Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 7 Machi 2018

WAZIRI UMMY AWAAHIDI AMBULANCE WAKAZI WA LUBANDA- ILEJE,

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akitoa udongo wakati wa  uchimbaji wa msingi katika ziara yake ya ufunguzi wa kituo cha Afya cha Mtura kata ya Lubanda wilaya ya Ileje.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akiendelea na ukaguzi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mtura kilicho katika kata ya Lubanda Wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akielekea eneo la gari lililokwama kutokana na changamoto ya Barabara, wakati akiwa katika ziara yake ya ufunguzi wa kituo cha Afya cha Mtura kata ya Lubanda wilaya ya Ileje. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Haji Mnasi, Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Kheri Kagya.
.
Wananchi wa kata ya Lubanda katika kijiji cha Mtura wilaya ya Ileje wakimsalimia Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu.

 
Na WAMJW. Songwe
 
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewaahidi wananchi wa kata ya Lubanda Wilayani Ileje kuwapatia gari ya kubebea wagonjwa mapema mwaka huu.

Ahadi hiyo ameitoa jana wakati alipotembelea kijij i hicho kujionea ujenzi wa kituo cha afya cha Lubanda kinachojengwa kupitia mpango wa kuboresha vituo vya afya nchini kwa kujenga chumba cha upasuaji wa dharura.

Waziri Ummy alitoa ahadi hiyo baada ya kujionea umbali wa Zahanati ya Lubanda hadi kufika hospitali ya Isoko, pia hali ya barabara kijijini hapo.

"kwakuwa nategenea kununua magari ya kubebea wagonjwa yapatayo 60,Tanzania ni kubwa, nyie mtakuwa namba moja, kwani hali ya barabara nimeiona"alisema Waziri Ummy.

Aidha, alisema anataka kushuhudia  mwanamke mjamzito wa kijiji hicho anaokolewa maisha yake kwa kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha afya ili huduma zote za upasuaji ukiwemo wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni kwa mama mjamzito zinatolewa katika kituo hicho mapema iwezekanavyo

"Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kumuokoa mama mjamzito pale anapopata uzazi pingamizi, hivyo Serikali kuu imetoa shilingi milioni 500 kwa ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya vipatavyo 174 nchini.
Hata hivyo Waziri huyo wa Afya amewataka wananchi hao kujenga utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara ili kuweza kupata tiba haraka pale wanapogundulika na matatizo.
 
"hivi sasa wanawake wengi wamegundulika na saratani ya shingo ya kizazi na asilimia 80 ya wanawake wanaofika hospitalini wapo hatua za mwisho hivyo badala ya kutibiwa wanapunguziwa maumivu" aliendelea Mhe.Ummy
 
Wilaya ya Ileje ina vituo vya kutolea huduma za afya vipatavyo 33 ikiwemo hospitali mbili, kituo cha afya kimoja na zahanati 30 zinazomilikiwa na serikali, dini pamoja na watu binafsi.

0 on: "WAZIRI UMMY AWAAHIDI AMBULANCE WAKAZI WA LUBANDA- ILEJE,"