Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo HabariPicha. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo HabariPicha. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 21 Agosti 2020

TUSHIRIKIANE KUPAMBANA DHIDI YA MAGONJWA YASIYO AMBUKIZA - MGANGA MKUU WA SERIKALI.

- Hakuna maoni

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (watatu kutoka kushoto) akikagua taarifa za mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Kaskazini KCMC, pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma katika Hospitali hiyo.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (watatu kutoka kushoto) akipokea taarifa za hali ya mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Kaskazini KCMC, pindi alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma katika Hospitali hiyo.

Kiwanda cha uzalishaji mitungi ya oksijeni kilichopo katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya kaskazini KCMC. 

Baadhi ya mashine za uzalishaji wa gesi ya oksijeni inazotumika katika matibabu  ya wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya kaskazini KCMC.


TUSHIRIKIANE KUPAMBANA DHIDI YA MAGONJWA YASIYO AMBUKIZA - MGANGA MKUU WA SERIKALI.

Na WAMJW- KILIMANJARO

MGANGA Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ametoa wito kwa watoa huduma za Afya kushirikiana kwa pamoja kwa kutoa elimu, katika mapambano dhidi ya magonjwa yasiyo ambukiza yanayosababishwa na mtindo wa maisha ikiwemo ulaji usiofaa, matumizi ya vileo na kutofanya mazoezi.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Makubi ametoa rai hiyo wakati alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Kaskazini KCMC kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo kwa wananchi.

Prof. Makubi amesema kuwa, ni muhimu watoa huduma za afya kuungana kwa pamoja kushirikiana kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu magonjwa yasiyo ambukiza (NCD), kwa njia ya kuwafuata wagonjwa katika maeneo yao, jambo ambalo litasaidia kupunguza mzigo wa wagonjwa katika hospitali za Rufaa nchini.

"Mshirikiane kwa pamoja kutoa Elimu ya ufahamu, na kupima angalau mara 2 kwa mwaka juu ya  magonjwa yasiyo ambukiza  kupitia njia ya kuwafuata wateja katika maeneo yao na kuwafanyia upimaji (outreach program)" alisema Prof. Makubi.

Hata hivyo, Prof. Makubi ametoa rai kwa watoa huduma za afya kuhakikisha wanatoa huduma kwa wakati kwa wagonjwa ili kuepusha msongamano unaoweza sababisha mlipuko wa magonjwa mengine katika hospitali na kupunguza usumbufu kwa wagonjwa.

Aidha, Prof. Makubi ameridhishwa kwa kiasi kikubwa hali ya utoaji huduma katika Hospitali hiyo, huku akiwataka kuongeza jitihada ili kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na kupunguza malalamiko yanayoweza kuepukika kwa urahisi.

"Mimi kwa KCMC, sipati malalamiko mengi sana, simamìeni katika ubora huo, na mhakikishe mnaongeza Juhudi zaidi, na kwa hilo nawapongèza sana sana" alisema Prof. Abel Makubi.

Hata hivyo, Prof. Makubi amewapongeza watumishi wa Hospitali ya KCMC wakiongozwa na Mkurugenzi wao Prof. Gileard Masenga kwa kuanzisha mradi wa uzalishaji wa gesi ya oksijeni, jambo linalosaidia kuongeza mapato na kuokoa kiasi kikubwa cha pesa ambacho kingetumika kununua mitungi ya gesi, na pesa hizo kuelekezwa katika kuboresha huduma kwa wananchi.

Naye, Mkurugenzi wa huduma za tiba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Grace Maghembe amewataka watumishi kutobweteka, katika kuwahudumia wananchi, licha ya kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa na uongozi kwa kushirikiana na Mkoa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uhakika ubora huduma Wizara ya Afya Dkt. Eliakim Eliud amewataka watoa huduma kuhakikisha wanafuata miongozo ya kujikinga ya utoaji huduma (IPC guidelines) wakati wa kuhudumia wagonjwa ili kujikinga wao na wagonjwa wanaowahudumia.

Mwisho.

Jumatatu, 24 Februari 2020

VIFO VYA WANAWAKE WAJAWAZITO VYAPUNGUA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA TEMEKE



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiangalia kifaa cha uchunguzi kwenye idara ya meno    ambapo hivi sasa hospitali ya rufaa ya mkoa temeke wanatoa huduma za kibingwa za huduma ya meno.
Waziri Ummy Mwalimu akiwajulia hali wagonjwa waliofika hospitalini hapo

Waziri Ummy Mwalimu akiwajulia hali akina mama wajawazito waliolazwa kwenye wodi ya uzazi hospitalini hapo


Jengo la huduma za dharura lililofanyiwa ukarabati


Na. Catherine Sungura - Dar es Salaam 
 
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa temeke imejipanga kuokoa maisha ya wakina mama, wajawazito hususan katika kipindi cha kujifungua, kutimiza lengo hilo imeboresha miundombinu yake, vifaa tiba pamoja na kuimarisha huduma za afya kwenye ngazi za msingi.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, wakati wa ziara yake ya kikazi hospitalini hapo, ambako alikwenda kwa lengo la kusikiliza maoni na changamoto kutoka kwa wananchi na watumishi wa hospitali hiyo.

“Mwaka 2018 walikuwa na vifo 19 vya wajawazito na 2019 walikuwa na vifo 8 tu, lakini kwa takwimu za kuanzia Novemba 2019 hadi leo hakuna mwanamke mjamzito aliyekuja hospitalini hapa na kupoteza maisha, niwapongeze madaktari, wauguzi na watoa huduma wote wa hapa kwa hatua hii," amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa jitihada za makusudi, kuwekeza kwenye huduma za afya nchini sambamba na ujenzi wa vituo vya afya na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa.

“Sasa hivi hapa temeke kuna huduma za kibingwa za meno ambapo zamani haikuwepo," amesema.

Waziri Ummy amesisitiza Wizara ina mpango pia wa kuhakikisha huduma zote za kibingwa zinazohitajika zinakuwepo kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa.

Hata hivyo amesema kuwa wanawake 15 kati ya wanawake 100 ndio ambao huhitaji kupelekwa kujifungulia kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa hususan wale wenye changamoto za ujauzito, kwa mfano mtoto amekaa vibaya au viashiria vya uzazi pingamizi.

Kwa upande  wa vipimo waziri huyo amesema kuwa Wizara yake imeongeza vipimo vya utra sound hivi sasa serikali imeboresha vituo vya afya na kwamba vipimo hivyo vinaanza kutolewa kuanzia ngazi za vituo vya afya vya umma na hospitali za wilaya nchini.

Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma kuanzia ngazi ya msingi na hospitali za rufaa za mikoa ni kwa wagonjwa watakaopata rufaa.

“Kwa yeyeote atakayefanya makusudi kukorofisha vipimo ili watu waende kupima kwenye vutuo binafsi tutawachukulia hatua kwani ni wahujumu uchumi, tunataka vipimo vyote vifanyike ndani ya hospitali ila pale mashine haipo tutaruhusu, lengo letu ni kujitosheleza kwa vipimo vyote kwenye vituo vya afya vya umma," amesisitiza Waziri Ummy.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Yudas Ndungile amesema kuwa kutokana na maboresho ya miundombinu, wataalam na vifaa tiba kwa mkoa huu wameweza kupunguza vifo vipatavyo arobaini kwa mwaka ukilinganisha na vifo186 mwaka 2018 hadi vifo 140 mwaka 2019 na matarajio yao ni kupunguza zaidi.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke Dkt. Meshack Shimwela amesema kuwa  hospitali hiyo imeondoa msongamano wa wajawazito kwa kuwa hivi sasa wananchi wengi wanafuata mfumo wa rufaa.

"Hivyo wakina mama wajawazito wanaofika kwenye hospitali hii ni wale wenye changamoto ya uzazi kwa maana hiyo wengi wanajifungulia kwenye ngazi za chini ambapo huduma za afya nazo zimeboreshwa," amesema.

MWISHO

Jumanne, 17 Desemba 2019

KAYA ZENYE VYOO BORA ZIMEONGEZEKA KUFIKIA ASILIMIA 62.4 NCHINI

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, akisisitiza jambo katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Musa Sima akitoa maelekezo kwa maafisa Afya katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akiwasalimia Maafisa Afya, katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Dkt. Ntuli Kapologwe akitoa salamu za Waziri wa OR TAMISEMI katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akieleza jambo katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Afya waliohudhuria katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma. 

Baadhi ya Maafisa Afya kutoka Mikoa,halmashauri  wakifuatilia kwa makini maagizo kutoka kwa mgeni rasmi, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha).

Washindi wa Makala Televisheni ya Usafi wa Mazingira wanaotoka ITVwakipokea tuzo na zawadi kutokana na kuibuka namba moja.

Waandishi waliofanikiwa kushinda tuzo mbali mbali na zawadi kwa kuandaa makala na vipindi (Radio na Televisheni) kuhusu usafi wa mazingira wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Afya na Wadau wa Mazingira.



KAYA ZENYE VYOO BORA ZIMEONGEZEKA KUFIKIA ASILIMIA 62.4 NCHINI

Na. Catherine Sungura,Dodoma

Kaya zenye vyoo bora nchini zimeongezeka hadi kufikia asilimia 62.4 mwaka 2019 kutoka asilimia 34 mwaka 2015 kupitia kampeni ya usichukulie poa, nyumba ni choo iliyoendeshwa kipindi cha miaka miwili na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini hapa .

“Katika kipindi cha miaka miwili ya kampeni hii  kaya zenye vyoo bora zimeongezeka ,vile vile  kaya zisizokuwa na vyoo kabisa imepungua kutoka asilimia 7.5 hadi asilimia 1.9 katika kipindi hiki”Amesema Waziri Ummy.

Aidha, amesema  kwa upande wa wa vijiji ambavyo kaya zake zote zina vyoo imeongezeka kutoka 743 hadi 4,311 na kwa upande wa taasisi wameweza kuboresha  huduma ya maji na usafi wa mazingira katika vituo vya tiba  1,267 kati ya lengo  la vituo 1,000.

“Haya si mafanikio  ya kubeza na kimsingi ninapenda kuwashukuru wadau  kwa kushirikiana  na serikali kufanikisha kapeni hii,lengo letu ni kufuta kabisa  kaya zisizokuwa  na vyoo  na kuongeza kaya zenye vyoo boras hadi asilimia 75 ifikapo Juni,2021”.

Kwa upande wa maeneo ya kutupia taka ngumu,Waziri huyo amesema kuwa  Serikali ya awamu ya tano ina nia ya dhati ya kuboresha maeneo ya kutupia taka  hususan madampo yaliyopo kwenye miji ili yawe ya kisasa.

Hata hivyo amesema kuwa uchakuzi wa mazingira utokanao na taka ngumu umeendele kuwa changamoto  katika maeneo ya mijini,hivyo serikali imejipanga kuongeza nguvu kwenye mamlaka za serikali za mitaa ili kuboresha miundombinu iliyopo katika mitaa hapa nchini.

“Serikali pia imeandaa mwongozo wa uwekezaji  katika taka ngumu ili kuhamasisha  uwekezaji na kuongeza jitihada  za kuboresha usimamizi wa taka hapa nchini”.

Tafiti zinaonesha kwamba nchi inapoteza takribani  asilimia moja ya pato ghafi la taifa(GDP) kutokana na hali duni ya usafi na utafiti uliofanywa na benki ya dunia mwaka 2012 ulionesha kwamba kila mwaka shilingi bilioni 450 zinapotea kutokana na madhara ya uchafu.

#TunaboreshaAfya

Jumatatu, 16 Desemba 2019

MAOFISA AFYA WATAKIWA KUWAKINGA WANANCHI DHIDI YA MAGONJWA-DKT. SUBI

Mkurugenzi wa Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akieleza jambo mbele ya Maafisa Afya wa Mikoa na Halmashauri, wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya usafi wa mazingira.

Afisa kutoka Idara ya Mazingira Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto Bw. Anyitike Mwakitalima akieleza mafanikio mbali mbali yaliyopatikana kutokana na afua mbali mbali za usafi wa mazingira zinazotekelezwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau.

Maafisa Afya kutoka Mikoa, Halmashauri na Wadau wakifuatilia kwa makini neno kutoka kwa Mkurugenzi wa Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi.


MAOFISA AFYA WATAKIWA KUWAKINGA WANANCHI DHIDI YA MAGONJWA-DKT. SUBI

Na Catherine Sungura, WAMJW - Dodoma

Maofisa afya wa mikoa na halmashauri wametakiwa kusimamia afya ya jamii kwenye maeneo yao ili wananchi wajikinge dhidi ya magonjwa yakuambukiza na yele yasiyoambukiza.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa kinga Dkt. Leonard Subi wakati akiongea na maofisa hao ambao wanakutana jijini hapa  kwa  kikao kazi cha siku tatu wakijadili utekelezaji wa maazimio yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa kwanza mwaka jana  na  Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

“Mkutano huu ni wa pili mwaka huu,ni mkutano muhimu kwa maofisa afya kwani ndio wasimamizi wa shughuli za afya katika ngazi za jamii kwa kuhakikisha wananchi wanajikinga na maradhi, kula chakula bora kuishi makazi bora,usafi wa mazingira pamoja na kuwa vyoo bora”.Amesema Dkt. Subi

Aidha, amesema katika mkutano huu mambo mbali mbali yatajadiliwa ikiwemo  afya mazingira,usafi na uchafuzi wa mazingira na kila kinachotumiwa na kumzunguka  mwananchi ,pia wataangalia mabadiliko ya tabia nchi na kupata taarifa kutoka ngazi za mikoa ni jinsi gani walivyotekeleza majukumu yao.

