Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 21 Aprili 2020

SERIKALI YAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA







Na WAMJW – Dar es Salaam

Serikali imepongezwa kwa jitihada inazozifanya katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19) hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na mwakilishi wa Ubalozi wa Pakistani hapa nchini Muhammad Saleem wakati akikabidhi vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Saleem alisema tangu ugonjwa huo ulipoingia  hapa nchini mwezi uliopita kasi ya maambukizi ni ndogo ukilinganisha na nchi zingine, hiyo yote ni kutokana na hatua thabiti zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na ugonjwa huo.

“Nchi yetu ya Pakistani imekuwa na ushirikiano mzuri na Tanzania, hivyo basi  tumeona nasi tutoe msada wa vifaa kinga. Tunaomba mpokee mchango wetu ambao ni kidogo ili watoa huduma wa afya waweze kutumia vifaa hivi wakati wanawahudumia wagonjwa kwani ugonjwa huu ni janga la Dunia”, alisema Saleem.

Mwakilishi huyo wa Ubalozi wa Pakistani aliishauri Serikali kuendelea kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii katika kutoa elimu ya ugonjwa wa COVID-19  ili wananchi waendelee kupata elimu ya kutosha ambayo itawasaidia kujikinga na ugonjwa huo.

Kwa upande wake mganga mkuu wa Serikali Prof. Muhamad Bakari Kambi aliushukuru Ubalozi wa Pakistani kwa msaada walioutoa na kusema kuwa utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Prof. Kambi alisema ugonjwa wa COVID -19 ni janga la Dunia,  watu wengi wamepata madhara kutokana ugonjwa huo hivyo basi hakuna msaada mdogo. "Msaada wowote unaotolewa kwa Serikali utanasaidia kwa kiasi kukubwa katika kukabiliana na ugonjwa".

Ubalozi wa Pakistani umetoa msaada wa barakoa za upasuaji 1800, kofia ambazo zinavaliwa na  wahudumu wa afya wakati wanahudumia wagonjwa 1800, kava za viatu za kuvaliwa wodini 800, barakoa za N95 zipatazo 500, magauni ya kuvaa watoa huduma za afya 100, glovu 8000 pamoja na miwani ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona  60. Thamani ya vifaa hivyo ni zaidi ya milioni 11.

Mwisho

0 on: "SERIKALI YAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA"