya TB Duniani, natoa wito kwa kila mmoja wetu na jamii kushiriki katika kutokomeza TB. Tunahitaji kumfikia kila mhitaji wa huduma za kupima na matibabu ya TB popote Tanzania. Tuhimize watu wote wenye dalili za TB kwenda kwenye Vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupima TB na kupata matibabu. Dalili za TB ni pamoja na kukohoa zaidi ya wiki 2, homa ya zaidi ya wiki 2, kutoka jasho sana, kupungua uzito na kukosa hamu ya kula. TB inatibika na kupona kabisa, dawa za TB zinatolewa bila malipo. 

Stop TB Tanzania!

Ummy Mwalimu, Mb
WAMJW
24 March 2018.
————-

# Kifua Kikuu (TB) ni ugonjwa wa kuambukiza unaoongoza kwa kusababisha vifo vingi Duniani. Ugonjwa huu unaambukiza kwa njia ya hewa.

# Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani(WHO) inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni 10.4 huugua Kifua Kikuu kila mwaka Duniani na Milioni Moja kati ya hao ni watoto wenye umri chini ya miaka 15.

# Nchini Tanzania kila mwaka jumla ya watu 160,000 wanakadiriwa kuwa na ugonjwa wa Kifua Kikuu.

# Kwa mwaka 2016 jumla ya watu 65,908 waligundulika na kuwekwa kwenye matibabu ya kifua kikuu. Asilimia 90 ya waliopata matibabu ya TB wamepona kabisa. Hata hivyo, takwimu pia zinaonyesha kuwa, wagonjwa wapatao 94,000 (59%) nchini Tanzania hawakuweza kugundulika na hivyo kukosa kupewa matibabu ya TB. 

# Kauli mbiu ya Siku ya TB Duniani 2018 ni “Viongozi Tuwe Mstari wa Mbele Kuongoza Mapambano ya Kutokomeza TB."

# Nitoe wito kwa viongozi wa ngazi zote kuifanya vita dhidi ya TB kuwa agenda muhimu na ya kipaumbele. Wakati ni sasa!Viongozi wenzangu wa kisiasa, taasisi na kijamii yatupasa kuyasimamia mapambano haya na kuwa mstari wa mbele ili kuleta mabadiliko na tija katika vita hii na kulielekeza taifa letu katika hatua ya kutokomeza TB.
 
# Napenda kuwakumbusha watanzania kuwa *TB inatibika na kupona kabisa, dawa zake zinatolewa bure na zinapatikana sehemu zote nchini katika vituo vya Umma na Binafsi.*

# Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na tatizo la Kifua Kikuu nchini ikiwemo kuimarisha Huduma za uchunguzi na ugunduzi wa Kifua Kikuu katika Vituo vya Afya. Katika kupambana na TB, Serikali ya Awamu ya 5 inayoongozwa na Mhe Rais, Dr John Pombe Magufuli imefanya yafuatayo:-

i. Kuboresha Mfumo wa uchunguzi na ugunduzi wa TB katika vituo vyetu “Quality Improvement in TB case detection” ili kuhakikisha kila mgonjwa au mtu anayefika katika kituo cha huduma kupata matibabu yoyote anafanyiwa uchunguzi ili kubaini kama ana TB au la.
 
Kwa mwaka 2017 tulianza kutumia mfumo huu mpya katika mikoa 16 ambapo karibu yote imepata ongezeko katika uibuaji wa wagonjwa wa TB kati ya asilimia 13 hadi 42. Ongezeko hili limetuwezesha kufikia wagonjwa wapya wa TB wapatao 69,819 mwaka 2017 ikilinganishwa na 62,180 mwaka 2015. 

ii. Huduma ya ugunduzi wa TB kwa kupima makohozi imeboreshwa na kuanza kutumia teknolojia mpya ya gene-Xpert badala ya hadubini.  Mashine hii sasa (Gene-Xpert) ndiyo kipimo cha awali cha kuchunguza makohozi ya wahisiwa wote wa TB.

