Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 5 Oktoba 2018

DKT. NDUGULILE AHIMIZA USHIRIKIANO WENYE MATOKEO YANAYOONEKANA BAINA SEKTA BINAFSI NA SEKTA ZA SERIKALI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya, kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa mwaka wa Sekta Binafsi na Sekta za Serikali.




Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akimkaribisha Mgeni rasmi katika Mkutano wa pili wa mwaka wa masuala ya Afya jlioshirikisha Sekta Binafsi na Sekta za Serikali leo jijini Dar es salaam.



Mwakilishi Kutoka Sekta Binafsi Bw. akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya, kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa mwaka wa Sekta Binafsi na Sekta za Serikali.



Wadau mbali mbali kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali walioshiriki katika Mkutano wa pili wa mwaka wa Masuala ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Bank Kuu ya Tanzania (BoT) leo jijini Dar es salaam


Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile baada ya kufungua Mkutano wa pili wa mwaka wa masuala ya Afya jlioshirikisha Sekta Binafsi na Sekta za Serikali leo jijini Dar es salaam.



DKT. NDUGULILE AHIMIZA USHIRIKIANO WENYE MATOKEO YANAYOONEKANA BAINA SEKTA BINAFSI NA SEKTA ZA SERIKALI.


Na WAMJW- Dar es salaam

NAIBU WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amehimiza ushirikiano wa karibu wenye tija na matokeo yanayoonekana baina ya Sekta Binafsi na Sekta za Serikali katika kuleta Maendeleo chanya kwa wananchi.

Amesema hayo mapema leo wakati akifungua  mkutano wa pili wa mwaka wa Sekta binafsi na Sekta ya Serikali uliofanyika katika ukumbi wa Bank kuu ya Tanzania (BoT) jijini Dar ea salaam.

Dkt. Ndugulile alisema kuwa katika kuboresha Sekta ya Afya nchini, Serikali inahitaji ushirikiano wa karibu na Sekta Binafsi ili kurahisisha utoaji wa Huduma za Afya kwa wananchi, huku akisisitiza matokeo yanayoonekana katika ushirikiano wa pande hizo .

"Kusudio la Serikali ni jema kabisa, na ndomana tumeweka Sera na Sheria, sisi kama Serikali hatuwezi kuyafanya yote, tunahitaji Sekta ya Binafsi tushirikiane, Serikali iliyopo saivi madarakani inataka matokeo, hatupo hapa kukutana kila mwaka wakati hatuna mradi ulioshirikisha pande zote" alisema Dkt. ndugulile.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile ameagiza watumishi wote wa Sekta ya Afya nchini kuacha ubabaishaji pindi Sekta Binafsi zinapohitaji ushirikiano katika kuleta Maendeleo kwa wananchi na kuagiza kumchukulia hatua yeyote atakaebainika kutenda kosa hilo.

"Niwaombe sana wafanyakazi wenzangu wa Sekta ya Serikali tuache urasimu, tuangalie jinsi gani yakurahisisha ushirikiano ili mawazo mazuri yalete Maendeleo, tunataka kuwekeza katika viwanda, bado tunahitaji Huduma zakibingwa, watu wapo tayari, nataka tuache vikwazo", alisema Dkt Ndugulile

Pia, Dkt Ndugulile alitoa ushauri kwa Afisa Tabibu juu ya namna yakudhibiti matumizi ya fedha nyingi ambayo yanatumika kununua vifaa vya matibabu na mashine za maabara na thieta kwa kutoa fursa kwa Sekta Binafsi kununua na kuendesha mashine hizo huku Serikali ikijikita katika kutoa Huduma zilizo bora kwa wananchi.

"Sioni sababu ya Serikali kuingia gharama za kununua vifaa vya kutibu, maabara na thieta, kwanini tusiweke utaratibu wa watu wa Sekta Binafsi,  wawekeze kwenye vifaa, sisi kama Serikali tujikite katika kutoa Huduma, itatusaidia sana sisi kutoa Huduma bora" alisema Dkt Ndugulile.

Dkt. Ndugulile aliendelea kusisitiza kwamba , Sekta Binafsi si washindani wala maadui wa Sekta za Serikali hivyo ni lazima kuhakikisha ushirikiano unakuwa katika kutoa Huduma bora kwa wananchi, hivyo kutoa mwanya kwa yoyote mwenye wazo zuri ikiwemo ujenzi wa viwanda vya dawa kuleta wazo hilo ofisini kwake na kuahidi kulitekeleza Mara moja.

Sambamba na hilo Dkt Ndugulile alisema kuwa Serikali imedhamiria kuja na Sera ambayo itamtaka kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya ili aweze kupata Huduma za Afya, hivyo kuwataka Sekta Binafsi kuja na mawazo jinsi gani inaweza kushiriki katika kufanikisha wazo hili.


0 on: "DKT. NDUGULILE AHIMIZA USHIRIKIANO WENYE MATOKEO YANAYOONEKANA BAINA SEKTA BINAFSI NA SEKTA ZA SERIKALI"