Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 28 Oktoba 2017

MH. UMMY AAGIZA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA VYOTE VYA SERIKALI KUTOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI.

Na WAMJWW

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu aagiza Hospitali na Vituo vya Afya vyote vya Serikali nchini kuanzia leo October 28 kutoa huduma ya uchunguzi wa Saratani kila siku wakati wa kliniki ya mama na mtoto, sambamba na huduma hizi, kila mwezi vyatakiwa kuwa na siku moja kwaajili ya kuchunguza na kufanya matibabu ya ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti.
Ameyasema hayo wakati alipofungua matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa Saratani ya matiti, yalifunguliwa  katika viwanja vya hospitali ya Ocean Road mapema leo jijini Dar es salaam.
Aidha Mh. Ummy ameipongeza kazi nzuri inayofanywa na Uongozi wa Hospitali ya Ocean Road katika kutimiza majukumu yake ikiwemo kuongeza vitanda  40 mpaka vitanda 100  kwa gharama zao kwaajili ya wagonjwa wa saratani pindi wanapopata huduma za matibabu ya Chemotherapy.
“Katika kuwaunga mkono Serikali ya awamu ya tano ya Mh. Magufuli imewapatia Bilioni 5 kwajili yakukamilisha mashine za kisasa za matibabu ya Saratani kwa kutumia mionzi.” Alisema Mh. Ummy Mwalimu
Aidha Mh. Ummy Mwalimu ametoa maelekezo kwa Uongozi wa Hospitali ya Ocean Road kuwa wanatakiwa kwenda kwenye shule za Msingi na Sekondari ili kuwajengea watoto uelewa kuhusu ugonjwa wa Saratani,  lakini ni vipi wataweza kujikinga na magonjwa yasiyo yakuambulizwa ikiwemo ugonjwa wa Saratani.
Pia Mh. Ummy alitoa rai kwa wananchi wote hususani wanawake kujitokeza kupima ugonjwa huo kwani unatibika endapo itagunduliwa mapema,  
Nae  Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Grace Maghembe ambae pia alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar Es salaam , ameipongeza Serikali ya awamu ya tano chini ya Raisi Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto kwa kazi kubwa wanayoifanya ikiwemo kuongeza kwa bajeti ya Dawa , vifaa tiba vya uchunguzi na matibabu.
Kwa upande mwingine Dkt. Grace Maghembe kwa niaba ya bodi ameahidi kuendelea kufanya kazi kwa  uaminifu na bidii kubwa katika kuhakikisha kwamba wanakabiliana na ugonjwa huu wa Saratani kwa wananchi hasa wale wa hali ya chini na kuahidi kuendelea kuboresha huduma hii.
“Niwaombe wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam kwenda kupima Saratani kwani ni bure, usisubiri mpaka kuugua, ukichelewa grarama zinaongezeka lakini pia uwezekano wa kupona unakuwa ni mdogo”. Alisema Dkt Grace Maghembe
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage amemhakikishia Mh. Ummy Mwalimu kwamba upatikanaji wa dawa katika Hospitali hiyo ni 80% na dawa za wagonjwa wengi zinapatikana kwa 100%, ukilinganisha na  2015/2016 upatikanaji wa dawa ilikuwa 4% tu,  jambo ambalo lilikuwa ni changamoto kubwa na kufanya malalamiko ya dawa kuwa makubwa sana katika hospitali hiyo, hivyo kuishukuru Serikali ya Magufuli kwa niaba ya Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu.
Mwisho Dkt. Julius Mwaiselage amemhakikishia Mh. Waziri kwamba Hospitali ya Ocean Road ipo katika hatua ya Mwisho ya kuweka mashine mpya mbili (Linear accerelators), hivyo zitasaidia kupunguza muda wa kusubiri kwa wagonjwa kusubiri huduma , lakini kubwa kupunguza wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi.

0 on: "MH. UMMY AAGIZA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA VYOTE VYA SERIKALI KUTOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI."