Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 25 Aprili 2018

MALARIA YASHUKA MPAKA ASILIMIA 7. 3 NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akipokea maelezo kutoka kwa mwakilishi wa kianda cha kutengeneza vyandarua cha (A to Z) Textile Bw. Slyvester Kazi wakati wa maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani ambayo kwa mwaka huu yanahadhimishwa leo Aprili 25 katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiwa na viongozi wa Serikali na viongozi wa mashirika mbali mbali ya kimataifa, wakiwa katika viwanja vya Umoja Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma katika maadhimisho ya siku ya Malaria duniani.

Mwakilishi kutoka mradi wa upuliziaji wa dawa ya viuatilifu ukoko majumbani  Bw. Christoper Mshana, akimpa maelekezo mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani ambayo kwa mwaka huu yanahadhimishwa leo Aprili 25 katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akionesha kitabu cha takwimu za Malaria pamoja na wadau mbali mbali wa sekta ya Afya  kilichozinduliwa leo katika maadhimisho ya siku ya Malaria duniani.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akipokea ramani ya Tanzania inayoonesha mikoa iliyopungua ugonjwa wa malaria nchini kutoka kwa Mkurugenzi wa Ofisi ya Takwimu Tanzania (TBS) Dkt. Albina Chuwa.

 Kikundi cha ngoma kutoka Umoja Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kikiburudisha Viongozi na wananchi waliofika katika viwanja vya Umoja ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani ambayo kwa mwaka huu yanahadhimishwa leo Aprili 25 katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.
Kundi la muziki wa Bongo fleva la WEUSI wakiwa jukwaani kutoa Burudani na Elimu juu ya kinga ya ugonjwa wa Malaria ambayo imehadhimishwa katika viwanja vya Umoja Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma katika maadhimisho ya siku ya Malaria duniani.

Kundi la wananchi lililojitokeza katika viwanja vya Umoja Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma katika maadhimisho ya siku ya Malaria duniani ili kusikiliza ujumbe kuhusu Malaria, mgeni rasmi wa tukio hilo ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (MB).


Na WAMJW- KASULU KIGOMA

KIWANGO cha maabukizi ya ugongwa wa Malaria nchini kimeshuka kwa nusu zaidi  kutoka asilimia 14. 4 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 7. 3 mwaka 2017. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani ambayo yamefanyika leo Wilayani Kasulu katika Mkoa wa Kigoma. 

"Katika kuhakikisha tunatokomeza kabisa ugonjwa huo Wizara ya Afya kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) tumepokea na kusambaza vitendanishi vya malaria (mRDT) , vipimo 21, 428, 725, dawa za mseto dozi 12, 916, 050 kwa ajili ya maralia isiyo kali, Sindano za kutibu Malaria kali vichupa 1, 668, 464 na vidonge vya SP dozi 6, 899, 700 kwa ajili ya tiba kinga dhidi ya athari za malaria wakati wa ujauzito" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa ili watanzania tuendelee kutokomeza kabisa ugonjwa wa malaria watanzania wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika kutumia afua zote za kupambana na ugonjwa huo ikiwemo kunyunyizia viuadudu vya kuua viluilui vinavyoweza kuleta malaria. 

Vilevile Waziri Ummy amesisitiza kuwa kila Halmashauri za kila wilaya kuunda kamati zitakazohamasisha usafi wa mazingira  ili kuondoa mazalia ya mbu katika kutokomeza malaria. 

Sambamba na hilo Waziri Ummy amezindua takwimu za  ugonjwa wa Malaria nchini ambao umefanywa na Taasisi ya Takwimu nchini NBS ambayo ndio Takwimu itayotumika na Serikali ya Tanzania. 

Kwa upande wake  Waziri Wa Elimu na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa atahakikisha wanafunzi wanapambana na ugonjwa wa Malaria kwa kuweka somo la afya kwa shule zote za msingi na sekondari nchini. 

Naye Mkuu wa Mkoa Wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emamanuel Maganga ametoa wito kwa wakazi wa kigoma kutumia vyandarua kwa matumizi sahihi na siyo kinyume na hapo ikiwemo kufungia kuku na kuvulia samaki. 

Kilele cha Maadhmisho ya Malaria kimefikia tamati leo kwa kufanyika katika wilaya ya Kasulu Mkoani kigoma ikiwa imebeba kauli mbiu isemayo "NIPO TAYARI KUTOKOMEZA MALARIA WEWE JE?

0 on: "MALARIA YASHUKA MPAKA ASILIMIA 7. 3 NCHINI"