Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 4 Aprili 2018

SERIKALI YAWATAKA WAWEKEZAJI KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA

Wadau na Wafanyabiashara wa Sekta ya Dawa wakifuatilia kwa umakini taarifa kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha) katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya Dawa, tukio limefanyika mapema leo jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akichangia hoja mbele ya Wadau na Wafanyabiashara wa Sekta ya Dawa katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya Dawa.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akisisitiza jambo mbele ya wadau na  Wafanyabiashara katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda uliofanyika katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiteta jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage katika kikao cha Wadau wa Sekta ya Dawa katika kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Idara Kuu ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya.

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijageakiteta akimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wake Prof. Elisante Ole Gabriel.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage wakiwa na Wadau wa Sekta ya Dawa katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya Dawa na vifaa Tiba hapa nchini.


Na WAMJW. Dar es salaam.

SERIKALI yawataka Wadau wa Uwekezaji nchini kujitokeza kwa wingi kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya dawa ili kusaidia kupunguza gharama kubwa za matumizi zinazotokana na kununua, kusafirisha na kuhifadhi dawa zinazotoka nje ya nchi.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe.  UMMY MWALIMU katika kikao cha kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini, kilichokutanisha wadau mbalimbali wa Uwekezaji katika Sekta ya Dawa, Vifaa na Vifaa tiba

Waziri Ummy alisema kuwa Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya tirion moja kunuua dawa kutoka nje, hivyo kupitia uwekezaji wa viwanda vya dawa nchini itasaidia kupunguza adha hiyo nchini kwa kiwango kikubwa.

Nae Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji nchini Mhe. Charles Mwijage amewataka wote wenye nia ya kuwekeza katika Ujenzi wa viwanda vya dawa, vifaa na vifaa tiba lazima wahakikishe wanashirikiana na taasisi za Utafiti zilizopo nchini ili kuangalia mahitaji na aina dawa zinazohitajika.

Aidha, Mhe. Charles Mwijage amesema kuwa Uwekezaji na ujenzi wa Viwanda nchini utasaidia kupunguza tatizo la ajira na kuchochea Maendeleo ya ukuaji wa Uchumi katika ngazi ya watu na taifa kwa ujumla.


0 on: "SERIKALI YAWATAKA WAWEKEZAJI KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA UJENZI WA VIWANDA VYA DAWA"