Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 28 Aprili 2018

MATIBABU YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NI BURE.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na mmoja ya wanawake waliofika kupima Saratani ya mlango wa Kizazi katika kituo cha Ngamiani Mkoani Tanga, wakati alipozindua Kampeni hiyo Mkoani hapo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya wanawake na mabinti waliojitokeza katika kupima na kupata Chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika Kituo cha Afya Ngamiani Mkoani Tanga mapema leo.


Kundi la Wanafunzi na Mabinti waliojitokeza kumsikiliza mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (MB), wakati alipozindua kampeni ya Uchunguzi wa  Saratani ya mlango wa Kizazi na uhamasishaji kwa walezi na wazazi wa mabinti walio na umri wa miaka 14 kupata chanjo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akijumuika na kikundi cha Burudani cha ngoma cha Msanja kutoka Mkoani Tanga katika uzinduzi wa kampeni ya Uchunguzi wa  Saratani ya mlango wa Kizazi na uhamasishaji kwa walezi na wazazi wa mabinti walio na umri wa miaka 14 kupata chanjo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimuunga mkono mmoja kati ya wanafunzi waliofika katika kituo cha Afya Ngamiani kupata Chanjo ya Mlango wa Kizazi mapema leo.




Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na viongozi mbali mbali wa Serikali na mabinti waliopata Chanjo ya Mlango wa Kizazi leo katika Kituo cha Afya Ngamiani Mkoani Tanga.

Na WAMJW- TANGA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa msisitizo kwa watoa huduma za afya kutoa matibabu ya saratani ya mlango wa kizazi bila ya malipo yeyote kwa wananchi. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa kampeni ya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi  iliyofanyika leo Mkoani Tanga. 

"Uchunguzi, matibabu na chanjo ya kukinga Saratani ya mlango wa kizazi inatolewa bila ya malipo yeyote katika vituo vya afya, zahanati na hospitali zinazomilikiwa na Serikali" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa ni lazima wazazi au walezi wa watoto wanaopata chanjo waridhie ili kuweza kuwapa chanjo hiyo kwani kinga ni bora kuliko tiba. 

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Tanga Dkt. Malisely amesems kuwa lengo la Mkoa wa Tanga ni kutoa Chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wapatao 38, 000 mkoani humo. 

Aidha Dkt. Malisely amesema kuwa ni lazima tuwaelimishe na tuwaeleze wazazi umuhimu wa mtoto kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi ili kujikinga na ugonjwa huo. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Bw. Thobias Mwilakwa amesema kuwa wazazi na walezi wa Mkoa Tanga wanatakiwa kuwapeleka watoto wao kupata huduma ya chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi. 

0 on: " MATIBABU YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NI BURE. "