Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 17 Machi 2018

WATUMISHI WA AFYA WAJIEPUSHE NA VITENDO VYA RUSHWA SEHEMU ZAO ZA KAZI

Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akifungua Mkutano Wa Balaza la Wafanyakazi Wa Wizara ya Afya mapema leo Jijini Dar es salaam.

Mganga Mkuu Wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akimkaribisha mgeni rasmi Waziri Wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha).

.
Mkurugenzi Wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt.Otilie  Gowelle wakwanza kulia akifuatilia kwa makini maagizo ya Waziri Wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.

Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu na mganga Mkuu wa Serikali Prof. Kambi wakati wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano kwa Wafanyakazi, pindi wakifanya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, Wakwanza ni Katibu wa Baraza hilo Mary Ntira na wa mwisho ni Afisa Elimu kazi na mratibu wa Jinsia taifa TUGHE Bw. Nsubisi Mwasandende.

Watumishi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Dorothy Gwajima wapili kutoka kulia.


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu katikati waliokaa akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kutoka Wizara ya Afya mara baada ya kikao cha Baraza hilo kilichofanyika Leo jijini Dar es salaam.


Na WAMJW-Dar es salaam.

WATUMISHI wa sekta ya Afya nchini wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kutaka rushwa kutoka kwa wananchi wanapokuwa sehemu zao za kazi ili kuendana na maadili ya utumishi wa Umma. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini  Dar es salaam ili kujadili mustakabari wa utoaji huduma za Afya nchini. 

"Marufuku Watumishi wa sekta ya afya nchini kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa na kama wapo naomba waache mara moja kwani atakayebainika anajihusisha na rushwa sheria itafuata mkondo wake mara moja" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa watumishi wa sekta ya afya hasa katika sehemu ya kutolea huduma za afya wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi pindi wanapotoa huduma sehemu zao za kazi. 

Mbali na hayo Waziri Ummy amewaambia watumishi wa sekta ya afya kuwa kipaumbele katika kutoa elimu juu ya magonjwa yasioambukiza kwani yamekuwa yakiongezeka kila kukicha kutokana na ukosefu  elimu ya kutosha kuhusu magonjwa hayo. 

"Watumishi wa Afya wanatakiwa kuwa mfano hasa katika kufanya mazoezi,  kula lishe bora pamoja na kutoa elimu ya magonjwa mbalimbali ili kuisaidia kuondoa ongezeko la magonjwa yasioambukiza" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa ili kufikia adhma ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe Magufuli la kujenga uchumi wa Viwanda ni lazima kuzingatia utoaji wa huduma bora za afya ili kuwa na wananchi  wenye afya ambao watasukuma gurudumu kufikia lengo hilo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu Taifa wa Balaza la Wafanya kazi TUGHE Bw. Nsubisi Mwasandende amesema kuwa katika kutatua changamoto za magonjwa mbalimbali watendaji wa Wizara ya Afya wanatakiwa kuzingatia hali ya upatikanaji wa chanjo ili kuboresha huduma za afya. 

Aidha Bw.  Mwasandende amesema kuwa watumishi wanatakiwa kulifanyia kazi haraka  agizo la Waziri Ummy Mwalimu la kutokomeza vitendo vya rushwa haraka iwezekanavyo  ikiwa kama moja la adhimio la katiba ya balaza la wafanyakazi. 

0 on: "WATUMISHI WA AFYA WAJIEPUSHE NA VITENDO VYA RUSHWA SEHEMU ZAO ZA KAZI"