Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 23 Aprili 2018

DKT. SUBI AFUNGUA MECHI YA FAINALI YA MASHINDANO YA KOMBE LA MALARIA, KIGOMA.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleoya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akikagua kikosi cha timu ya Sabasaba wakati wa mchezo wa kumtafuta bingwa wa Mashindano ya kombe la Malaria wa Wilaya ya Kigoma mjini ambae atakutana na Bingwa wa Wilaya ya Kasulu ili kumpata Bingwa wa Mkoa wa Kigoma.

Wachezaji wa timu ya Sabasaba na timu ya Ujiji Fc wakigombea mpira katika viwanja vya Tanganyika Mkoani Kigoma wakati wa mashindano ya kombe la Malaria yaliyofanyika leo katika kuelekea siku ya Malaria duniani itakayofanyika Aprili 25 mwaka huu.


Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleoya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akiongea na Wananchi waliojitokeza kushuhudia mchezo kati ya Sabasaba na timu ya Ujiji Fc katika kuelekea siku ya Malaria duniani itakayofanyika Aprili 25 mwaka huu, yenye kauli mbiu ya "Nipo tayari kutokomeza Malaria, Wewe Je".

Afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleoya Jamii,Jinsia,Wazee na WatotoWinfred Mwafongo akimkabidhi zawadi ya jezi na mipira nohodha wa timu ya Saba saba walioibuka washindi katika mchezo huo wenye lengo la kuhamasisha watu kupambana na ugonjwa wa Malaria katika Mkoa wa Kigoma.

Washindi wa Mchezo wa fainali (Sabasaba Fc) wakishangilia na baadhi ya mashabiki wao baada ya kushinda katika mchezo wa fainali ya mashindano ya Malaria uliowakutanisha na timu ya Ujiji Fc.


Na WAMJW-KIGOMA

MKURUGENZI wa Kinga kutoka Wizara ya Afya,  Dkt.  Leonard Subi amefungua mechi ya fainali kati ya timu ya  Sabasaba na Ujiji Fc kutoka Wilaya ya Kigoma Mjini ili kumpata mshindi wa mashindano ya Malaria cup ngazi ya Mkoa katika kuelekea maadhimisho ya siku ya Maralia Duniani. 

Katika ufunguzi huo Dkt. Subi amesema kuwa lengo la  michuano hiyo ni kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ambapo mshindi  wa mchezo huo atachuana na mshindi atakayepatikana Wilayani kasulu ili kumpata bingwa wa Mkoa wa Kigoma. 

"Serikali imedhamiria kuondoa ugonjwa wa malaria nchini hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana kwa pamoja ili kutokomeza ugonjwa huo na tunatakiwa kwenda kituo cha afya pindi unapohisi dalili za Malaria ili kupata vipimo na kupata dawa kama utakua una maambukizi ya ugonjwa huo" alisema Dkt.  Subi. 

Katika mchezo huo timu ya Sabasaba iliibuka na ushindi kwa jumla ya magoli 2-1 dhidi ya Ujiji fc hivyo kwenda kuchuana na timu ya Kasulu siku ya April  25 mwaka huu katika Wilaya ya Kasulu. 

Siku ya Maralia duniani huadhimishwa April 25 kila mwaka na mwaka huu maadhimisho hayo yatafanyika Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma huku Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo ni "NIPO TAYARI KUTOKOMEZA MALARIA WEWE JE? ". 

0 on: "DKT. SUBI AFUNGUA MECHI YA FAINALI YA MASHINDANO YA KOMBE LA MALARIA, KIGOMA."