Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 29 Septemba 2018

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI THABITI YA KUPAMBA DHIDI YA UGONJWA WA MOYO

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongoza Matembezi ya Siku ya Moyo Duniani yaliyoanzia viwanja vya Leaders Club na kumalizikia viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es sala, matembezi hayo yamebeba kauli mbiu ya "Moyo wangu Moyo Wako". Wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma Wizara ya Afya.

Matembezi ya Siku ya Moyo Duniani yakiendelea, ambayo kwa mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya 'Moyo wangu, Moyo wako"

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiambatana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya wakinyoosha viungo baada ya kumaliza matembezi ya Siku ya Moyo Duniani katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua moja kati ya mabanda yaliyokuwepo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam katika maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani. Kushoto kwake ni Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt. Robert Mvungi, kulia kwake ni Mkurugenzi wa kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma Wizara ya Afya Dkt. Amalberga Kasangala.


SERIKALI YAWEKA MIKAKATI THABITI YA KUPAMBA DHIDI YA UGONJWA WA MOYO

Na WAMJW-Dar es salaam.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeanza kuweka mikakati thabiti ya kupambana dhidi ya maradhi ya Moyo nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo katika maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.

Dkt. Ndugulile alisema kwamba Serikali imeendelea kutoa Elimu kupitia vyombo vya Habari na mitandao ya kijamii, kuanzisha Mpango wa Taifa wa magonjwa yasiyo yakuambukiza, na kuhakikisha TV zote katika Hospitali na Vituo vya Afya zinaonesha jumbe zinazohusu masuala ya Afya tu. 

“Serikali tumeona kwamba tunahitaji kuongeza msukumo kwemnye magonjwa yasiyo yakuambukiza, matamasha tunayofanya ni moja ya mkakati tunaofanya wa kutoa Elimu kwa jamii, kuoa Elimu kupitia njia mbali mbali ikiwemo TV, magazeti, pamoja na mtandao wa jamii, kuanzisha Mpango wa Taifa wa magonjwa yasiyo yakuambukiza, kuelekeza hospitali zote kuonesha jumbe mbali mbali za masuala ya Afya” Alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile alisema kwamba kuna ongezeko kubwa sana la magonjwa yasiyo yakuambukiza ikiwemo maradhi ya Moyo ambayo kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na kutofanya mazoezi, aina ya vyakula tunavyokula, matumizi yaliyopitiliza ya vilevi. 

“Kama taifa tunaona kuna ongezeko kubwa la magonjwa yasiyo yakuambukiza ikiwemo ugonjwa wa Moyo, na visababishi vikubwa ni aina ya vyakula tunavyokula, watu kutofanya mazoezi, matumizi ya pombe na sigara kupita kiasi”, alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile alisema kuwa Magonjwa ya moyo yanaongoza kwa kusababisha vifo duniani na inakadiriwa kuwa watu 17,500,000 hufa kila mwaka duniani kote kutokana na magonjwa ya moyo na kiharusi. 

Aidha, Dkt Ndugulile alisema kuwa kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaeleza kwamba asilimia 40% ya vifo vyote vinavyotokea duniani vinasababishwa na magonjwa ya moyo huku nusu ya vifo ambavyo vinatokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza vinatokana na magonjwa ya moyo.

Pia, Dkt. Ndugulile alisema kuwa matumizi ya Tumbaku na bidhaa zake yanakadiriwa kusababisha vifo vya watu 6,000,000 duniani kila mwaka na pia huchangia kusababisha asilimia 10% ya wagonjwa wenye magonjwa ya moyo. 

Mbali na Hayo Dkt. Ndugulile alisema kwamba kama hatua madhubuti za kinga, uchunguzi wa mapema na tiba stahiki hazitachukuliwa haraka, tatizo la Moyo ifikapo mwaka 2035 litaongezeka na kufikia makadirio ya wagonjwa wapya milioni 131,978,870 (sawa na ongezeko la 45% kutoka hali ilivyo kwa sasa), huku ongezeko kubwa likiwa katika ukanda wa nchi zinazoendelea, Tanzania ikiwa mojawapo.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile alisema kuwa nia thabiti ya Serikali ya Awamu ya tano ni kuboresha huduma za afya hapa nchini ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi vinavyohitajika katika kutoa huduma za afya nchini kwa kuongeza bajeti ya afya kila mwaka. 

“Sisi sote ni mashahidi wa juhudi hizi za Serikali kwa uwepo wa Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete yenye wataalamu wabobezi katika tiba ya magonjwa ya moyo” Alimaliza Dkt. Ndugulile. 


0 on: "SERIKALI YAWEKA MIKAKATI THABITI YA KUPAMBA DHIDI YA UGONJWA WA MOYO"