Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 17 Desemba 2019

KAYA ZENYE VYOO BORA ZIMEONGEZEKA KUFIKIA ASILIMIA 62.4 NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, akisisitiza jambo katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Musa Sima akitoa maelekezo kwa maafisa Afya katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akiwasalimia Maafisa Afya, katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Dkt. Ntuli Kapologwe akitoa salamu za Waziri wa OR TAMISEMI katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akieleza jambo katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Afya waliohudhuria katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini Dodoma. 

Baadhi ya Maafisa Afya kutoka Mikoa,halmashauri  wakifuatilia kwa makini maagizo kutoka kwa mgeni rasmi, Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha).

Washindi wa Makala Televisheni ya Usafi wa Mazingira wanaotoka ITVwakipokea tuzo na zawadi kutokana na kuibuka namba moja.

Waandishi waliofanikiwa kushinda tuzo mbali mbali na zawadi kwa kuandaa makala na vipindi (Radio na Televisheni) kuhusu usafi wa mazingira wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Afya na Wadau wa Mazingira.



KAYA ZENYE VYOO BORA ZIMEONGEZEKA KUFIKIA ASILIMIA 62.4 NCHINI

Na. Catherine Sungura,Dodoma

Kaya zenye vyoo bora nchini zimeongezeka hadi kufikia asilimia 62.4 mwaka 2019 kutoka asilimia 34 mwaka 2015 kupitia kampeni ya usichukulie poa, nyumba ni choo iliyoendeshwa kipindi cha miaka miwili na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katika kilele cha wiki ya usafi wa mazingira  kitaifa na mkutano wa maafisa afya wa mikoa,halmashauri  na wadau uliofanyika jijini hapa .

“Katika kipindi cha miaka miwili ya kampeni hii  kaya zenye vyoo bora zimeongezeka ,vile vile  kaya zisizokuwa na vyoo kabisa imepungua kutoka asilimia 7.5 hadi asilimia 1.9 katika kipindi hiki”Amesema Waziri Ummy.

Aidha, amesema  kwa upande wa wa vijiji ambavyo kaya zake zote zina vyoo imeongezeka kutoka 743 hadi 4,311 na kwa upande wa taasisi wameweza kuboresha  huduma ya maji na usafi wa mazingira katika vituo vya tiba  1,267 kati ya lengo  la vituo 1,000.

“Haya si mafanikio  ya kubeza na kimsingi ninapenda kuwashukuru wadau  kwa kushirikiana  na serikali kufanikisha kapeni hii,lengo letu ni kufuta kabisa  kaya zisizokuwa  na vyoo  na kuongeza kaya zenye vyoo boras hadi asilimia 75 ifikapo Juni,2021”.

Kwa upande wa maeneo ya kutupia taka ngumu,Waziri huyo amesema kuwa  Serikali ya awamu ya tano ina nia ya dhati ya kuboresha maeneo ya kutupia taka  hususan madampo yaliyopo kwenye miji ili yawe ya kisasa.

Hata hivyo amesema kuwa uchakuzi wa mazingira utokanao na taka ngumu umeendele kuwa changamoto  katika maeneo ya mijini,hivyo serikali imejipanga kuongeza nguvu kwenye mamlaka za serikali za mitaa ili kuboresha miundombinu iliyopo katika mitaa hapa nchini.

“Serikali pia imeandaa mwongozo wa uwekezaji  katika taka ngumu ili kuhamasisha  uwekezaji na kuongeza jitihada  za kuboresha usimamizi wa taka hapa nchini”.

Tafiti zinaonesha kwamba nchi inapoteza takribani  asilimia moja ya pato ghafi la taifa(GDP) kutokana na hali duni ya usafi na utafiti uliofanywa na benki ya dunia mwaka 2012 ulionesha kwamba kila mwaka shilingi bilioni 450 zinapotea kutokana na madhara ya uchafu.

#TunaboreshaAfya

0 on: " KAYA ZENYE VYOO BORA ZIMEONGEZEKA KUFIKIA ASILIMIA 62.4 NCHINI"