Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 18 Septemba 2020

HOSPITALI NA TAASISI ZAELEKEZWA KUSIMAMIA VYEMA WANATAALUMA WA AFYA WALIO KATIKA MAFUNZO KWA VITENDO (WATARAJALI-(INTERNS)

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi


Na.WAMJW-Dodoma

Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Abel Makubi amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Wakurugenzi wa taasisi, vyuo vya afya, na waganga wafawidhi kuhakikisha wanawafuatilia kwa karibu wanataaluma wa afya walio katika mafunzo kwa vitendo , yaani watarajali (interns) ili waweze kupata umahiri(competences), utalaamu(skills) na maadili yanayotegemewa. 

Prof. Makubi ameyabainisha hayo wakati akiongea na wasajili wa Mabaraza ya kitaaluma yaliyopo chini ya wizara afya katika ukumbi wa wizara jiji hapa.

Prof. Makubi alisema Serikali imeenza kupata changamoto za baadhi ya Hospitali kushindwa kuwapa mafunzo stahili  wataraji hao na kujikuta wanamaliza mafunzo yao bila umahiri unaotegemewa katika kutoa huduma kwa wananachi.

"Serikali imeanza kuchunguza hizo hospitali na kama hazitasimamia vyema hawa wanataaluma walio mafunzoni, tutazifutia kibali cha kuwapokea"Alisisitiza 

Aidha, Prof. Makubi aliwataka wanafunzi walio kwenye mafunzo kwa vitendo kujituma katika mafunzo yao, kuonyesha nia ya kujifunza na kuweka bidii katika mafunzo yao ya vitendo mahali walipo. 

"Hawa wanataaluma wanapaswa kuonyesha tabia njema wakati wa mafunzo, kuwa watiifu, kulinda viapo vyao kuzingatia maadili ya taaluma zao na kujiheshimu katika lugha zao na hata mavazi wanayovaa mbele ya wateja wao ambao wengi ni wagonjwa na ndugu zao"Aliongeza. 

Hata hivyo Prof. Makubi ameyaagiza mabaraza hayo kuhakikisha utaratibu wa watarajali 'interns' wote kufanya mitihani baada ya mafuzo, uharakishwe ndani ya   mwaka huu ili serikali iweze kupima umahiri wa wanataaluma wote wanaomaliza mafunzo kwa vitendo.

Prof. Makubi aliipongeza Baraza la  Famasi  kwa kuratibu mitihani kwa wafamasia wataraji  na kulitaka  Baraza la Madaktari nalo likamilishe utaratibu wa mitihani kwa madaktari watarajali wote ili kulinda hadhi ya taaluma ya tiba na viwango vya kutoa huduma kwa wananchi.

0 on: "HOSPITALI NA TAASISI ZAELEKEZWA KUSIMAMIA VYEMA WANATAALUMA WA AFYA WALIO KATIKA MAFUNZO KWA VITENDO (WATARAJALI-(INTERNS)"