Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 9 Julai 2018

WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA

Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akifungua Mkutano wa mafunzo wa nchi 21 ambazo zina maambukizi ya Ugonjwa wa Trakoma (Vikope) uliofanyika katika jiji la Arusha.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Timothy Wonanji  akiongea na Wadau  kutoka nchi mbali mbali wa magonjwa ya Trakoma(Vikope) katika kikao kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi katika nchi hizo 21.

Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele chini ya Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazeee na watoto  Dkt . Upendo Mwingila akionga kwa kifupi juu ya hali ya ugonjwa wa Trakoma nchini mbele ya Wadau wa ugonjwa wa Trakoma kutoka nchi 21.

Picha ya Wadau zaidi ya 100 kutoka nchi 21 ambao walihudhuria kikao chenye lengo la kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi kilichofanyika jijini Arusha

 Kundi namba 1 la Wataalamu likiongozwa na madaktari (Graders) wakijadili kuhusu ugonjwa wa Trakoma katika nchi zao.

Kundi namba 2 ni Wataalamu wa masuala ya Takwimu wakijadil namna ya uingizaji wa takwimu kwa usahihi.
Picha ya Pamoja ya Wadau  kutoka nchi 21 wa ugonjwa ya Trakoma(Vikope) walioshiriki katika kikao kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi katika nchi hizo 21.

WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA

Na WAMJW - ARUSHA

Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amethibitisha kuwa halmashauri 58 nchini zimefanikiwa kutibu ugonjwa wa trakoma kutokana na jitihada mbali mbali zilizofanywa na Serikali kwa ushirikiano na Wadau.

Alisema hayo wakati akifungua Mkutano wa Uzinduzi wa Mafunzo kwa wawakilishi wa nchi 21 ambazo zinamaambukizi ya ugonjwa wa Trakoma/ vikope huku lengo likiwa ni kuwajengea wataalamu hao uwezo ili waweze kupambana dhidi ya ugonjwa huu. 
"Mwanzoni tulikuwa na Wilaya takribani 75 ambazo zilikuwa na ugonjwa huu,  jitihada zimeweza kufanyika  tangu 2014 hadi leo Hii  Karibu Wilaya 58 zimeweza kushinda dhidi ya ugonjwa huu, tumebakiza Wilaya 13 na kama Serikali tutaendelea kutoa dawa na Elimu kwa umma ili waweze kujikinga  dhidi ugonjwa huu ", Alisema Dkt. Subi

Dkt Subi aliendelea kusema kuwa sifa mojawapo ya kudhibiti ugonjwa huu ni kupitia mafunzo yanayomjengea uwezo mtaalamu kuweza kujua namna ya kujua ugonjwa, na kuweza kudhibiti dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu  

Kwa upande mwingine Dkt. Subi ametoa wito kwa wananchi wote hususani waliokatika hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu wa trakoma kuwa Safi wakati wote kwa kunawa uso, kujenga vyoo na kusafisha mazingira yanayotuzunguka mara kwa mara. 
"ugonjwa huu unatokana na uchafu, kama huogi, kama hunawi uso, unaweza sababisha macho yako yakahathirika, ni vizuri kutumia Fursa ya maji vizuri kwa kufanya usafi vizuri mda wote" alisema Dkt. Subi 

Pia Dkt Subi aliwahasa wananchi kutumia dawa Kwani ni  salama na nzuri ndiomaana zimeponya watu katika halmashauri 58 kufanikiwa kupambana dhidi ya ugonjwa huu wa trakoma. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt Thimothy Wonanji alisema kuwa bado Wilaya tatu jijini Arusha zinaendelea kusumbuliwa na tatizo hili lá trakoma, Wilaya hizo ni Longido,  ngorongoro pamoja na Monduli na kusema kuwa tatizo kubwa limeonekana kuwa ni changamoto ya upatikaaji wa maji katika maeneo hayo.

Aliendelea kusema kuwa Serikali katika ngazi ya Mkoa kuna uratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambao kwa kushirikiana na wadau wamekuwa na mradi wa kwenda kijijini na kupita nyumba kwa nyumba kuwapima wakazi wa maeneo hayo na kuwaanzishia dawa (zitromas) kwa wanaogundulika kuwa na ugonjwa huu. 

Nae Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt Upendo Mwingila alisema kuwa idadi ya wagonjwa wamepungua kutoka 160 Mpaka mwaka huu wagonjwa elfu 25,000 hii inatoka na juhudi za Wizara ya Áfya kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na Wadau mbali mbali katika kupambana dhidi ya ugonjwa huu wa trakoma jambo lililosaidia kufanikisha kufanya upasuaji wa vikope takribani 12,000 kwa mwaka.

0 on: "WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA"