Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Julai 2018

DKT. NDUGULILE AUGIZA UONGOZI WA MKOA WA MWANZA KUHAKIKISHA 80% YA VITUO VYA AFYA HAVISHUKI CHINI YA NYOTA 3.

 Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akikagua list ya vituo vilivyofanya vizuri kupitia utaratibu wa ugawaji wa nyota katika vituo hivyo  wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

 Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile  akikagua Fiji ya kuhifadhia damu salama pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza, kulia kwake ni mtaalamu wa maabara katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe.

Naibu Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile  akiongea na wagonjwa waliofika katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.


DKT. NDUGULILE AUGIZA UONGOZI WA MKOA WA MWANZA KUHAKIKISHA 80% YA VITUO VYA AFYA HAVISHUKI CHINI YA NYOTA 3.
Na WAMJW – UKEREWE, MWANZA
Serikali kupitia Wizara ya Afya imeuagiza uongozi wa Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kwamba vituo vyote vya Afya vya Serikali na vya binafsi hazishuki chini ya nyota 3, hii ikiwa moja ya jitihada za kuboresha hali ya utoaji wa huduma Afya nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utaji huduma leo katika Wilaya ya Ukerewe Mkoa wa Mwanza.
“Tuhakikishe kwamba Asilimia 80 ya vituo vyetu vyote vya kutolea huduma za Afya vyote kuwa na nyota 3 hicho kiwe ni kiwango cha chini sana,” Alisema Dkt. Faustine Ndugulile.
Dkt. Ndugulile aliendelea kusisitiza kwa watoa huduma za Afya juu ya nidhamu na matumizi ya lugha nzuri pindi wanapokuwa wanawahudumia wagonjwa ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi  yasiyo na lazima,
Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kwamba Serikali imeweka utaratibu wa kuzitambua dawa zake kwa  kuziwekea rebo ya MSD GOT katika dawa zote inazizitoa na kusisitiza kwamba dawa hizo zinastahili kupatikana katika  vituo vya Afya vya Serikali au kwa mgonjwa tu.
“Sisi kama Serikali tumeanza kuweka utaratibu wa kuziwekea rebo dawa zote za Serikali lebo ya MSD GOT, tumeziweka kwenye boksi na kwenye dawa , anaepaswa kuwa nazo ni hospitali zetu na mgonjwa tu, mtu yoyote wa katikati akiwa na hizo dawa basi huyo ametuibia, msimfumbie macho” Alisema Dkt Ndugulile.
Pia, Dkt Ndugulile ameahidi kuwapelekea huduma za dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe jambo linalopelekea kupoteza maisha kwa wahitaji wa huduma hizo kutokana hali ya ugumu wa usafiri kutoka kisiwani Ukerewe mpaka kufika katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza SoukeToure
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Ukerewe Mhe. Joseph Mkundi  amefarijika juu ya ujio wa Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile jambo lililompa fursa ya kuona mazingira halisi na kuziona changamoto ambazo wananchi kutoka Ukerewe wanakumbana nazo.
Kisha Mhe. Joseph Mkundi alimuomba Dkt. Faustine Ndugulile (MB) kuwasaidia  kuboresha huduma za hospitali hiyo ya Wilaya ya Ukerewe kwa kuwajengea chumba cha upasuaji , chumba cha wagonjwa mahututi na boti kwaajili ya kubebea wagonjwa ili kuwavusha kwenda hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza .

“Mambo ambayo nimekuwa nikiyapigania ni juu ya kuboresha hospitali yetu ya Wilaya ili iweze kutoa huduma kamilifu, kwa maana kwa mazingira yetu tunaichukulia kuwa ndio Hospitali ya Rufaa, ikitokea mgonjwa kakosa usafiri inakuwa ni vigumu sana kuweza kusaidia hali yake,” alisema Mhe. Mkundi.


0 on: "DKT. NDUGULILE AUGIZA UONGOZI WA MKOA WA MWANZA KUHAKIKISHA 80% YA VITUO VYA AFYA HAVISHUKI CHINI YA NYOTA 3."