Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 27 Oktoba 2017

MH. UMMY AHIMIZA UTARATIBU UFUATWE ILI KUWACHUKULIA HATUA MADAKTARI.






Na WAMJWW  
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ahimiza weledi na kukemea vitendo vya baadhi ya Viongozi  kuwachukulia hatua madaktari na badala yake kuwataka wafuate utaratibu uliowekwa.
Mhe. Ummy aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 49 la Afya na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Cha Madaktari.
Nae Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameliagiza Baraza la Mitihani kufanya uhakiki haraka ili wataalamu wa Sekta za Afya wapangiwe vituo.
“Tangu tuingie madarakani  serikali imeweza kutoa vibali vya ajira mpya vipatavyo 3,410 kwa awamu mbili, awamu ya kwanza vibali vya madaktari 258 na awamu ya pili vibali 3,150 kwa wataalamu wa kada ya afya na taratibu za ajira kwa wataalamu hawa 3150 zimekamilika na imebakia hatua ya uhakiki wa vyeti katika Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA)” alisema Mh. Samia Suluhu.
Makamu wa Rais aliwapongeza Chama cha Madaktari kwa kuweza kuandaa Kongamano la 49 na kuweka historia ya kuandaa Makongamano tangu mwaka 1965.
Kauli mbiu ya mwaka huu inayosema “ Malengo ya Maendeleo Endelevu: Uweledi wa Kitaaluma na Utoaji Bora wa Huduma za Afya Nchini Tanzania.” Mada hii ni muhimu sana katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza kwa vitendo wajibu wake wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapatiwa huduma za afya zenye viwango na zinazokidhi mahitaji.

0 on: "MH. UMMY AHIMIZA UTARATIBU UFUATWE ILI KUWACHUKULIA HATUA MADAKTARI."