Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 10 Aprili 2018

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan akifungua mkutano wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi uliofanyika mapema leo katika viwanja vya Mbagala Zakim jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimuakimkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan akiangalia Chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi baada ya kukabidhiwa na wataalamu wa masuala ya Afya, wa kwanza kushoto ni Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy (MB).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan akikata utepe ishara ya uzinduzi rasmi wa Chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi shughuli iliofanyika mapema leo katika viwanja vya Mbagala Zakim jijini Dar es salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan akipokea sindano ya chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi kutoka mtoa huduma za Afya, kulia ni Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy (MB).

Picha ya pamoja ikiongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi uliofanyika mapema leo katika viwanja vya Mbagala Zakim jijini Dar es salaam.


Picha ya pamoja ikionesha baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi waliohudhuria kumuunga mkono Mhe. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan wakati wa uzinduzi wa chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi.


NA WAMJW-DAR ES salaam

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu  Hassan amezindua chanjo ya kukinga Saratani ya Mlango wa Kizazi ili kutokomeza vifo vitokanavyo na magonjwa hayo nchini. 

Katika ufunguzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa chanjo hiyo imewalenga wasichana wote wanaotimiza umri wa miaka 14 ili kuanza kujikinga mapema na ugonjwa huo. 

"Ili kupata kinga kamili,  wasichana watahitajika kupata dozi mbili ambapo dozi ya kwanza itatolewa muda wowote binti anapofikisha umri wa miaka 14 na dozi ya pili itatolewa miezi site baada ya kupata dozi ya kwanza" alisema Mhe. Samiah Suluhu. 

Aidha,Mhe. Samia amesema kuwa chanjo hiyo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi inatolewa bila ya malipo  pamoja na uchunguzi wake kwani Serikali imedhamiria kutokomeza tatizo hilo nchini. 

"Niwaagize Waganga wa Mikoa na Wilaya kuandaa kambi za wazi angalau mara tatu kwa mwaka ili kutoa huduma hiyo tena bila ya malipo kwa wanawake na wasichana wote nchini" alisisitiza Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu. 

Mbali na hayo Mhe. Samia Suluhu amesema kuwa takribani wasichana laki 616, 734 wanatarajia upata chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi kwa mwaka 2018 na chanjo hiyo imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani(WHO). 

Kwa upande wake Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa chanjo hii itakuwa ya saba kati ya chanjo ambazo zinatolewa kwa watoto ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali. 

"Ukiacha chanjo ya kukinga Saratani ya mlango wa Kizazi, hapa nchini chanjo nyingine zinazotolewa ni  ya kifua kikuu, Polio, Nimonia, Kuharisha ama Rota, Surua na Rubella , Donda Koo, Kifaduro, Homa ya Ini, Uti wa mgongo na Pepopunda kwa watu wazima" alisema Waziri Ummy. 

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imefanikiwa kuweka maghala  kuhifadhia chanjo katika mikoa yote nchini ambayo yana uwezo wa kuhifadhi chanjo kwa miezi sita bila ya kuharibika. 

Kwa Mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa zawadi za fedha taslimu zitatolewa kwa Mikoa mitatu itakayofanya vizuri katika utoaji wa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi hapa nchini. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema kuwa wananchi wajitokeze kwa wingi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kwenda kupata vipimo na chanjo za kukinga saratani pindi wanapogundulika wana magonjwa hayo. 

"Natoa rai kwa wananchi mliojitokeza hapa kuwapeleka watoto zenu wake zenu na wanawake wote hususan wasichana wenye umri wa miaka 14 kwenda kupata chanjo hii na mkifika majumbani kwenu muwakumbushe watu wenu wa karibu kushiriki katika upataji wa chanjo hii" alisema Mhe.  Makonda. 

0 on: "MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI"