Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 7 Oktoba 2020

SERIKALI IMEFANIKIWA KUWEKEZA KWENYE UTOAJI HUDUMA ZA AFYA NCHINI




Na. Catherine Sungura.WAMJW-DSM

erikali kupitia Wizara ya Afya imefanikiwa kuwekeza kwenye utoaji huduma za afya kwa wananchi wote nchini kwa kuboresha majengo,dawa,vifaa na vifaa tiba.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) Bernad Konga mwanzoni mwa wiki wakati wa uzinduzi wa mpango wa dunduliza utakaomuwezesha mwananchi kudunduliza fedha kidogokidogo za mchango wa bima ya afya kupitia bank ya NMB.

Konga alisema kuwa ili wananchi kuwa na uhakika wa matibabu,Serikali iliona kutafuta namna nyepesi ya mwananchi wa hali ya chini aweze kujiunga na mfuko wa bima ya afya kwa kuweka kidogo kidogo kwa muda atakaochagua na atakapokamilisha kiwango husika atapatiwa kadi ya matibabu na kuanza kunufaika na huduma za matibabu kupitia NHIF.

"Serikali imejipanga kumfikia kila mwananchi bila kujali hali yake kikazi na hata makazi,lengo ni kila mwananchi kuwa na uhakika wa matibabu katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya kwa kuwa na bima ya afya ya NHIF".Alibainisha

Hata hivyo Mkurugenzi huyo alisema Serikali inaendelea na utoaji elimu yenye lengo la kuwajengea wananchi utamaduni wa kuwa na bima kabla ya kuugua na sasa imekuja na mpango wa kujiwekea fedha kwa njia ya benki kwa ajili yake na familia yake.

"Menejimenti ya mfuko iliona uwezo wa wananchi kulipa fedha zote kwa awamu moja itakua ni changamoto,hivyo tumefungua milango wananchi wadundulize kidogo kidogo ili wawe na uhakika wa matibabu wakati wowote ".

Mwananchi anayehitaji kujiunga na huduma za NHIF ambaye atahitaji kuweka fedha kidogo kidogo  kwa muda atakaochagua ni yule,anayejiunga kupitia mpango wa vifurushi ambavyo vinajulikana kwa majina ya Najali Afya,Wekeza Afya na Timiza Afya ambavyo pia vinampa fursa  mwananchi anayehiraji kuchangia kuchagua huduma kulingana na mahitaji yake,umri na wanufaika anaohitaji kuwajumuisha.

Mpango huu unamwezesha mwananchi kujiwekea fedha kwa ajili yake mwenyewe ama kwa ajili yake na mwenza wake ama kwa ajili yake na mtoto ama watoto alionao.

Mfumo huo pia ni rahisi kuutumia kwa kuwa unahitaji mtumiaji kuwa na,simu ya mkononi ya aina yoyote na kuzingatia hatua zilizoweka na endapo atakwama hatua za kujisajili anaweza kupiga simu bila malipo kwa namba 0800110063 kupatiwa maelezo namna ya kufanya.

-Mwisho-

0 on: "SERIKALI IMEFANIKIWA KUWEKEZA KWENYE UTOAJI HUDUMA ZA AFYA NCHINI"