Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 17 Julai 2020

PROF. MCHEMBE AWATAKA WAFAMASIA KUSIMAMIA MAADILI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akiongea na wafamasia na wadau wa mnyororo wa ugavi na usambazaji wa bidhaa za afya (hawapo pichani) wakati akifungua kikao kinachoendelea mkoani Morogoro.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Prof. Mabula Mchembe akiwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa ununuzi Serikalini Prof. Geraldine wakifuatilia moja ya mada zilizokua zinawasilishwa katika kikao cha wadau wa mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya nchini.
Mfamasia Mkuu Ndg. Daud Msasi akitolea ufafanuzi moja ya hoja wakati akiwasilisha mada katika kikao cha wafamasia na wadau wa mnyororo wa ugavi na usambazaji wa bidhaa za afya kinachoendelea Mkoani Morogoro.

Picha za Wafamasia na Wadau mbalimbali waliohudhuria kikao cha Wadau wa mnyororo wa ugavi na usambazaji wa bidhaa za afya kutoka Sekta mbalimbali za Serikali na Binafsi waliokutana Mkoani Morogoro.


Na WAJMW-MOROGORO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Prof. Mabula Mchembe amewataka Wafamasia nchini kote kuzingatia maadili na kutumia taaluma waliyonayo ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Prof. Mchembe amesema hayo wakati akifungua semina inayojumuisha Wadau wa mnyororo wa ugavi na usambazaji wa bidhaa za afya kutoka Sekta mbalimbali za Serikali na Binafsi waliokutana Mkoani Morogoro.

“Ninawataka Wafamasia wote mbadilike kulingana na mazingira yaliyopo, hivi sasa nchi imeingia kwenye uchumi wa kati, hii inamaana mboreshe utaalamu wenu ili kukidhi mahitaji ya nchi. Corona imekuja na faida kubwa, imetufanya sasa tunaweza kutengeneza Vitakasa mikono vyetu (Hand Sanitizer) na barakoa jambo ambalo hapo awali halikuwepo”. Amesema Katibu Mkuu Prof. Mchembe.

Prof. Mchembe amesisitiza kuboreshwa kwa huduma za dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya zikiwemo Zahanati na vituo vya afya vya umma kuhakikisha dawa zote muhimu zinapatikana ili mwananchi anapofika kupata huduma asikose dawa na kulazimika kwenda kununua kwenye maduka ya watu binafsi.

Aidha, Prof. Mchembe amewataka wataalamu hao kutochagua vituo vya kazi kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kuwa wanadidimiza taaluma yao kwa kufanya kazi maeneo ambayo hayana vifaa.
“Rais wetu ana nia njema katika kuboresha huduma za afya nchini, utakuta Hospitali fulani ina vifaa vizuri sana vya kufanyia kazi lakini haina wataalam wa kuvitumia”. Amesema Katibu Mkuu huyo.

Katika kutatua changamoto hizo Katibu Mkuu Mchembe amemuagiza Mfamasia Mkuu wa Serikali Ndg. Daud Msasi kuweka muongozo mzuri katika kuwapangia vituo vya kazi Wafamasia na wataalam wengine ili wananchi waweze kupata huduma bora za afya popote walipo.

Pia Prof. Mchembe amesisitiza matumizi ya data katika kutoa huduma na kutunza kumbukumbu kupitia mifumo ya GOTHOMIS na mingineyo ili kurahisisha utoaji wa huduma na kutunza rekodi za wagonjwa na pia kuweka mnyororo wa huduma zote za Hospitali kuwa katika hali nzuri.

Kwa upande wake Mfamasia Mkuu wa Serikali Ndg. Daud Msasi amewataka wadau waliohudhuria katika kikao hicho kuhakikisha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya unatekelezwa ipasavyo kwa kuzingatia mambo ya msingi ambayo ni Pamoja na uzuiaji wa kukua kwa madeni yasiyolipika, nyaraka za mali za serikali zitunzwe vizuri, matumizi ya miongozo ili kuepika gharama zisizo za lazima, uwepo wa maduka ya dawa yanayojiendesha bila kuathiri huduma nyingine Pamoja na kuweka taarifa zilizo sahihi.

MWISHO



8 on: "PROF. MCHEMBE AWATAKA WAFAMASIA KUSIMAMIA MAADILI"
  1. WhatsApp Plus Rosado APK is a modified version of the popular WhatsApp messaging app, offering additional features like enhanced customization options, improved privacy settings, and extra themes. The "Rosado" variant specifically stands out due to its pink-themed user interface. As a third-party app, it is not officially supported by WhatsApp, so users should be cautious of potential security risks.

    JibuFuta
  2. banana hub script blox fruits no oficial creado para hacer trampas en Blox Fruits, ofreciendo funciones como automatización y ventajas desbalanceadas. Su uso va en contra de las reglas de Roblox y puede terminar en un baneo permanente de tu cuenta. Además, estos scripts pueden incluir riesgos de seguridad, por lo que es más seguro evitarlos.

    JibuFuta
  3. Maoni haya yameondolewa na mwandishi.

    JibuFuta
  4. banksholidays are public holidays when banks, schools, and many businesses close, giving people a day off work. In the UK, they include fixed dates like New Year’s Day and Christmas, as well as movable dates like Good Friday and Easter Monday. They provide opportunities for rest, leisure, and spending time with family and friends.

    JibuFuta
  5. zieloboff is a platform that focuses on gaming rewards, offering users chances to get items like Robux, Free Fire passes, and rare skins. It also features a word-puzzle game that can be played without logging in and hosts community events for earning rewards. However, there are concerns about its legitimacy, as some of its domains have low trust scores according to ScamAdviser.

    JibuFuta
  6. chick-fil-a lunch hours its full lunch menu at 10:30 AM, immediately after breakfast hours end, and continues until closing, which is usually around 9 PM or 10 PM depending on the location. Most restaurants operate Monday through Saturday, while all locations remain closed on Sundays. This schedule allows customers to enjoy a variety of lunch options throughout the day.

    JibuFuta
  7. emiratesinside is a website that provides practical guidance for living, working, and navigating daily life in the UAE, covering topics like housing, employment, transportation, and lifestyle. It helps both newcomers and long-term residents understand local culture, visa requirements, and living costs. Users should verify key information through official sources, as the site has some trust concerns.

    JibuFuta
  8. Downloading from Scribd lets users save documents, books, and articles to read offline, providing convenient access without needing an internet connection. This can be useful for studying, research, or reference purposes. However, it’s important to remember that downloading content without proper authorization may violate Scribd’s terms of service Clickhere.

    JibuFuta