“Maafisa afya muendelee kuishauri wizara kwa kutumia takwimu kwani tunatarajia mkutano huu mtabadilishana uzoefu  kutoka sehemu zenu za kazi,kama wizara tumekua tukitengeneza sera na miongozo mbali mbali ya kudhibiti maradhi yote yanayoweza kuathiri afya za binadamu hivyo kazi ya wizara ni kukusanya taarifa,kuchakata na kuzitolea miongozo na maelekezo”. Aliongeza Dkt. Subi.

Hata hivyo amesema maofisa hao wana majukumu ya kusimamia na  kulinda afya mipakani ili kusiingie magonjwa ya milipuko kutoka nje hususan  nchi za jirani pamoja na utoaji wa chanjo ambapo Tanzania ipo vizuri.

Mkutano huo ambao utafunguliwa kesho na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu umebeba Kauli mbiu isemayo “Huduma bora za afya mazingira na usafi ni kichocheo muhimu cha uchumi endelevu.


Jumapili, 22 Septemba 2019

KINGA NI BORA KULIKO TIBA – RC SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Tellack akisisitiza jambo wakati akiongea na Wananchi wa Shinyanga katika mji wa Kahama ikiwa ni siku ya kufunga kwa Kampeni ya Kitaifa ya ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” iliyofanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama.

Mkuu wa Wilaya ya SShinyanga Mhe. Jasinta Mboneko  akieleza jambo wakati akiongea na Wananchi wa Shinyanga katika mji wa Kahama ikiwa ni siku ya kufunga kwa Kampeni ya Kitaifa ya ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” iliyofanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama.

Mratibu wa kampeni  ya ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” akitoa salamu za Wizara ya  Afya mbele ya Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa ya Shinyanga Mhe Zainab Tellack, wakati wa kufunga Kampeni hiyo katika mikoa ya kanda ya ziwa, tukio limefanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama Shinyanga.

Meza kuu ikiongozwa na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Tellack  wakati wa kufunga kwa Kampeni ya Kitaifa ya ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” iliyofanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama.

Umati wa watu uliojitokeza kumsikiliza mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Tellack wakati wa  kufunga Kampeni ya Kitaifa ya ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” iliyofanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama.


KINGA NI BORA KULIKO TIBA – RC SHINYANGA

Na Rayson Mwaisemba WAMJW-SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Tellack amewaasa Wananchi wa Mkoa huo kujikita katika huduma za kukinga kuliko kutibu magonjwa ili kuondokana na gharama kubwa zinazotumika katika kutibu kwenye ngazi ya familia na Serikali.

Wito huo ameutoa wakati akiongea na Wananchi wa Shinyanga katika mji wa Kahama ikiwa ni siku ya kufunga kwa Kampeni ya Kitaifa ya ujenzi wa vyoo bora na kuvitumia kwa usahihi ” USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” iliyofanyika katika viwanja vya Majengo, Kahama.

Mhe. Zainab Tellack amesema kuwa idadi kuwa ya magonjwa ya mlipuko nchini kama vile kuhara na kipindupindu yanatokana na tatizo la kutokuwa na vyoo bora na kutonawa mikono kwa maji safi chirizika na sabuni hali inayopelekea kuingia gharama kubwa kutibu magonwa hayo.

“kuna maradhi mbali mbali ambayo Watanzania wanayapata, ambayo si ya lazima, maradhi kama Kipindupindu, Kuhara, Minyoo ambayo yanasababishwa na ukosefu wa vyoo, na kuvitumia kwa usahihi, huku wengine wakitoka vyooni hawanawi mikono matokeo yake wanakula kinyesi jambo linalopelekea kupata magonjwa ambayo yanawagharimu katika matibabu” Alisema Mhe. Zainab Tellack.

Aliendelea kutoa wito kwa kusisitiza, ujenzi wa choo bora na matumizi sahihi utasaidia kupunguza  matumizi ya dawa mara kwa mara ambayo hayana ulazima, jambo litalosaidia kupunguza usugu dawa, na madhara mengine madogo madogo yatokanayo na matumizi ya dawa.

Aidha, Mhe. Zainab Tellack ameahidi kuwa, kama Mkoa ifikapo Disemba 31 kaya zote katika Mkoa wa Shinya lazima zitakuwa na vyoo bora, na kuvitumia vyoo hivyo kwa usahihi ili kuendelea kujikinga dhidi ya magonjwa ya Kipindu pindu, kuhara na minyoo.

