Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 17 Machi 2018

JIEPUSHENI NA RUSHWA, MHE. UMMY MWALIMU





WATUMISHI wa sekta ya Afya nchini wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kutaka rushwa kutoka kwa wananchi wanapokuwa sehemu zao za kazi ili kuendana na maadili ya utumishi wa Umma. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini  Dar es salaam ili kujadili mustakabari wa utoaji huduma za Afya nchini. 

"Marufuku Watumishi wa sekta ya afya nchini kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa na kama wapo naomba waache mara moja kwani atakayebainika anajihusisha na rushwa sheria itafuata mkondo wake mara moja" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa watumishi wa sekta ya afya hasa katika sehemu ya kutolea huduma za afya wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi pindi wanapotoa huduma sehemu zao za kazi. 

Mbali na hayo Waziri Ummy amewaambia watumishi wa sekta ya afya kuwa kipaumbele katika kutoa elimu juu ya magonjwa yasioambukiza kwani yamekuwa yakiongezeka kila kukicha kutokana na ukosefu  elimu ya kutosha kuhusu magonjwa hayo. 

"Watumishi wa Afya wanatakiwa kuwa mfano hasa katika kufanya mazoezi,  kula lishe bora pamoja na kutoa elimu ya magonjwa mbalimbali ili kuisaidia kuondoa ongezeko la magonjwa yasioambukiza" alisema Waziri Ummy. 

0 on: "JIEPUSHENI NA RUSHWA, MHE. UMMY MWALIMU"