Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 7 Septemba 2018

DKT. NDUGULILE ATOA SIKU 14 KUKAMILISHWA KWA MASHINE YA X RAY HOSPITALI YA RUFAA DODOMA.

Naibu waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wagonjwa waliokua wanasubiri huduma katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Naibu Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua maboksi ya sindano katika stoo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Naibu waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto akikagua kitabu cha taarifa mbalimbali za hospitali wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma, kulia kwake ni katibu wa afya wa hospitali hiyo Mwanaisha Hassan
 
Naibu Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto akitoa maelekezo kwa viongozi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali hiyo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua mashine ya X Ray.

DKT. NDUGULILE ATOA SIKU 14 KUKAMILISHWA KWA MASHINE YA X RAY HOSPITALI YA RUFAA DODOMA. 

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameutaka uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma kuhakikisha mashine ya kutolea huduma za X-ray  inafanya kazi ndani ya siku 14. 

Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza yenye lengo la kuangalia na kujiridhisha na hali ya utoaji huduma za afya  katika Hospitali hiyo leo jijini Dodoma. 

"Ifikapo Septemba 21 nataka kuona mashine ya kutolea huduma za X-ray na vifaa vingne viwe tayari kutoa huduma kwa wananchi wa Dodoma na maeneo yanayoizunguka kwani Hospitali hii ni tegemezi kwa wakazi wa mkoa huu la sivyo hatua stahiki zitachukuliwa bila ya kumuonea mtu haya" alisisitiza Dkt. Ndugulile

Aidha,Dkt. Ndugulile ametoa siku 30 kwa uongozi wa hospitali hiyo kukarabati jengo la bima ya afya baada ya kukagua na kutoridhishwa na muonekano wake kwani linaleta kero kwa wateja wanaokwenda kupata huduma Hospitalini hapo. 

Mbali na hayo Dkt.  Ndugulile ameonekana kukerwa na uzembe  wa watendaji wa Hospitali  hiyo na kusababisha kuwakemea vikali na kuhaidi maagizo aliyoyatoa yasipotekelezwa kwa wakati hatua za kinidhamu zitakuchululiwa kwa vitendo.

Wakati huo huo dkt.Ndugulile ameuagiza uongozi wa hospitali hiyo kuwarudishia fedha wagonjwa walizotumia kununua dawa pamoja na sindano kwenye maduka yaliopo nje ya hospitali hiyo ilihali wana vifaa hivyo  takribani ya kutosha miezi sita kwenye stoo yao


0 on: "DKT. NDUGULILE ATOA SIKU 14 KUKAMILISHWA KWA MASHINE YA X RAY HOSPITALI YA RUFAA DODOMA."