Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 9 Septemba 2018

WANAUME WASISITIZWA JUU YA KUPIMA VVU.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wakazi wa Naipanga wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi wakati wa kilele cha Kampeni ya Furaha yangu iliyofanyika mkoani humo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipima Virusi vya Ukimwi wakati wa kilele cha kampeni ya Furaha yangu iliyofanyika katika wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi.

Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati ajumjulia hali mkazi wa Nachingwea aliyejifungua wakati wa ziara yake ya kuangalia hali ya utoaji huduma  katika hospitali ya Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi .

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua dawa zilizopo kwenye stoo ya kuhifadhia dawa wakati wa ziara yake ya kujua hali ya utoaji huduma za afya katika hospitali ya Wilaya ya Nachingwea mkoani lindi.

Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa pili kulia akisikiliza taarifa ya Wilaya ya Nachingwea kutoka kwa Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Rukia Mwango aliyesimama kushoto wakati wa ziara yake Wilayani humo Mkoa wa Lindi.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kushoto akisikiliza maelezo kuhusu upimaji wa VVU kutoka kwa Muuguzi Mkunga Bi. Hidaya Nyenje Hospitali ya Nachingwea wakati wa Kilele cha kampeni ya Furaha yangu Wilayani humo.




Viongozi wa dini zote na Wazee  wa Naipanga wakifuatilia kwa makini hotuba ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile hayupo pichani wakati wa kilele cha Kampeni ya Furaha yangu Wilayani Nachingwea Mkoani Lindi.




WANAUME WASISITIZWA JUU YA KUPIMA VVU. 


Na WAMJW-NACHINGWEA

WANAUME Mkoani Lindi Wilaya ya Nachingwea wamesisitizwa juu ya masuala ya kupima virusi vya Ukimwi ili kujua hali ya maambukizi kwa wakazi wa mkoa huo. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa kilele cha kampeni ya Furaha yangu leo katika Tarafa ya Naipanga wilaya ya Nachingwea Mkoani humo. 

"Kwa sasa Serikali imejipanga kutomomeza maambukizi ya Ukimwi kwani kila takayepima na kugundulika ana maambukizi ataanza kutumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi mara moja ili kufikia lengo la 909090 ifikapo mwaka 2020" alisema Dkt. Ndugulile. 

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa bado idadi ya wanaume wanaojitokeza kupima VVU ni ndogo hivyo kuwataka wanawake wawahimize waume na vijana wao wa kiume kujitokeza kutambu afya zao.

Sambamba na hilo Dkt. Ndugulile aliutaka uongozi w Hospitali ya Wilaya ya Nchingwea kuboresha mazingira ya kutunzia dawa,  chanjo , damu na vitendanishi kwani bado havipo kwenye mpangilio mzuri wa kuhifadhi. 

"Kiukweli mazingira ya Hospitali sijayapenda hivyo nawapa onyo kwa mara ya mwisho na mchukue hatua haraka ya kuboresha mazingira yenu na hali ya utoaji huduma na kuhakikisha kila mtumishi awe Daktari au Muuguzi kujaza taarifa za mgonjwa kila anapomuhudumia kabla ya Serikali kuchukua hatua stahiki dhidi yenu" alisisitiza Dkt. Ndugulile. 

Aidha Dkt. Ndugulile alibainisha kuwa Serikali imeipatia Wilaya hiyo kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Hospitali ya Wilaya hiyo ili kuweza kutoa huduma bora za Afya kwa wananchi wa Wilaya hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Mhe. Rukia Mwango amesema kuwa anayo furaha kusikia hali ya  maambukizi katika mkoa wao umepungua kutoka asilimia 3. 7 mpaka kufikia asilimia 0. 3. 
Aidha Bi. Mwango amesema kuwa wananachingwea hawana budi kujitokeza kupima VVU kwani maendeleo yao yataletwa na wananchi wenye afya njema na kujitambua kwa uchumi wa Nachingwea. 

0 on: " WANAUME WASISITIZWA JUU YA KUPIMA VVU."