Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 8 Agosti 2020

WAZIRI UMMY APIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUPEWA VIDONGE VYA FOLIC ACID MASHULENI











Picha mbalimbali zikimuonesha Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela pamoja viongozi mbalimbali wakipita katika mabanda yaliyopo kwenye maonesho ya Nanenane kanda ya Mashariki yanayofanyika Mkoani Morogoro kuona bidhaa na huduma katika mabanda hayo.


NA EMMANUEL MALEGI-MOROGORO

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amepiga marufuku shule zote nchini kuwapa wasichana dawa aina ya Folic Acid na badala yake shule zimetakiwa kulima kuwajengea uwezo wa kulima maboga na mbogamboga katika bustani za shule.

 Waziri Ummy amesema hayo leo wakati alipokua akihitimisha kilele cha Maonesho ya Nanenane kanda ya Mashariki inayojumuisha Mikoa ya Dar Es Salaam, Pwani, Tanga na Morogoro ambayo yamefanyika mkoani Morogoro.

 Waziri Ummy amesema kuwa ni marufuku kuwapa wanafunzi na wasichana balehe vidonge vya Folic Acid, badala yake fedha hizo zinazotolewa kwa ajili ya dawa hizo zitumike kuanzisha bustani shuleni ili kuzalisha vyakula vinavyotoa madini hayo.

 

“Mbali na kuanzishwa kwa bustani shuleni lakini pia fedha hizo zinaweza kupelekwa kwa vijana ili waanzishe miradi ya bustani za mboga kwa ajili ya kuzalisha mazao yanayozalisha asidi hiyo yakiwemo maboga, matunda na hata karoti badala ya kutoa vidonge kwa wanafunzi”. Amesema Ummy.

 

Kuhusu unywaji wa maziwa mashuleni, Waziri Ummy amesema kuwa atamwandikia barua ya pendekezo Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako ili kuanzia Septemba mosi mwaka huu kila shule iwe na kibanda cha maziwa kwa ajili ya wanafunzi kununua.

 Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa  utafiti wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaonesha kwamba kila mtu anatakiwa kunywa nusu lita ya maziwa sawa na lita 180 kwa mwaka, lakini kwa sasa kila mtu anakunywa lita 40 kwa mwaka sawa na vijiko 10 vya chai kwa siku.

 Pia Waziri amesema udumavu kwa watoto wa chini ya miaka mitano umepungua nchini kutoka asilimia 34.4 mwaka 2014 hadi asilimia 31.8 mwaka 2018 licha ya kuwa jitihada zinatakiwa kuendelea kuchukuliwa.

 Pamoja na hayo Waziri Ummy ameupongeza mkoa wa Morogoro kwa kuwa mwenyeji wa maonesho hayo ambayo yamekua chachu ya ukuaji wa kilimo, uvuvi, ufugaji na ujasiriamali nchini na amewataka waratibu wake kutoishia hapo na badala yake ujuzi huo upelekwe vijijini kwa ajili ya kuendeleza sekta hiyo muhimu ambayo kwa kiasi kikubwa inachangia pato la taifa.


0 on: "WAZIRI UMMY APIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUPEWA VIDONGE VYA FOLIC ACID MASHULENI"