Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 7 Julai 2018

DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.

Mtabibu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Bw.  Wilfred Mandala akiwaelekeza Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund namna ya  kusafisha mguu wa Bw. Juma ambae ni mwasilika  wa ugonjwa wa Matende

Afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Hope Rusibamayila akishirikiana na wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro kutoa maelekezo kwa wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund namna ya Kibuyu Chirizi kikifanya kazi ya kuosha mikono kwa sabuni baada yakutoka Chooni.

Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakiendelea na ziara yao yakukagua baadhi ya miundombinu waliyoisaidia katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro.
Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakigawa kalamu za kuandikia kwa wanafunzi wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro 

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method akiongea na Wanafunzi pamoja na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund wakati walipotembelea katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyopo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro

 Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi akifanya utambulisho kwa Wanafunzi pamoja na Wageni waliofika katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni kutembelea na kujionea maendeleo ya mchango waliotoa katika shule hiyo.

 Afisa Mipango wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya  Bw. Oscar Kaitaba akitoa salam kutoka Wizara ya Afya mbele ya Wanafunzi pamoja na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund

Mwanafunzi Kutoka Shule ya Msingi ya Kilari Vaileth Wilfred akimkabidhi ujumbe Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi baada ya kumaliza Shairi lao, kulia kwake ni  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method na wa mwisho ni Afisa Mipango wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya Bw. Oscar Kaitaba.

Picha yapamoja ya Watumishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund baada ya kumaliza shughuli ya kutembelea na kukagua miundombinu katika Shule ya Msingi Kilari wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro.

Picha ya Pamoja ya Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Kilari wakionesha kalamu zao juu kuonesha furaha zao baada ya kupokea kutoka katika Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund


DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.

Na WAMJW - SIHA KILMANJARO

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Endrew Method amesema kuwa Wilaya ya Siha imepiga hatua kubwa katika kukabiliana na changamoto ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, huku akidai kuwa  97% ya watoto tayari wameshapata dawa hizo za minyoo.
Ameyasema hayo alipowapokea wageni kutoka Bill and Melinda Gate na THE END FUND waliokuja kuangalia utekelezaji wa miradi waliyoifadhili na kufuatilia namna ya wanufaika wanavyofaidika na miradi hiyo katika Wilaya ya Siha.
“Ukiangalia utoaji wa Dawa za minyoo mashuleni kwa Wilaya tulifikia 97% jambo ambalo linasaidia watoto kutopata changamoto za ugonjwa wa minyoo, hata hivyo kwa wagonjwa wa  n je tu matatizo ya minyoo yanafikia hadi nafasi ya tatu hivyo kuna umuhimu mkubwa wa wa kuufanya uwe mkakati endelevu” Alisema Dkt. Method
Dkt. Method aliendelea kusema kuwa Taasisi ya Bill and Melinda Gate na THE END FUND wamekuja kuangalia ni jinsi gani miradi hiyo imekuwa ikitekelezwa na namna ambavyo matumizi ya fedha wanazotoa yamekuwa yakiwanufaisha wahusika.
 “Wamekuja kuangalia, ni jinsi gani yale mambo waliyokuwa wakititusaidia tunatekeleza, na miongoni mwa mambo hayo ni  unyweshaji wa watoto dawa za minyoo kwaajili ya kukabiliana na minyoo mashuleni, usafi wa vyoo na ujenzi wa vyoo bora katika mashule yetu ambayo tumefanya kwa zaidi ya miaka Sita, pia wamekuja kuangalia namna ya kukabiliana na ugonjwa wa trakoma”. Alisema Dkt. Method 
Aidha, Dkt. Method amewashukuru wafadhili hao kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na THE END FUND kwa msaada mkubwa ambao wamekuwa wakitoa katika kuisaidia Serikali ya Tanzania na jamii kwa ujumla kwaajili ya kupambana na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.
Kwa upande wake Afisa Mipango kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Oscar Kaitaba akieleza namna Taasisi ya THE  FUND na Bill and Melinda Gate ilivyosaidia Wizara amesema kuwa ;-
“THE END FUND imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Afya katika kudhibiti ugonjwa wa Vikope (Trakoma) na ugonjwa wa Matende na Mabusha kwa kuwafanyia upasuaji katika Mikoa ya Tanga, Pwani na sehem chache Mkoa wa Dar es salaam”,Alisema Oscar Kaitaba
Oscar Kaitaba aliendelea kuwa Kwa ugonjwa wa Trakoma wamesaidia kufanya upasuaji wa Kope katika Mikoa ya Kilimanjaro katika Wilaya ya SIHA na Arusha katika maeneo ya watu waliohathirika zaidi na ugonjwa huu.


0 on: "DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA."