Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 3 Septemba 2018

WANAHABARI WAFUNDWA JUU YA MLIPUKO WA UGONJWA WA EBOLA NCHINI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa taarifa mbele ya Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) juu ya ugonjwa wa Ebola wakati akifungua Semina juu ya kurepoti kuhusu Ugonjwa wa Ebola iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara leo jijini Dar es salaam.

Waandishi wa Habari waliojitokeza waliojitokeza kupata Elimu juu ya namna kurepoti kuhusu Ugonjwa wa Ebola iliyozinduliwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika Ofisi ndogo za Wizara leo jijini Dar es salaam.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu naMganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohamed Bakari Kambi leo akifungua Semina juu ya kurepoti kuhusu Ugonjwa wa Ebola iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara leo jijini Dar es salaam.

Waandishi wa Habari wakiendelea na Semina  kuhusu namna ya kuripoti Ugonjwa wa Ebola iliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara leo jijini Dar es salaam.

Dkt. Mohamed Ally Mohamed akitoa Elimu juu ya Ugonjwa wa Ebola na namna ya Kuripot ugonjwa huo mbele ya Waandishi wa Habari waliojitokeza leo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.

WANAHABARI WAFUNDWA JUU YA MLIPUKO WA  UGONJWA WA EBOLA NCHINI
Na WAMJW-DAR ES SALAAM.
Waandishi wa Habari wametakiwa kushirikiana na Serikali katika kuihabarisha jamii ili kuepukana na janga hatari la ugonjwa wa Ebola.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  ameyabainisha hayo wakati wa kufungua mafunzo maalum kwa waandishi wa namna ya kutoa taarifa za ugonjwa huo wa Ebola.
 “Ugonjwa huu wa Ebola kiukweli ni ugonjwa hatari. Na tokea kutokea katika nchi za wenzetu umesababisha madhara makubwa sana ikiwemo Uchumi ikiwemo masuala ya biashara na uwekezaji na Sisi tulikuwa na wasiwasi sana ndio maana tulienda wenyewe huko kufuatilia ,mimi nilienda mipakani Rusumo na Mganga Mkuu yeye alienda mipaka ya Ngala na maeneo mengine.” Amesema Waziri Ummy Mwalimu.
Aidha Waziri Ummy ameongeza kuwa, tatizo kubwa ni suala la wasafiri wanaopita njia za panya kwani zimekuwa zikiwapa changamoto na wameomba Kamati za Ulinzi na Usalama kuhakikisha wanalinda maeneo hayo.
Hata hivyo Waziri Ummy amebainisha kuwa, Wizara imejipanga kutafuta  njia bora zaidi mara kwa mara ambapo wameomba Wanahabari kushirikiana na Wizara kupata taarifa na uelewa zaidi.
“Ndugu wanahabari kupitia semina hii itaongeza uelewa wa ugonjwa wa Ebola. Nimefurahi sana Wanahabari na wachora vibonzo wameanza kutoa taarifa na kuchora vibonzo juu ya ebola.
“Nimalizie kwa kusema tena Hadi saa Tanzania hakuna mgonjwa yeyote aliyehisiwa au kuthibitishwa kuwa na Virusi vya Ebola hapa Nchini. Hata hivyo kutokana na ukweli kwamba kuna mwingiliano mkubwa wa wananchi kati ya nchi hizi mbili na ugonjwa huu kugunduliwa kwenye jimbo la Kivu Kaskazini ambalo linapakana na nchi ya Uganda ni ukweli unaotuweka kwenye hali ya wasiwasi mkubwa” Alimalizia Waziri Ummy.
Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Adiele Onyeze amebainisha kuwa wataendelea kushirikiana na Tanzania katika kuzuia milipuko ya magonjwa mbalimbali ikiwemo  ugonjwa huo wa Ebola ambao umekuwa ukiripotiwa mara kwa mara katika nchi za Afrika.
“Dunia kwa sasa ipo katika mapambano ya kuzuia milipuko ya magonjwa. Sisi WHO tumejipanga kusaidia juhudi za Mataifa yote yenye hatari hivyo tutasaidia kutoa elimu na uwelewa kwa Wananchi wote” alieleza Dkt. Adiele Onyeze.
Kwa upande wa mafunzo hayo kwa wanahabari yaliyotolewa watalaam mbalimbali kutoka nje ya Nchi na wa hapa nchini akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Ally Mohammed  alibainisha kuwa: tangu kuripotiwa kwa taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) uliotangazwa na WHO, Agosti Mosi Mwaka huu, Jumla ya wagonjwa 26 na vifo 10 (CFR = 38.5%) vilitokea katika  Nchi hiyo.
Hata hivyo tangu kutoka kwa tamko hilo hali ya ugonjwa imeendelea kwa kasi sana na kufikia wagonjwa 91 na vifo 50 (CFR = 54.9%). Aidha wagonjwa hao imeelezwa kutokea maeneo matano ya afya (Health zones) katika jimbo la Kivu Kaskazini na eneo jingine moja la Ituri ambapo huu ni mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola kutokea nchini DRC, na umetokea wiki moja tu baada ya nchi hiyo kutangaza kumalizika kwa mlipuko mwingine uliotokea mwezi Mei 2018.
Takwimu  zilizotolewa na WHO, Wafanyakazi tisa (9) wa Afya wamethibitishwa kuugua ugonjwa huu, huku ikifanya jumla yao kufikia 10 (9 wamethibitika na 1 anafuatiliwa); na hadi sasa mfanyakazi mmoja amepoteza maisha.
MWISHO.

0 on: "WANAHABARI WAFUNDWA JUU YA MLIPUKO WA UGONJWA WA EBOLA NCHINI"