Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 21 Septemba 2018

MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA SIMU KUSAIDIA KUTOKOMEZA TATIZO LA KIFUA KIKUU (TB)

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Wadau wa Masuala ya Afya wakati akizindua Huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsikiliza Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na na Ukoma wakati akizindua Huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam.

Wadau mbali mbali wa Masuala ya Afya wakishiriki katika Uzinduzi wa Huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam uliofanywa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

Picha ya pamoja ikionesha nyuso za Bashasha kuashiria Uzinduzi rasmi wa Huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam uliofanywa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizindua Huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam.
MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA SIMU KUSAIDIA KUTOKOMEZA TATIZO LA KIFUA KIKUU (TB)

Na WAMJW-DSM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa wito kwa wananchi kutumia Teknolojia ya simu vizuri ikiwemo kupata Elimu kuhusiana na masuala ya Afya.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katika Uzinduzi wa huduma ya TB kupitia Teknolojia ya simu za mikononi leo jijini Dar Es salaam.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa zaidi ya Wananchi wa Tanzania Milion 40 wanamiliki simu hivyo kuwataka kutumia fursa hiyo kupata Elimu ya Afya ikiwemo Elimu ya maambukizi ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).

“zaidi ya Watanzania Milion 40 wanamiliki simu za mikononi, wapo kwenye mfumo wa mawasiliano katika taifa lenye watu zaidi ya Milioni 55,  nawapongeza kwa kuliona na kutambua hili kuangalia jinsi gani tunaweza kutumia teknolojia katika masuala ya Afya” Alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) unashika nafasi ya 9 kwa kusababisha vifo duniani kote na ni ugonjwa pekee wa kuambukiza unaoongoza ukifuatiwa na VVU.

Aidha, Dkt Ndugulile alisema kuwa mwaka 2016 watu milioni 10.4 duniani waliugua  TB, milioni  1.7 walifariki dunia wakati milioni 4.3 million hawakugunduliwa huku ripoti ya TB ya Shirika la Afya Duniani ya mwaka 2017 ikibainisha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi 30 duniani zenye wagonjwa wengi wa TB.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile alisema kuwa jumla ya wagonjwa 69,818 wa TB waligunduliwa ambapo asilimia 90 walitibiwa na kupona, huku ikikadiliwa wagonjwa wanaofikiwa ni asilimia 44  ambapo kuna wagonjwa 84,000 wenye TB ambao bado wapo kwenye jamii na wanaendelea kuambukiza. 

Mbali na hayo Dkt Ndugulile alisema kuwa Lengo la Mpango Mkakati huo ni kupunguza maambukizi ya TB nchini Tanzania ifikapo mwaka 2020 na kupunguza maambukizi mapya ya TB kwa asilimia 20 na idadi ya vifo vinavyotokana na TB kwa asilimia 35.

Hata hivyo Dkt Ndugulile alisema kuwa Wizara itawezesha ufanisi na ufuatiliaji wa mfumo huo na kuhakikisha kuwa taarifa zinakusanywa na kutumika ipasavyo mfano idadi ya watu waliosajiliwa, idadi ya ujumbe uliotumwa kwa walengwa, idadi ya wagonjwa wa TB waliogunduliwa na ufuatiliaji wa wagonjwa kwa wakati muafaka. 

Mwisho Dkt. Ndugulile alitoa Rai kwa Wadau wote wa Masuala ya Afya kwenda kutoa Elimu ya kupambana dhidi ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu kwenye maeneo yenye changamoto ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu.

“Niwaombe sana Wadau wetu, tusiende kwenye maeneo kwa urahisi wenu nyie wa kufika, nawataka muende kwenye kwenye maeneo ambayo yanachangamoto kweli ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu” alisema Dkt. Ndugulile.

Nae Afisa Mwamasishaji kutoka Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kikufua Kikuu na Ukoma Agatha Mshanga alisema kuwa Malengo ya Huduma ya TB kupitia Mtandao wa Simu ni kuongeza uibuaji wa Wagonjwa wa Kifua Kikuu, Waliopo kwenye matibabu waweze kuwa na ufuasi mzuri wa Matibabu, kupambana na unyanyapaa na kutengwa kwa wagonjwa wa TB na kupeleka Elimu ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).


0 on: "MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA SIMU KUSAIDIA KUTOKOMEZA TATIZO LA KIFUA KIKUU (TB)"