Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 30 Aprili 2020

SAFARI ZA KWENDA KUWATEMBELEA NDUGU VIJIJINI ZISUBIRI CORONA IISHE - DKT. SUBI

- Hakuna maoni
Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akieleza jambo wakati akiongea na Waandishi wa habari katika juu ya mwenendo wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkurugenzi msaidizi wa Afya mazingira Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Khalid Massa akimkaribisha Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akieleza jambo, mbele ya Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi (hayupo kwenye picha) wakati akiongea na Waandishi wa habari katika juu ya mwenendo wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi, akifuatilia taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi (hayupo kwenye picha).

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) akifuatilia mjadala kutoka kwa Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi (hayupo kwenye picha).

Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akinawa  mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akiwa na timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya na taasisi isiyo yakiserikali ya Project CLEAR juu ya elimu ya kujikinga  dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.



SAFARI ZA KWENDA KUWATEMBELEA NDUGU VIJIJINI ZISUBIRI CORONA IISHE - DKT. SUBI

Na WAMJW- DSM

Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi ametoa wito kwa wananchi kutosafiri kwenda vijijini kwa lengo la kuwasalimia ndugu katika kipindi hiki ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona kusambaa zaidi nchini.

Wito huo ameutoa leo, wakati akiongea na Waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam juu ya mwenendo wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

"Kwa wanaotaka kwenda kuwatembelea Wazee kijijini, wasubiri Corona iishe, kwasababu tunaona watu watatoka kwenye miji ambayo inamaambukizi wanaenda vijijini kuwatembelea wazazi ambao umri wao umeenda, inawezekana wana magonjwa ya uzeeni, kunauwezekano mkubwa wakuwaambukiza huko" alisema.

Aliendelea kusisitiza kuwa, katika maeneo yote yenye msongamano hususan maeneo  ya biashara na huduma za Afya, waweke utaratibu mzuri, utaosaidia wateja kukaa umbali wa mita moja au zaidi pindi wanaposubiri kupata huduma, hali itayosaidia kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

"Maeneo ya kutoa huduma mbali mbali, ikiwemo Hospitali na vituo vya Afya, waweke utaratibu mzuri, watu wanaokuja kupata huduma wakae katika utaratibu wa mita moja au zaidi ili watu hawa wasiweze kuambukizana maradhi, lengo likiwa kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine " alisema

Aliendelea kusema, ni muhimu uvaaji wa Barakoa uzingatiwe katika ngazi zote, hasa katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu, huku akisisitiza kuwa, ni muhimu kuzichoma moto Barakoa zilizotumika ili kuepusha usambaaji wa magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza.

"Tunasisitiza uvaaji wa Barakoa, hasa unapokuwa kwenye mkusanyiko wa watu, lakini barakoa sio kitu salama baada ya kumaliza kukitumia, kinakuwa kichafu na maambukizi, kwa mantiki hiyo, hakikisha unaitupa sehemu salama na unachoma moto ili mtu mwingine asiweze kuikokota na kuitumia tena " alisema

Aidha, Dkt. Subi amesema kuwa, bado elimu ya kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka haijaeleleweka vizuri, hivyo kuitaka timu ya hamasa kuongeza nguvu katika hatua zote tano za unawaji mikono ili elimu hiyo isaidie katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

"Tunaposema kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni tunamaana kwamba, unapokwenda kunawa hakikisha sabuni imekolea vizuri kwenye kiganja cha mikono, hakikisha umesugua vizuri, povu la sabuni limeshika vizuri, na hakikisha umenawa vizuri mbele, nyuma, kwenye vidole na kila eneo la mikono vizuri kwa sekunde zisizopungua 20"alisema

Akiwasilisha ripoti ya utendaji kazi wa kampeni ya "mikono safi, Tanzania salama," Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima ameweka wazi kuwa, mpaka sasa timu hiyo ya uhamasishaji imeshatembelea jumla ya maeneo 145 kati ya 213 yaliopangwa yametembelewa ikiwa ni sawa na asilimia 68.

Mbali na hayo amesema kuwa, licha ya kutoa elimu ya tahadhari, kikosi cha uhamasishaji kimekuwa kikitoa zawadi kwa taasisi na watu ambao wanazingatia maelekezo yanayotolewa na Wizara, vikiwemo vitakasa mikono (Sanitizer), viang'azi (Reflectors) na khanga za Kampeni.


Mwisho.

Jumatano, 29 Aprili 2020

WAGONJWA WAPYA WA CORONA 196 WAONGEZEKA NCHINI

- Hakuna maoni
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia Wabunge na Wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya ugawaji wa magari ya kubebea wagonjwa  50 yaliyotolewa na Wizara ya Afya kwa Mikoa mbalimbali nchini iliyofanyika katika ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa Jijini Dodoma. Kushoto ni Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu

Baadhi ya Wabunge wakiwa kwenye magari ya majimbo yao waliyotolewa na Wizara ya Afya na kukabidhiwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi funguo za Magari ya kubebea wagonjwa Mbunge wa Urambo Bi. Magreth Sitta kwa niaba ya wabunge wengine.

Waziri Mkuu Kassim majaliwa akiongeza na Mbunge wa Ulanga Mhe. Goodluck Mlinga wakati wa hafla ya makabidhiano ya magari ya kubebea wagonjwa iliyofanyika ofisini kwa waziri mkuu jijini Dodoma. Katikati ni Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

Na WAJMW-Dodoma

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ametangaza ongezeko la wagonjwa wa Corona 196 nchini huku Tanzania Bara ikiwa na Wagonjwa 174 na Zanzibar wagonjwa 22 ambao walitolewa taarifa na Waziri wa Afya Wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid na kufanya idadi ya wagonjwa wa Corona nchini kufikia 480.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema hayo wakati akigawa magari 50 ya kubebea wagonjwa kwa wabunge wa majimbo mbalimbali tukio lililofanyika leo katika ofisi ya Waziri Mkuu iliyopo Mlimwa jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema jumla ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 197, huku Zanzibar waliopona wakiwa 36 na Tanzania bara 83. Pia Waziri Mkuu amesema kumekuwa na ongezeko la vifo vya watu sita (6) na kufanya kuwa na vifo vilivyotoka na Corona nchini kufikia 16.

Kati ya wenye maambukizi 297 waliobaki, 283 wanaendelea vizuri na tiba na kusubiri ufuatiliaji wa afya zao na wengine 14 wako chini ya uangalizi maalumu wa madaktari ambao wanahitaji oksjeni  (Oxygen) ya kuwasaidia kupumua pamoja na wale wenye magonjwa mengine ambayo yamejitokeza kwenye wodi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuwaondoa washukiwa waliokua karantini ambao walishatimiza siku 14 baada ya uchunguzi wa kiafya kuonekana hawana maambukizi na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Hadi kufikia jana tarehe 28 Aprili, watu 644 wameruhusiwa kutoka karantini katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Arusha, Zanzibar, Kilimanjaro, Mwanza, kagera, Songwe, Kigoma na Dodoma.

Hata hivyo Waziri Mkuu amekemea tabia ya upotoshaji na utoaji wa takwimu ambazo sio rasmi na kuzua taharuki kwa jamii kwamba kila kifo kimetokana na Corona kuwa sio sahihi na kusisitiza kuwa kuna magonjwa mengine ambayo yanaua pia.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari zote zinazotolewa na wataalamu wa afya huku Serikali ikiendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuweza kupambana na vita hii ya ugonjwa wa Corona.

Katika makabidhiano hayo ya magari, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya  imetoa magari 50 nchiniyenye Tsh. Bilioni 6 ili yaweze kuwezesha rufaa za akinamama Wajawazito na kuepusha vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na kukabiliana na magonjwa ya milipuko kama Corona.

Magari 18 yamepekwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa, magari 32 yatatumika kwa ajili ya vituo vya afya na Hospitali za Wilaya.

Aidha, Waziri Ummy amemshukuru Waziri Mkuu kwa kutoa ushirikiano mkubwa unaoutoa kwa Wizara ya Afya kwa kuwezesha mambo mbalimbali lengo likiwa ni kufikisha huduma bora za afya kwa wananchi wote.



Jumanne, 28 Aprili 2020

TEKETEZA/HARIBU BARAKOA YAKO VIZURI KABLA YAKUITUPA/ BAADA YA KUMALIZA KUTUMIA.

- Hakuna maoni
Barakoa (mask) iliyotupwa baada ya matumizi, katika maeneo ambayo sio rasmi, hali inayoweza sababisha kusambaa kwa maambukizi.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi, akitoa elimu kwa wafanyabiashara katika kituo cha daladala cha feli Jijini Dar es Salaam.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR wakiendelea na uhamasishaji jinsi  ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa wafanyabiashara katika eneo la soko la Mabibo Jijini Dar es Salaam.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR wakiendelea na utoaji  elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa wafanyabiashara katika kituo  cha daladala cha feli Jijini Dar es Salaam.


TEKETEZA/HARIBU BARAKOA YAKO VIZURI KABLA YAKUITUPA/ BAADA YA KUMALIZA KUTUMIA.

Na WAMJW- DSM

Serikali kupitia Wizara ya Afya, imetoa wito kwa wananchi kuteketeza Barakoa zao vizuri baada ya kumaliza matumizi yake kisha kuitupa sehemu salama ili kuepusha kusambaa kwa magonjwa ya mlipuko hususan ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Wito huo, ameutoa Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

"Wale ambao mmevaa Barakoa (mask) zile ambazo zinatakiwa kutupwa baada ya kutumika (disposable mask) , ukumbuke kabla hujaitupa uitoboe ili mtu mwingine asiweze kuiokota na kuisafisha na kuirudisha katika mzunguko jambo litalosaidia kuepusha magonjwa ya mlipuko hususan ugonjwa wa Corona" alisema.

Alisema, katika baadhi ya nchi imethibitika kuwa, mgonjwa mmoja wa Corona anaweza kuambukiza mpaka watu kumi kwa wakati mmoja hii inatokana na mwingiliano uliopo baina ya watu, hivyo kutoa wito juu ya kuchukua tahadhari kwa hali ya juu.

"Kwa baadhi ya nchi zilizopata maambukizi, inasemekana kuwa, mtu mmoja aliyeambukizwa virusi hivi anauwezo wa kuambukiza mpaka watu kumi kwa wakati mmoja" alisema.

Aidha, alisema kuwa, kwa wale ambao wanatumia Barakoa za kitambaa, kuhakikisha wanabadirisha mask hizo kila baada ya masaa manne ili kuepusha kupata magonjwa mengine, huku akisisitiza kuwa, ni muhimu kabla ya kuivaa zifuliwe kwa maji na sabuni kisha ipigwe pasi ili kujiweka salama zaidi dhidi ya magonjwa.

"Kwa wale ambao mnavaa Barakoa (mask) za kitambaa basi mkumbuke kuwa, mask hiyo inatakiwa ivuliwe kila baada ya masaa manne mpaka sita, na hakikisha kuwa, unaifua kwa maji na sabuni, umeinyoosha ili kama kuna virusi humo waweze kufa, usivae barakoa (mask) ambazo ni chafu" alisema

Kwa upande wake, Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi, alisisitiza kuwa, wazazi watoe elimu kwa watoto kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha wananawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, huku akisisitiza waepuke kuzulula mtaani kuepusha kuokota Barakoa zilizotupwa hovyo bila utaratibu.

Nae Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), amewakumbusha Watanzania kuepuka msongamano katika maeneo yote, huku akisisitiza kuwa, kama hakuna sababu yakutoka nje ni vema watulie majumbani.

Mwisho.

Jumatatu, 27 Aprili 2020

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 14.9

- Hakuna maoni









 
Na WAMJW-Dar es Salaam

Serikali  imepokea msaada wa shilingi bilioni 14.9 kutoka Global Fund, Airtel Tanzania, Rotary Club Tanzania ambazo sehemu kubwa zitatumika kununua vifaa kinga kwa watumishi wa afya na vifaa tiba kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wenye maambukizi ya COVID-19.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo wakati akipokea msaada wa fedha na lita 1,250 za vitakasa mikono ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona.

Waziri Ummy amefafanua kwamba Global Fund imetoa shilingi bilioni 14, Airtel Tanzania shilingi milioni 700 na Rotary Club Tanzania shilingi milioni 250.

“Tumepokea shilingi bilioni 14 kutoka Global Fund, shilingi bilioni 9.6 tumezitoa kwa ajili ya kununua vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa Afya, lakini pia fedha zilizotolewa na Airtel na Rotary Club Tanzania tutazielekeza huko. Kipaumbele chetu ni kuwalinda watumishi wa afya,” amesema Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.

“Natumia fursa hii kuwashukuru watumishi wa afya ambao wamekuwa wakijitoa usiku na mchana katika kutoa huduma kwa watu waliopata maambukizi ya virusi vya Corona (Covid-19) pamoja na wale wahisiwa.

"Kipaumbele cha Serikali ni kuwalinda watumishi wa Afya kwa kununua vifaa kinga kwani fedha tulizozipata hapa tutazielekeza kwenye ununuzi wa vifaa kinga.  Niendelee kuwaisistiza Watumishi wa Afya wazingatie miongozo ya magonjwa ya kuambukiza,” Amesema Waziri Ummy .

Amesema watumishi wa afya ambao wamepatiwa mafunzo katika vituo vya kutoa huduma kwa wenyr maambukizi ya  ugonjwa huo,  hakuna aliyepata maambukizi kwa kuwa wanazingatia miongozo ya Serikali ya kutoa matibabu kwa wagonjwa wa Covid-19 pamoja na miongozo ya magonjwa ya kuambukiza.

Waziri amesema ushiriki wa kila mdau katika mapambano dhidi ya maambikizi ya virusi vya Corona ni muhimu na kwamba msaada uliotolewa na kampuni hizo ni mkubwa katika mapambano ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

“Napenda kurudia tena kwa niaba Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, nawashukuru Airtel Tanzania, Serengenti Breweries na Rotary Club kwa hiki mlichotupatia. Asanteni sana,” amesema Waziri Ummy.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Gabriel Malata amesema Airtel Tanzania imetoa shilingi milioni 700 ikiwa ni sehemu ya  kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na janga la Corona.

“Sisi bodi ya wakurugenzi wa Airtel na kwa niaba ya Airtel Tanzania, tunatambua juhudi za Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Corona, lakini pia tumejitathimini na kutambua kuwa sisi kama 

Airtel hatuwezi kuendelea bila kuwepo watu wanaotumia huduma zetu. Watu hawa ndio mtaji wa Kampuni,” amesema Bw. Gabriel.

Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia ya Serengenti, Bw. John Wanyancha amesema kuwa kampuni hiyo imetoa lita 1,250 ya vitakasa mikono nyenye thamani ya shilingi milioni 15  kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na maambukiza ya virusi.

Mwenyekiti wa Rotary Club, Bi. Agnes Batenga amesema Rotary imetoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya kupambana na ugonjwa wa homa ya mapafu (COVID-19).

“Shilingi milioni 183 zitatumika kutoa msaada wa vifaa vya kujikinga (PPE), vifaa vya maji safi ambavyo vitasambazwa katika vituo maalumu vya kuhudumia wagonjwa wa Corona jijini Dar es Salaam, Hospitali ya Amana, Zanzibar, Hospitali ya Mawenzi na Hospitali ya Mount Meru,” amesema Bi. Agnes.

Amesema shilingi milioni 67 zitatumika katika kutekeleza miradi ya kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini kupitia Club za Rotary.

Jumapili, 26 Aprili 2020

TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA - ASP SWEBE

- Hakuna maoni
Mrakibu mwandamizi wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam ASP Edith Swebe akieleza jambo mbele ya timu ya uhamasishaji wa elimu juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona katika kituo cha polisi Pangani Ilala.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR wakiendelea na uhamasishaji jinsi  ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa abilia na bodaboda katika kituo cha daladala cha Mbezi kwa Msuguli.

Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi akiongea na madereva boda boda wa kituo cha Mbezi mwisho Jijini Dar es Salaam juu ya tahadhari za kuchukua ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Flavour) Banana Zolo akinawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, ishara ya kuunga mkono kampeni ya kusafisha mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kama moja ya nyenzo ya kupambana dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkazi wa Mbezi Mwisho Jijini dar es salaam aliyeweka uzio wa kamba kwenye duka lake kujitenganisha na mteja, inayosaidia kumzuia mteja kuingia dukani kabla ya kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka na kuzuia mteja asikae karibu nae wakati anamhudumia, ikiwa ni muitikio chanya kutoka Wizara ya Afya wa kukaa mita moja au zaidi baina ya mtu mmoja na mwingine na kusafisha mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kabla ya kupata huduma yoyote ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), pamoja na askari polisi kituo cha polisi Pangani Ilala wakinyoosha mikono, ishara ya kuunga mkono kampeni ya mikono safi, Tanzania salama inayohamasisha kunawa mikono kwa sabuni  na maji safi yanayotiririka.



TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA - ASP SWEBE

Na WAMJW- DSM

Mrakibu mwandamizi wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam ASP Edith Swebe ametoa wito kwa wananchi, hususan Wana Dar es Salaam kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Ameyasema hayo wakati akiwa katika majukumu yake ya ukaguzi wa namna gani kituo cha Polisi Pangani kilichopo Ilala Jijini Dar es Salaam kimechukua hatua ya kukabiliana dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

"Tunaendelea kukumbusha Wananchi wa hususan Wanaotoka Jijini Dar es Salaam kunawa mikono na kuchukua hatua zote za tahadhari zinazotakiwa, tunaendelea kusisitiza kila mmoja katika familia yake aendelee kuchukua hatua ambazo Wizara ya Afya inapendekeza" alisema

Kwa upande mwingine, ASP Swebe ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuja na kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayohamasisha wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona, hali inayoonesha jinsi gani Serikali imewekeza kwenye Afya ya wananchi.

"Kwanza nitoe shukrani kwa Serikali kupitia Wizara ya Afya, kwa Kampeni inayoendelea ya "Mikono safi, Tanzania salama", hii inaonesha ni jinsi gani Serikali imewekeza kwenye Afya ya wananchi" alisema.

Aidha, ameishukuru Wizara ya Afya kwa kuendelea kulisaidia Jeshi la polisi vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona ikiwemo vitakasa mikono na Barakoa (mask).

Kwa upande wake, Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi, amewataka madereva wote wa vyombo vya moto hususan bodaboda na bajaj kuhakikisha wanavitakasa vyombo vyao vya usafiri kwa sabuni mara kwa mara ili kuua maambukizi ya virusi vya Corona endapo vitakuwepo.

Uhamasishaji huu unafanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inaratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam.

Mwisho

Ijumaa, 24 Aprili 2020

WAGONJWA 37 WA CORONA WAPONA NA KURUHUSIWA HUKU 71 WAKISUBIRI VIPIMO VYA MWISHO

- Hakuna maoni


Na.WAMJW-Dar es Salaam

Wagonjwa 37 waliokuwa wameambukizwa virusi vya Corona (COVID-19) wamepona na kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya vipimo vya mwisho kuthibitisha kwamba hawana maambukizi ya COVID-19.

Hayo yamesemwa leo  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akipokea msaada wa sabuni na fedha kutoka kampuni ya Azania group ya jijini hapa

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa wagonjwa hao 37 ni kati ya wagonjwa 108 waliothibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona lakini hivi sasa hawana dalili zozote za ugonjwa kama homa, mafua na kikohozi.

“Watu hawa 108 hawana dalili zozote za ugonjwa kama vile homa au mwili kuchoka isipokuwa wapo katika vituo vya matibabu kusubiri vipimo vya mwisho ili kuthibika kwamba hawana virusi vya corona kabla ya kuruhusiwa kutoka vituoni, hivyo wamepona na wameruhusiwa kurejea nyumbani,” amesema Waziri wa Afya.

Waziri Ummy Mwalimu amewataka watu waliopona ugonjwa huo kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ili kujikinga na maambukizi mapya ya COVID-19 kwani zipo tafiti zilizofanyika nchi mbalimbali ikiwamo China zimeonyesha kuwa watu wanaweza kupata  maambukizi mapya kama asilimia 14.

“Tunapenda kuwahimiza watu waliopona watoe elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) kwa jamii. Pia, Nitumie fursa hii kwa niaba ya Serikali  kutoa shukrani zetu za thati kwa watumishi wa afya kwa kuendelea kutoa huduma kwa watu wenye maambukizi ya COVID-19. Asanteni sana watumishi wa afya,” amesema Waziri.

Waziri pia ametoa wito kwa watumishi wa afya kuendelea kutoa huduma za afya kwa watu wote wanaohitaji huduma za matibabu wakiwamo wenye dalili za ugonjwa wa Corona.

“Tumeona kumeanza tabia ambayo ni kinyume na taratibu za afya, hatutakiwi kuwakataa wagonjwa wenye dalili za maambukizi ya virusi vya Corona. Nasisitiza kwamba watumishi wa afya wanakumbushwa kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia nwongozo wa Taifa wa kudhibiti maambukizi (National Infection Prevention and Control Guidelines for Health care Services in Tanzania) wa Juni, 2018 pamoja na mwongozo wa Menejimenti ya Matibabu ya Ugonjwa wa COVID-19 wa Januari, 2020 ili kujikinga na maambukizi wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa,” amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Wakati huo  Waziri Ummy Mwalimu ameishukuru kampuni ya Azania group kwa msaada wa sabuni 300 na fedha shilingi milioni 50 kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Msaada huo utatumika kwa chakula cha wagonjwa na usafi kwenye vituo vya tiba cha Temeke,Amana na Kisoka-Mloganzila.

Jumatano, 22 Aprili 2020

WAZAZI TUWAKINGE WATOTO WETU DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Wakazi wa eneo la Keko Jijini Dar es Salaam wakisikiliza elimu kuhusu mbinu za kujikinga wao na Watoto wao kupata maambukizi ya virusi vya Corona kutoka kwa timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR.

Dereva boda boda wa eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam wakisikiliza elimu kuhusu mbinu za kujikinga kupata maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akikabidhi vitakasa mikono kwa askari wa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani ili viwasaidie kujilinda dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona wakati wa kutoa huduma kwa wananchi, katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), akikabidhi boksi la vitakasa mikono (sanitizer) Mrakibu msaidizi wa polisi (ASP) Angelica, makao makao makuu ndogo ya jeshi la polisi, Posta Jijini Dar es Salaam.

Afisa kutoka jeshi polisi kitengo chaushrikishaji jamii Stafu Sajenti Valentino Ngowi akiongea na Dereva boda boda na Bajaji, kuhusu elimu ya kujikinga kupata maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkurugenzi wa Lemutuz Brand, vyombo vya utoaji habari za kwa njia ya mtandao, Ndg. Lemutuz akinawa mikono yake kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji kwa wananchi juu ya kunawa mikono, kama moja ya njia ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR na kampuni ya Mjomba Gallery ikiendelea na utoaji elimu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.



WAZAZI TUWAKINGE WATOTO WETU DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Na WAMJW- DSM

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa wito kwa wazazi na walezi nchini kuwalinda Watoto wao dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha wanajikinga vizuri na kuwakinga watoto wao dhidi ya virusi hivyo,

Wito huo ameutoa, Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona

Ndg. Anyitike Mwakitalima amesema kuwa, Watoto wanaweza kuwa chanzo cha kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya Corona katika jamii na familia, hivyo amesisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanawadhibiti watoto kuzulula mitaani katika kipindi hiki cha mlipuko wa virusi hivyo.

