Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 6 Aprili 2018

CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NI SALAMA, WAZIRI UMMY



Mhe. Ummy Mwalimu (MB) awatoa hofu viongozi wa dini pamoja na wananchi kwa ujumla kwamba chanjo hii haizuii binti kutopata watoto katika maisha yake ya baadae bali ni kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi".  Kinga ni bora kuliko tiba, hivyo ni vyema tukashirikiana kuweza kuwaokoa mabint wetu na vifo".

Chanjo mpya ya kuwakinga wasichana wenye umri wa miaka 14 dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi itaanza kutolewa mara baada ya uzinduzi wa kitaifa tarehe 10 Aprili, 2018 na itahusisha mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar pia itatolewa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya Serikali, binafsi na huduma mkoba kwenye shule na sehemu mbalimbali. Chanjo hii itatolewa mara mbili ili kupata kinga kamili(chanjo ya pili itatolewa baada ya miezi sita)

0 on: "CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NI SALAMA, WAZIRI UMMY"