Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 31 Mei 2020

TANZANIA IPO TAYARI KUPOKEA WATALII - DKT. KIGWANGALLA

- Hakuna maoni
 Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pindi walipofanya ziara ya kukagua utayari katika uwanja wa KIA.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akieleza jambo katika sehemu ya kukagua mizigo pindi aliooongozana na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla katika uwanja wa ndege wa KIA.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pindi walipofanya ziara ya kukagua utayari katika uwanja wa KIA.

Magari manne yakubeba wagonjwa yaliyotolewa na yametolewa na wakala wa huduma za utalii kama sehemu ya tahadhari katika kuhakikisha usalama wa Watalii wataoingia nchini kwaajili ya utalii.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel wakisikiliza jambo kutoka  kwa Mtaalamu kutoka wakala wa huduma  za utalii nchini wakati wa makabidhiano wa magari hayo manne.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel wakikagua maendeleo ya utengenezaji wa gari linalotumia umeme.


TANZANIA IPO TAYARI KUPOKEA WATALII - DKT. KIGWANGALLA

Na WAMJW- Kilimanjaro

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla ameweka wazi kuwa, Tanzania ipo tayari kupokea wageni kutoka sehemu yoyote Dunia kwa ajili ya utalii, kufuatia kuimarisha mifumo ya tahadhari zote za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Dkt. Kigwangalla ameyasema hayo leo katika ziara iliyomjumuisha Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ikiwa na lengo la kukagua utayari wa nchi katika kudhibiti ugonjwa wa Corona katika uwanja wa ndege wa KIA na kupokea magari manne ya kubeba wagonjwa endapo watatokea pindi wawapo nchini kwenye utalii.

Dkt. Kigwangalla amesema kuwa, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kudhibiti maambukizi ya Virusi vya Corona, ikiwemo kuweka miongozo wakati wa kuingia na kutoka uwanja wa ndege, muongozo wa namna ya kusafirisha watalii pamoja na muongozo wa namna ya kuandaa chumba cha wageni

"Katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona Duniani, tumeweka miongozo kwa pale uwanja wa ndege, tumeweka muongozo wakati wa kuingia na kutoka tumeweka muongozo namna ya kusafisha Watalii kutoka uwanja wa ndege mpaka hotelini, tumeweka muongozo namna ya kuandaa chumba cha mgeni, namna ya kuandaa chakula, kila kitu tumeweka muongozo " alisema

Aliendelea kusema kuwa, Serikali imechagua baadhi ya vituo vya Afya mahususi kwa ajili ya watalii Mkoani Arusha, Serengeti na Ngorongoro lengo ni kuthibitisha usalama wa afya ya Watalii waingiapo nchini.

Naye Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa, Serikali imepokea magari manne ya kubeba wagonjwa(ambulance) yaliyokidhi miongozo ambayo yametolewa na wakala wa huduma za utalii nchini ikiwa ni sehemu ya tahadhari katika kuhakikisha usalama wa Watalii wataoingia nchini.

"Tumeona magari ambayo yamezingatia zile taratibu  na miongozo yote ambayo inatakiwa kuhakikisha Watalii wetu wapo salama na endapo kutakuwa na tatizo litaweza fanyiwa utatuzi mara moja " alisema Dkt. Mollel.

Aidha, alisema kuwa, katika kuboresha tahadhari zaidi magari yaliyotolewa yanalenga kuwakinga madereva na Watalii kwa kutenganishwa kwa kioo ili kudhibiti mnyororo wa maambukizi ya virusi vya Corona endapo atatokea.

"Magari yenyewe yatakuwa Dereva anaingia ndani, lakini kunakuwa na kinga inayowatenganisha Watalii na madereva wetu jambo litalosaidia kudhibiti maambukizi endapo yatatokea " alisema.

Mwisho.

Jumamosi, 30 Mei 2020

HONGERENI WATUMISHI WOTE WA AFYA KWA JINSI MLIVYO PAMBANA KATIKA JANGA LA CORONA.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akisisitiza jambo wakati akiongea na Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma (hawapo kwenye picha).

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akiteta jambo na Mkurugenzi wa tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe, wakati alipofanya ziara ya kuongea na Watumishi wa Sekta ya Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Mkurugenzi wa tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe akiteta jambo na Mkururugenzi msaidizi anaesimamia hospitali za Rufaa Dkt. Caroline, wakati alipofanya ziara ya kuongea na Watumishi wa Sekta ya Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wakifuatilia neno kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel pindi alipofanya ziara katika Hospitali hiyo. 

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akimjulia hali mtoto aliefika na mzazi wake kupata matibabu katika wodi ya watoto, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akiwa na baadhi ya Watumishi kutoka Wizara ya Afya, katika chumba cha Watoto njiti, katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. 

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akimjulia hali mama aliyempeleka mtoto kupata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. 

 Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel akiwa na viongozi kutoka Wizara ya Afya na Watumishi wa Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma pindi alipofanya ziara ya kuongea na Watumishi hao.

Jengo la Idara ya magonjwa ya wanawake na uzazi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.



HONGERENI WATUMISHI WOTE WA AFYA KWA JINSI MLIVYO PAMBANA KATIKA JANGA LA CORONA.

Na WAMJW- DOM

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amewashukuru Watumishi wote wa Sekta ya Afya nchini kwa namna walivyojitoa katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Dkt. Mollel ameyasema hayo leo, wakati alipofanya ziara ya kuongea na Watumishi wa Sekta ya Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Rufaa ya kanda ya kati ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

"Jinsi ambavyo nyie mmepambana dhidi ya virusi vya Corona na bado mkamuunga mkono Mhe. Rais na ushauri alioutoa yeye na Wataalamu wengine wa Wizara kupitia Waziri wa Afya, nyie mmekuwa mashujaa na jeshi la uzalendo wa hali ya juu, nawashukuru sana" alisema Dkt. Mollel.

Dkt. Mollel aliendelea kwa kukemea tabia za wanasiasa wachache kupotosha Watanzania na Dunia kwa ujumla juu ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa Corona kwa Watumishi wa Sekta ya Afya nchini jambo ambalo sio kweli.

"Kuna wanasiasa wanapiga kelele kuhusu Corona kuliko sisi, nawaomba watu tuache kupiga siasa, sisi watumishi wa afya ndio watu wakwanza kukutana na wagonjwa wa Corona laikini leo watumishi mpo 504 je niambieni kuna yoyote amelazwa, watumishi walijibu hapana, kama kweli kuna Watumishi wanakufa basi nyie mngekuwa wa kwanza kuugua na kupoteza maisha" alisema.

Aidha, Dkt Mollel alitoa wito kwa Watumishi wa Sekta ya Afya nchini kufanya kazi kwa bidii katika kuwahudumia wananchi ili kutoa huduma bora, huku akiweka wazi kuwa kazi ya kuwahudumia wananchi ni ya wito na ya uzalendo.

Pia, Mhe Mollel alielezea kuwa Rais alikuwa na maono ya kusitisha matibabu ya nje ya nchi kwa kuboresha huduma za kibingwa nchi na hii imejizihirisha baada ya dunia kupata janga la corona nchi yetu imeendelea kutoa huduma za kibingwa pasipo kutegemea matibabu ya nje kwa wananchi ambao walikuwa na sifa za kutibiwa nje .

Nae Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma Dkt. Ibenzi Ernest ameweka wazi kuwa Hospitali hiyo imeendelea kutoa huduma za Afya bila kutetereka na kutoa elimu kwa umma licha ya kupitia katika kipindi cha mlipuko wa virusi vya Corona ulioikumba nchi.

"Tumeendelea kutoa huduma bora kwa wananchi bila kutetereka hata katika wakati huu wa janga la mlipuko wa maambukizi ya virusi vya Corona ulioikumba nchi, Watumishi wetu wamesimama imara huku wakiendelea kutoa elimu ya kujikinga dhidi ya Corona "alisema.

Ijumaa, 29 Mei 2020

MWONGOZO WA UDHIBITI WA MAAMBUKIZI YA UGONJWA WA CORONA (COVID-19) KATIKA SHULE, VYUO NA TAASISI ZA ELIMU NCHINI

- Hakuna maoni






MWONGOZO WA KUZINGATIWA WAKATI WA KUENDESHA SHUGHULI ZA MICHEZO KATIKA KIPINDI CHOTE CHA MLIPUKO WA COVID-19 NCHINI KWA LENGO LA KUDHIBITI MAAMBUKIZI

- Hakuna maoni







BOFYA HAPA KUPAKUA MWONGOZO HUO KUTOKA TOVUTI YA WIZARA YA AFYA

Jumamosi, 23 Mei 2020

WANAWAKE WENYE TATIZO LA FISTULA WATAKIWA KWENDA KUPATA MATIBABU MAPEMA

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Mhe. Ummy Mwalimu

Na WAMJW-Dodoma

Wanawake wenye matatizo ya Fistula nchini wametakiwa kuacha tabia ya kujifungia ndani na badala yake wametakiwa kwenda kupata matibabu katika Hospitali zilizoainishwa na Serikali bila gharama yeyote.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika kuadhimisha siku ya Fistula duniani inayoadhimishwa tarehe 23 Mwezi Mei kila Mwaka, yenye kauli mbiu mwaka huu inayosema “Tokomeza unyanyasaji wa kijinsia: Tokomeza huduma ya afya isiyo na usawa; Tokomeza Fistula sasa!”.

Waziri Ummy amesema takwimu za Shirika la Afya Duniani za mwaka 2018 zinaonyesha kuwa kuna wanawake takribani millioni mbili (2,000,000) wanaoishi na Fistula Duniani kote. Inakadiriwa kuwa wagonjwa wapya kati ya 50,000 na 100,000 hupatikana kila mwaka, wakati juhudi za kutibu Fistula ulimwenguni kote huishia kutibu wagonjwa 20,000 tu.

Kwa upande wa Tanzania, Waziri Ummy amesema inakadiriwa kuwa na wanawake takribani 2500 ambao wanapata fistula kila mwaka, huku idadi ya wanaopatiwa matibabu ikiwa ni  takribani wanawake 1,000 na kuongeza kuwa Tanzania imepiga hatua katika matibabu haya.

“Katika kipindi cha miaka Mitano kuanzia 2015 hadi Disemba, 2019 wanawake zaidi ya 5,500 wametibiwa Fistula. Mafanikio haya yanatokana na kampeni iliyoendeshwa kwa ushirikiano baina ya Serikali na Wadau ambayo imeweka Mabalozi wa Fistula zaidi ya 3,000 nchi nzima wanaosaidia kuratibu rufaa na usafiri kwa wagonjwa kwenda Hospitali zinazotoa huduma ya Fistula”.  Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ametaja takwimu zinazoonyesha kuwa idadi ya Wanawake wanaojitokeza kutibiwa Fistula kwenye Hospitaii za CCBRT, Bugando, Nkinga na Kuvulini Maternity Center imepungua kwa zaidi ya 30% kuanzia mwaka 2015 mpaka 2019. Mwaka 2015, wanawake 1337 walipatiwa matibabu ya Fistula, Mwaka 2016 walikuwa 1356, mwaka 2017 idadi hiyo ikashuka na kufikia 1060, mwaka 2018 ikashuka tena na kufikia  idadi ya wanawake 900, na mwaka 2019 ikashuka zaidi na kufikia wanawake 852.  Hii imetokana na kuimarika kwa huduma za Afya ya mama wajawazito ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa huduma za upasuaji wa dharura chini ya Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli.

Waziri Ummy amewataka akinamama wajawazito kuhudhuria kliniki mara tu anapojihisi mjamzito ili kuweza kuchunguza afya yake pamoja na mtoto.

“Mama mjamzito endapo atawahi kliniki mapema kwa ajili ya uchunguzi wa maendeleo ya afya yake na mtoto na kuhakikisha anajifungulia katika kituo cha kutolea huduma za afya atapunguza uwezekano wa kupata tatizo la Fistula. Nitumie fursa hii kuendelea kuhimiza akina mama wajawazito kuwahi kliniki mapema, kukamilisha mahudhurio yote manne na kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya”. Ameongeza Waziri Ummy.

Huduma za Fistula nchini zinapatikana kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, CCBRT, Bugando, Hospitali ya Kanda ya Rufaa-Mbeya, Hospitali ya Nkinga Tabora, KCMC na Kivulini Maternity Center iliyoko Arusha. Tuna wataalamu waliobobea kwenye tiba ya Fistula kwenye Hospitali hizi.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amesema ili kutokomeza Fistula nchini kunahitajika juhudi za pamoja za wadau mbalimbali wakiwemo watumishi wa Afya kwenye ngazi zote, Wizara mbalimbali, wadau wa Maendeleo, Wanahabari na Mashirika ambayo yamekuwa yakijihusisha na uhamasishaji wa matibabu ya Fistula. 

MWISHO