Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 7 Mei 2020

VIFO VYA CORONA KUCHUNGUZWA


Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi akisema jambo kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Bugando (hawapo pichani)

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (wa upande wa kulia) akipokea zawadi za kwaheri kutoka kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa - Bugando alipokuw akifanya kazi awali kabla ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania  Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kuwa Mganga Mkuu wa Serikali. 

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (wa upande wa kushoto) akipokea zawadi za kwaheri kutoka kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa - Bugando alipokuw akifanya kazi awali kabla ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania  Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kuwa Mganga Mkuu wa Serikali. 




Na WAMJW – Mwanza
Vituo vya kutolea huduma za afya nchini vyatakiwa kufanya uchunguzi juu ya kifo chochote kitakachotokana na ugonjwa wa corona ili kubaini kama mgonjwa alihudumiwa ipasavyo kabla ya kifo kutokea.

Agizo hilo limetolewa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi akiwa Jijini Mwanza mara baada ya kuagana na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa – Bugando alipokuwa akifanya kazi awali kama Mkurugenzi Mtendaji kabla ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mganga Mkuu wa Serikali.

“Kwakweli tusingependa kuona mgonjwa anafariki kwa sababu zisizo na msingi, naagiza hospitali zote zenye kamati ya uchunguzi (Clinical Audit) kufanya uchunguzi wa vifo vinavyohusiana au kutokana na corona ili kuona kama kulikuwa na tatizo lolote katika kumpokea mgonjwa au katika kumhudumia” alisema Prof. Makubi

Prof. Makubi amewataka wananchi kuelewa kuwa sio kila kifo kinachotokea hivi sasa kinasababishwa na ugonjwa wa corona kwa kuwa yapo magonjwa mengine pia ambayo yanatushamblia binadamu.

“Siyo kweli kwamba mgonjwa akiwa na presha, kisukari, figo au kansa akifariki iwe imesababishwa na corona, tuendelee kuwahudumia wananchi, kuepusha vifo vinavyoweza kuwa na uhusiano wa corona”. Alisema Prof. Makubi.

Aidha Prof. Makubi ametoa rai kwa vituo vya afya kuwapokea wagonjwa wote na kuwapatia matibabu bila kuwabagua kuwa na dalili za corona.

“Serikali inapenda kuona wagonjwa wa corona wanapokelewa nakupata matibabu, tuendelee kuwapokea na kuwahudumia huku tukichukua tahadhari ya maambukizi”. Alisema Prof. Makubi.

“Watumishi wa afya wasiwe na ubaguzi wa kuchagua wagonjwa wa kuwahudumia au mpaka apimwe kipimo cha covid-19 ndio ahudumiwe, tuwapokee wote lakini wakati huo tukichukua tahadhari zote za kujikinga na ugonjwa”.  Alisisitiza Prof. Makubi.

Katika hatua nyingine Prof. Makubi amesema kuwa Serikali inaendelae kusambaza vifaa kinga kwa ajili ya kuwawezesha watoa huduma kujikinga na ugonjwa huo wakati wakitoa huduma.

“Serikali imeanza kugawa vifaa kinga kama vile PPE, masks pia sanitizer kwa ajili ya vituo vyote vya afya Tanzania, kwahiyo pasIwepo kisingizio chochote cha kushindwa kumhudumia mgonjwa wa corona kwa sababu ya vifaa kinga”.

Mwisho

0 on: "VIFO VYA CORONA KUCHUNGUZWA"