Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 20 Aprili 2018

HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA AFYA 2018/2019





Katika kipindi cha Mwaka 2017/2018, Wizara ilisimamia shughuli za utoaji wa chanjo kwa   watoto ili kuhakikisha kuwa malengo yaliyowekwa kitaifa na kimataifa yanafikiwa. Takwimu za Januari hadi Desemba 2017 zinaonyesha kuwa asilimia101.2 ya Watoto waliolengwa nchini walipatiwa chanjo zote muhimu ili kuwakinga na magonjwa.  Mnamo mwezi Desemba 2017, Serikali yaTanzania ilipongezwa Shirika la Afya Duniani na wadau wa Kimataifa wa Chanjo kwa kufikia kiwango cha juu chachanjo kwa asilimia 97 ya uchanjaji watoto kwa chanjo ya pentavalent kwa takwimu za mwaka 2016. Lengo la Mkakati wa Dunia kupitia Shirika la Afya
Duniani ni nchi kufikia kiwango cha uchanjaji wa asilimia 90. Mikakati ya Wizara imewezesha nchi yetu kufikia kiwango hicho ambapo inakuwa nchi ya Tatu barani Afrika ikitanguliwa na Zambia yenye kiwango cha asilimia 99 ikifuatiwa na Rwanda yenye asilimia 98

Hotuba nzima, bofya link ya chini hapa.
http://afyablog.moh.go.tz/2018/04/hotuba-ya-waziri-wa-afya-maendeleo-ya.html

Jumatano, 11 Aprili 2018

ALICHOSEMA MAKAMU WA RAIS KATIKA UZINDUZI WA CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI

- Hakuna maoni


Katika ufunguzi huo uliofanyika jana jijini Dar es salaam Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan alisema kuwa chanjo hiyo imewalenga wasichana wote wanaotimiza umri wa miaka 14 ili kuanza kujikinga mapema na ugonjwa huo. 

"Ili kupata kinga kamili,  wasichana watahitajika kupata dozi mbili ambapo dozi ya kwanza itatolewa muda wowote binti anapofikisha umri wa miaka 14 na dozi ya pili itatolewa miezi site baada ya kupata dozi ya kwanza"alisema Mhe. Samiah Suluhu.

Ijumaa, 6 Aprili 2018

CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NI SALAMA, WAZIRI UMMY

- Hakuna maoni


Mhe. Ummy Mwalimu (MB) awatoa hofu viongozi wa dini pamoja na wananchi kwa ujumla kwamba chanjo hii haizuii binti kutopata watoto katika maisha yake ya baadae bali ni kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi".  Kinga ni bora kuliko tiba, hivyo ni vyema tukashirikiana kuweza kuwaokoa mabint wetu na vifo".

Chanjo mpya ya kuwakinga wasichana wenye umri wa miaka 14 dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi itaanza kutolewa mara baada ya uzinduzi wa kitaifa tarehe 10 Aprili, 2018 na itahusisha mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar pia itatolewa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya Serikali, binafsi na huduma mkoba kwenye shule na sehemu mbalimbali. Chanjo hii itatolewa mara mbili ili kupata kinga kamili(chanjo ya pili itatolewa baada ya miezi sita)

Alhamisi, 5 Aprili 2018

WAWEKEZAJI 38 WAONESHA UTAYARI UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA NA VIFAA TIBA,...

- Hakuna maoni


Aliyoyasema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. UMMY MWALIMU katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini, kilichokutanisha wadau mbalimbali wa Uwekezaji katika Sekta ya Dawa, Vifaa na Vifaa tiba

Alhamisi, 29 Machi 2018

HOSPITALI YA KANDA YA RUFAA MBEYA YAPIGA HATUA KATIKA KUMALIZA TATIZO LA WAGONJ...

- Hakuna maoni


Ameyasema hayo Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Godlove Mbwanji katika ofisi yake jijini Mbeya, 
Dkt. Mbwanji hakusita kuupongeza Uongozi na Wafanyakazi wa Hospitali hiyo kwa kujitoa kwa moyo katika kuwatumikia wananchi, pia aliwashukuru wananchi wa Mbeya hususani madereva wa Boda boda kwa moyo wakujitolea katika kuboresha Sekta ya Afya ikiwemo kutoa michango yakifedha.