"Serikali kupitia Wizara ya Afya inatoa wito ambao inautoa ni kwamba wazazi na walezi tukumbuke kuwalinda watoto wetu, wakae na watulie majumbani kwa kipindi hiki shule zimefunga, msiwaruhusu waende kuzulula maeneo mbali mbali, kwani wanaweza kupata maambukizi huko wanakoenda kucheza" alisema.

Mbali na hayo, alisisitiza kuwa, wazazi watoe elimu kwa watoto kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha wananawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, huku akisisitiza waepuke kushika macho, pua na mdomo ili kuzuia kupata maambukizi hayo.

"Wazazi na walezi tuwakumbushe Watoto kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, tuwakumbushe Watoto kuepuka kushika pua, mdomo na macho kwa mikono kwa kufanya hivyo tutakuwa tumewalinda watoto watoto wetu na tutajilinda sisi wenyewe kupata maambukizi ya virusi vya Corona " alisema

Kwa upande wake, Afisa kutoka jeshi polisi kitengo chaushrikishaji jamii Stafu Sajenti Valentino Ngowi amewaagiza madereva na makondakta wao kuhakikisha kila siku jioni wanapokuwa wamemaliza kazi zao Kutakasa magari yao kwa dawa maalum aina ya jiki, ili kuua virusi vinavyoweza kuwepo na kupelekea maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

Nae Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), amewakumbusha Watanzania kufuata maelekezo ya Wataalamu wa Afya ikiwemo kuepuka msongamano katika maeneo yote, huku akisisitiza kama hakuna sababu yakutoka nje ni watulie majumbani.

“Nitumie fursa hii kuwakumbusha Watanzania kuendelee kufuata maelekezo ya wataalam wa afya, ikiwemo kuepuka misongamano isiyo na ulazima, na kama huna sababu ya kutoka nyumbani ni vyema ukabaki nyumbani" alisema

Mwisho.

Jumanne, 21 Aprili 2020

SERIKALI YAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA

- Hakuna maoni






Na WAMJW – Dar es Salaam

Serikali imepongezwa kwa jitihada inazozifanya katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19) hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na mwakilishi wa Ubalozi wa Pakistani hapa nchini Muhammad Saleem wakati akikabidhi vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Saleem alisema tangu ugonjwa huo ulipoingia  hapa nchini mwezi uliopita kasi ya maambukizi ni ndogo ukilinganisha na nchi zingine, hiyo yote ni kutokana na hatua thabiti zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na ugonjwa huo.

“Nchi yetu ya Pakistani imekuwa na ushirikiano mzuri na Tanzania, hivyo basi  tumeona nasi tutoe msada wa vifaa kinga. Tunaomba mpokee mchango wetu ambao ni kidogo ili watoa huduma wa afya waweze kutumia vifaa hivi wakati wanawahudumia wagonjwa kwani ugonjwa huu ni janga la Dunia”, alisema Saleem.

Mwakilishi huyo wa Ubalozi wa Pakistani aliishauri Serikali kuendelea kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii katika kutoa elimu ya ugonjwa wa COVID-19  ili wananchi waendelee kupata elimu ya kutosha ambayo itawasaidia kujikinga na ugonjwa huo.

Kwa upande wake mganga mkuu wa Serikali Prof. Muhamad Bakari Kambi aliushukuru Ubalozi wa Pakistani kwa msaada walioutoa na kusema kuwa utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Prof. Kambi alisema ugonjwa wa COVID -19 ni janga la Dunia,  watu wengi wamepata madhara kutokana ugonjwa huo hivyo basi hakuna msaada mdogo. "Msaada wowote unaotolewa kwa Serikali utanasaidia kwa kiasi kukubwa katika kukabiliana na ugonjwa".

Ubalozi wa Pakistani umetoa msaada wa barakoa za upasuaji 1800, kofia ambazo zinavaliwa na  wahudumu wa afya wakati wanahudumia wagonjwa 1800, kava za viatu za kuvaliwa wodini 800, barakoa za N95 zipatazo 500, magauni ya kuvaa watoa huduma za afya 100, glovu 8000 pamoja na miwani ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona  60. Thamani ya vifaa hivyo ni zaidi ya milioni 11.

Mwisho