Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 25 Aprili 2018

MARUFUKU KUUZA DAWA YA MALARIA.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimjulia hali mtoto aliyefika na mama yake katika Zahanati ya Mwandiga ili kupata huduma za Afya wakati akikagua ubora wa  huduma zitolewazo katika Zahanati hiyo ikiwa ni siku moja kuelekea siku ya Malaria Duniani katika Wilaya ya Kasulu Aprili 25.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimsikiliza moja ya mama aliyekuja kipata huduma katika Zahanati ya Mwandiga Mkoani Kigoma wakati akikagua ubora wa  huduma zitolewazo katika Zahanati hiyo kulia kwake ni Mkurugenzi wa USAID nchini Tanzania Andy Karas.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akigawa vyandarua kwa mmoja wa mama wajawazito katika Zahanati ya Mwandiga alipotembelea kukagua ubora wa huduma zitolewazo na Zahanati hiyo, kulia kwake ni Mbunge wa Viti maalum Iringa Rose Tweve, anaefuata ni Mkurugenzi wa USAID nchini Tanzania Andy Karas.

Mkurugenzi wa USAID nchini Tanzania Andy Karas akitoa ujumbe kutoka makao makuu ya Shirika hilo kuhusu ugonjwa wa Malaria na namna ya kujikinga, ikiwa ni kuelekea siku ya Malaria Duniani.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu   akisisitiza jambo kuhusu kinga dhidi ya ugonjwa wa Malaria katika Zahanati ya Mwandiga ikiwa ni kuelekea siku ya Malaria duniani ambayo kitaifa itakuwa katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.

Kikundi cha burudani kutoka Mwandiga Wilaya ya Kigoma mjini mkoani Kigoma kikiburudisha wananchi waliojitokeza kumsikiliza mgeni rasmi katika Zahanati ya Mwandiga , mgeni rasmi ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu kushoto kwake ni Mbunge wa Viti maalum Iringa Rose Tweve.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiwa na wadau kutoka mashirika mbali mbali wakiwa wamebeba mitungi ya kunyunyizia mazalio ya mbu wanaosababisha ugonjwa wa Malaria.






Na WAMJW-KIGOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea na msisitizo wa vituo vya Afya, zahanati na hospitali za Serikali kuacha tabia ya kuuza dawa za kutibu malaria nchini. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea zahanati ya Mwandiga iliyopo wilayani Kigoma katika kuangalia hali ya matibabu dhidi ya Malaria wilayani humo kuelekea kilele cha siku ya Malaria Duniani. 

"Nawaagiza waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini kuweka matangazo yanayoonyesha kipimo cha haraka cha Malaria , dawa Mseto za kutibu Malaria  kali ni bure kwenye kila vituo vya kutolea huduma za afya za Serikali" alisistiza Waziri Ummy. 

Aidha,Waziri Ummy amesisitiza kuwa endapo mtoa huduma yeyote atakayemtoza mwananchi malipo  ya matibabu na vipimo vya Malaria hatua stahiki itachukuliwa bila ya kumuonea huruma. 

Waziri Ummy amesema kuwa waganga wakuu wa vituo kwa ngazi ya zahanati na waganga wakuu wa wilaya kuweka namba zao za simu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini ili kuwasaidia Watanzania kutoa malalamiko yao pindi wanapopatiwa huduma ambazo za hazikidhi viwango ili kuendelea kuboresha huduma za afya nchini. 

Waziri Ummy amesema kuwa katika kujikinga na Malaria wananchi wanatakiwa kutumia vyandarua vyenye dawa, kusafisha mazingira na kuondoa mazalia ya mbu waenezao ugonjwa huo kwani kinga ni bora kuliko tiba. 

Sambamba na hilo Waziri Ummy alitoa vyandarua vyenye dawa ya kukinga  mbu aenezaye Malaria katika kijiji cha Mwandiga ili kuendelea 
 juhudi za kutokomeza Malaria nchini katika kuelekea siku ya Malaria Duniani. 

Aidha Waziri Ummy ameshiriki zoezi la kunyunyizia viuatilifu pamoja na kuzindua vikosi kazi vya kunyunyizia dawa hizo  ili kuua viluilui vinavyoweza kusababisha mazalia na ongezeko la ugonjwa wa malaria  katika kaya mbalimbali manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani humo.

Mbali na hayo Waziri Ummy alijibu kero za wazee kuhusu vitambulisho vya matibabu ambapo alisistiza mpaka Juni 15 mwaka huu vitambulisho hivyo viwe vimepatikana kwa wazee wasiojiweza na katika Kijiji cha Mwandiga Mkoani Kigoma. 


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.  Leonard Subi amesema kuwa katika  kuhakikisha Malaria inatakiwa kujikita kwenye kinga ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo. 


Siku ya Malaria Duniani huadhimishwa kila Aprili 25 kila mwaka na maadhimisho ya Mwaka huu yatafanyika wilayani Kasulu na kauli  mbiu ya mwaka huu inasema "NIPO TAYARI KUTOKOMEZA MALARIA WEWE JE?

0 on: "MARUFUKU KUUZA DAWA YA MALARIA. "