“Ndugu zangu Wanakahama na Shinyanga kwa ujumla sisi kama Mkoa tumeahidi, kwamba ifikapo Disemba 31, kaya zetu zote kwenye Mkoa huu lazima ziwe na vyoo, hilo ndugu zangu tunaweza, kama vijana wetu wanathamani kubwa kwanini tushindwe kujenga vyoo” alisema  Mhe. Zainab Tellack.

Katika Mkutano huo, Mhe. Zainab Tellack alikubaliana na Wananchi wa Mkoa huo kuwa ifikapo Disemba 31 kwa Wananchi wataokuwa hawana vyoo watapigwa faini ya kiasi cha shilingi 500,000 na kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.

“Ambae hatokuwa na Choo bora ifikapo Disemba 31, faini 500,000 tumekubaliana hivyo, na mmesema wenyewe, na mimi nabariki hilo, kwa hiyo tujipange ili tusifike huko” Mhe. Zainab Tellack.

Kwa upande wake Mratibu wa Kampeni ya “USICHUKULIE POA, NYUMBA NI CHOO” Bw. Anyitike Mwakitalima amesema kuwa kila dakika moja Dunia inapoteza watu 4,  sawa na  watu 6000 kila siku, huku sababu ya vifo hivyo ikiwa kula  kinyesi hali inayotokana na kutotumia vyoo na kunawa mikono kwa maji safi tiririka na sabuni, huku wahanga wakubwa wa tatizo hili wakiwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

"Kila dakika moja Dunia inapoteza watu 4, ikiwa inamaana kwamba kila siku Dunia inapoteza watu 6000, na hawa ni kwasababu tu wamekula kinyesi na wengi wao ni Watoto wenye umri chini ya miaka mitano" alisema Bw. Anyitike Mwakitalima

MWISHO.

Jumatatu, 9 Septemba 2019

TANZANIA NA CUBA KUENDELEZA USHIRIKIAKO KWENYE SEKTA YA AFYA

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile pamoja na mgeni wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez (hayupo pichani) katika kikao kujadili mahusiano baina ya nchi mbili kwenye Sekya ya Afya.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez akifafanua jambo kwenye kikao kujadili mahusiano baina ya nchi mbili kwenye Sekya ya Afya.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akiagana na mbeni wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez (kushoto) mara baada ya kumaliza kikao kujadili mahusiano baina ya nchi mbili kwenye Sekya ya Afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile leo amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez Jijini Dodoma.

Katika mazungumzo yao, Dkt. Ndugulile ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Cuba kwa kuendelea kusaidia Sekta ya Afya nchini kwa kutoa madaktari bigwa kufanya kazi kwenye hospitali hapa nchini Tanzania.

Dkt. Ndugulile ametaka mahusiano hayo chanya yaendelee kuimarika ili Watanzania wengi wanufaike kwa kuweza kupata huduma bora za matibabu ya kibingwa. 

“Nchi ya Cuba imepiga hatua kubwa kwenye Sekta ya Afya na wana madaktari bingwa wengi ambao tunaweza kuwatumia kuja hapa nchini kuhudumia Watanzania wengi zaidi ndani ya muda mfupi kuliko kupeleka wagonjwa nje” amesema Dkt.Ndugulile na kuendelea kusema kuwa pindi Madaktari hao wa kigeni wanapokuja hapa nchini, madaktari wa Kitanzania wanapata fursa ya kujifunza kwa vitendo na kutibu hapa hapa nchini kwa kutumia miundombinu iliyokuwepo hivyo kupunguza gharama kwa Serikali kusafirisha wagonjwa kwenda nje ya nchi.

Kwa upande wake Mhe. Marcelino Gonzalez ameipongeza Tanzania kwa juhudi kubwa inazozifanya kuwekeza kwenye Sekta ya Afya na kuhakikisha Madaktari wanapata utaalamu wa kutosha ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema kuwa nchi ya Cuba iko tayari kutoa nafasi za masomo kusomea fani ya udaktari ili kuja kutibu Watanzania.

Nchi ya Cuba imekuwa na mahusiano ya karibu na Tanzania  kwa  kipindi kirefu. Mnamo Mwaka 1964 ubalozi wa Cuba ulifunguliwa rasmi nchini Tanzania na miaka 10 baadaye  mwaka 1974 Rais Fidel Castrol, alifika Tanzania kumtembelea Mwl.Julius Nyerere.Nchi ya Cuba na Tanzania Imekuwa na Mahusiano kwenye mambo mengi ikiwemo ushirikiano katika kutoa huduma za Afya.