Jumanne, 27 Machi 2018

DKT. MAGUFULI ATHIBITISHA UWEPO WA DAWA ZAKUTOSHA

- Hakuna maoni


ILI kufikia katika uchumi wa kati kwakutumia sekta ya viwanda Serikali inatak iw a kujikita katika kuimarisha sekta ya afya kwa watanzania ili kuwa na rasilimali watu wenye afya njema kwa ajili yakuleta mafanikio hayo kupitia viwanda.
Hayo yamesemwa na Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa magari 181ya kusambazia dawa uliofanyika leo katika Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD) jijini Dar es salaam.
“Tunatakiwa kuwekeza kwenye uchumi wa Viwanda ili tufikie uchumi wa kati hivyo ni lazima tuwekeze kwenye sekta ya afya kwa kiwango kikubwa ili kuwa na wananchi wenye afya njema tayari kutumikia viwanda vyetu kwa muda wote” alisema Rais Magufuli.
Aidha Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania inatakiwa kujijengea viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini ili fedha zinazotumika kununua bidhaa hizo nje ya nchi zirudi mikononi kwa watanzania wenyewe pamoja na kutoa ajira kupitia viwanda hivyo.
Mbali na hayo Rais Magufuli amesema kuwa katika kuimarisha Sekta ya afya Serikali imetenga shilingi Bilioni 269 za kununua dawa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kutoka bilioni 31 katika bajeti ya fedha mwaka 2016/2017.
Kwa upande wake Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa katika kuimarisha Afya ya mama na Mtoto Serikali imepunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa asilimia 60 kutoka asilimia 20 ya upunguzaji wa vifo hivyo.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya dawa zina mawanyo ikiwemo asilimia 42 zahanati na vituo vya afya ,asilimia 16 zinatumika kwa chanjo za watoto ,asilimia 10.2 zianenda hospitali za wilaya ,asilimia  6.8 zinatumia hospitali za mikoa ,asilimia 3.4 zinaenda hospitali maalum na asilimia 3 zinatumika kwa ajili ya dawa za saratani.

Ijumaa, 23 Machi 2018

AGIZO LA WAZIRI UMMY KWA WAGANGA WAFAWIDHI

- Hakuna maoni




Nawaagiza waganga wafawidhi wote wa hospitali na vituo vya huduma kuhakikisha watoto wote wanaoanza shule za bweni wanafanyiwa uchunguzi wa TB kikamilifu kabla ya  kuanza masomo.

Ameyasema hayo mapema leo katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dodoma wakati akitoa tamko la Kifua Kikuu (TB) mbele ya Waandishi wa habari.

Jumatano, 21 Machi 2018

MAJUMUHISHO KIKAO MAWAZIRI WA ECSA

- Hakuna maoni



 Mkutano wa 65 wa Jumuiya ya Mawaziri wa Afya wa Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA umemalizika leo jijini hapa kwa nchi wanachama kukubaliana maazimio mbali mbali yanayolenga  kutekeleza kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kama vile kisukari, saratani, magonjwa ya moyo na ya mfumo wa hewa.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema makubaliano hayo yamelenga kuimarisha na kuboresha sekta hiyo na afya ya wananchi kwa ujumla.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa  wamekubaliana pia kuongeza uwajibikaji kwenye afya ya mama na mtoto ili kuepusha vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.

“Tumekubaliana kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza tumegundua katika nchi hizo magonjwa
yanayoongoza ni pamoja na kisukari, saratani, magonjwa ya moyo na ya mfumo wa hewa" alisema Waziri Ummy.

Kwa mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa Suala lingine walilokubaliana ni kutilia mkazo suala la heshima kwa wajawazito kwa sababu mawaziri wameshauri pia Tanzania kukitambua Chuo cha Upasuaji cha Afrika Mashariki, Kati na Kusini.  

Waziri Ummy ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, amesema wamkubaliana wamekubaliana pia kuimarisha ushirikiano na ulinzi katika maeneo ya mipaka.

DALILI ZA DENGUE HIZI HAPA, MHE. UMMY MWALIMU

- Hakuna maoni



WAZIRI wa Afya, Maendeleo yaJamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu a mewashauri wananchi kwenda vituo vya tiba haraka mara baada ya kugundua kuwa wana dalili za ugonjwa wa dengue.

Hayo ameyasema wakati alipotoa tamko juuya kuingia kwa ugonjwa wa dengue hapa nchini mara baada ya kufunga Mkutano  wa 65 wa Jumuiya ya Mawaziriwa Afya wa Nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini ECSA leo jijini Dar essalaam.

“Kuna dalili za Ugonjwa Dengue zikiwemo homa ya ghafla, kuumwa kichwa hususan sehemu za macho, maumivu ya viungo  na uchovu. Dalili hizi huanza kujitokeza kati ya siku 3 hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa virusi vya homa ya Dengue hivyo Wizara inashauri kuwa wananchi wasiwe na hofu, bali mara tu  anapoona dalili za ugonjwa waende katika vituovya tiba" alisema Waziri Ummy.

Jumamosi, 17 Machi 2018

JIEPUSHENI NA RUSHWA, MHE. UMMY MWALIMU

- Hakuna maoni




WATUMISHI wa sekta ya Afya nchini wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kutaka rushwa kutoka kwa wananchi wanapokuwa sehemu zao za kazi ili kuendana na maadili ya utumishi wa Umma. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini  Dar es salaam ili kujadili mustakabari wa utoaji huduma za Afya nchini. 

"Marufuku Watumishi wa sekta ya afya nchini kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa na kama wapo naomba waache mara moja kwani atakayebainika anajihusisha na rushwa sheria itafuata mkondo wake mara moja" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa watumishi wa sekta ya afya hasa katika sehemu ya kutolea huduma za afya wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi pindi wanapotoa huduma sehemu zao za kazi. 

Mbali na hayo Waziri Ummy amewaambia watumishi wa sekta ya afya kuwa kipaumbele katika kutoa elimu juu ya magonjwa yasioambukiza kwani yamekuwa yakiongezeka kila kukicha kutokana na ukosefu  elimu ya kutosha kuhusu magonjwa hayo. 

"Watumishi wa Afya wanatakiwa kuwa mfano hasa katika kufanya mazoezi,  kula lishe bora pamoja na kutoa elimu ya magonjwa mbalimbali ili kuisaidia kuondoa ongezeko la magonjwa yasioambukiza" alisema Waziri Ummy. 

Jumatatu, 12 Machi 2018

ALIYOYASEMA NAIBU WAZIRI WA AFYA KATIKA SIKU YA MACHO

- Hakuna maoni

MATEMBEZI YA SIKU YA FIGO DUNIANI

- Hakuna maoni

Ijumaa, 9 Machi 2018

ZIARA YA MHE. UMMY MWALIMU WILAYA YA ILEJE, SONGWE

- Hakuna maoni

MAGONJWA YA FIGO YANAATHIRI ZAIDI WANAWAKE

- Hakuna maoni

Jumatano, 28 Februari 2018

SERIKALI YATARAJIA KUWA NA WATOA HUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII ZAIDI YA ...




SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inatarajia kuwa na watoa huduma wa Afya ngazi ya jamii (CHWz) Zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka 2020 katika vijiji Zaidi ya 15,000 nchini.
Hayo yamesemwa leo na  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu  katika Mkutano wa Wadau wa Afya, mashirika yasiyo Yakiserikali, na Serikali katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.
“Tunataka itakapofika mwaka 2020, tuwe na angalau Wahudumu wa Afya zaidi ya 30,000 katika vijiji Zaidi ya 15,000 tulivyonavyo Tanzania, Eneo hili tumeliona ni eneo muhimu kwasababu tutapata matokeo ya haraka, ni bora kutumia Bilioni 40 kwa ajili ya kinga ya magonjwa kwa Watanzania .” Alisema Mhe. Ummy Mwalimu.
Mhe. Ummy alisema kuwa lengo la Mkutano huo ni kujadiliana na Wadau wa Maendeleo na Mashirika yasiyo Yakiserikali juu ya kuimarisha huduma ya Afya ya msingi hasa katika kuwakinga wananchi dhidi ya maradhi kupitia mikakati ambayo inakubalika kimataifa ya kuwa na watoa huduma katika ngazi ya jamii.

Jumanne, 27 Februari 2018

TANZANIA KUONDOA TATIZO LA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI KWA WANAWAKE



SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imedhamiria kupambana na Saratani ya mlango wa kizazi nchini kwa kuwapa kinga wasichana kuanzia umri wa miaka 9 mpaka 14 ili kuondoa tatizo hilo nchini.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (MB) mapema leo wakati akifungua mkutano wa wadau wa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi jijini Dar es salaam.

“Katika kukabiliana na ugonjwa wa Saratani, kuimarisha afya ya wanawake Tanzania pamoja na kupunguza vifo vitokanavyo na Saratani , Wizara ya Afya itaanza kutoa chanjo ya kuwakinga wasichana dhidi ya Saratani ya mlango wa kizazi mwaka huu”. Alisema Mhe. Ummy Mwalimu.

Jumatatu, 26 Februari 2018

TANZANIAI YAPOKEA TUZO YA KUPAMBANA NA UGONJWA WA MALARIA KUTOKA SHIRIKA ...






SERIKALI ya Jamhuri wa Muungano Tanzania imepata tuzo kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kutambua mchango mkubwa uliofanywa katika jitihada ya kudhibiti Ugonjwa wa Malaria nchini.
Akikabidhiwa Tuzo hiyo wakati wa mkutano wa siku mbili ulioanza leo wa kujadili mafanikio na changamoto katika kudhibiti Malaria,Mganga Mkuu wa Serikali  Profesa Muhammad Bakari Kambi alisema tuzo hiyo imetolewa kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla na Shirika hilo  kanda ya Tanzania

Ijumaa, 23 Februari 2018

SERIKALI YAPANGA KUSITISHA UTOAJI HUDUMA YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA K...

- Hakuna maoni














SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepanga kusitisha shughuli za utoaji wa huduma zinazofanywa na waganga wa tiba asili na tiba mbadala pindi muda wa kujisajili utakapokuwa umwekwisha.
Amebainisha hayo Kaimu Mkurugenzi msaidizi wa tiba asili na tiba mbadala kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Poul Mhame mapema leo pindi alipoongea na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.
“waganga wa Tiba asili na Tiba mbadala na vituo vyao watalazimika kusitisha utoaji huduma wanazotoa pindi muda wa usajili cha itafika mwisho” Alisema Dkt. Mhame

Jumatano, 21 Februari 2018

Usitumie Dawa bila ushauri wa mtoa huduma za Afya

Jumanne, 20 Februari 2018

CHUKUA TAADHARI DHIDI YA UGONJWA WA KIPINDUPINDU