Wizara imeweza kuongeza mashine hizi kutoka mashine 66 mwaka 2014 hadi kufikia 189 mwezi Machi, 2018. Teknolojia ya mashine hizi inatuwezesha kupata majibu ndani ya masaa 2 badala ya kusubiri kwa zaidi ya masaa 24 kama ilivyo kwa njia za kawaida za hadubini. Mashine hizi pia zina uwezo wa kupima usugu wa dawa za TB wakati huo huo wa ugunduzi wa vimelea vya TB; na hivyo kugundua TB sugu kwa urahisi zaidi. Mashine hizi zimesambazwa kwenye hospitali zote za rufaa za kanda, mikoa, wilaya na baadhi ya vituo vikubwa vya afya.
Napenda kusisitiza na kuvitaka vituo vyote ambavyo vimepata teknolojia hii vitumie njia hii ya gene-Xpert kupima makohozi ya wahisiwa wote wa TB na siyo hadubini kama ilivyozoeleka. *Huduma za kupima TB kwa kutumia gene-Xpert ni bure*
 
Wiki hii, ikiwa ni mojawapo ya shughuli ya maadhimisho haya, tumetoa mashine za gene-Xpert tano (5) kwa hospitali binafsi za jijini Dar es Salaam ili kudhihirisha nia ya serikali ya kutaka kila mtoa huduma kushiriki kikamilifu na kumfikia kila Mtanzania mwenye uhitaji wa huduma za TB. Hospitali hizi ni Aga khan, Kairuki, Regency Medical center, TMJ na Hindul Mandal. Mashine hizi tulizotoa kila moja ina thamani ya Tshs. milioni 38. 
 
iii. Tarehe 20 March 2018, Serikali imezindua dawa mpya za TB za watoto ili kuhakikisha tunakidhi matakwa ya shirika la Afya Duniani (WHO) yaliyotolewa mwaka 2017 kwa nchi wanachama. Dawa hizi mpya za watoto ni za mseto (RHZ/RH) ulioboreshwa, zina ladha nzuri ya matunda, zinayeyuka kwa urahisi zikiwekwa kwenye maji na hivyo hazihitaji kukatwa katwa ili kupata dozi sahihi.  
 
iv. Mwaka 2017 tulikamilisha tahmini ya awali ya hali ya TB mashuleni, na kubaini ya kuwa kuna idadi kubwa ya wanafunzi wanaougua TB na Wizara yangu ikishirikiana na OR-TAMISEMI na Wizara ya Elimu tulitoa maagizo kwa ma-Katibu Tawala wa mikoa kuhakikisha wanafunzi wote hasa wa Shule za Bweni wanachunguzwa TB kabla ya kuanza shule. Nichukue fursa hii pia, kurudia kuwaagiza waganga wafawidhi wote  wa hospitali na vituo vya huduma kuhakikisha watoto wote wanaoanza shule za Bweni wafanyiwa uchunguzi wa TB kikamilifu kabla ya kuanza masomo hasa wale wa shule za bweni. Ni marufuku kujaza fomu za uchunguzi wa Afya tu bila kumpima mwanafunzi husika, hii ni kuliangamiza taifa kwa makusudi na uzembe ambao hauwezi kuendelea kuvumiliwa. 
 
v. Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika kuibua wagonjwa wa TB umeonyesha ongezeko katika miaka ya hivi karibuni. Kwa mwaka 2017, takribani wagonjwa 7,281 ambao ni sawa na 10.4% waligunduliwa na sekta binafsi ikilinganishwa na wagonjwa 3,476 ( 5.5%) mnamo mwaka 2014.
 
vi. Serikali na wadau mbali mbali tunaendelea na utekelezaji wa kampeni za uhamasishaji na upimaji wa wananchi katika maeneo ya migodi, makazi duni kwenye miji mikubwa, magerezani na shule za bweni.
 
vii. Kwa kuzingatia kwamba wahisiwa wengi wa kifua kikuu hutafuta huduma za afya kwa waganga wa jadi, serikali imejipanga mwaka huu wa fedha kujenga uwezo kwa waganga hao ili watambue mapema na kuwapa rufaa wahisiwa wote wa kifua kikuu wanaofika kwenye maeneo yao. Ushirikishwaji huu utafanyika katika wilaya zote katika mikoa ya Simiyu, Mara, Tanga, Shinyanga, Mbeya, Kagera, Dodoma na Ruvuma.
 
viii. Ugatuzi wa huduma za Kifua kikuu sugu unaendelea na hadi kufikia Februari 2018, vituo 60 vinatoa matibabu haya ikilingalishwa na kituo kimoja cha hospitali ya Kibong’oto (Kilimanjaro) miaka mitatu iliyopita. Mafanikio haya yamewawezesha wagonjwa wa TB sugu kutibiwa katika hospitali karibu wakitokea majumbani kwao badala ya Kibong’oto wilayani Siha, Kilimanjaro ambako pia walikuwa wanakaa kwa muda mrefu.
 
# Bado kuna changamoto ambazo zinatukabili katika kukabiliana na TB kama vile Idadi kubwa ya watu wenye TB kutoweza kufikiwa na kuwekwa kwenye matibabu kila mwaka, Wagonjwa wa TB kuchelewa kujitokeza katika vituo vya huduma ili kuweza kuchunguzwa na kupatiwa matibabu kwa wakati na Ushiriki mdogo wa watoa huduma kutoka sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali.

 # Serikali itaendelea kuchukua hatua za haraka na za makusudi ili kukabiliana na changamoto hizi kwa lengo la kutokomeza TB nchini.

# Tunawashukuru wadau wetu wa maendeleo kwa kutuunga mkono na kuboresha huduma za Afya nchini zikiwemo huduma za TB. Wadau hawa ni pamoja na Global Fund, USAID, CDC/PEPFAR, Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la UNITAID, Global Drug Facility (GDF) na wengine wengi wa hapa nchini na nje pia.  

# Pia nazishukuru asasi zisizo za serikali na sekta binafsi kwa kutuunga mkono katika mapambano dhidi ya kifua kikuu. Kwa umuhimu huo huo mkubwa, napenda kuwashukuru wanahabari kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha wananchi wanapata taarifa muhimu na elimu juu ya magonjwa mbali mbali ikiwemo TB.
 
“VIONGOZI TUWE MSTARI WA MBELE KUONGOZA MAPAMBANO YA KUTOKOMEZA TB”

Jumamosi, 24 Machi 2018

DKT. NDUGULILE AWAHASA VIONGOZI KUWA MSATARI WA MBELE KUTOKOMEZA TB

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulileakitoa neno mbele ya Kamati ya Afya na Huduma za Jamii (Hawapo kwenye picha) wakati wa Semina ya Kifua Kikuu (TB) iliyoandaliwa na kuratibiwa na Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Wizara ya Afya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akifafanua  shughuli na vitengo mbali mbali vinavyopatikana ndani ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto - Idara kuu ya Afya.

Waheshimiwa wa Bunge walio katika kamati ya Afya na Huduma za Jamii, wakifuatilia kwa umakini semina ya masuala ya TB iliyoandaliwa na Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Wizara ya Afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akifuatilia kwa ukaribu elimu juu ya ugonjwa wa Kifua Kikuu(TB) iliyokuwa ikitolewa, pembeni yake ni Mwenyekiti wa kamati ya Afya na huduma za jamii na Mbunge wa Chemba Mhe. Juma Nkamia.

Na WAMJW. Dodoma

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewahasa viongozi nchini kote hususani viongozi wa Siasa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB), kutokana na ukaribu wao na kuaminiwa na jopo kubwa la wananchi.

Ameyasema hayo  akiwa katika Seminar ya Kifua Kikuu (TB) iliyoandaliwa na kuratibiwa na Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Wizara ya Afya iliyofanyika jana katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Bunge jijini Dodoma.

Semina hiyo iliyolenga kuwaelimisha Waheshimiwa wa Bunge walio katika kamati ya Afya na Huduma za Jamii, ili kuisaidia Serikali kupaza sauti juu ya masuala ya Kifua Kikuu (TB) na kubadilisha mitazamo ya jamii juu ya ugonjwa huo.

Alisema kuwa tafiti nyingi zinaonesha kuwa karibia theluthi moja ya Watanzania tayari wamepata maambukizo ya Kifua Kikuu na wanaishi na vimelea mwilini mwao hivyo kuwakumbusha kuwakumbusha TB inatibika na kupona kabisa, dawa zake zinatolewa bure na zinapatikana sehemu zote nchini katika vituo vya Umma na Binafsi.


EMPLOYMENT OPPORTUNITY

- Hakuna maoni





THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
THE MINISTRY OF HEALTH, COMMUNITY DEVELOPMENT, GENDER, ELDERLY AND
CHILDREN




 Employment Opportunity
Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children through the CDC-funded project Tanzania Ministry of Health HIV Response under the President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR) is looking for enthusiastic, creative and energetic individuals to fill the following vacant positions:-

Job Tittle: National Laboratory Director (1 Position)
Location: Dar es Salaam/Dodoma  
Reporting To: Head of Diagnostic Services
Position Purpose:
The National Laboratory Director is the head of the NHL-QATC and expected provide strategic leadership and oversight to the implementation and management of the core functions at NHL_QATC to ensure adherence to the National policies and the National Health Laboratory Strategic Plan (NHLSP). Working closely with MOHCDGEC, CDC and other Lab Partners she/he will link and coordinate all the Lab Support Program related to NH-QATC, ensure timely and cost-effective of activity implementation, reporting of activities, and responsible for all the Program related NHL-QATC deliverables. The Lab Director shall ensure collaboration with regional and international partner in support of organizational core functions.
Duties and Responsibilities:

Leadership and Management.
·         Assist and advice the Head of Diagnostic Services on technical matters pertaining to the NHL-QATC and the national laboratory network services.
·         Develop and oversee the implementation of a strategic plan for the NHL-QATC.
·         Direct the planning, implementation and management of the NHL-QATC and ensure its administrative and financial integrity and ability to achieve its goals and objectives.
·         Oversee the development of NHL-QATC annual plans including budgets and other resources required for implementation.
·         Oversee staff performance planning and supervise the Laboratory Manager, Training Officer, Public Health Officer, Biomedical Engineer and Quality Officer.
·         Coordinate and collaborate with partner on their National laboratory support for diagnostic, equipment and training.
·         Work with and Provide technical assistance to clinical and preventive services and National program in the MOHCDGEC.
·         Oversee and manage positive relations with and service to clients both public and in private sector.
·         Ensure liaison with MSD and healthcare technical services to ensure constant availability of reagents, supplies and functional equipment for the NHL-QATC and other public sector laboratories.
·         Develop and maintain excellent relationship with the Department of Curative Services (DCS), Department of Preventive Services (DPS), Department of Quality Assurance Services (DQAS), and National Institute for Medical Research (NIMR), Centre for Disease Control and Prevention (CDC) and all Lab Partners and stakeholders.
·         Provide update on the progress made, direction, approaches and success of NHL-QATC to MOHCDGEC and other counterparts
Quality Assurance.
·         Oversee the preparation, distribution, analysis and dissemination of Laboratory proficiency test in collaboration with Diagnostic Services Section of the MOHCDGEC.
·         Ensure validation and calibration of equipment and oversee the evaluation of equipment, reagents and test methodologies.
·         Oversee the development and implementation of high standard of laboratory quality system for accreditation of laboratories in the country.
·         Oversee the development and standardization of laboratory testing procedure according to national and international standards (ISO-15189).
·         Oversee the performance of specialized or referral laboratory test from within and outside the country.
·         Provide technical leadership to activities improving implementation of Quality Management system national wide.
·         Collaborate with Lab Technical Working Group and National Laboratory Training team to oversee NHL-QATC activities, ensure timely implementation, and timely and accurate reporting to MOHCDGEC.
Training.
·         Provide leadership in the development of national and regional training programs and ensure training of laboratory staff in collaboration with Training Officer.
·         Mentor, Support and manage team of highly qualified staff and align their effort in concert with the National Health Laboratory Strategic plan goals.
·         Link and coordinate through NHL-QATC all national and regional training programs for both in services and pre-service laboratory peroneal to supported by Development Partner such as WB, CDC,WHO and other Lab Partner through Laboratory Support Program.
 Public Health.
·         Play a leading role in integrating public health laboratory at national, zonal, regional, district and health Centre levels.
·         Participate in development and implementation in research protocol according to Tanzania health priorities.
·         Oversee laboratory integrate disease surveillance and response support to outbreak
Experience and Qualifications:
·         Medical degree, with advance training, MMED or PHD in Microbiology or Infectious diseases
·         With at least five year experience in related field
·         Significant experience of working and collaborating with all levels of Tanzanian Government within the health sector.
·         Experience of working in collaboration with local and international partners.
·         Fluent in both English oral and written, as well as good communication skills.

Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)





Job Tittle: Program Implementation Coordinator (1 Position)
Location: Dar es Salaam/Dodoma  
Reporting To: Principal Investigator (PI)
Position Purpose:
The Program Implementation Coordinator is expected to provide vision, direction, leadership, and management to ensure the strategic, programmatic, technical and financial integrity of the program. The PM will guide overall program administration, technical implementation, and fiscal management and will be the primary point of contact (along with the Business Official) with the funder in-country, MOH counterparts, local government counterparts, and implementing partner institutions.

Duties and Responsibilities:
·         Lead, manage and coordinate the  implementation, monitoring and evaluation of project activities with all PMs and staff (Diagnostic, NACP, NTLP, NBTS, QI)- as per approved work plan and budget and ensure the Ministry attains and exceeds assigned targets
·         Supervise, provide technical support on project implementation and perform periodic and perform performance evaluation to other project staff under him/her
·         Develop an annual costed budget and work plans in line with agreed project plan, objectives, outcome and deliverables
·         Oversee and ensure efficient management of project expenditure and other resources as approved work plan and budget
·         Prepare routine  CDC technical  and financial progress reports and other ad hoc project reports, share them for review with Technical Advisor and PI before sharing with CDC as per agreed timelines
·         Prepare and write grants and proposals for fund request to PEPFAR
·         Ensure adequate data collection and timely, complete and clean reporting to the central level from health facilities, to District to Regional to Central level MOHCDGEC and to the funder 
·         Oversee the M&E and QI teams
·         Oversee the training/orientation of staff to USG Government and Tanzania Government`s rules and regulations for implementation of activities and reporting
·         Organize periodic project review meetings as approved work plan and ensure active engagement of relevant key focal points
·         Perform any other relevant duties as assigned by his/her supervisor

Experience and Qualifications:
·         Medical degree, with a Master’s degree in Health Related Fields. A Master’s degree in Public Health or Epidemiology will be preferable.
·         Extensive field experience including working within the Tanzania Government’s health system.
·         A proven record of excellent management, leadership, decision-making, and interpersonal skills.
·         At least 5 years of senior-level experience in designing, implementing, and managing HIV-related projects.
·         Significant experience of working and collaborating with all levels of Tanzanian Government within the health sector.
·         Experience of working in collaboration with local and international partners.
·         Demonstrated experience of managing CDC or other donor-financed projects.
·         Fluent in English both oral and written, as well as good communication skills.


Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)




Job Tittle: Health Laboratory Scientist (1 Position)
Location: Dar es Salaam/Dodoma  
Reporting To: Director of Health Quality Assurance (DHQA)
Position Purpose:
The Health Laboratory Scientist is expected to assist the HQAD in the coordination of POCT – Site Certification activities. She/he will also coordinate the activities of all POCT – Site Certification Stakeholders as well as providing a linkage to the Health Laboratory Practitioners’ Council (HLPC) activities related to Certification of Non Lab Testers. Also, she/he will work closely (in a team spirit) with other staff in the Health Services Inspectorate and Quality Assurance Section, which is under the HQAD in execution and coordination of the POCT Non Lab Testers and Site certification activities.

Duties and Responsibilities:
·         Coordinate assessment of POCT – Site Certification.
·         Keep all data related to Site Auditors, Site Assessments, and Assessment Reports.
·         Liaise with the HLPC on various issues concerning Non-Laboratory Testers Certification.
·         Collaborate with all NGOs performing POCT – Site Certification.
·         Act as a link between the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MoHCDGEC) and the Centers for Disease Control and Prevention (CDC) Country Office.
·         Collaborate with all Ministries, Departments and Agencies (MDAs) owning Health Facilities; the Association of Private Health facilities in Tanzania (APHFTA); and the Christian Social Services Commission (CSSC).
·         Perform other related duties as assigned by the Director of Health Quality Assurance or Assistant Director of Health Services Inspectorate and Quality Assurance.

Experience and Qualifications:
·         Bachelor Degree in Health Laboratory Sciences.
·         At least two years working experience with NGOs in HIV and AIDS services or Government Institutions (e.g., Health Facilities; Research Institutions; Academic Institutions; MDAs, etc.) or Private Sector.
·         Basic Computer Skills
·         Fluent in English both oral and written, as well as good communication skills.

Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)

Job Tittle: Data Manager (1 Position)
Location: MOHCDGEC - Head Office
Reporting To: Program Manager - NACP
Position Purpose:
Data Manager will be responsible in managing data for Monitoring and Evaluation of Care and Treatment Programmes including development, maintenance and updating of database.

Duties and Responsibilities
·         Develop and regularly update data management plan for NACP care and treatment programmes
·         Facilitate collection of quality data from various sources through appropriate training of responsible personnel
·         Carry out supportive supervision to the sites using appropriate tools
·         Use filled data collection forms received from the sites and supervision reports to identify training needs and organise focused training for the field data handling personnel
·         Supervise data entry activities
·         Monitor quality and quantities of data entered during a specified period and advise NACP on data entry needs.
·         Coordinate a process of development, maintenance and updating of appropriate programme monitoring software/database
·         Collaborate with technical partners to link various M&E software and database.
·         Facilitate data use at care and treatment facilities through training of personnel on data collection and simple data analysis.
·         Carry out regular data analysis to produce statistical summaries that will update NACP on the progress in the implementation.
·         Provide regular feedback to care and treatment  personnel at the implementing facilities as well as district and regional authorities
·         Perform other duties as assigned by the Programme Manage of the National AIDS Control Programme

Experience and Qualifications:
·         Degree in statistics and epidemiology. Degree/diploma in Information Technology will be an added advantage.
·         Qualification in public health and Information Technology will be an asset.
·         At least 2 years’ experience in management of information systems or monitoring and evaluation activities.
·         Excellent oral and written skills in English and Kiswahili.
Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)

Job Tittle: Laboratory Program Officer (1 Position)
Location: Dar es Salaam/Dodoma
Reporting To: Head – Pharmaceuticals and Laboratory Services Unit - NACP
Position Purpose:
The laboratory Program Officer leads the laboratory component of the Pharmaceuticals and Laboratory Services Unit of the National AIDS Control Programme (NACP). He /she oversees planning and implementation of laboratory diagnostics for high quality HIV/AIDS services of NACP.  

Duties and Responsibilities
·         Coordinate the development of laboratory training materials including standard operating procedures (SOP) for HIV/AIDS treatment and care tests.
·         Oversee the training of trainers to for new approved HIV/AIDS related laboratory diagnostics and coordinate their scale towards improving HIV/AIDS treatment and care outcomes.
·         Build teams of laboratory experts to enhance uptake of emerging HIV/AIDS technologies in the country.
·         Coordinate adaption and implementation of laboratory information systems and data management initiatives that inform and enhance HIV/AIDS services in the country.
·         Select, quantify, support procurement and distribution of laboratory equipment, reagents and supplies as needed to ensure uninterrupted patient centered HIV/AIDS services according to the national HIV/AIDS treatment and care package in collaboration with Diagnostic Section and PSU of MOHCDGEC and stakeholders.
·         Support implementation of laboratory quality management systems to enhance highest quality possible laboratory services support to HIV/AIDS prevention, care and treatment services in the country.
·         Support quality improvement efforts including supportive supervision and mentorship to health facilities staff providing HIV related services.
·         Compile, interpret laboratory data and reports and share accordingly with relevant levels and stakeholders as required.
·         Promote operational research on various on various HIV/AIDS services delivery.
·         Perform other technical duties as assigned by his/her supervisors

