Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 21 Machi 2018

MAWAZIRI WA AFYA WA JUMUIYA YA ECSA WAKUBALIANA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA


Matukio ya Mkutano wa 65 wa Mawaziri wenye dhamana ya Sekta ya Afya katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Mashariki, kati na kusini mwa Afrika (Eastern, Central and Southern Africa Health Community, ECSA-HC), yanayoendelea jijini Dar es salaam, yakiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, kikao hicho kilifunguliwa juzi machi 19 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitembelea Mabanda ya LAB EQUIP LMTD na Banda la Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi TFDA baada ya mapumziko mafupi ya Mkutano wa 65 wa Mawaziri wenye dhamana ya Sekta ya Afya katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Mashariki, kati na kusini mwa Afrika (Eastern, Central and Southern Africa Health Community, ECSA-HC).




Kikao cha ndani cha Mawaziri wenye dhamana ya Sekta ya Afya katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Mashariki, kati na kusini mwa Afrika (Eastern, Central and Southern Africa Health Community, ECSA-HC), huku wakikubaliana kuimarisha utawala na kuweka mikakati ya pamoja ya kudhibiti na kupambana na magonjwayanayolipuka baina ya nchi hizo, pia kudhibiti magonjwa yasiyoyakuambukiza kama vile magonjwa ya Saratani, ambayo yanasababishwa na aina ya vyakula vyenye mafuta kupita kiasi, matumizi ya vilevi na matumizi ya sigara.
Pia kuongeza uwajibikaji ili kuimarisha Sekta ya Afya hasa katika Afya ya mama na mtoto.




Viongozi wa Serikali kutoka Wizara ya Afya wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara kuu ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya (Watatu kutoka Kushoto) wakwanza ni Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya Dkt. Mohamed Mohamed, wa pili ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhamed Bakari Kambi na wa mwisho ni Dkt. Kwasi. wakiwa katika hafla ya chakula cha usiku baada ya Mkutano wa 65 wa Mawaziri wenye dhamana ya Sekta ya Afya katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Mashariki, kati na kusini mwa Afrika (Eastern, Central and Southern Africa Health Community, ECSA-HC) uliofanyika katika Hotel ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam.

NA WAMJW-DAR ES SALAAM


Mkutano wa 65 wa Jumuiya ya Mawaziri wa Afya wa Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA umemalizika leo jijini hapa kwa nchi wanachama kukubaliana maazimio mbali mbali yanayolenga  kutekeleza  kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kama vile kisukari, saratani, magonjwa ya moyo na ya mfumo wa hewa.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema makubaliano hayo yamelenga kuimarisha na kuboresha sekta hiyo na afya ya wananchi kwa ujumla.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa  wamekubaliana pia kuongeza uwajibikaji kwenye afya ya mama na mtoto ili kuepusha vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.

“Tumekubaliana kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza tumegundua katika nchi hizo magonjwa yanayoongoza ni pamoja na kisukari, saratani, magonjwa ya moyo na ya mfumo wa hewa" alisema Waziri Ummy.

Kwa mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa Suala lingine walilokubaliana ni kutilia mkazo suala la heshima kwa wajawazito kwa sababu mawaziri wameshauri pia Tanzania kukitambua Chuo cha Upasuaji cha Afrika Mashariki, Kati na Kusini.  

Waziri Ummy ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, amesema wamkubaliana wamekubaliana pia kuimarisha ushirikiano na ulinzi katika maeneo ya mipaka.

“Kwa sababu nchi zina mipaka lakini magonjwa hayana mipaka tukiimarisha itasaidia kuondoa na kudhibiti uwezekano wa magonjwa hasa ya mlipuko kuenea ikiwemo Zika, Ebola, Dengue, Chikungunya na mengineyo,” alisema Waziri Ummy.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Ummy  amesema pia wamekubaliana kuimarisha masuala ya utawala kwamba kila mmoja ana wajibu kwa nafasi yake kwani sekta ya afya ni mtambuka.

“Tumeona kuna umuhimu mkubwa wa kushirikisha sekta zingine ikiwamo kilimo, maji, elimu, utumishi, mazingira zinahusika kwa ukaribu na masuala ya Afya” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa azimio la saba walilokubaliana katika mkutano huo ni kuweka mkakati wa pamoja kukabiliana na magonjwa akitolea mfano nchi ya Uganda ambao wamepata ugonjwa wa Marbugy unaofanana dalili na ugonjwa wa Ebola.


Mkutano huo wa kujadili masuala mbalimbali ya afya yalijumuisha nchi 9 kutoka  Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA umefanyika nchini Tanzania kwa siku tatu.

0 on: "MAWAZIRI WA AFYA WA JUMUIYA YA ECSA WAKUBALIANA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA"