Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 6 Aprili 2018

TAARIFA KWA UMMA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewaomba viongozi wakuu wa madhehebu ya dini kuwahimiza wananchi kuwapeleka wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14 kupata chanjo ya kuwakinga na saratani ya mlango wa kizazi inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 10 Aprili,2018 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan jijini Dar es Salaam

Waziri Ummy amesema kwamba kama viongozi wa dini ni vyema kufikisha ujumbe huu kwa waumini wao na kuwaunga mkono ili kuweza kuwafikia wasichana laki 6 nchi nzima ili kuweza kuwaokoa na vifo vipatavyo asilimia 50 vitokanavyo na saratani nchini"idadi hii ni kubwa sana,hivyo juhudi na ushirikiano zaidi vinahitajika katika kupunguza vifo hivi.

Aidha, alisema hapa nchini kati ya wagonjwa mia moja wa Saratani, wagonjwa 34 wana saratani ya kizazi". saratani  ya mlango wa kizazi inaongoza na inafuatiwa na saratani ya matiti kwa asilimia 13 ya wagonjwa wa Saratani nchini"alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo aliwatoa hofu viongozi hao pamoja na wananchi kwa ujumla kwamba chanjo hii haizuii binti kutopata watoto katika maisha yake ya baadae bali ni kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi".  Kinga ni bora kuliko tiba, hivyo ni vyema tukashirikiana kuweza kuwaokoa mabint wetu na vifo".

Chanjo mpya ya kuwakinga wasichana wenye umri wa miaka 14 dhidi ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi itaanza kutolewa mara baada ya uzinduzi wa kitaifa tarehe 10 Aprili, 2018 na itahusisha mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar  pia itatolewa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya Serikali, binafsi na huduma mkoba kwenye shule na sehemu mbalimbali. Chanjo hii itatolewa mara mbili ili kupata kinga kamili(chanjo ya pili itatolewa baada ya miezi sita)


Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-afya
6/4/2018

0 on: "TAARIFA KWA UMMA"