Experience and Qualifications:
·         Degree in medical laboratory sciences from a recognized university, Post graduate degree is an added advantage.
·         Experience of working with the Ministry of Health, International health organization or NGO.
·         Minimum of 5 years of working in a regional, zonal or national laboratory.
·         Excellent interpersonal skills and demonstrated ability to interact with multidisciplinary staff, experts and clients.
·         Excellent written and oral communication in English and Kiswahili.
·         Excellent computer skills in data management and Microsoft office.
·         Registered with the Health Laboratory Practitioners Board.

Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)

Job Tittle: Program Officer-TB/HIV (1 Position)
Location: Dar es Salaam/Dodoma
Reporting To: Head – Care, Treatment and Support Unit - NACP
Position Purpose:
The Program Officer-TB/HIV is responsible for Development and review of TB/HIV policy and guidelines, development and review of TB/HIV training packages, development of proposal and operational plans for TB/HIV collaboration activities, monitoring of TB/HIV collaborative activities, evaluation and other administrative duties fall under the unit.
Duties and Responsibilities

·         In collaboration with NTLP, regional, district and partners develops and reviews TB/HIV policy and    guidelines for the management of patients with TB HIV co-infection, including ICF and IPT; Conduct follow-up visits to ensure adherence to the policy and guidelines; attend meetings to discuss the same; and advise the NACP.
·         Participate in the development and review of TB/HIV training packages; organize training of health care workers on TB/HIV collaborative activities; Ensure regional, district and partners are adhering to national training    curriculum; Participate in the quantification/forecasting of drugs for management of TB/HIV collaborative activities.
·         Develop short and long-term government and donor-funded operational plans on TB/HIV collaborative activities; Implement approved operational plans on the TB/HIV collaborative activities.
·         Develop a feedback mechanism to ensure that approved reports of TB/HIV activities are disseminated to lower levels of the health system and partners; Liaise with the Epidemiology unit of the NACP to ensure that reports are produced on a timely basis; Visit health facilities regularly as part of supportive supervision and mentoring to ensure that the TB/HIV activities are conducted accordingly; Coordinate supportive supervision and mentoring on TB/HIV collaborative activities.
·         Develop an assessment tool to assist in evaluating performance of the TB/HIV collaborative activities in the region and districts; Evaluate the performance of the system from time to time to ensure its efficiency and effectiveness; Develop measures for improvement of the system in provision of TB/HIV services in the health facilities. 
·         Collect and maintain important data and records related to TB/HIV services in the health; Prepare detailed progress reports on TB/HIV collaborative activities and submit them to the Head of the CTU and the Programme Manager.

Experience and Qualifications:
·         Medical Doctor with 3 - 5 years’ experience in HIV care and treatment including TB/HIV, preferably with an MPH or equivalent
·         Excellent interpersonal, diplomacy and facilitation skills 
·         Sensitivity to cultural differences & understanding of the political & ethical issues surrounding HIV &TB
·         Computer skills including, Microsoft Word and Excel
·         Fluent in written and spoken English and Kiswahili
·         Registered with the Tanganyika Medical Council.

Terms of Employment: 1 year Contract (Renewable based on Performance)

Details on How to Apply: If you believe you are the ideal person we are looking for, please send your cover letter describing why you are the right candidate for the position, a curriculum vitae/resume detailing your experience, relevant copy of certificates and three (3) professional referees from previous and current place of employment. Only shortlisted candidates will be contacted and all interview costs will be borne by the applicants. Successfully candidates should be ready to relocate to Dodoma. To find out more about these positions kindly visit www.moh.go.tz
Note: All applications should be sent to Permanent Secretary, Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (Health) via email; maombiyakazi@moh.go.tz on or before 05th April, 2018.