Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 24 Desemba 2019

HOSPITALI YA KANDA YA KUSINI KUANZA KAZI MWAKANI






Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya kanda ya kusini kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ili ianze kutoa huduma ifikapo juni 2020.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati alipotembelea na  kukagua maendeleo ya ujenzi wa hosputali hiyo ambayo na shirika la Taifa la nyumba (NHC)

“Nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa hospitali  hii,ninakutaka  ufanye kazi usiku na mchana ili ikiwezekana Hospitali ianze kutoa huduma ifikapo Juni,2020".Alisisitiza Waziri Ummy

Katika Ziara yake Waziri huyo pia alitembelea zahanati ya Ufukoni iliyopo Manispaa ya Mtwara na kukagua utoaji wa huduma ambapo katika kliniki ya watoto alikutana na changamoto ya uhaba wa chanjo hususan chanjo ya Surua na kuelekeza mkoa ufanye mawasiliano ya haraka na Mpango wa taifa wa  Chanjo ili kupatiwa chanjo hizo.

Aidha, Waziri Ummy aliwataka wananchi waliokuwa wamefika kupata huduma kwenye zahanati hiyo  wajiunge na Bima za Afya ili waondokane na tatizo la kukosa fedha za matibabu pindi wanapohitaji matibabu

Hata hivyo katika ziara yake kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa ya mtwara Ligula,Waziri Ummy ameridhishwa na hali ya upatikanaji wa dawa muhimu na hivyo kuwata viongozi wa hospitali hiyo.kuhakikisha wanatoa.vipaumbele katika masuala yanayojitokeza ikiwemo kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi mapema kwa kufuata taratibu na miongozo ya kazi zao ili kuweza kuwahudumia wananchi kwa wakati.

0 on: "HOSPITALI YA KANDA YA KUSINI KUANZA KAZI MWAKANI"