Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 19 Aprili 2020

TUACHE MZAHA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Wafanya biashara ndogo ndogo katika kituo cha mabasi Makumbusho wakipata mafunzo juu ya namna yakunawa mikono kwa sabuni na maji yanayotiririka wakati,   elimu ya kujikinga dhidi ya Corona ilipokuwa ikitolewa kituoni hapo.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira kutoka Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akiwaelekeza madereva bajaji namna ya kunawa  kwa kufuata taratibu za unawaji mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kwa usahihi kulingana na miongozo ya Wizara.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira kutoka Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akielekeza  jambo wakati wa kampeni ya uhamasishaji kwa Jamii juu ya namna ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), akisisitiza jambo kwa wafanyabiashara katika eneo la Coco Beach Dar es salaam juu ya umuhimu wa kuchukua tahadhari wakati wote ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) akisisitiza kukaa umbali wa mita moja au zaidi ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona pindi watu wanapoongea au mtu anapopiga chafya au kukohoa.


TUACHE MZAHA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Na WAMJW- DSM

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ndg. Anyitike Mwakitalima ametoa wito kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kuacha mzaha na kufuata taratibu kutoka kwa Wataalamu wa Afya ili kujikinga dhidi ya virusi vya Corona.

Ameyasema hayo leo, wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona

"Watanzania tusifanye mzaha, huu ugonjwa sio wakufanyiwa mzaha, wenzetu wa nchi zilizoendelea pamoja na uchumi wao kuwa mkubwa na sayansi yao kubwa, lakini wamefika mahali wameshindwa, hizi tahadhari za msingi ambazo tunaelekeza ni muhimu kuzizingatia " alisema.

Alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Afya, inaendelea kutoa elimu ya Corona kwa jamii kupitia vyombo vya habari, lakini pia kuwafuata wananchi walipo ili kuwapa elimu hiyo na kujibu maswali yanayowatatiza, hali itayosaidia watu kufahamu njia zote za kujikinga na kuepuka kupata maambukizi ya virusi hivyo.

"Tunafahamu kwamba , bado suala la elimu halijaweza kufika kwa Jamii vyakutosha, kwahiyo tunatumia njia mbali mbali, tunatumia vyombo vya habari kama tv na redio, lakini tumeona tunakila sababu yakushuka na kwenda ambako Jamii hipo ili tuweze kuzungumza nao, na kujibu maswali ya msingi yanayowatatiza" alisema.

Aidha, alisema kuwa, kwa sehemu kubwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanachukua tahadhari, kwa kuweka vifaa vya kunawia mikono na sabuni, na kusafisha mikono ya abiria kabla yakupenda usafiri.

"Kwa sehemu kubwa tumeona wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanachukua tahadhari, ikiwemo kutengeneza jiki kwaajili yakutakasa chombo chake cha usafiri, lakini katika sehemu za biashara watu wameweka vyombo vya kunawia mikono na wanaelekezwa kunawa kabla ya kufanya manunuzi" alisema

Nae Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) amewaasa wananchi kunawa mikono mara kwa mara kwa kufuata hatua tano muhimu, kama ifuatavyo moja ni kulowanisha mikono, pili kupakaa sabuni kwenye mikono ili kuua virusi vyote, tatu ni sugua mikono yako kwenye kucha, viganja, vidole na sehemu zote, nne ni kusuuza mikono kwa maji yanayotiririka, na hatua ya tano ni kufuta mikono kwa kitambaa safi.

Aliendelea kusisitiza kuwa, kulingana na miongozo kutoka kwa Wataalamu wa Afya, hairuhusiwi kufuta mikono kwenye nguo baada ya kunawa mikono kwenye hatua tano, kwani kufanya hivyo hupelekea kurudisha maambukizi mikononi endapo vitakuwepo katika nguo hizo.

Uhamasishaji huu unafanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inaratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam.

Mwisho

0 on: " TUACHE MZAHA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA"